Paite

Swahili: New Testament

1 Corinthians

9

1Noplen ka hi ka hia? Sawltak ka hi ka hia? I Toupa Jesu ka muta ka hia? Noute Toupa a ka nasep gah na hi kei ua hia?
1Je, mimi si mtu huru? Je, mimi si mtume? Je, mimi sikumwona Yesu Bwana wetu? Je, ninyi si matokeo ya kazi yangu kwa ajili ya Bwana?
2Mi dangte din sawltak hi kei mah leng, nou ading bekin jaw ka hi; Toupa a ka sawltak hihna chiamtehna noumau neive ua.
2Hata kama kwa watu wengine mimi si mtume, lakini walau kwenu ninyi mimi ni mtume. Ninyi ni uthibitisho wa mtume wangu kwa sababu ya kuungana kwenu na Bwana.
3Hiai honsengte ka dawn na ahi,
3Hoja yangu kwa wale wanaonipinga ndiyo hii:
4Ne ding leh dawn dingin thu ka neikei ua hia?
4Je, hatuna haki ya kula na kunywa?
5Sawltak dangte leh Toupa unaute leh Kifa bangin ji gingtami pi vialvial dingin thu ka neikei ua hia?
5Je, hatuna ruhusa kumchukua mke Mkristo katika ziara zetu, kama vile wafanyavyo mitume wengine, ndugu zake Bwana, na pia Kefa?
6Ahihkeileh, koumau kivakna ding khut nasem lou dingin kei leh Barnabain thu ka neilou tuam ua hia?
6Au ni mimi tu na Barnaba ambao tunapaswa kujipatia maslahi yetu kwa kufanya kazi?
7Sepaih kua ahia amah kivaka gal kap ngei? Kuan ahia, a gah leh ne loua, grep huan bawl ngei? Ahihkeileh, kuan ahia, ganhon nawitui neloua, ganhon vul ngei?
7Je, mwanajeshi gani anayelipia utumishi wake jeshini? Mkulima gani asiyekula matunda ya shamba lake la mizabibu? Mchungaji gani asiyekunywa maziwa ya mifugo yake?
8Huai thute mihing bangmaiin ka gen hia? Dan thu mah inleng huai ngei a gen sam ka hia?
8Je, nasema mambo haya kibinadamu tu? Je, Sheria nayo haisemi hivyo?
9Mosi dan Laibu ah, Bawngtalin buh a chil laiin a muk gak ken, chih gelh ahi ngala. Pathianin bawngtal ading kia hia a ngaihtuah sak?
9Imeandikwa katika Sheria ya Mose: "Usimfunge kinywa ng'ombe anapoliwata nafaka." Je, ndio kusema Mungu anajishughulisha na ng'ombe?
10Eia ding kia gen ahi hia? Hi e, eia dinga a gelh ahi; leiletpan lamet neia leh ding ahi a, buhvopan leng tan neih sam lamenin vuak ding ahi ngala.
10Je, hakuwa anatufikiria sisi aliposema hivyo? Naam, haya yaliandikwa kwa ajili yetu; kwani yule anayelima na yule anayevuna, wote wawili wana haki ya kutumaini kupata sehemu ya mavuno.
11Kouten khalam thilte na kiang ua ka tuh ngal uleh, na salam thilte uh at mahle ung, thil kilawmlou ahi dia hia?
11Ikiwa sisi tumepanda mbegu ya kiroho kati yenu, je, ni jambo kubwa tukichuma kwenu faida ya kidunia?
12Midangin bawn, na tung ua thuneihna a tan uleh kou tang sem lou ding ka hi uh maw? Himahleh, huai thuneihna ka zang kei uh; Kris Tanchin Hoih ka dal louhna ding un bangkim ka thuak teitei jaw uhi.
12Ikiwa wengine wanayo haki ya kutazamia hayo kutoka kwenu, je, sisi hatuna haki zaidi kuliko hao? Lakini, sisi hatukuitumia haki hiyo, Badala yake, tumestahimili kila kitu ili tusiiwekee kizuizi chochote Habari Njema ya Kristo.
13Thil tan bawl vialvialten Pathian biakin a om thil a nek uleh, maitama nasemten maitam toh tan a nei uh chih na theikei ua hia?
13Je, hamjui kwamba wanaotumikia Hekaluni hupata chakula chao Hekaluni, na kwamba wanaotolea sadaka madhabahuni hupata sehemu ya hiyo sadaka?
14Huchi mahbangin, Toupan Tanchin Hoih gente Tanchin Hoih thu a nek muhna ding un a sep ahi.
14Bwana aliagiza vivyo hivyo; wahubiri wa Habari Njema wapate riziki zao kutokana nayo.
15Himahleh ken jaw tuate khat leng ka zang kei hi; ka tunga huchi na hihna ding un hiai thu ka gelh sam kei hi; kuapeuhin ka suanpen bangmah loua a bawl sang un, si mai leng kei dingin a hoihzo ngala.
15Lakini, mimi sikutumia hata mojawapo ya haki hizo. Na wala siandiki nijipatie haki hizo; kwangu mimi ni afadhali kufa kuliko kumfanya yeyote aone kwamba najisifu bure.
16Tanchin Hoih gen mahleng, huai jaw kisaktheih nading san ahi kei. Hihlouh theihlouh ka tungah a kinga ahi; Tanchin Hoih gen kei leng, ka tung gik ding ahi ngala.
16Ikiwa ninaihubiri Habari Njema, hilo si jambo la kujivunia; hilo ni jukumu nililopewa. Na, ole wangu kama sitaihubiri Habari Njema!
17Huai tuh keimah thuthua hih hi leng, kipahman ka nei hi; himahleh, keimah thuthu a hih keingal leh Tanchin Hoih kepnana kemsak a om ka hi.
17Ningekuwa nimeichagua kazi hii kwa hiari, basi, ningetazamia malipo; lakini maadam naifanya ikiwa ni wajibu, hiyo ina maana kwamba ni jukumu nililopewa nitekeleze.
18Ka kipahman bang ahia leh? Tanchin Hih ka genin, loh loua, Tanchin Hoih athawna pia ka hehtheihna tuh ahi.
18Mshahara wangu ni kitu gani, basi? Mshahara wangu ni fursa ya kuihubiri Habari Njema bure, bila kudai haki ninazostahili kwa kuihubiri.
19Kuamah sikha hi kei mah leng, mi tam sem ka lak theihna dingin mi tengteng sikhain ka kibawlta.
19Kwa hiyo, ingawa mimi si mtumwa wa mtu yeyote, nimejifanya mtumwa wa kila mtu ili nimpatie Kristo watu wengi iwezekanavyo.
20Huchiin, Judate ka laklut theihna dingin Judate kiangah Juda mi bangin ka om jel; dan nuaia omte ka lak lut theihna dingin dan nuaia omte kiangah dan nuaia om bangin ka om jel, dan nuaia om tuanlouin;
20Kwa Wayahudi nimeishi kama Myahudi ili niwapate Wayahudi; yaani, ingawa mimi siko chini ya Sheria, nimejiweka chini ya Sheria kwao, ili niwapate hao walio chini ya Sheria.
21Dan neilou te ka lak lut theihna dingin dan neiloute kiangah dan neilou bangin ka om jel, Pathian dana om lou tuan louin, Kris dan jawm ngalin.
21Na kwa wale walio nje ya Sheria, naishi kama wao, nje ya Sheria, ili niwapate hao walio nje ya Sheria. Hii haimaanishi kwamba mimi niko nje ya sheria ya Mungu, maana nabanwa na sheria ya Kristo.
22Hatloute ka lak lut theihna dingin hatlou te kiangah hatlou bangin ka om jel; bang chichi hiam beka khenkhatte bek ka hotdam theihna dingin mi tengteng kiangah bangkim ka hita hi.
22Kwao walio dhaifu nimejifanya dhaifu ili niwapate hao walio dhaifu. Nimejifanya kila kitu kwa wote ili nipate kuwaokoa baadhi yao kwa kila njia.
23Tanchin Hoih jiakin bangkim ka hih jela, a vualjawlnate ka tan sam theihna dingin.
23Nafanya haya yote kwa ajili ya Habari Njema, nipate kushiriki baraka zake.
24Kitaitehte tuh a vek un a tai ua, himahleh khat kian kipahman a mu jel chih na theikei ua hia? Na muh theihna ding un huchi mahbangin tai un.
24Je, hamjui kwamba katika uwanja wa michezo, ingawa wapiga mbio wote hukimbia, ni mmoja tu anayejinyakulia zawadi?
25Huan, kidemna a mawlmi peuhmah bangkimah mahni kithununin a om nak hi. Amau jaw lallukhu se thei mu dingin a hih ua, eiten bel lallukhu setheilou mu dingin.
25Wanariadha hujipa mazoezi na nidhamu kali; hufanya hivyo ili wajipatie taji iharibikayo! Lakini sisi twafanya hivyo tupate taji ya kudumu daima.
26Huchiin, tuamahbangin ka taia, a jiak bei hi louin; huihkhua leltak noh louin, ka pang hi:Ka pumpi ka hihsidupa; sikha in ka bawl zo jel hi; huchilou injaw midangte kianga ka tangkoupih nungin leng bangchichi hiamin keimah tak kipahman mutakloua koihin ka om khakha ding.
26Ndivyo basi, ninavyopiga mbio nikiwa na nia ya kushinda; ndivyo ninavyopigana, na si kama bondia anayetupa ngumi zake hewani.
27Ka pumpi ka hihsidupa; sikha in ka bawl zo jel hi; huchilou injaw midangte kianga ka tangkoupih nungin leng bangchichi hiamin keimah tak kipahman mutakloua koihin ka om khakha ding.
27Naupa mwili wangu mazoezi magumu na kuutia katika nidhamu kamili, nisije mimi mwenyewe nikakataliwa baada ya kuwahubiria wengine.