Paite

Swahili: New Testament

John

2

1Huan, ni thum niin, Galili gama Kana khua ah kitenna a om a, huai ah Jesu nu a om hi.
1Siku ya tatu kulikuwa na arusi mjini Kana, mkoani Galilaya. Mama yake Yesu alikuwapo,
2Jesu leh a nungjuite leng kitenna ah achial ua.
2naye Yesu alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.
3Huan, uain a beita a, Jesu nun a kiangah, Uain a tasamta u e, a chi a.
3Divai ilipokwisha, mama yake akamwambia, "Hawana divai!"
4Huan, Jesuin a kiangah, Numei, nang non na theisak ding bang ahia om! ka hun a tungnai kei hi, a chi a.
4Yesu akamjibu, "Mama, usiniambie la kufanya. Saa yangu bado."
5Huan, a nun sikhate kiangah, Na kiang ua a gen peuhmah hih jel un, a chi a.
5Hapo mama yake akawaambia watumishi, "Lolote atakalowaambieni, fanyeni."
6Huan, Jadate silsiang dan bangin suang tuibel guk, buk sawmli mun nih hiam, mun thum hiam ta chiat, huaiah a tung uhi.
6Hapo palikuwa na mitungi sita ya mawe, ambayo kila mmoja uliweza kuchukua kiasi cha madebe mawili au matatu. Ilikuwa imewekwa hapo kufuatana na desturi ya Kiyahudi ya kutawadha.
7Huan, Jesun a kiang uah, Tuibelte tuiin dimsak un, a chi a. Huan, a gong toh kikimin a dimsak chiat ua.
7Yesu akawaambia, "Ijazeni mitungi hiyo maji." Nao wakaijaza mpaka juu.
8Huan, a kiang uah, Tuiin dim unla, nekbawl thusa kiangah paipih un, achia. Huan, a paipih ta uhi.
8Kisha akawaambia, "Sasa choteni mkampelekee mkuu wa karamu."
9Huan, nekbawl thusain, tui uain a hong suakta tuh achiama, a hongkipatna lam a theikei a, (tui dim sikhaten lah a thei ua), zi nei dingpa a samta a, a kiangah,
9Mkuu wa karamu alipoonja hayo maji, kumbe yalikuwa yamegeuka kuwa divai. Yeye hakujua ilikotoka, (lakini wale watumishi waliochota maji walijua). Mkuu wa karamu akamwita bwana arusi,
10Mi chihin a tungin uain hoih deuh a hawm jel ua, a tamdeuh a dawn nungun, a hoihlou deuh a hawm uh; nang bel tutanin uain hoih na nakem lailaia, a chi a.
10akamwambia, "Kila mtu huandaa divai nzuri kwanza hata wakisha tosheka huandaa ile hafifu. Lakini wewe umeiweka divai nzuri mpaka sasa!"
11Jesun hiai a thillamdang hihpatna tuh Galili gam Kana khuaa a hih ahi; a thupidan a langsakta a; huan, a nungjuiten amah tuh a gingta uhi.
11Yesu alifanya ishara hii ya kwanza huko Kana, Galilaya, akaonyesha utukufu wake; nao wanafunzi wake wakamwamini.
12Huan, huai khitin Kapernaum khua ah a hoh suka, amah leh a nu toh, a unaute toh, a nungjuite toh; huaiah ni tam lou chik a om uhi.
12Baada ya hayo, Yesu alishuka pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, wakaenda Kafarnaumu ambako walikaa kwa siku chache.
13Huan, Jadate paikan Ankuangluina a naita a, Jesu Jerusalem khua ah a hohtou ta a.
13Sikukuu ya Wayahudi ya Pasaka ilikuwa imekaribia; hivyo Yesu akaenda Yerusalemu.
14Huan, Pathian biakina bawng khawng, belam khawng, vakhu khawng juak leh, dangka khengte tu a mu a.
14Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ng'ombe, kondoo na njiwa, na wavunja fedha walikuwa wamekaa kwenye meza zao.
15Huan, khauhualin jepna ding a bawla, belam leh bawngte a vek un Pathian biakina kipanin a delh khia a, dangka khengte dangka a sungbua a, a dohkante uh leng a sawnpuk saka;
15Akatengeneza mjeledi wa kamba, akawafukuza wote nje ya Hekalu pamoja na kondoo na ng'ombe wao, akazimwaga sarafu za wenye kuvunja fedha na kupindua meza zao.
16huan, vakhu juakte kiangah, Hiai thilte hiai lai akipanin pai pih un, ka Pa in sumsinna in dingin bawl kei un, a chi a.
16Akawaambia wale waliokuwa wanauza njiwa, "Ondoeni vitu hivi hapa. Msiifanye nyumba ya Baba yangu kuwa soko!"
17Huan, Na ina ka phatuamngaihnain a hon gai ding, chih gelh ahi chih, a nungjuiten a thei nawnta uhi.
17Wanafunzi wake wakakumbuka kwamba Maandiko yasema: "Upendo wangu kwa nyumba yako waniua."
18Huchiin, Judaten a kiangah, Hiai thil na hih, chiamtehna bang ahia non lak theih? a chi ua, a dong ua.
18Baadhi ya Wayahudi wakamwuliza Yesu, "Utafanya muujiza gani kuonyesha kwamba unayo haki kufanya mambo haya?"
19Jesun a kiang uah, Hiai in hihse le uchin, ni thum sungin ka tung ding nawn ding, a chi a, a dawng a.
19Yesu akawaambia, "Vunjeni Hekalu hili, nami nitalijenga kwa siku tatu."
20Huan, Judaten, Hiai in kum sawmli leh guk lam ahi, nang ni thum sungin na tung ding ding maw? a chi ua.
20Hapo Wayahudi wakasema, "Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita. Je, wewe utalijenga kwa siku tatu?"
21Himahleh a sapum in thu gen ahi zo ngala.
21Lakini Yesu alikuwa anaongea juu ya Hekalu ambalo ni mwili wake.
22Huai jiakin, misi laka kipana a thoh nawnin, huai thu tuh a genta chih a nungjuiten a thei nawnta ua; huan, laisiangthou thu Jesu thugen tuh a gingta uhi.
22Basi, alipofufuliwa kutoka wafu, wanafunzi wake walikumbuka kwamba alikuwa amesema hayo, wakaamini Maandiko Matakatifu na yale maneno aliyokuwa akisema Yesu.
23Huan, Paikan Ankuangluinaa, Jerusalem khuaa a om laiin, a thillam dang hihte a mu ua, mi tampiin a min a gingta ta uhi.
23Yesu alipokuwa Yerusalemu kwa sikukuu ya Pasaka, watu wengi walimwamini walipoona ishara alizozifanya.
24Himahleh, Jesu tuh a lak uah a kikangkoiha, mi tengteng a theia,mihing thu kuamah hilh chet a kiphamoh louh jiakin; Amah mahin mihing sunga om peuhmah tuh a thei ngala.
24Lakini Yesu hakuwa na imani nao kwa sababu aliwajua wote.
25mihing thu kuamah hilh chet a kiphamoh louh jiakin; Amah mahin mihing sunga om peuhmah tuh a thei ngala.
25Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.