Lithuanian

Swahili: New Testament

Mark

3

1Jis vėl atėjo į sinagogą, o ten buvo žmogus su padžiūvusia ranka.
1Yesu aliingia tena katika sunagogi na mle ndani mlikuwa na mtu aliyekuwa na mkono uliopooza.
2Jie stebėjo Jį, ar Jis gydys šį sabato dieną, kad galėtų Jėzų apkaltinti.
2Humo baadhi ya watu walimngojea amponye mtu huyo siku ya sabato ili wapate kumshtaki.
3Jėzus tarė žmogui su padžiūvusia ranka: “Stok į vidurį!”
3Yesu akamwambia huyo mtu aliyekuwa na mkono uliopooza, "Njoo hapa katikati."
4O juos paklausė: “Ar sabato dieną leistina daryti gera, ar bloga? Gelbėti gyvybę ar žudyti?” Bet anie tylėjo.
4Kisha, akawauliza, "Je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuua?" Lakini wao hawakusema neno.
5Tada, rūsčiai juos apžvelgęs ir nuliūdęs dėl jų širdies kietumo, tarė tam žmogui: “Ištiesk ranką!” Šis ištiesė, ir ranka tapo sveika kaip ir kita.
5Hapo akawatazama wote kwa hasira, akaona huzuni kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao. Kisha akamwambia huyo mtu, "Nyosha mkono wako!" Naye akaunyosha mkono wake, ukawa mzima tena.
6Išėję fariziejai tuojau pradėjo tartis su erodininkais, kaip Jėzų pražudyti.
6Mara Mafarisayo wakatoka nje, wakafanya shauri pamoja na watu wa kikundi cha Herode jinsi ya kumwangamiza Yesu.
7O Jėzus su savo mokiniais pasitraukė prie ežero. Jį sekė didelė minia iš Galilėjos. Ir iš Judėjos,
7Yesu aliondoka hapo pamoja na wanafunzi wake, akaenda kando ya ziwa, na umati wa watu ukamfuata. Watu hao walikuwa wametoka Yerusalemu, Yudea,
8Jeruzalės ir Idumėjos, iš anapus Jordano bei Tyro ir Sidono šalies atvyko daugybė žmonių, kurie buvo girdėję apie Jo didelius darbus.
8Idumea, ng'ambo ya mto Yordani, Tiro na Sidoni. Watu hao wengi walimwendea Yesu kwa sababu ya kusikia mambo mengi aliyokuwa ameyatenda.
9Jėzus liepė mokiniams laikyti Jam paruoštą nedidelę valtį, kad minia Jo nesuspaustų.
9Yesu akawaambia wanafunzi wake wamtayarishie mashua moja, ili umati wa watu usije ukamsonga.
10Mat Jis buvo daugelį išgydęs, ir visi, kuriuos kankino ligos, veržėsi prie Jo, norėdami Jį paliesti.
10Alikuwa amewaponya watu wengi, na wagonjwa wote wakawa wanamsonga ili wapate kumgusa.
11Taip pat netyrosios dvasios, vos tik Jį pamačiusios, parpuldavo priešais Jį ir šaukdavo: “Tu esi Dievo Sūnus!”
11Na watu waliokuwa wamepagawa na pepo wachafu walipomwona, walijitupa chini mbele yake na kupaaza sauti, "Wewe ni Mwana wa Mungu!"
12Bet Jėzus griežtai jas drausdavo, kad Jo negarsintų.
12Lakini Yesu akawaamuru kwa ukali wasimjulishe kwa watu.
13Jėzus užkopė ant kalno ir pasišaukė, kuriuos pats norėjo, ir jie atėjo pas Jį.
13Yesu alipanda kilimani, akawaita wale aliowataka. Basi, wakamwendea,
14Jis paskyrė dvylika, kad jie būtų kartu su Juo ir kad galėtų siųsti juos pamokslauti
14naye akawateua watu kumi na wawili ambao aliwaita mitume, wakae naye, awatume kuhubiri
15ir jie turėtų valdžią gydyti ligas ir išvarinėti demonus:
15na wawe na mamlaka ya kuwafukuza pepo.
16Simoną, pavadinęs jį Petru;
16Basi, hao kumi na wawili walioteuliwa ndio hawa: Simoni (ambaye Yesu alimpa jina, Petro),
17Zebediejaus sūnų Jokūbą ir Jokūbo brolį Joną (juos pavadinęs Boanerges, tai yra “griaustinio vaikai”);
17Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo (Yesu aliwapa hawa ndugu wawili jina Boanerge, maana yake "wanangurumo"),
18Andriejų, Pilypą, Baltramiejų, Matą, Tomą, Alfiejaus sūnų Jokūbą, Tadą, Simoną Kananietį
18Andrea na Filipo, Batholomayo, Mathayo, Thoma, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkanani na
19ir Judą Iskarijotą, kuris Jį ir išdavė. Ir jie grįžo namo.
19Yuda Iskarioti ambaye alimsaliti Yesu.
20Vėl susirinko tiek žmonių, kad jie nebegalėjo nė pavalgyti.
20Kisha Yesu alikwenda nyumbani. Umati wa watu ukakusanyika tena, hata Yesu na wafuasi wake wasiweze kupata nafasi ya kula chakula.
21Saviškiai, apie tai išgirdę, ėjo sulaikyti Jo, sakydami, kad Jis išėjęs iš proto.
21Basi, watu wa jamaa yake walipopata habari hiyo wakatoka kwenda kumchukua maana walikuwa wanasema kwamba amepatwa na wazimu.
22Atvykę iš Jeruzalės Rašto žinovai sakė: “Jis turi Belzebulą”, ir: “Demonų kunigaikščio jėga Jis išvaro demonus”.
22Nao walimu wa Sheria waliokuwa wametoka Yerusalemu, wakasema, "Ana Beelzebuli! Tena, anawafukuza pepo kwa nguvu ya mkuu wa pepo."
23O Jėzus, pasivadinęs juos, kalbėjo palyginimais: “Kaip gali šėtonas išvaryti šėtoną?
23Hapo Yesu akawaita, akawaambia kwa mifano, "Shetani anawezaje kumfukuza Shetani?
24Jei karalystė suskilusi, tokia karalystė negali išsilaikyti.
24Ikiwa utawala mmoja umegawanyika makundimakundi yanayopigana, utawala huo hauwezi kudumu.
25Ir jei namai suskilę, tokie namai negali išsilaikyti.
25Tena, ikiwa jamaa moja imegawanyika makundimakundi yanayopingana, jamaa hiyo itaangamia.
26Ir jei šėtonas sukyla pats prieš save ir tampa susiskaldęs, jis negali išsilaikyti ir žlunga.
26Ikiwa basi, utawala wa Shetani umegawanyika vikundivikundi hauwezi kudumu, bali utaangamia kabisa.
27Niekas negali įeiti į galiūno namus ir pasigrobti jo turto, pirmiau nesurišęs galiūno. Tik tada jis apiplėš jo namus.
27"Hakuna mtu awezaye kuivamia nyumba ya mtu mwenye nguvu na kumnyang'anya mali yake, isipokuwa kwanza amemfunga huyo mtu mwenye nguvu; hapo ndipo atakapoweza kumnyang'anya mali yake.
28Iš tiesų sakau jums: bus atleistos žmonių vaikams visos nuodėmės ir piktžodžiavimai, kaip jie bepiktžodžiautų;
28"Kweli nawaambieni, watu watasamehewa dhambi zao zote na kufuru zao zote;
29bet jei kas piktžodžiautų Šventajai Dvasiai, tam niekada nebus atleista, ir jis amžiams bus pasmerktas”.
29lakini anayesema mabaya dhidi ya Roho Mtakatifu, hatasamehewa kamwe; ana hatia ya dhambi ya milele."
30Mat jie sakė: “Jis turi netyrąją dvasią”.
30(Yesu alisema hivyo kwa sababu walikuwa wanasema, "Ana pepo mchafu.")
31Atėjo Jėzaus motina ir broliai ir, lauke sustoję, prašė Jį pakviesti.
31Mama yake Yesu na ndugu zake walifika hapo, wakasimama nje, wakampelekea ujumbe kutaka kumwona.
32Aplink Jį sėdėjo minia, kai Jam pranešė: “Štai Tavo motina ir broliai bei seserys lauke stovi ir ieško Tavęs”.
32Umati wa watu ulikuwa umekaa hapo kumzunguka. Basi, wakamwambia, "Mama yako na ndugu zako wako nje, wanataka kukuona."
33O Jis atsakė: “Kas yra mano motina ir mano broliai?”
33Yesu akawaambia, "Mama yangu na ndugu zangu ni kina nani?"
34Ir, apžvelgęs aplinkui sėdinčius, tarė: “Štai mano motina ir mano broliai!
34Hapo akawatazama watu waliokuwa wamemzunguka, akasema, "Tazameni! Hawa ndio mama yangu na ndugu zangu.
35Kas vykdo Dievo valią, tas mano brolis, ir sesuo, ir motina”.
35Mtu yeyote anayefanya anayotaka Mungu, huyo ndiye kaka yangu, dada yangu na mama yangu."