Paite

Swahili: New Testament

John

4

1Huan, Jesun, Johan sangin, nungjui tamjaw a bawl chih leh a baptis chih Pharisaiten a ja uh chi Toupan a theih takin,
1Mafarisayo walisikia kwamba Yesu alikuwa anabatiza na kuwapata wanafunzi wengi kuliko Yohane.
2(Himahleh, Jesu hialin jaw a baptis kei, a nungjuiten a baptis zo jel uhi),
2(Lakini ukweli ni kwamba Yesu hakuwa anabatiza ila wanafunzi wake.)
3Judia gam a paisan a, Galili gamah a kik nawnta hi.
3Basi, Yesu aliposikia hayo, alitoka Yudea akarudi Galilaya;
4Huchiin Samari gam a kantan ding ahi a.
4na katika safari hiyo ilimbidi apitie Samaria.
5Huchiin, Samari gam kho khat, Saikar a chih uah a hongtunga, Jakobin a tapa Joseph kianga mun a piakna kiang;
5Basi, akafika Sukari, mji mmoja wa Samaria, karibu na shamba ambalo Yakobo alikuwa amempa mwanawe, Yosefu.
6Jakob tuileh leng huaiah a om hi. Huchiin, Jesu a pai gim jiakin tuileh geiah a tu a; sunannek hun khawng ahi a.
6Mahali hapo palikuwa na kisima cha Yakobo, naye Yesu, kutokana na uchovu wa safari, akaketi kando ya kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7Huan, Samari numei khat tui tawiin a hongkuan a, Jesun a kiangah, Dawnding honpia in, a chi a.
7Basi, mwanamke mmoja Msamaria akafika kuteka maji. Yesu akamwambia, "Nipatie maji ninywe."
8A nungjuite lah nek ding leiin khua ah a hohta ngal ua.
8(Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9Huchiin, Samari numeiin a kiangah, Nang Juda mi na hi a, kei Samari numei ka hi ngala, bangchidan ahia ka kianga dawn ding non nget? a chi a. Judaten Samari mite bangmahin a zang ngei ngal kei ua.
9Lakini huyo mwanamke akamwambia, "Wewe ni Myahudi; mimi ni mwanamke Msamaria! Unawezaje kuniomba maji?" (Wayahudi hawakuwa na ushirikiano na Wasamaria katika matumizi ya vitu.)
10Huan, Jesun a dawnga, a kiangah, Pathian thilpiak leh, Dawn ding honpia in, na kianga chipa thei le tehjaw, nang a kianga ngen zota ding china, huchia aman tui hing honpe ta ding hi a, a chi a.
10Yesu akamjibu, "Kama tu ungalijua zawadi ya Mungu na ni nani anayekwambia: Nipatie maji ninywe, ungalikwisha mwomba, naye angekupa maji yaliyo hai."
11Huan, numeiin a kiangah, Pu, suahna ding bangmah lah na neikeia, tuileh a thukthuk toh, koia kipanin ahia huai tui hing na muh?
11Huyo mama akasema, "Mheshimiwa, wewe huna chombo cha kutekea maji, nacho kisima ni kirefu; utapata wapi maji yaliyo hai?
12Ka pu uh Jakob sangin na thupijaw ahia? Aman hiai tuileh honpia a, aman leng a dawna, a tate, a ganten leng, a chi a.
12Au, labda wewe wajifanya mkuu kuliko babu yetu Yakobo? Yeye alitupa sisi kisima hiki; na yeye mwenyewe, watoto wake na mifugo yake walikunywa maji ya kisima hiki."
13Huan, Jesun a dawnga, a kiangah, Kuapeuh hiai tui dawn a dangtak nawn ding uh;
13Yesu akamjibu, "Kila anayekunywa maji haya ataona kiu tena.
14Kuapeuh a kianga ka piak ding tui dawn bel, a dangtak ngei kei ding; ken a kiang a tui ka piak ding tuh amah ah tuinak a honghi dinga, khantawn hin phain a kikhohtou ding, a chi a.
14Lakini atakayekunywa maji nitakayompa mimi, hataona kiu milele. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji ya uzima na kumpatia uzima wa milele."
15Huan, numeiin a kiangah, Pu, huai tui honpe ve, ka dangtak nawn louhna ding leh, hiai tantana tui tawi dinga ka hongkuan louhna din, a chi a.
15Huyo mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, nipe maji hayo ili nisione kiu tena; nisije tena mpaka hapa kuteka maji."
16Huan, Jesun a kiangah, Na pasal va sam inla, hiaiah hongkik nawn in, a chi a.
16Yesu akamwambia, "Nenda ukamwite mumeo uje naye hapa."
17Huan, numeiin a kiangah, Pasal ka nei sama, a chi a, a dawnga, Jesun a kiangah, Pasal ka nei sama, na chih jaw, na chi dik ve;
17Huyo mwanamke akamwambia, "Mimi sina mume." Yesu akamwambia, "Umesema kweli, kwamba huna mume.
18Pasal nga na neita a, tu a na neihpa na pasal ahi kei him ahi, hiai thu na chi dik ve, a chi a.
18Maana umekuwa na waume watano, na huyo unayeishi naye sasa si mume wako. Hapo umesema kweli."
19Numeiin a kiangah, Pu, jawlnei na hi chih ka theita.
19Huyo Mwanamke akamwambia, "Mheshimiwa, naona ya kuwa wewe u nabii.
20Kou piputen hiai tangah Pathian a be jel ua; himahleh, nou bel, Mihingin Pathian a biakna mun ding uh Jerusalem khua ah a om, na chi sese ua, a chi a.
20Babu zetu waliabudu juu ya mlima huu, lakini ninyi mwasema kwamba mahali pa kumwabudu Mungu ni kule Yerusalemu."
21Huan, Jesun a kiangah, Numei, ka thuhilh gingta in, hiai tangah chitchiat lou leng, Jerusalem khua chitchiat ah lou leng Pa na biak hun uh a tung dekta.
21Yesu akamwambia, "Niamini; wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba juu ya mlima huu, wala kule Yerusalemu.
22Nou na theih louhpi uh na be nak ua; kou jaw ka theih uh ka bia uhi. Hotdamna Judate kianga kipan ahi ngala.
22Ninyi Wasamaria mnamwabudu yule msiyemjua, lakini sisi tunamjua huyo tunayemwabudu, kwa maana wokovu unatoka kwa Wayahudi.
23Himahleh a hun a tung dekta, tuin leng a tungkhin lel, huai hun chiangin Pathian be taktakten kha leh thutaka Pa be ding uh ahi, Pan huchibang mi a bemi dingin a zong hi.
23Lakini wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wanaoabudu kweli, watamwabudu Baba kwa nguvu ya Roho; watu wanaomwabudu hivyo ndio Baba anaotaka.
24Pathian jaw Kha ahi; a bemiten kha leh thutaka a biak ngeingei ding uh ahi, a chi a.
24Mungu ni Roho, na watu wataweza tu kumwabudu kweli kwa nguvu ya Roho wake."
25Huan, numeiin a kiangah, Messia, (Kris a chih uh) a hongpai ding chih ka thei, amah a hongpai chiangin bangkim a honhilh ding, a chi a.
25Huyo mama akamwambia, "Najua kwamba Masiha, aitwaye Kristo, anakuja. Atakapokuja atatujulisha kila kitu."
26Huan, Jesun a kiangah, Keimah nang honhoupihpa, huai amah ka hi, a chi a.
26Yesu akamwambia, "Mimi ninayesema nawe, ndiye."
27Huan, huchihlaiin a nungjuite a hongpai ua, numei a houpih lamdang a sa mahmah ua; himahleh, kuamahin, Bang zong na hia? Bangdia numei houpih? leng a chi kei uh.
27Hapo wanafunzi wake wakarudi, wakastaajabu sana kuona anaongea na mwanamke. Lakini hakuna mtu aliyesema: "Unataka nini?" au, "Kwa nini unaongea na mwanamke?"
28Huan, numeiin a tuibel a paisana, khua ah a vapaia, mite kiangah,
28Huyo mama akauacha mtungi wake pale, akaenda mjini na kuwaambia watu,
29Ka thil hih peuh hon hilh jelpa mi khat a oma, hong unla, en dih uh; Kris a hih theih tuak hiam? a chi a.
29"Njoni mkamwone mtu aliyeniambia mambo yote niliyotenda! Je, yawezekana kuwa yeye ndiye Kristo?"
30Huan, amau tuh khua akipan a hongpawt ua, a kiang lam a juanta ua.
30Watu wakatoka mjini, wakamwendea Yesu.
31Huai kalin nungjuiten a kiangah, Sinsakpa, ne vo, a chi ua.
31Wakati huohuo wanafunzi wake walikuwa wanamsihi Yesu: "Mwalimu, ule chakula."
32Himahleh, aman, a kiang uah, An na theih louh uh nek ding ka nei, a chi a.
32Lakini Yesu akawaambia, "Mimi ninacho chakula msichokijua ninyi."
33Huan, nungjuite a kihou ua, A nek ding min a hontawi sak ua eita maw? a kichi ua.
33Wanafunzi wake wakaulizana, "Je, kuna mtu aliyemletea chakula?"
34Huan, Jesun a kiang uah, a gena, Honsawlpa deihlam hih leh, a na sep zoh ding ka an ahi.
34Yesu akawaambia, "Chakula changu ni kufanya anachotaka yule aliyenituma na kuitimiza kazi yake.
35Nou, Buh lakna ding kha li a om lai, na chi uh hi lou hia? Ngai un kon hilh ahi, dak unla lou khawng en un, tu mahmahin lak dingin a min ahi.
35Ninyi mwasema: Bado miezi minne tu, na wakati wa mavuno utafika! Lakini mimi nawaambieni, yatazameni mashamba; mazao yako tayari kuvunwa.
36A lapain loh a mu a, khantawn hin tana om ding in gah a la, huchia a tuhpa leh a lapa a kipah tuak theihna dingun.
36Mvunaji anapata mshahara wake, na anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele; hivyo mpandaji na mvunaji watafurahi pamoja.
37Khatin a tuha, midang in a la hi, chih thu, huai ah a dik ngel hi.
37Kwa sababu hiyo msemo huu ni kweli: Mmoja hupanda na mwingine huvuna.
38Na sep gim louh uh at dia honsawl ka hi; mi dangin a sem ua, nou a sepsa uh na sunzom uh ahi, a chi a.
38Mimi nimewatuma mkavune mavuno ambayo hamkuyatolea jasho, wengine walifanya kazi, lakini ninyi mnafaidika kutokana na jasho lao."
39Huan, numeiin, Ka thil hih peuh honhilh jel, chia, a theihsak thu jiakin, huai khuaa om Samari mi tampiin Jesu a gingta ua.
39Wasamaria wengi wa kijiji kile waliamini kwa sababu ya maneno aliyosema huyo mama: "Ameniambia mambo yote niliyofanya."
40Huchiin, Samari mite Jesu kiangah a hongpai ua, a kiang ua om dingin a khou ngutngut ua; huan, huaiah ni nih a tam hi.
40Wasamaria walimwendea Yesu wakamwomba akae nao; naye akakaa hapo siku mbili.
41Huan, mi dang tampiin amah thu jiakin a gingta sam ta uhi.
41Watu wengi zaidi walimwamini kwa sababu ya ujumbe wake.
42Huan, amau, numei kiangah, Tun tuh na thu gen jiaka gingta ka hi kei uh; koumau ngeiin a thu ka ja ua, hiai mipa khovel Hondampa ahi ngei chih ka theita uh, a chi ua.
42Wakamwambia yule mama, "Sisi hatuamini tu kwa sababu ya maneno yako; sisi wenyewe tumesikia, na tunajua kwamba huyu ndiye kweli Mwokozi wa ulimwengu."
43Huan, ni nih nungin huaia kipanin a pawta. Galili gamah a hohta a.
43Baada ya siku mbili Yesu aliondoka hapo, akaenda Galilaya.
44Jesu ngeiin, jawlnei jaw amah kho lamah pahtawiin a om ngei kei chih a theisaka.
44Maana Yesu mwenyewe alisema waziwazi kwamba, "Nabii hapati heshima katika nchi yake."
45Huchiin, Galili gam a hongtunin Galili gama miten a na kipahpih ua, Jerusalem khuaa ankuanglui laia a thilhih tengteng a muh tak jiakun; amau mah leng ankuangluina ah a hohsam ngal ua.
45Basi, alipofika Galilaya, Wagalilaya wengi walimkaribisha. Maana nao pia walikuwa kwenye sikukuu ya Pasaka, wakayaona mambo yote Yesu aliyotenda huko Yerusalemu wakati wa sikukuu hiyo.
46Huan, Galili gama Kana khua, tui uain a suahsak mun a hongtung nawnta a. Huan, upa kua hiam a om a, a tapa Kapernaum khua ah a chi a na a.
46Yesu alifika tena huko mjini Kana, mkoani Galilaya, mahali alipogeuza maji kuwa divai. Kulikuwa na ofisa mmoja aliyekuwa na mtoto mgonjwa huko Kafarnaumu.
47Huan, Jesu Judia gama kipan Galili gamah a hong chih a jak takin a kiangah a hoh tou a, Va hohsuka a tapa vahihdamsak dingin achialchiala, a si dekdek ngala.
47Basi, huyo ofisa aliposikia kuwa Yesu alikuwa ametoka Yudea na kufika Galilaya, alimwendea akamwomba aende kumponya mtoto wake aliyekuwa mgonjwa mahututi.
48Huan, Jesun a kiangah, Chiamtehnate leh thillamdangte na muh kei uh leh na gingta kei hial ding uh, a chi a.
48Yesu akamwambia, "Msipoona ishara na maajabu hamtaamini!"
49Huan, upain a kiangah, Pu, ka ta sih main hongsuk tanla, a chi a.
49Huyo ofisa akamwambia, "Mheshimiwa, tafadhali twende kabla mwanangu hajafa."
50Huan, Jesun a kiangah, Pai nawnta mai in, na tapa damta hi, a chi a. Huan, huai mipan Jesun a kianga thu a gen tuh a gingta a, a paita hi.
50Yesu akamwambia, "Nenda tu, mwanao yu mzima." Huyo mtu akaamini maneno ya Yesu, akaenda zake.
51Huan, a pai suk lel laiin a sikhaten a na dawn ua, Na tapa a damta, a na chi ua.
51Alipokuwa bado njiani, watumishi wake walikutana naye, wakamwambia kwamba mwanawe alikuwa mzima.
52Huan, aman a kiang uah a dam tung lai a dong a. Huan, amau, a kiangah, Janin ni kihek lelin a khosik a daita ahi, a chi ua.
52Naye akawauliza saa mtoto alipopata nafuu; nao wakamwambia, "Jana saa saba mchana, homa ilimwacha."
53Huchiin, apan Jesun a kianga, Na tapa a damta hi, a chih lai ahi chih a theita a; huan amah leh a inkuanpihten a vek un, a gingta ta uhi.Huai tuh Jesun a thillamdang hih a nih veina ahi, Judia gam akipan Galili gama a hongin.
53Huyo baba akakumbuka kwamba ilikuwa ni saa ileile ambapo Yesu alimwambia: "Mwanao yu mzima." Basi, yeye akaamini pamoja na jamaa yake yote.
54Huai tuh Jesun a thillamdang hih a nih veina ahi, Judia gam akipan Galili gama a hongin.
54Hii ilikuwa ishara ya pili aliyoifanya Yesu alipokuwa anatoka Yudea kwenda Galilaya.