Paite

Swahili: New Testament

Acts

5

1Himahleh, mi khat a min Anania, a ji Sapphira toh a om ua; Ananiain a neih uh a juaka, a ji theihin a man a khen a imta a;
1Mtu mmoja aitwaye Anania na mkewe Safira waliuza shamba lao vilevile.
2huan, a khen a hontawia, sawltakte khebul ah a koih a.
2Lakini, mkewe akiwa anajua, Anania akajiwekea sehemu ya fedha alizopata na ile sehemu nyingine akawakabidhi mitume.
3Himahleh, Peterin, Kha Siangthou khem ding leh gamman a khen imdingin bangdia Setanin na lungtang hihkhauh ahia?
3Basi, Petro akamwuliza, "Anania, mbona Shetani ameuingia moyo wako na kukufanya umdanganye Roho Mtakatifu kwa kujiwekea sehemu ya fedha ulizopata kutokana na lile shamba?
4A om laiteng nanga ahi gige ka hia? na juak nungin leng na thuthuin a om ka hia? bangachia hiai thute na lungtanga ngaihtuah? Mihing khem na hi kei, Pathian khem na hi jaw, a chi a.
4Kabla ya kuliuza lilikuwa mali yako, na baada ya kuliuza, bado hizo fedha zilikuwa zako uzitumie utakavyo. Kwa nini basi, uliamua moyoni mwako kufanya jambo la namna hii? Hukumdanganya mtu; umemdanganya Mungu!"
5Huan, Ananiain huai thu a jak takin a puka, a sita a; huan, a za peuhin a lau mahmahta uh.
5Anania aliposikia hayo, akaanguka chini, akafa. Watu wote waliosikia habari ya tukio hilo waliogopa sana.
6Huan, tangval hon a thou ua, a tuam ua, a jawng khia ua, a vuita uh.
6Vijana wakafika wakaufunika mwili wake, wakamtoa nje, wakamzika.
7Huan, dakkal thum ding hiam nung in, thil omdan theilouin a ji a hongluta.
7Baada ya muda wa saa tatu hivi, mke wake, bila kufahamu mambo yaliyotukia, akaingia mle ndani.
8Huan, Peterin a kiangah, honhilh in, gam, hiai zah phetin maw na juak uh? a chi a. Huan, aman, He, hiai zah phetin ahi, a chi a.
8Petro akamwambia, "Niambie! Je, kiasi hiki cha fedha ndicho mlichopata kwa kuuza lile shamba?" Yeye akamjibu, "Naam, ni kiasi hicho."
9Huan, Peterin a kiangah, bangachia Toupa Kha zeet dinga kithutuak na hi ua? Ngaiin, kongkhak bul ah na pasal vuite khepek a hongomta, nang leng a honjawng khe ding uh, a chi a.
9Naye Petro akamwambia, "Mbona mmekula njama kumjaribu Roho wa Bwana? Sikiliza! Wale watu waliokwenda kumzika mume wako, sasa wako mlangoni na watakuchukua wewe pia."
10Huan, thakhatin a khe bul ah a puk paha, a sita hi; huan, tangval hon a honglut ua, amah tuh siin a hongmu ua, a jawngkhia ua, a pasal kiangah a vuita uhi.
10Mara Safira akaanguka mbele ya miguu ya Petro, akafa. Wale vijana walipoingia, walimkuta amekwisha kufa; hivyo wakamtoa nje, wakamzika karibu na mume wake.
11Huan, saptuamte tengteng leh huai thu za peuhten a lauta mahmah uhi.
11Kanisa lote pamoja na wote waliosikia habari ya tukio hilo, waliogopa sana.
12Huan, mi lakah Pathianin sawltakte khutin chiamtehna leh thillamdang tampi a hih jel hi. Huan, amaute a vek un lungsim mun khatin Solomon in lim ah a kikhawm jel uhi.
12Mitume walifanya miujiza na maajabu mengi kati ya watu. Waumini walikuwa wakikutana pamoja katika ukumbi wa Solomoni.
13Mi dang bel kuamah a lak uah a pang ngamta kei uh; himahleh, min amaute a phat ngal ua.
13Mtu yeyote mwingine ambaye hakuwa mwamini hakuthubutu kujiunga nao. Hata hivyo, watu wengine wasiokuwa wa imani hiyo waliwasifu.
14Huan, a gingthak hon numei leh pasal tampi takin Toupa kiangah a honbehlap tuantuan uh.
14Idadi ya watu waliomwamini Bwana, wanaume kwa wanawake, iliongezeka zaidi na zaidi.
15Huchiin mi damloute leng kongzing khawngah a lumsak ua, Peter pai kawma a lim bekin a lak ua khat bek a liah theihna ding in, a chi ua.
15Kwa sababu hiyo, watu walikuwa wakipeleka wagonjwa barabarani na kuwalaza juu ya vitanda na mikeka ili Petro akipita, walau kivuli chake kiwaguse baadhi yao.
16Huan, Jerusalem kho kim khua akipan mipite leng huai damloute dawi nin hihgimte honpiin a hongkhawm ua; huaite leng a hongdam chiatta uh.
16Watu wengi walifika kutoka katika miji ya kando kando ya Yerusalemu, wakiwaleta wagonjwa wao na wale waliokuwa na pepo wachafu, nao wote wakaponywa.
17Huan, siampu lianpen leh a lawmte tengteng a hongkisa ua, (huai a lawmte tuh Saddukai pawl ahi uh) a haza mahmah ua.
17Kisha, Kuhani Mkuu na wenzake waliokuwa wa kikundi cha Masadukayo wa mahali hapo, wakawaonea mitume wivu.
18Sawltakte a man ua, vantang khumna ah a khumta uhi.
18Basi, wakawatia nguvuni, wakawafunga ndani ya gereza kuu.
19Himahleh, janin Toupa angel khatin kongkhakte a honhonga, a pikhia a.
19Lakini usiku malaika wa Bwana aliifungua milango ya gereza, akawatoa nje, akawaambia,
20Pathian biakin ah vading unla, mi kiangah hiai hinna thute vagen un, a chi a.
20"Nendeni mkasimame Hekaluni na kuwaambia watu kila kitu kuhusu maisha haya mapya."
21Huan, huai thu a jak un khovak hun laiin, Pathian biakin ah a valut ua, thu a vahilhta uh. Himahleh, Siampu Lian leh a lawmte a hong ua, vaihawmte leh Israel suante upate tengteng a sam khawm ua, sawltakte hon pi sak dingin suangkulh ah mi a sawl uhi.
21Mitume walitii, wakaingia Hekaluni asubuhi na mapema, wakaanza kufundisha. Kuhani Mkuu na wenzake walipofika, waliita mkutano wa Baraza kuu, yaani halmashauri yote ya wazee wa Wayahudi halafu wakawatuma watu gerezani wawalete wale mitume.
22Himahleh, upate a vahoh ua, suangkulh ah lah amau a mu kei ua; huchiin a kik nawn uh.
22Lakini hao watumishi walipofika huko hawakuwakuta mle gerezani. Hivyo walirudi, wakatoa taarifa mkutanoni,
23Suangkulh bit tak a kikhakin, a vengte leng kongkhak bulah dingin a mu ngal ua, himahleh, ka hong ua, a sungah kuamah ka mu sam kei ua, chiin a gen ua.
23wakisema, "Tulikuta gereza limefungwa kila upande na walinzi wakilinda milango. Lakini tulipofungua hatukumkuta mtu yeyote ndani."
24Huan, Pathian biakin upa leh siampu lalten, huai thute a jak un, Hiai bang, bangchi phetin a thang de aw? chiin, a thu ah a mang uh a bang petpeta.
24Mkuu wa walinzi wa Hekalu na makuhani wakuu waliposikia habari hiyo wakawa na wasiwasi, wasijue yaliyowapata.
25Huan, mi khat a honga, a kiang uah, Ngai un, suang kulha na mi khumte un Pathian biakina dingin mi a hilh uh, ka chi! chiin a honggen a.
25Akafika mtu mmoja, akawaambia, "Wale watu mliowafunga gerezani, hivi sasa wamo Hekaluni, wanawafundisha watu."
26Huchiin upa tuh upate toh a vahoh ua vantang a kihtak jiak un, hiamgamna om louin a honpi ua, huchi hikei leh suanga den ahi kha ding uh.
26Hapo mkuu wa walinzi wa Hekalu pamoja na watu wake walikwenda Hekaluni, akawaleta. Lakini hawakuwakamata kwa kutumia nguvu, maana waliogopa kwamba watu wangewapiga mawe.
27Huan, a honpi tun tak un, vaihawmmite maah a dingsak ua. Huan, siampu lianpenin, a kiang uah,
27Basi, wakawapeleka, wakawasimamisha mbele ya Baraza. Kuhani Mkuu akawaambia,
28Huai minin thu hilh louh ding ka honchita ua; thei un, na thuhilh un Jerusalem khua a hihdim vekta uh, hiai mipa sisan honkhuksak tum nei ve ua, chiin a sal a.
28"Tuliwakatazeni waziwazi kufundisha kwa jina la mtu huyu; sasa mmeyaeneza mafundisho yenu pote katika Yerusalemu na mnakusudia kutuwekea lawama ya kifo cha mtu huyo."
29Himahleh, Peter leh sawltakten, Mihing thu sangin Pathian thu i man a kiphamohjaw hi.
29Hapo Petro, akiwa pamoja na wale mitume wengine, akajibu, "Lazima tumtii Mungu, na siyo binadamu.
30Nou singah Jesu khaikangin na hihlumua, i pipute Pathianin a kaithou nawnta ahi.
30Mungu wa babu zetu alimfufua Yesu baada ya ninyi kumwua kwa kumtundika msalabani.
31Amah mah tuh Pathianin Kumpipa leh Hondampa a om dingin a taklam ah a hihlianta a, Israelte khelhna pan kiheisak ding leh ngaidam dingin.
31Huyu ndiye yule aliyekwezwa na Mungu mpaka upande wake wa kulia, akawa kiongozi na Mwokozi, ili awawezeshe watu wa Israeli watubu, wapate kusamehewa dhambi zao.
32Huai thute kou a theihpihte ka hi ua; Kha Siangthou, Pathianin a thu jui peuhte kianga a piak tak, a theipa ahi nawn lai, a chi ua, a dawng ua.
32Sisi ni mashahidi wa tukio hilo, naye Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wale wanaomtii, anashuhudia pia tukio hilo."
33Huan, amau, huai thu a jak un a sin uh a thak mahmaha, hihlup a tumta uh.
33Wajumbe wote wa lile Baraza waliposikia hayo, wakawaka hasira, hata wakaamua kuwaua.
34Himahleh, vaihawmte lakah, a min Gamaliel, Pharisai, Dantheimi, mi tengteng laka minthangpi mi khat a dinga, tua mite khah takdih ding thu a pia a.
34Lakini Mfarisayo mmoja aitwaye Gamalieli ambaye alikuwa mwalimu wa Sheria na aliyeheshimika sana mbele ya watu wote, alisimama mbele ya lile Baraza, akataka wale mitume watolewe nje kwa muda mfupi.
35Huan, vaihawmte kiangah, Nou Israel mite aw, hiai mite tunga na thilhih tup uh pilvang un.
35Kisha akawaambia wale wajumbe wa Baraza, "Wananchi wa Israeli, tahadhari kabla ya kutekeleza hicho mnachotaka kuwatenda watu hawa!
36Tumalamin leng, Theuda, mi lian kichiin, a hongoma, huai mipa kiangah mi tampi, za li phial, a na awn ua, amah tuh hihlupin a omta a; a thu jui peuhmah a vek un a dalhjakta uh, bangmah a hita kei uhi.
36Zamani kidogo, kulitokea mtu mmoja jina lake Theuda, akajisema kuwa mtu wa maana na watu karibu mia nne wakajiunga naye. Lakini aliuawa, kisha wafuasi wake wote wakatawanyika na kikundi chake kikafa.
37Huai mi om nungin min gelh laiin, Galili gama mi huai Juda a hongom nawna; a lamah mi khenkhat a hip nawna; himahleh amah leng a sita a, a thu jui peuhmah tuh a vek un a dalhjakta uh.
37Tena, baadaye, wakati ule wa kuhesabiwa watu, alitokea Yuda wa Galilaya. Huyu naye, aliwavuta watu wakamfuata; lakini naye pia aliuawa, na wafuasi wake wakatawanyika.
38Huai jiakin tuin ka honhilh ahi, hiai mite khoih kei unla, amau om omin omsak un; hiai a thiltup uh leh a thilhih uh mihing akipan ahihleh a mang ding;
38Na sasa pia mimi nawaambieni, msiwachukulie watu hawa hatua yoyote; waacheni! Kwa maana, ikiwa mpango huu au shughuli hii yao imeanzishwa na binadamu, itatoweka yenyewe.
39ahihhangin Pathian akipan ahihleh amau na hihmang theikei ding uh; huchilouin jaw Pathian dou na nahi zenzen kha ding uh, a chi a.
39Lakini kama imeanzishwa na Mungu, siyo tu kwamba hamtaweza kuwashinda, bali mtajikuta mnapigana na Mungu." Basi, wakakubaliana naye.
40Huan, a gen tuh lem a sata ua; huchiin, sawltakte tuh a sam ua, a vua ua; a vuak khit un, Jesu mina thu gen louh ding chi bikbekin a khahta uh.
40Hivyo wakawaita wale mitume, wakaamuru wachapwe viboko na kuwaonya wasifundishe tena kwa jina la Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
41Huchiin, vaihawmte laka kipan a pawtkhia ua, tua Min jiaka daina thuak taka seh ahihjiak un a kipak mahmah uhi.Huan, nitengin Pathian biakin ah leh amau in khawng bangah, Jesu tuh Kris ahi, chiin, thuhilh leh gen a tawp tuan kei uhi.
41Basi, mitume wakatoka nje ya ule mkutano wa halmashauri wakiwa wamejaa furaha, kwani walistahili kuaibishwa kwa ajili ya jina la Yesu.
42Huan, nitengin Pathian biakin ah leh amau in khawng bangah, Jesu tuh Kris ahi, chiin, thuhilh leh gen a tawp tuan kei uhi.
42Wakaendelea kila siku kufundisha na kuhubiri Habari Njema ya Kristo, Hekaluni na nyumbani mwa watu.