Paite

Swahili: New Testament

John

10

1Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Kuapeuh belam huanga kongkhaka lut lou a, lam danga kah lut, huai mi mah tuh guta leh suamhat ahi.
1Yesu alisema "Kweli nawaambieni, yeyote yule asiyeingia katika zizi la kondoo kwa kupitia mlangoni, bali hupenya na kuingia kwa njia nyingine, huyo ni mwizi na mnyang'anyi.
2Kuapeuh kongkhaka lut tuh, belam chingpa ahi.
2Lakini anayeingia kwa kupitia mlangoni, huyo ndiye mchungaji wa kondoo.
3Kongkhak ngakpan amah a na honsak a; belamten a aw a ja uh; aman belamte a min un a sam chiat a, a pi khe jel hi.
3Mngoja mlango wa zizi humfungulia, na kondoo husikia sauti yake, naye huwaita kondoo wake kila mmoja kwa jina lake na kuwaongoza nje.
4Amaha tengteng a pawt sak takin, ama uh a kaia, belamten amah a juijel uh, a aw a thei ngal ua.
4Akisha watoa nje huwatangulia mbele nao kondoo humfuata, kwani wanaijua sauti yake.
5Midang jaw a jui kei ding uh, a tai mangsan zo ding uh; mi dangte aw jaw a theih louh jiakun, a chi a.
5Kondoo hao hawawezi kumfuata mgeni, bali watamkimbia kwa sababu hawaijui sauti yake."
6Hiai gentehna thu tuh Jesun a kiang uah a gen hi; himahleh, bang thu ahia a kiang ua a gen chih a theikei uhi.
6Yesu aliwaambia mfano huo, lakini wao hawakuelewa alichotaka kuwaambia.
7Huchiin, Jesun a kiang uah a gen nawna, Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, kei belam kongkhak ka hi.
7Basi, akasema tena, "Kweli nawaambieni, mimi ni mlango wa kondoo.
8Ka maa hongpai tengteng gutate; suamhatte ahi vek uh; himahleh, belamten a thu uh a ngaihsak kei uhi.
8Wale wengine wote waliokuja kabla yangu ni wezi na wanyang'anyi, nao kondoo hawakuwasikiliza.
9Kei kongkhak ka hi; keimaha mi a lut leh, humbitin a om dinga, a lutin a pawt dinga, nek ding leng a mu ding hi.
9Mimi ni mlango. Anayeingia kwa kupitia kwangu ataokolewa; ataingia na kutoka, na kupata malisho.
10Guta jaw, gu ding leh hihlum ding leh hihse ding louin a hongpai kei; kei jaw hinna a neihna ding ua, tampitaka a neihna ding ua, hong ka hi.
10Mwizi huja kwa shabaha ya kuiba, kuua na kuharibu. Mimi nimekuja mpate kuwa na uzima--uzima kamili.
11Kei belamchingpa hoih ka hi; belamchingpa hoihin belamte din a hinna a pe nak hi.
11"Mimi ni mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo wake.
12Kiloh, belamchingpa tak hilou, belamte amaha hilouin, ngia hongpai a muhin belamte a taisan nak; huan, ngiain amau tuh a keia, huchiin a hihdalh hi.
12Mtu wa kuajiriwa ambaye si mchungaji, na wala kondoo si mali yake, anapoona mbwa mwitu anakuja, huwaacha kondoo na kukimbia. Kisha mbwa mwitu huwakamata na kuwatawanya.
13Kiloh ahia, belamte adinga deihsakna himhim a neih louh jiakin a tai mang nak ahi.
13Yeye hajali kitu juu ya kondoo kwa sababu yeye ni mtu wa mshahara tu.
14Kei jaw belamchingpa hoih ka hi;
14Mimi ni mchungaji mwema. Nawajua walio wangu, nao walio wangu wananijua mimi,
15Pa in a hontheih leh ken Pa ka theih bangin keia ka thei hi, keia in leng honthei hi; huan, belamte din ka hinna ka pia.
15kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Mimi nayatoa maisha yangu kwa ajili yao.
16Huan, hiai belam huanga lou, belam dangte ka nei; amau leng ka honpi ding, ka aw leng a za ding ua; huchiin hon khatin a om ding ua, a chingpa khat toh.
16Tena ninao kondoo wengine ambao hawamo zizini humu. Inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu, na kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
17Hiai jiakin Pain kei honit ahi; lak nawn dinga ka hinna ka piak ding jiakin.
17"Baba ananipenda kwani nautoa uhai wangu ili nipate kuupokea tena.
18Kuamahin honlaksak kei ding, keimah thuthuin ka pe zo ding ahi. Pe thei ka hi a la nawn thei leng ka hi. Hiai thupiak ka Pa kianga pat ka muh ahi, a chi a.
18Hakuna mtu anayeninyang'anya uhai wangu; mimi na nautoa kwa hiari yangu mwenyewe. Ninao uwezo wa kuutoa na uwezo wa kuuchukua tena. Hivi ndivyo Baba alivyoniamuru nifanye."
19Hiai thu jiakin Judate a kikhen ua, a kilang nawnta ua.
19Kukawa tena na mafarakano kati ya Wayahudi kwa sababu ya maneno haya.
20A khen tampiin, Dawi a jawla, hai eive; bang dia a thu ngaikhia na hi uh? a chi ua.
20Wengi wao wakasema, "Ana pepo; tena ni mwendawazimu! Ya nini kumsikiliza?"
21A khenin, Hiai thu khawng dawi jawl thu hi kei e. Dawiin mittaw mit a hihvak thei ahia? a chi ua.
21Wengine wakasema, "Haya si maneno ya mwenye pepo. Je, pepo anaweza kuyafumbua macho ya vipofu?"
22Huan, Jerusalem khuaa Tempul latna Ankuanglui lai ahi a; huai tuh phalbi lai ahi.
22Huko Yerusalemu kulikuwa na sikukuu ya Kutabaruku. Wakati huo ulikuwa wa baridi.
23Huan, Jesu Pathian biakin ah, Solomon inlim ah a kivial lehleha.
23Naye Yesu akawa anatembea Hekaluni katika ukumbi wa Solomoni.
24Huan, Judaten hong-um pelpul ua, a kiangah, Bangtan ahia vanglaka nonbawl ding? Kris na hih leh, chiantakin honhilh in, a chi ua.
24Basi, Wayahudi wakamzunguka, wakamwuliza, "Utatuacha katika mashaka mpaka lini? Kama wewe ndiye Kristo, basi, tuambie wazi."
25Jesun a kianguah, Ka honhilhta hi, na gingta tuan kei uh; ka Pa mina thil ka hih, hiaiten ka tanchin a theisak uhi.
25Yesu akawajibu, "Nimewaambieni, lakini hamsadiki. Kazi ninazozifanya mimi kwa jina la Baba yangu zinanishuhudia.
26Himahleh, na gingta ngal kei uh, ka belam laka mi na hih louh jiak un.
26Lakini ninyi hamsadiki kwa sababu ninyi si kondoo wangu.
27Ka belamten ka aw a ja uh, ken leng amau ka theia, amau a honjui jel uhi;
27Kondoo wangu huisikia sauti yangu; mimi nawajua, nao hunifuata.
28a kiang uah khantawna hinna ka pia; khantawnin a mangthang kei ding ua, kuamahin ka khut a kipan honsut sam kei ding.
28Mimi nawapa uzima wa milele; nao hawatapotea milele, wala hakuna mtu atakayeweza kuwatoa mkononi mwangu.
29Amau honpepa, ka Pa, mi tengteng sanga thupijaw ahi; kuamahin Pa khuta kipan a sut theikei ding hi.
29Baba yangu ambaye ndiye aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote, wale hakuna awezaye kuwatoa mikononi mwake Baba.
30Kei leh Pa lah pumkhat ka hi uh, chiin, a dawng a.
30Mimi na Baba, tu mmoja."
31Huan, Judaten a denna dingin suang a tawm nawn ua.
31Basi, Wayahudi wakachukua mawe ili wamtupie.
32Huan, Jesu amau a houpih a, Pa akipana pawt nasep hoih tampi ka honensaka, huai nasepte lakah bang nasep jiakin ahia suanga na honden dek uh? a chi a.
32Yesu akawaambia, "Nimewaonyesheni kazi nyingi kutoka kwa Baba. Ni ipi kati ya hizo inayowafanya mnipige mawe?"
33Judaten a kiangah, Nasep hoih tungah suangin ka hondeng dek kei uh; Pathian na gensiat tungah leh, nang, mihing hi ngala, Pathian a na kibawl jiak ahi jaw, chiin, a dawng ua.
33Wayahudi wakamjibu, "Hatukupigi mawe kwa ajili ya tendo jema, ila kwa sababu ya kukufuru! Maana wajifanya kuwa Mungu hali wewe ni binadamu tu."
34Jesun a kianguah, Na Dan laibu uah, Pathiante na hi uh, ka chi, chih gelh ahi ka hia?
34Yesu akawajibu, "Je, haikuandikwa katika Sheria yenu: Mimi nimesema, ninyi ni miungu?
35Pathian thu tunnate bawn pathiante a chih leh, (Laisiangthou tawp theih ahi ngal keia),
35Mungu aliwaita miungu wale waliopewa neno lake; nasi twajua kwamba Maandiko Matakatifu yasema ukweli daima.
36Pathian Tapa ka hi, ka chih jiakin, Pain a seha, khovela a sawlpa kiangah, Pathian na gensia, na chi uh ahi maw?
36Je, yeye ambaye Baba alimweka wakfu na kumtuma ulimwenguni, mnamwambia: Unakufuru, eti kwa sababu nilisema: Mimi ni Mwana wa Mungu?
37Ka Pa nasem ka hih kei leh, hon gingta kei un.
37Kama sifanyi kazi za Baba yangu msiniamini.
38Ahihhangin, sem ka hih leh, kei hon gingta keimah le uchin nasepte bek gingta un; huchia Pa keimah ah a om chih leh, kei Pa ah ka om chih na theih ua, na theihsiam nadingun, a chi a, a dawnga.
38Lakini ikiwa ninazifanya, hata kama hamniamini, walau ziaminini hizo kazi mpate kujua na kutambua kwamba Baba yuko ndani yangu, nami niko ndani yake."
39Huchiin, amah mat a tum nawn ua, himahleh a khut ua kipan a suaktata.
39Wakajaribu tena kumkamata lakini akachopoka mikononi mwao.
40Jordan lui galah, Johanin a tunga mi abaptisna lamah a paimang nawn, huaiah a omta nilouh a.
40Yesu akaenda tena ng'ambo ya mto Yordani, mahali Yohane alipokuwa akibatiza, akakaa huko.
41Huan, mi tampi a kiangah a hong ua, Johanin thillamdang bangmah a hih keia; himahleh Johanin hiai mi tungtang thu agen peuhmah a na dik mahmah hi, a chi ua.Huan, huaiah mi tampiin amah a gingta ta uh.
41Watu wengi walimwendea wakasema, "Yohane hakufanya ishara yoyote. Lakini yale yote Yohane aliyosema juu ya mtu huyu ni kweli kabisa."
42Huan, huaiah mi tampiin amah a gingta ta uh.
42Watu wengi mahali hapo wakamwamini.