Lithuanian

Swahili: New Testament

Matthew

26

1Baigęs visa tai kalbėti, Jėzus tarė savo mokiniams:
1Yesu alipomaliza kusema hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2“Jūs žinote, kad po dviejų dienų bus Pascha, ir Žmogaus Sūnus bus atiduotas nukryžiuoti”.
2"Mnajua kwamba baada ya siku mbili tutakuwa na sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mtu atatolewa ili asulubiwe."
3Tuomet aukštieji kunigai, Rašto žinovai bei tautos vyresnieji susirinko į vyriausiojo kunigo Kajafo rūmus
3Wakati huo makuhani wakuu na wazee wa watu walikutana pamoja katika ukumbi wa Kayafa, Kuhani Mkuu.
4ir nusprendė suimti Jėzų klasta ir Jį nužudyti.
4Wakashauriana jinsi ya kumtia Yesu nguvuni kwa hila wamuue.
5Bet jie sakė: “Tik ne per šventes, kad žmonėse nekiltų sąmyšio”.
5Lakini wakaamua jambo hilo lisifanyike wakati wa sikukuu, kusije kukatokea ghasia kati ya watu.
6Kai Jėzus buvo Betanijoje, Simono Raupsuotojo namuose,
6Yesu alipokuwa Bethania, nyumbani kwa Simoni, aitwaye Mkoma,
7atėjo moteris su alebastriniu labai brangaus kvapiojo aliejaus indu ir Jam sėdinčiam prie stalo išpylė ant galvos.
7mama mmoja aliyekuwa na chupa ya alabasta yenye marashi ya thamani kubwa, alimjia pale mezani alipokuwa amekaa kula chakula, akammiminia hayo marashi kichwani.
8Tai pamatę, mokiniai pasipiktino ir kalbėjo: “Kam toks eikvojimas?
8Wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, "Ya nini hasara hii?
9Juk buvo galima aliejų brangiai parduoti ir išdalyti pinigus vargšams”.
9Marashi haya yangaliweza kuuzwa kwa bei kubwa, maskini wakapewa hizo fedha."
10Tai sužinojęs, Jėzus tarė: “Kam skaudinate moterį? Ji man padarė gerą darbą!
10Yesu alitambua mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnamsumbua huyu mama? Yeye amenitendea jambo jema.
11Vargšų jūs visuomet turite su savimi, o mane ne visuomet turėsite.
11Maskini mnao daima pamoja nanyi, lakini mimi sitakuwapo pamoja nanyi daima.
12Išpildama aliejų ant mano kūno, ji tai padarė mano laidotuvėms.
12Huyu mama amenimiminia marashi ili kunitayarisha kwa maziko.
13Iš tiesų sakau jums: visame pasaulyje, kur tik bus skelbiama ši Evangelija, jos atminimui bus pasakojama ir tai, ką ji padarė”.
13Nawaambieni kweli, popote ambapo hii Habari Njema itahubiriwa ulimwenguni, kitendo hiki alichofanya mama huyu kitatajwa kwa kumkumbuka yeye."
14Tada vienas iš dvylikos, vardu Judas Iskarijotas, nuėjo pas aukštuosius kunigus
14Kisha, Yuda Iskarioti, mmoja wa wale kumi na wawili, akaenda kwa makuhani wakuu,
15ir tarė: “Ką man duosite, jeigu Jį jums išduosiu?” Tie suderėjo su juo trisdešimt sidabrinių.
15akawaambia, "Mtanipa kitu gani kama nikimkabidhi Yesu kwenu?" Wakamhesabia sarafu thelathini za fedha;
16Ir nuo to laiko jis ieškojo progos išduoti Jį.
16na tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta nafasi ya kumsaliti.
17Pirmąją Neraugintos duonos dieną mokiniai priėjo prie Jėzaus ir paklausė: “Kur nori, kad Tau paruoštume valgyti Paschą?”
17Siku ya kwanza kabla ya Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, wanafunzi walimwendea Yesu wakamwuliza, "Unataka tukuandalie wapi chakula cha Pasaka?"
18Jis atsakė: “Eikite į miestą pas tokį žmogų ir sakykite jam: ‘Mokytojas sako: Mano metas arti. Pas tave švęsiu Paschą su savo mokiniais’ ”.
18Yeye akawajibu, "Nendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie: Mwalimu anasema, wakati wangu umefika; kwako nitakula Pasaka pamoja na wanafunzi wangu."
19Mokiniai padarė, kaip Jėzus nurodė, ir paruošė Paschą.
19Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaandaa Pasaka.
20Atėjus vakarui, Jėzus su dvylika sėdosi prie stalo.
20Kulipokuwa jioni, Yesu akakaa mezani pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili.
21Jiems bevalgant, Jėzus tarė: “Iš tiesų sakau jums: vienas iš jūsų mane išduos”.
21Walipokuwa wakila, Yesu akasema, "Nawaambieni kweli, mmoja wenu atanisaliti."
22Jie labai nuliūdo ir kiekvienas klausė Jo: “Nejaugi aš, Viešpatie?”
22Wanafunzi wakahuzunika sana, wakaanza kuuliza mmojammoja, "Bwana! Je, ni mimi?"
23Jis atsakė: “Mane išduos dažantis kartu su manim duoną dubenyje.
23Yesu akajibu, "Atakayechovya mkate pamoja nami katika bakuli ndiye atakayenisaliti.
24Žmogaus Sūnus, tiesa, eina, kaip apie Jį parašyta, bet vargas tam žmogui, per kurį Žmogaus Sūnus išduodamas. Geriau būtų buvę tam žmogui negimti”.
24Naam, Mwana wa Mtu anakwenda zake kama Maandiko Matakatifu yasemavyo, lakini ole wake mtu yule atakayemsaliti Mwana wa Mtu! Ingalikuwa afadhali kwa mtu huyo kama hangalizaliwa."
25Jo išdavėjas Judas paklausė: “Nejaugi aš, Rabi?!” Jis atsakė: “Tu pasakei”.
25Yuda, ambaye ndiye aliyetaka kumsaliti, akamwuliza, "Mwalimu! Je, ni mimi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
26Kai jie valgė, Jėzus paėmė duoną, palaimino, laužė ją ir davė mokiniams, sakydamas: “Imkite ir valgykite: tai yra mano kūnas”.
26Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
27Po to paėmė taurę, padėkojo ir davė jiems, tardamas: “Gerkite iš jos visi,
27Kisha akatwaa kikombe, akamshukuru Mungu, akawapa akisema, "Nyweni nyote;
28nes tai yra mano kraujas, Naujosios Sandoros kraujas, kuris už daugelį išliejamas nuodėmėms atleisti.
28maana hii ni damu yangu inayothibitisha agano, damu inayomwagwa kwa ajili ya watu wengi ili kuwaondolea dhambi.
29Ir sakau jums: nuo šiol nebegersiu šito vynmedžio vaisiaus iki tos dienos, kada su jumis gersiu jį naują savo Tėvo karalystėje”.
29Nawaambieni, sitakunywa tena divai ya zabibu mpaka siku ile nitakapoinywa mpya pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu."
30Pagiedoję himną, jie išėjo į Alyvų kalną.
30Baada ya kuimba wimbo, wakaondoka, wakaenda katika mlima wa Mizeituni.
31Tada Jėzus jiems kalbėjo: “Šią naktį jūs visi manimi pasipiktinsite, nes parašyta: ‘Ištiksiu piemenį, ir kaimenės avys išsisklaidys’.
31Kisha Yesu akawaambia, "Usiku huu wa leo, ninyi nyote mtakuwa na mashaka nami, maana Maandiko Matakatifu yasema: Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
32Bet kai prisikelsiu, Aš pirma jūsų nueisiu į Galilėją”.
32Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulieni Galilaya."
33Petras atsiliepė: “Jei net visi Tavimi pasipiktins, aš niekuomet nepasipiktinsiu!”
33Petro akamwambia Yesu "Hata kama wote watakuwa na mashaka nawe na kukuacha, mimi sitakuacha kamwe."
34Jėzus jam tarė: “Iš tiesų sakau tau: šią naktį, dar gaidžiui nepragydus, tu tris kartus manęs išsiginsi”.
34Yesu akamwambia, "Kweli nakwambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu."
35Bet Petras tvirtino: “Jei man reikėtų net mirti kartu su Tavimi, aš vis tiek Tavęs neišsiginsiu!” Taip kalbėjo ir visi mokiniai.
35Petro akamwambia, "Hata kama ni lazima nife pamoja nawe, sitakukana kamwe." Wale wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
36Tuomet Jėzus su jais atėjo į vietą, vadinamą Getsemane, ir tarė mokiniams: “Pasėdėkite čia, kol Aš ten nuėjęs melsiuos”.
36Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, "Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali."
37Pasiėmęs Petrą ir abu Zebediejaus sūnus, pradėjo liūdėti ir sielvartauti.
37Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko.
38Tada tarė jiems: “Mano siela mirtinai nuliūdusi. Likite čia ir budėkite su manimi”.
38Hapo akawaambia, "Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami."
39Paėjęs kiek toliau, Jėzus parpuolė veidu į žemę ir meldėsi: “Mano Tėve, jeigu įmanoma, teaplenkia mane ši taurė. Tačiau ne kaip Aš noriu, bet kaip Tu!”
39Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: "Baba yangu, kama inawezekana, aacha kikombe hiki cha mateso kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe."
40Jis sugrįžo pas mokinius ir, radęs juos miegančius, tarė Petrui: “Nepajėgėte nė vienos valandos pabudėti su manimi?
40Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, "Ndiyo kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
41Budėkite ir melskitės, kad nepatektumėte į pagundymą. Dvasia ryžtinga, bet kūnas silpnas”.
41Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho i tayari lakini mwili ni dhaifu."
42Ir vėl nuėjęs antrą kartą, meldėsi: “Mano Tėve, jei ši taurė negali praeiti mano negerta, tebūnie Tavo valia!”
42Akaenda tena mara ya pili akasali: "Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kinipite bila mimi kukinywa, basi, mapenzi yako yafanyike."
43Sugrįžęs vėl rado juos miegančius, nes jų akys buvo apsunkusios.
43Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi.
44Tada, palikęs juos, vėl nuėjo ir trečią kartą meldėsi tais pačiais žodžiais.
44Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale.
45Paskui grįžo pas mokinius ir tarė: “Jūs vis dar miegate ir ilsitės... Štai atėjo valanda, ir Žmogaus Sūnus išduodamas į nusidėjėlių rankas.
45Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, "Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi.
46Kelkitės, eime! Štai mano išdavėjas čia pat”.
46Amkeni, twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti."
47Dar Jam tebekalbant, štai pasirodė Judas, vienas iš dvylikos, o su juo didelė minia, ginkluota kalavijais ir vėzdais, pasiųsta aukštųjų kunigų ir tautos vyresniųjų.
47Basi, Yesu alipokuwa bado anasema nao, mara akaja Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili. Pamoja naye walikuja watu wengi wenye mapanga na marungu ambao walitumwa na makuhani wakuu na wazee wa watu.
48Jo išdavėjas nurodė jiems ženklą, sakydamas: “Kurį pabučiuosiu, tai Tas! Suimkite Jį!”
48Huyo aliyetaka kumsaliti Yesu, alikuwa amekwisha wapa ishara akisema: "Yule nitakayembusu ndiye; mkamateni."
49Ir tuojau priėjęs prie Jėzaus, tarė: “Sveikas, Rabi!”, ir pabučiavo Jį.
49Basi, Yuda akamkaribia Yesu, akamwambia, "Shikamoo, Mwalimu!" Kisha akambusu.
50O Jėzus jam tarė: “Bičiuli, ko atėjai?” Tada jie priėjo, čiupo Jėzų rankomis ir suėmė.
50Yesu akamwambia, "Rafiki, fanya ulichokuja kufanya." Hapo wale watu wakaja, wakamkamata Yesu, wakamtia nguvuni.
51Ir štai vienas iš buvusių su Jėzumi ištiesė ranką, išsitraukė kalaviją, puolė vyriausiojo kunigo tarną ir nukirto jam ausį.
51Mmoja wa wale waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono, akauchomoa upanga wake, akampiga mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52Tuomet Jėzus jam tarė: “Kišk kalaviją atgal, kur buvo, nes visi, kurie griebiasi kalavijo, nuo kalavijo ir žus.
52Hapo Yesu akamwambia, "Rudisha upanga wako alani, maana yeyote anayeutumia upanga, atakufa kwa upanga.
53O gal manai, jog negaliu paprašyti savo Tėvą ir Jis bematant neatsiųstų man daugiau kaip dvylika legionų angelų?
53Je, hamjui kwamba ningeweza kumwomba Baba yangu naye mara angeniletea zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
54Bet kaip tada išsipildytų Raštai, kad šitaip turi įvykti?!”
54Lakini yatatimiaje Maandiko Matakatifu yasemayo kwamba ndivyo inavyopaswa kuwa?"
55Tą valandą Jėzus tarė miniai: “Kaip prieš plėšiką išėjote su kalavijais ir vėzdais suimti mane. Aš kasdien sėdėjau šventykloje su jumis ir mokiau, ir manęs nesuėmėte.
55Wakati huohuo Yesu akauambia huo umati wa watu waliokuja kumtia nguvuni, "Je, mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama kwamba mimi ni mnyang'anyi? Kila siku nilikuwa Hekaluni nikifundisha, na hamkunikamata!
56Bet viskas šitaip įvyko, kad išsipildytų pranašų Raštai”. Tada visi mokiniai paliko Jį ir pabėgo.
56Lakini haya yote yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie." Kisha wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
57Tie, kurie suėmė Jėzų, nuvedė Jį pas vyriausiąjį kunigą Kajafą, kur buvo susirinkę Rašto žinovai ir vyresnieji.
57Basi, hao watu waliomkamata Yesu walimpeleka nyumbani kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokusanyika walimu wa Sheria na wazee.
58O Petras sekė Jį iš tolo iki vyriausiojo kunigo rūmų kiemo ir įėjęs atsisėdo su tarnais pasižiūrėti, kaip viskas baigsis.
58Petro alimfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani Mkuu, akaingia ndani pamoja na walinzi ili apate kuona mambo yatakavyokuwa.
59Tuo tarpu aukštieji kunigai, vyresnieji ir visas sinedrionas ieškojo melagingo parodymo prieš Jėzų, kad galėtų Jį nuteisti mirti,
59Basi, makuhani wakuu na Baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu wapate kumwua,
60tačiau nerado, nors buvo išėję į priekį daug melagingų liudytojų. Pagaliau išėjo priekin du
60lakini hawakupata ushahidi wowote, ingawa walikuja mashahidi wengi wa uongo. Mwishowe wakaja mashahidi wawili,
61ir tarė: “Šitas sakė: ‘Aš galiu sugriauti Dievo šventyklą ir per tris dienas ją atstatyti’ ”.
61wakasema, "Mtu huyu alisema: Ninaweza kuliharibu Hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu."
62Tada atsistojo vyriausiasis kunigas ir paklausė Jėzų: “Tu nieko neatsakai į šituos kaltinimus?!”
62Kuhani Mkuu akasimama, akamwuliza Yesu, "Je, hujibu neno? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?"
63Bet Jėzus tylėjo. Tuomet vyriausiasis kunigas Jam tarė: “Prisaikdinu Tave gyvuoju Dievu, kad mums pasakytum, ar Tu esi Kristus, Dievo Sūnus?!”
63Lakini Yesu akakaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, "Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, twambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu!"
64Jėzus atsakė: “Taip yra, kaip sakai. Bet Aš jums sakau: nuo šiol jūs matysite Žmogaus Sūnų, sėdintį Galybės dešinėje ir ateinantį dangaus debesyse!”
64Yesu akamwambia, "Wewe umesema! Lakini nawaambieni, tangu sasa mtamwona Mwana wa Mtu ameketi upande wa kulia wa Mwenyezi, akija juu ya mawingu ya mbinguni."
65Tada vyriausiasis kunigas persiplėšė drabužius ir sušuko: “Jis piktžodžiauja! Kam dar mums liudytojai?! Štai girdėjote Jo piktžodžiavimą.
65Hapo, Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akasema, "Amekufuru! Tuna haja gani tena ya mashahidi? Sasa mmesikia kufuru yake.
66Kaip jums atrodo?” Jie atsakė: “Vertas mirties!”
66Ninyi mwaonaje?" Wao wakamjibu, "Anastahili kufa!"
67Tada jie ėmė spjaudyti Jam į veidą ir daužyti Jį kumščiais. Kiti mušė Jį per veidą,
67Kisha wakamtemea mate usoni, wakampiga makofi. Wengine wakiwa wanampiga makofi,
68sakydami: “Pranašauk mums, Kristau! Kas Tau smogė?”
68wakasema, "Haya Kristo, tutabirie; ni nani amekupiga!"
69Tuo metu Petras sėdėjo kieme. Viena tarnaitė priėjo prie jo ir tarė: “Ir tu buvai su Jėzumi Galilėjiečiu”.
69Petro alikuwa ameketi nje uani. Basi, mtumishi mmoja wa kike akamwendea, akasema, "Wewe ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya."
70Bet jis išsigynė visų akivaizdoje: “Aš nežinau, ką tu sakai”.
70Petro akakana mbele ya wote akisema, "Sijui hata unasema nini."
71Einantį vartų link, jį pastebėjo kita tarnaitė ir kalbėjo aplinkiniams: “Šitas buvo su Jėzumi Nazariečiu”.
71Alipokuwa akitoka mlangoni, mtumishi mwingine wa kike akamwona, akawaambia wale waliokuwa pale, "Mtu huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti."
72Jis ir vėl išsigynė, prisiekdamas: “Aš nepažįstu to žmogaus!”
72Petro akakana tena kwa kiapo: "Simjui mtu huyo."
73Po kiek laiko priėjo ten stovėjusieji ir sakė Petrui: “Tikrai tu vienas iš jų, nes tavo tarmė tave išduoda”.
73Baadaye kidogo, watu waliokuwa pale wakamwendea Petro, wakamwambia, "Hakika, wewe pia ni mmoja wao, maana msemo wako unakutambulisha."
74Tada jis ėmė keiktis ir prisiekinėti: “Aš nepažįstu to žmogaus!” Ir tuojau pragydo gaidys.
74Hapo Petro akaanza kujilaani na kuapa akisema, "Simjui mtu huyo!" Mara jogoo akawika.
75Petras prisiminė Jėzaus žodžius: “Dar gaidžiui nepragydus, tu tris kartus manęs išsiginsi”. Jis išėjo laukan ir karčiai verkė.
75Petro akakumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu: "Kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu." Basi, akatoka nje akalia sana.