Lithuanian

Swahili: New Testament

Mark

2

1Po kelių dienų Jėzus vėl atėjo į Kafarnaumą. Žmonės, išgirdę Jį esant namuose,
1Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
2nedelsiant susirinko, ir taip gausiai, jog nė prie durų nebeliko vietos. O Jis skelbė jiems žodį.
2Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
3Tada keturi vyrai atnešė pas Jį paralyžiuotą žmogų.
3wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
4Negalėdami dėl minios prinešti jo prie Jėzaus, jie praplėšė stogą namo, kur Jis buvo, ir, padarę skylę, nuleido žemyn neštuvus, ant kurių gulėjo paralyžiuotasis.
4Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
5Išvydęs jų tikėjimą, Jėzus tarė paralyžiuotajam: “Sūnau, atleidžiamos tau tavo nuodėmės!”
5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako."
6Tenai sėdėjo keletas Rašto žinovų ir svarstė savo širdyse:
6Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
7“Kodėl Jis taip piktžodžiauja? Kas gali atleisti nuodėmes, jei ne vienas Dievas?!”
7"Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake."
8Jėzus, iš karto savo dvasia supratęs jų mintis, tarė: “Kam taip svarstote savo širdyse?
8Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9Kas lengviau­ar pasakyti paralyžiuotam: ‘Tau atleidžiamos nuodėmės’, ar liepti: ‘Kelkis, imk neštuvus ir vaikščiok’?
9Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
10Bet, kad žinotumėte Žmogaus Sūnų turintį valdžią atleisti žemėje nuodėmes,­čia Jis tarė paralyžiuotajam,­
10Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
11sakau tau: kelkis, imk savo neštuvus ir eik namo!”
11"Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!"
12Šis tuojau atsikėlė ir, visiems matant, pasiėmęs neštuvus, išėjo. Visi stebėjosi ir garbino Dievą, sakydami: “Tokių dalykų mes niekad nesame matę”.
12Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, "Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili."
13Jėzus vėl nuėjo į paežerę. Didelė minia rinkosi prie Jo, ir Jis juos mokė.
13Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
14Praeidamas Jis pamatė Levį, Alfiejaus sūnų, sėdintį muitinėje, ir tarė jam: “Sek paskui mane!” Šis atsikėlė ir nusekė paskui Jį.
14Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, "Nifuate!" Lawi akasimama, akamfuata.
15Kai Jėzus Levio namuose valgė, drauge prie stalo su Jėzumi ir mokiniais sėdėjo daug muitininkų bei nusidėjėlių, nes tokių buvo daug ir jie sekė paskui Jį.
15Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
16Rašto žinovai ir fariziejai, išvydę Jį valgantį su muitininkais ir nusidėjėliais, klausė Jo mokinių: “Kodėl Jis valgo su muitininkais ir nusidėjėliais?”
16Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, "Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
17Tai išgirdęs, Jėzus atsiliepė: “Ne sveikiesiems reikia gydytojo, bet ligoniams! Aš atėjau šaukti ne teisiųjų, bet nusidėjėlių atgailai”.
17Yesu alipowasikia, akawaambia, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi."
18Jono mokiniai ir fariziejai pasninkavo. Jie atėję klausė Jėzų: “Kodėl Jono ir fariziejų mokiniai pasninkauja, o Tavieji ne?”
18Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, "Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?"
19Jėzus atsakė: “Argi gali vestuvininkai pasninkauti, kol su jais yra jaunikis? Kol jie turi su savim jaunikį, jie negali pasninkauti.
19Yesu akajibu, "Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
20Bet ateis dienos, kai jaunikis bus iš jų atimtas, ir tada, tomis dienomis, jie pasninkaus.
20Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
21Niekas nesiuva lopo iš naujo audinio ant sudėvėto drabužio; antraip naujasis atplėštų nuo senojo gabalą, ir pasidarytų dar didesnė skylė.
21"Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
22Taip pat niekas nepila jauno vyno į senus vynmaišius. Antraip vynas suplėšytų vynmaišius, ir nueitų niekais ir vynas, ir vynmaišiai. Jaunam vynui būtini nauji vynmaišiai!”
22Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!"
23Sabato dieną Jėzus ėjo per javų lauką, ir Jo mokiniai eidami skabė varpas.
23Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
24Fariziejai Jam sakė: “Žiūrėk, kodėl jie daro per sabatą tai, kas draudžiama?”
24Mafarisayo wakawaambia, "Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?"
25Jėzus atsakė: “Nejaugi niekad neskaitėte, ką prireikus padarė Dovydas, kai jis ir jo palydovai neturėjo maisto ir buvo išalkę?
25Yesu akawajibu, "Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
26Prie vyriausiojo kunigo Abjataro jis įėjo į Dievo namus ir valgė padėtinės duonos ir davė savo palydovams, nors niekam neleistina jos valgyti, tik kunigams”.
26naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake."
27Ir pridūrė: “Sabatas padarytas žmogui, o ne žmogus sabatui;
27Basi, Yesu akawaambia, "Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
28taigi Žmogaus Sūnus yra ir sabato Viešpats”.
28Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato."