Lithuanian

Swahili: New Testament

Revelation

1

1Jėzaus Kristaus apreiškimas, kurį Dievas Jam davė, kad Jis atskleistų savo tarnams, kas turi greitai įvykti. Per savo pasiųstą angelą Jis padarė jį žinomą savajam tarnui Jonui,
1Hizi ni habari za mambo ambayo yalifunuliwa na Yesu Kristo. Mungu alimpa Kristo ufunuo huu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo yanapaswa kutukia karibuni. Kristo alimtuma malaika wake amjulishe Yohane, mtumishi wake, mambo hayo,
2kuris paliudijo Dievo žodį bei Jėzaus Kristaus liudijimą­visa, ką buvo matęs.
2naye Yohane, ameyasema yote aliyoyaona. Na hii ndio taarifa yake kuhusu ujumbe wa Mungu na ukweli uliofunuliwa na Yesu Kristo.
3Palaimintas, kas skaito bei klauso šios pranašystės žodžių ir laikosi, kas joje parašyta, nes laikas yra arti.
3Heri yake mtu anayesoma kitabu hiki; heri yao wale wanaosikiliza maneno ya ujumbe huu wa kinabii na kushika yaliyoandikwa humu, maana wakati umekaribia ambapo mambo haya yatatukia.
4Jonas septynioms Azijos bažnyčioms: malonė ir ramybė jums nuo To, kuris yra, kuris buvo ir kuris ateina, ir nuo septynių dvasių, esančių prieš Jo sostą,
4Mimi Yohane nayaandikia makanisa yaliyoko mkoani Asia. Nawatakieni neema na amani kutoka kwake yeye aliyeko, aliyekuwako na anayekuja; na kutoka kwa roho saba walio mbele ya kiti chake cha enzi,
5ir nuo Jėzaus Kristaus, ištikimojo Liudytojo, mirusiųjų Pirmagimio, žemės karalių Valdovo. Tam, kuris pamilo mus ir nuplovė savo krauju mūsų nuodėmes,
5na kutoka kwa Yesu Kristo, shahidi mwaminifu, wa kwanza kufufuliwa kutoka wafu, na ambaye ni mtawala wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda, na kwa damu yake ametufungua kutoka vifungo vya dhambi zetu,
6ir padarė iš mūsų karalystę bei kunigus savo Dievui ir Tėvui,­ Jam šlovė ir galybė per amžių amžius! Amen.
6akatufanya sisi kuwa ufalme wa makuhani, tumtumikie Mungu, Baba yake. Kwake Yesu Kristo uwe utukufu na nguvu, milele na milele! Amina.
7Štai Jis ateina su debesimis, ir išvys Jį kiekviena akis, net ir tie, kurie Jį perdūrė; ir dėl Jo raudos visos žemės giminės. Taip, amen!
7Tazama! Anakuja katika mawingu! Kila mtu atamwona, hata wale waliomchoma. Makabila yote duniani yataomboleza juu yake. Naam! Amina.
8“Aš esu Alfa ir Omega, Pradžia ir Pabaiga”,­sako Viešpats, kuris yra, kuris buvo ir kuris ateina, Visagalis.
8"Mimi ni Alfa na Omega," asema Bwana Mungu Mwenye Uwezo, aliyeko, aliyekuwako na anayekuja.
9Aš, Jonas, jūsų brolis ir sielvarto, karalystės ir Jėzaus Kristaus kantrybės bendrininkas, buvau saloje, vardu Patmas, dėl Dievo žodžio ir Jėzaus Kristaus liudijimo.
9Mimi ni Yohane, ndugu yenu; na kwa kuungana na Kristo nashiriki pamoja nanyi katika kustahimili mateso yanayowapata wale walio wa Utawala wake. Mimi nilikuwa kisiwani Patmo kwa sababu ya kuhubiri ujumbe wa Mungu na ukweli wa Yesu.
10Aš buvau Dvasioje Viešpaties dieną ir išgirdau už savo nugaros galingą balsą, tarsi trimitą,
10Basi, wakati mmoja, siku ya Bwana, nilikumbwa na Roho, nikasikia nyuma yangu sauti kubwa kama sauti ya tarumbeta.
11sakantį: “Aš esu Alfa ir Omega, Pirmasis ir Paskutinysis. Ką matai, surašyk į knygą ir pasiųsk septynioms bažnyčioms Azijoje: į Efezą, į Smirną, į Pergamą, į Tiatyrus, į Sardus, į Filadelfiją ir į Laodikėją”.
11Nayo ilisema, "Andika katika kitabu yote unayoyaona, ukipeleke kwa makanisa haya saba: Efeso, Smurna, Pergamoni, Thuatira, Sarde, Filadelfia na Laodikea."
12Tuomet aš atsigręžiau pažiūrėti balso, kalbančio su manimi, ir atsigręžęs išvydau septynis aukso žibintuvus,
12Basi, nikageuka nimwone huyo aliyesema nami, nikaona vinara vya taa saba vya dhahabu,
13o septynių žibintuvų viduryje­ panašų į Žmogaus Sūnų, apsivilkusį ilga mantija ir persijuosusį per krūtinę aukso juosta.
13na katikati yake kulikuwa na kitu kama mtu, naye alikuwa amevaa kanzu ndefu na ukanda wa dhahabu kifuani.
14Jo galva ir plaukai buvo balti kaip balčiausia vilna ar sniegas, Jo akys tarsi ugnies liepsna,
14Nywele zake zilikuwa nyeupe kama pamba safi, kama theluji; macho yake yalimetameta kama moto;
15Jo kojos panašios į krosnyje įkaitintą skaistvarį, ir Jo balsas buvo tarytum daugybės vandenų šniokštimas.
15miguu yake iling'aa kama shaba iliyosafishwa katika tanuru ya moto na kusuguliwa, na sauti yake ilikuwa, kama sauti ya poromoko la maji.
16Dešinėje rankoje Jis laikė septynias žvaigždes, iš Jo burnos ėjo aštrus dviašmenis kalavijas, o Jo veidas buvo tarytum saulė, spindinti visu skaistumu.
16Katika mkono wake wa kulia, alikuwa na nyota saba, na kinywani mwake mlitoka upanga wenye makali kuwili. Uso wake uling'aa kama jua kali.
17Jį išvydęs, aš puoliau Jam po kojų tarsi negyvas. Bet Jis uždėjo ant manęs savo dešinę ir prabilo: “Nebijok! Aš esu Pirmasis, ir Paskutinysis,
17Basi, nilipomwona tu, nilianguka mbele ya miguu yake kama maiti. Lakini yeye akaweka mkono wake wa kulia juu yangu, akasema, "Usiogope! Mimi ni wa kwanza na wa mwisho.
18ir Gyvasis. Aš buvau numiręs ir štai esu gyvas per amžius. Amen. Aš turiu mirties ir pragaro raktus.
18Mimi ni yeye aliye hai! Nilikuwa nimekufa, lakini, tazama, sasa ni mzima milele na milele. Ninazo funguo za kifo na Kuzimu.
19Tad užrašyk tai, ką regėjai, kas yra ir kas vėliau įvyks.
19Basi, sasa andika mambo haya unayoyaona, mambo yanayotukia sasa na yale yatakayotukia baadaye.
20Štai septynių žvaigždžių, kurias matei mano dešinėje, ir septynių aukso žibintuvų paslaptis: septynios žvaigždės­tai septynių bažnyčių angelai, o septyni žibintuvai, kuriuos matei,­tai septynios bažnyčios”.
20Siri ya nyota zile saba ulizoziona katika mkono wangu wa kulia, na siri ya vile vinara saba vya taa hii: zile nyota saba ni malaika wa makanisa; na vile vinara saba vya taa ni makanisa saba.