1Huchiin, nang, kata, Kris Jesu a hehpihna om ah thil hihtheihna nei in om in.
1Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
2Huan theihpih tanpite laka ka kam a thu nazakte, huaite mi muanhuai, midangte hilhsawn theidingte kiang ah kemsak in.
2Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
3Kris Jesu sepaih hoihtak bangin gimthuak hon thuakpih in.
3Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
4Sepaih a om ding a atelpa kipahsak theihna dingin, sepaih kuamah kidoulai in hiai damsung khosaknate in a ki subuai ngeikei a;
4Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
5huan, kidemnate bangah leng mi pangmahleh, dan bang a ahih keileh khuksak in a om ngeikei hi.
5Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
6Lou neipa semgim tuh agah tang masapa ahiding ahi.
6Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
7Kathugentak ngaihtuah in; Toupan tuh banglam peuha ah theihtheihna honpeding ahi ngala.
7Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
8Jesu Kris, David suan, ka tanchinhoih gen banga misi laka kipana thounawnpa thei gige in.
8Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
9Huai tanchinhoih ziakin thilhihkhialpa bangin hen hialin gimna bang ka thuakzel ahi; himahleh Pathian thu tuh hen in a om ngalkei a.
9Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
10Huaziakin, Kris Jesu a hotddamna tuh khantawna thupina toh a muhsam theihna ding un, telte ziakin bangkim ka thuak gige hi.
10na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele.
11Hiai thugen a dik hi: asihna a isih khit ngalleh, ahinna ah ihing ding hi;
11Usemi huu ni wa kweli: "Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
12ithuakleh avaihawmna ah vai ihawm sam ding hi; Amah iki theihmohbawl leh Aman leng hon kitheihmohbawl ding hi;
12Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
13Eite muanhuailou in om mahleng Amahzaw muanhuai in a om gige hi- Amah leh amah akitheihmawhbawl thei ngalkei a.
13Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe."
14Hiai theisak inla, thute leltak tunga akisel louhna ding un Toupa muh in phatuamngaitakin theisak in; huai kiselna tuh bangmah a phatuam kei a, angaikhete ading in siatna ahizaw nak hi.
14Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
15Nasemtu, zumnading neilou, thutak thudiktaka zang, Pathian pomtak hiding a nangmah kipe ding in theihtawpsuah in kizil in.
15Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
16Ahihhangin, Pathian zahlouh lam thugen mawkmawkte khawng nungngat san in; huchibang mite tuh Pathian limsaklouhna lam ah a pai gamla semsem ding ua,
16Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
17athu untuh meima sia nek bangin a nezel ding; alak uah tuh Himenaia leh Phileta a pang uhi;
17Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
18huaimiten tuh, thawhnawnna a omkhinta, chi in, thutak lam a paikawisan ua, mikhenkhatte ginna ahihmang sak uhi.
18Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
19Himahleh, Pathian suangphum kip tuh ading nalai a, hiai chiamtehna tuh a nei hi: Toupan amah ate athei, chihleh Toupa min lou peuhmah in diktatlouhna paisan hen, chih.
19Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: "Bwana anawafahamu wale walio wake," na "Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu."
20Himahleh in thupi ah tuh tuium belsuan dangkaeng leh dangka a bawlte kia a om kei a, sing leh bellei a bawlte bangleng a om hi; khenkhatte manphataka a zat a om a, khenkhatte tuh manphalou tak a zat leng a om sam hi.
20Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
21Huaziakin, mi huai thil giloute lak a akihep leh, tuium belsuan mahpha taka a zat ding, siangthou, Toupa zattak, nasep hoih chiteng dia mansa, ahi ding hi.
21Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
22Himahleh valnou duhgawlnate khawng taisan inla, lungtang siangthou a Toupa lou peuhmahte lak a diktatnate, ginnate, itnate, lametnate delh in.
22Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
23Himahleh kidounate a suaksaknak chih thei in, kiselna haihuai leh pillou ah pang nuam ken.
23Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
24Toupa sikha in a dou ding ahi kei a, mitengteng tung a siam tum in, thuhilh siam in, gitlouh tunga thuakzou thei in,
24Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
25a dou ding a kibawlte tuh thunuailuttakin a thuhilh zaw ding ahi. Huchi in Pathian in thutak tuh atheihna ding un a kisiksak zenzen kha ding a,huchiin khua a hon theithei ding ua, amau te suaklehsal a man a a utut a bawlpa Diabol thang a kipan a suakta thei ding uh.
25ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
26huchiin khua a hon theithei ding ua, amau te suaklehsal a man a a utut a bawlpa Diabol thang a kipan a suakta thei ding uh.
26Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.