1“Efezo bažnyčios angelui rašyk: ‘Tai sako Tas, kuris laiko savo dešinėje septynias žvaigždes, kuris vaikščioja tarp septynių aukso žibintuvų.
1"Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.
2Aš žinau tavo darbus, tavo triūsą ir tavo kantrybę. Žinau, kad tu negali pakęsti piktųjų ir ištyrei tuos, kurie sakosi esą apaštalai, bet tokie nėra, ir radai juos esant melagius.
2Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.
3Tu ištvėrei, esi kantrus ir dėl mano vardo triūsei ir nepailsai.
3Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.
4Bet Aš turiu prieš tave tai, kad palikai savo pirmąją meilę.
4Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.
5Taigi prisimink, nuo kur nupuolei, atgailauk ir vėl imkis pirmykščių darbų, o jeigu ne,jei neatgailausi,greitai ateisiu ir patrauksiu iš vietos tavo žibintuvą.
5Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
6Savo naudai tu turi, kad nekenti nikolaitų darbų, kurių ir Aš nekenčiu’.
6Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.
7Kas turi ausis, teklauso, ką Dvasia sako bažnyčioms: ‘Nugalėtojui Aš duosiu valgyti nuo gyvybės medžio, esančio Dievo rojaus viduryje’ ”.
7"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.
8“Smirnos bažnyčios angelui rašyk: ‘Tai sako Pirmasis ir Paskutinysis, kuris buvo miręs ir vėl grįžo į gyvenimą.
8"Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.
9Aš žinau tavo darbus ir priespaudą, ir tavo skurdą,o vis dėlto tu turtingas!ir kaip tau piktžodžiauja tie, kurie sakosi esą žydai, bet nėra tokie, o tik šėtono sinagoga.
9Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.
10Nebijok būsimųjų kentėjimų. Štai velnias įmes kai kuriuos jūsiškius į kalėjimą, kad būtumėte išbandyti. Jūsų laukia dešimties dienų priespauda. Būk ištikimas iki mirties, ir Aš tau duosiu gyvenimo vainiką’.
10Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.
11Kas turi ausis, teklauso, ką Dvasia sako bažnyčioms: ‘Nugalėtojas nenukentės nuo antrosios mirties’ ”.
11"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.
12“Pergamo bažnyčios angelui rašyk: ‘Tai sako Tas, kuris turi aštrų dviašmenį kalaviją.
12"Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: "Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.
13Aš žinau tavo darbus ir kur tu gyveni: ten, kur šėtono sostas. Bet tu tvirtai laikaisi mano vardo ir neišsigynei mano tikėjimo net tomis dienomis, kada pas jus,kur gyvena šėtonas,buvo nužudytas mano ištikimasis liudytojas Antipas.
13Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.
14Vis dėlto turiu šį tą prieš tave: tu tenai turi besilaikančių Balaamo mokslo, kuris mokė Balaką suvedžioti Izraelio sūnus, kad šie valgytų stabams aukojamas aukas ir ištvirkautų.
14Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.
15Ir tu taip pat turi besilaikančių nikolaitų mokslo, kurio Aš nekenčiu.
15Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.
16Tad atgailauk! O jeigu ne, Aš greitai ateisiu ir kovosiu su jais savo burnos kalaviju’.
16Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.
17Kas turi ausis, teklauso, ką Dvasia sako bažnyčioms: ‘Nugalėtojui Aš duosiu paslėptos manos ir baltą akmenėlį, o ant akmenėlio bus įrašytas naujas vardas, kurio niekas nežino, tiktai gavėjas’ ”.
17"Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! "Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.
18“Tiatyrų bažnyčios angelui rašyk: ‘Tai sako Dievo Sūnus, kurio akys tarytum ugnies liepsna ir kurio kojos panašios į skaistvarį.
18"Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: "Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.
19Žinau tavo darbus, meilę, tikėjimą, tarnavimą, kantrybę ir kad tavo paskutinieji darbai didesni už pirmuosius.
19Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.
20Bet Aš turiu šį tą prieš tave: tu leidi moteriškei Jezabelei, kuri sakosi esanti pranašė, mokyti bei suvedžioti mano tarnus, kad jie ištvirkautų ir valgytų stabams paaukotas aukas.
20Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.
21Aš jai daviau laiko atgailauti dėl ištvirkavimo, bet ji neatgailavo.
21Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.
22Štai Aš ją nublokšiu į ligos patalą, o ištvirkavusius su jaį didelį sielvartą, jeigu jie neatgailaus dėl savo darbų.
22Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.
23Jos vaikus išžudysiu, ir visos bažnyčios sužinos, kad Aš esu Tas, kuris ištiria protus ir širdis; Aš atsilyginsiu jums kiekvienam pagal jūsų darbus.
23Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.
24O jums ir kitiems tiatyriečiams, kurie nesilaiko ano mokslo, kurie, kaip sakosi, nėra pažinę šėtono gelmių, Aš sakau: neužkrausiu jums kitokios naštos,
24"Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.
25tiktai tvirtai laikykitės to, ką turite, iki ateisiu.
25Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.
26Tam, kuris nugali ir iki galo laikosi mano darbų, Aš ‘duosiu valdžią tautoms:
26"Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.
27jis valdys jas geležine lazda, ir jos bus sudaužytos tarsi moliniai indai’,kaip ir Aš esu gavęs valdžią iš savo Tėvo;
27Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.
28ir jam duosiu aušrinę žvaigždę’.
28Tena nitawapa nyota ya asubuhi.
29Kas turi ausis, teklauso, ką Dvasia sako bažnyčioms!”
29"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!