1A tungin Thu a om, Thu tuh Pathian kiangah a om, Thu tuh Pathian ahi.
1Hapo Mwanzo, Neno alikuwako; naye alikuwa na Mungu, naye alikuwa Mungu.
2Huai tuh a tungin Pathian kiangah a om hi.
2Tangu mwanzo Neno alikuwa na Mungu.
3Bangkim a vekin amah siam ahi; thil siam tengteng amah siam louh bangmah a om kei.
3Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa; hakuna hata kiumbe kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.
4Amah ah hinna a om; huai hinna tuh mihingte vakna ahi.
4Yeye alikuwa chanzo cha uhai na uhai huo ulikuwa mwanga wa watu.
5Vak tuh mial lakah a hongvaka; mialin huai tuh a zou kei hi.
5Na mwanga huo huangaza gizani, nalo giza halikuweza kuushinda.
6Pathian sawl mi khat a hongom, a min Johan ahi.
6Mungu alimtuma mtu mmoja jina lake Yohane,
7Huai mi tuh theisak dingin a hong, huai vak theisak din, amah jiaka mi tengtengin a gin theihna ding un.
7ambaye alikuja kuwaambia watu juu ya huo mwanga. Alikuja ili kwa ujumbe wake watu wote wapate kuamini.
8Amah bel vak tuh ahi kei a, vak thu tuh theisak dinga hong ahi jaw hi.
8Yeye hakuwa huo mwanga, ila alikuja tu kuwaambia watu juu ya huo mwanga.
9Vak dik mi chih hihvak nak a om a, khovel ah a honglel ahi.
9Huu ndio mwanga halisi, mwanga unaokuja ulimwenguni, na kuwaangazia watu wote.
10Amah tuh khovel ah a om, khovel amah siam ahi, ahihhangin khovelin amah a theikei hi.
10Basi, Neno alikuwako ulimwenguni; na kwa njia yake ulimwengu uliumbwa, lakini ulimwengu haukumtambua.
11Amah a mite kiangah a honga, amah a miten a na kipahpih kei uh.
11Alikuja katika nchi yake mwenyewe, nao walio wake hawakumpokea.
12Himahleh, amah kipahpih-a pom, a min gingtate, tengteng Pathian tate suahtheihna a pia;
12Lakini wale wote waliompokea na kumwamini, hao aliwapa uwezo wa kuwa watoto wa Mungu.
13huai mite bel sisan suan ahi kei ua, sa deihna suan leng ahi kei ua, mihing deihna suan leng ahi sam kei ua, Pathian suan ahi jaw uhi.
13Hawa wamekuwa watoto wa Mungu si kwa uwezo wa kibinadamu, wala kwa nguvu za kimwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali Mungu mwenyewe ndiye baba yao.
14Huan, Thu tuh sa a hongsuaka, eite lakah a teng, hehpihna leh thutak-a dimin; a thupina Pa Tapa tang neihsun thupina bangbang, eiten i muta.
14Naye Neno akawa mwanadamu, akakaa kwetu. Nasi tumeuona utukufu wake, utukufu wake yeye aliye Mwana wa pekee wa Baba; amejaa neema na ukweli.
15(Johanin amah theihpihna a piaa, Ka nunga hongpaipan honkheng, amah ka maa omsa him a hihmanin, chi-a a thu ka genpa hiai ahi, a chi hi. )
15Yohane aliwaambia watu habari zake, akasema kwa sauti, "Huyu ndiye niliyemtaja wakati niliposema: Anakuja mtu mmoja baada yangu ambaye ni mkuu kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa."
16Huan, eiten a tangchinna akipan i tangchiat, hehpihna tunga hehpih nawnsawnna.
16Kutokana na ukamilifu wake sisi tumepokea neema mfululizo.
17Banghanghiam chih leh, Danthu Mosi zanga piak ahi a; hehpihna leh thutak Jesu Kris-a hongpai ahi.
17Maana Mungu alitoa Sheria kwa njia ya Mose, lakini neema na kweli vimekuja kwa njia ya Kristo.
18Kuamahin chiklai mahin Pathian a mu ngei kei; Tapa tang, Pa angsunga om-in theih-in amah a bawlta.
18Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wowote ule. Mwana wa pekee aliye sawa na Mungu ambaye ameungana na Baba, ndiye aliyetujulisha habari za Mungu.
19Huan, Judaten, Kua na hia? chia, dong dinga, Jerusalem khuaa kipana a kianga siampute leh Levi chia mite a sawl lai un hiaite Johan thu na theihsak tuh ahi uh:
19Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa wakati viongozi wa Wayahudi kule Yerusalemu walipowatuma makuhani wa Walawi kwake wamwulize: "Wewe u nani?"
20Panglouin a pulaka, Kris tuh ka hi kei hi, chiin, a pulaka.
20Yohane hakukataa kujibu swali hilo, bali alisema waziwazi, "Mimi siye Kristo."
21Huan, amau a kiangah, Kua na hia leh? Elija na hi hia? a chi ua, a dong ua. Huan aman, Ka hi kei, a chi a. Huai jawlnei kha’ na hi hia? a chi ua. Huan, aman, Hi lou e, a chi a, a dawng a.
21Hapo wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Je, wewe ni Eliya?" Yohane akajibu, "La, mimi siye." Wakamwuliza, "Je, wewe ni yule nabii?" Yohane akawajibu, "La!"
22Huan, amau a kiangah, A hih leh, kua na hia? honsawlte ka dawn theihna ding un honhilh tanla. Na tanchin himhim bang ahia na gen ding? a chi ua.
22Nao wakamwuliza, "Basi, wewe ni nani? Wasema nini juu yako mwenyewe? Tuambie, ili tuwapelekee jibu wale waliotutuma."
23Huan, aman, Toupa lampi hihtang un, chia, gamdaia kikoupa aw ka hi, jawlnei Isai gen bangin, a chi a.
23Yohane akawajibu, "Mimi ndiye yule ambaye nabii Isaya alisema habari zake: Sauti ya mtu imesikika jangwani: Nyoosheni njia ya Bwana."
24A mi sawlte uh Pharisaite kianga kipan kuate hiam ahi ua.
24Hao watu walikuwa wametumwa na Mafarisayo.
25Huan, amau tuh a kiangah, Kris bek, Elija bek, jawlnei bek na hih kei ngal leh, bang achia baptis nak na hia leh? a chi ua, a dong nawn ua.
25Basi, wakamwuliza Yohane, "Kama wewe si Kristo, wala Eliya, wala yule nabii, mbona wabatiza?"
26Huan, Johanin a kiang uah, Ken tuiin ka baptis jel, na lak uah mi khat na theih louh uh a ding ahi, amah tuh ka nunga honjuipa hia,
26Yohane akawajibu, "Mimi nabatiza kwa maji, lakini yuko mmoja kati yenu, msiyemjua bado.
27A khedap khau sut tak leng ka hi kei, a chi a, a dawnga.
27Huyo anakuja baada yangu, lakini mimi sistahili hata kumfungua kamba za viatu vyake."
28Huai tuh Jordan gala Bethabaraa Johanin a baptisna muna thil-om ahi.
28Mambo haya yalifanyika huko Bethania, ng'ambo ya mto Yordani ambako Yohane alikuwa anabatiza.
29Huan, a jingin Johanin Jesu a kiangah hongpaiin a mu a. Huan, a gen a; En un, Pathian Belamnou khovel khelhna lamangpa!
29Kesho yake, Yohane alimwona Yesu akimjia, akasema, "Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu!
30Hiai ahi Amah, Mi khat honkhengpan honjui, Ka maa omsa him ahi, ka chihpa.
30Huyu ndiye niliyesema juu yake: Baada yangu anakuja mtu mmoja aliye mkuu zaidi kuliko mimi, maana alikuwako kabla mimi sijazaliwa!
31Amah, lah ka nathei ngal keia; himahleh, Israelte kianga amah latsak ahihna dingin, tuia baptisin ka hongpai ahi, a chi a.
31Mimi mwenyewe sikumfahamu, lakini nimekuja kubatiza kwa maji ili watu wa Israeli wapate kumjua."
32Huan, Johanin a thu a theisaka, a gen a: Kha tuh vakhu bangin van akipana hongsuk ka mu a, a tungah a tu nilouh.
32Huu ndio ushahidi Yohane alioutoa: "Nilimwona Roho akishuka kama njiwa kutoka mbinguni na kutua juu yake.
33Amah lah ka thei ngal keia; himahleh, tuia baptis dinga honsawlpan ka kianga, Kua tungah leng Kha hongsuka a tunga om na muh peuh, hiai tuh Kha Siangthoua baptispa ahi, a honchi a.
33Mimi sikumjua, lakini yule aliyenituma nikabatize watu kwa maji alikuwa ameniambia: Mtu yule utakayemwona Roho akimshukia kutoka mbinguni na kukaa juu yake, huyo ndiye anayebatiza kwa Roho Mtakatifu.
34Huai tuh ka muta a, hiai mipa tuh Pathian Tapa ahi chih ka theisakta, a chi a.
34Mimi nimeona na ninawaambieni kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu."
35Huan, a jing nawnin Johan a dinga, a nungjui nihte toh; Huan, Jesu vial vakvak lai a en a,
35Kesho yake, Yohane alikuwa tena mahali hapo pamoja na wanafunzi wake wawili.
36En un, Pathian Belamnou, a chi a.
36Alipomwona Yesu akipita akasema, "Tazameni! Huyu ndiye Mwana-kondoo wa Mungu."
37Huan, a nungjui nihten a thu gen tuh a ja ua, Jesu a juita ua.
37Hao wanafunzi walimsikia Yohane akisema maneno hayo, wakamfuata Yesu.
38Huan, Jesu a kiheia, a honjui uh a mu a, a kiang uah, Bang na zong ua? a chi a. Huan, amau Rabbi, (huai tuh Sinsakpa, chihna ahi, ) kaw teng na hia? a chi ua.
38Basi, Yesu aligeuka, na alipowaona hao wanafunzi wanamfuata, akawauliza, "Mnatafuta nini?" Nao wakamjibu, "Rabi (yaani Mwalimu), unakaa wapi?"
39Aman a kiang uah, Hong le uchin na mu ding uh, a chi a. Huchiin, a hong ua, a omna a mu ua; huai niin a kiangah a tam ua, nitakan huan hun phial a hihmanin.
39Yesu akawaambia, "Njoni, nanyi mtaona." Hao wanafunzi wakamfuata, wakaona mahali alipokuwa anakaa, wakashinda naye siku hiyo. Ilikuwa yapata saa kumi jioni.
40Johan thu gen jaa Jesu juite nih tuh a khat zopen Andru, Simon Peter unaupa ahi.
40Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa hao wawili waliokuwa wamemsikia Yohane akisema hivyo, wakamfuata Yesu.
41Aman a masapenin amah unau Simon a mu a, a kiangah, Messia ka muta uh, a chi a, (Huai tuh Kris chihna ahi).
41Andrea alimkuta kwanza Simoni, ndugu yake, akamwambia, "Tumemwona Masiha" (maana yake Kristo).
42Huchiin Jesun amah a na en a, Johan tapa Simon na hi, Kifa a honchii ding uh, a chi a (huai tuh Peter chihna hi).
42Kisha akampeleka Simoni kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama Simoni akasema, "Wewe ni Simoni mwana wa Yohane. Sasa utaitwa Kefa." (maana yake ni Petro, yaani, "Mwamba.")
43Huan, a jingin Jesun Galili gama hoh a tum a, Philip amu a, a kiangah, Honjui in, a chi a.
43Kesho yake Yesu aliamua kwenda Galilaya. Basi, akamkuta Filipo, akamwambia, "Nifuate."
44Philip bel Bethsaida khuaa ahi a, huai tuh Andru leh Peter omna khua mah ahi.
44Filipo alikuwa mwenyeji wa Bethsaida, mji wa akina Andrea na Petro.
45Philipin Nathanael a mu a, a kiangah, A tanchin Mosiin dan laibu-a a gelh leh jawlneiten a gelh uh, amah ka muta uh, Nazaret Jesu, Joseph tapa tuh, a chi a.
45Naye Filipo akamkuta Nathanieli, akamwambia, "Tumemwona yule ambaye Mose aliandika juu yake katika kitabu cha Sheria, na ambaye manabii waliandika habari zake, yaani Yesu Mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti."
46Huan, Nathanaelin a kiangah, Nazaret khuaah thil hoih a pawtthei ahia? achia. Philipin a kiangah, Hongpai inla, enin, a chi a.
46Naye Nathanieli akamwuliza Filipo, "Je, kitu chema chaweza kutoka Nazareti?" Filipo akamwambia, "Njoo uone."
47Jesun Nathanael a kianga hong dekin a mu a a tanchin a na gen a, En un, Israel mi tak, zekhemna himhim neilou, a chi a.
47Yesu alipomwona Nathanieli akimjia alisema juu yake, "Tazameni! Huyo ni Mwisraeli halisi: hamna hila ndani yake."
48Nathanaelin a kiangah, Nang bang chidana honthei na hia? a chi a. Jesun a kiangah, Philipin nang honsap ma a, theipi bula na om laiin, ka honmu hi a chi a, a dawnga.
48Naye Nathanieli akamwuliza, "Umepataje kunijua?" Yesu akamwambia, "Ulipokuwa chini ya mtini hata kabla Filipo hajakuita, nilikuona."
49Nathanaelin a kiangah, Rabbi, Pathian Tapa na hi, Israelte kumpipa na hi, chiin, a dawnga.
49Hapo Nathanieli akamwambia, "Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu. Wewe ni Mfalme wa Israeli!"
50Jesun a kiangah, Theipi bula nang ka honmu hi, na kianga ka chih jiakin na gingta ahi maw? Hiaite sanga thil thupi jaw na mu lai ding, a chi a, a dawnga.Huan, Jesu mahin a kiangah, Chihtaktakin, chihtaktakin ka honhilh ahi, van kihonga, Pathian angelte Mihing Tapa tunga kah leh kum na mu ding, a chi a.
50Yesu akamwambia, "Je, umeamini kwa kuwa nimekwambia kwamba nilikuona chini ya mtini? Utaona makubwa zaidi kuliko haya."
51Huan, Jesu mahin a kiangah, Chihtaktakin, chihtaktakin ka honhilh ahi, van kihonga, Pathian angelte Mihing Tapa tunga kah leh kum na mu ding, a chi a.
51Yesu akaendelea kusema, "Nawaambieni kweli, mtaona mbingu zinafunguka na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Mtu."