Paite

Swahili: New Testament

John

5

1Huai thil nungin Judate ankuangluina a om a; Jesu Jerusalem khua ah a hoh tou a.
1Baada ya hayo kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi, naye Yesu akaenda Yerusalemu.
2Huan, Jerusalem ah belam kongkhak kiangah dil a oma, huai tuh Hebru pauin Bethsaida a chi ua, inlim nga neia.
2Huko Yerusalemu, karibu na mlango uitwao Mlango wa Kondoo, kulikuwa na bwawa la maji liitwalo kwa Kiebrania Bethzatha, ambalo lilikuwa na baraza tano zenye matao.
3Huai ah damloute, mittawte, khebaite, jawte tampi a lum phengphung ua, tui hongtat ngakin.
3Humo barazani mlikuwa na wagonjwa wengi wamekaa: vipofu, viwete na waliopooza. Walikuwa wakingojea maji yatibuliwe,
4Bang chiang hiamin huai dil ah angel a hoh suk a, tui a vatok a; huchiin, kuapeuh huai tui a kitoh khita valut masa penpen tuh, bangchibang natna nei hileh leng hihdamin a om jel hi.
4maana mara kwa mara malaika alishuka majini nyakati fulani na kuyatibua. Mtu yeyote aliyekuwa wa kwanza kuingia majini baada ya maji kutibuliwa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.
5Huan, huaiah kum sawmthum leh giat damlou mi kuahiam a om a.
5Basi, hapo palikuwa na mtu mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa muda wa miaka thelathini na minane.
6Huan, Jesun a lum tuh a mu a, huchi bangin sawtpi a omta chih a thei a, a kiangah, Hihdam na ut hia? a chi a.
6Naye alipomwona huyo mtu amelala hapo, akatambua kwamba alikuwa amekaa hapo kwa muda mrefu, akamwuliza, "Je, wataka kupona?"
7Huan, damloupan, Pu, tui kitohin dila honkoih ding mi ka neikei hi, ka hoh sungin mi dangin honmakhelh nak uh, achia, a dawng a.
7Naye akajibu, "Mheshimiwa, mimi sina mtu wa kunipeleka majini wakati yanapotibuliwa. Kila nikijaribu kuingia, mtu mwingine hunitangulia."
8Huan, Jesun a kiangah, Thou inla, na awngphah la inla, khein paita in, a chi a.
8Yesu akamwambia, "Inuka, chukua mkeka wako utembee."
9Huan, thakhatin huai mi tuh a dam pah a, a awngphah a la a, a paita hi.
9Mara huyo mtu akapona, akachukua mkeka wake, akatembea. Jambo hili lilifanyika siku ya Sabato.
10Huai ni tuh Khawlni ahi, Huchiin Judaten a dampa kiangah, Khawlni ei ve, na awngphah na lak a siang kei, a chi ua.
10Kwa hiyo baadhi ya Wayahudi wakamwambia huyo mtu aliyeponywa, "Leo ni Sabato, si halali kubeba mkeka wako."
11Huan, aman a kiang uah, Honhihdampa ngeingeiin ka kiangah, Na awngphah la inla, khein paita in, honchi ahi, a chi a, a dawnga.
11Lakini yeye akawaambia, "Yule mtu aliyeniponya ndiye aliyeniambia: Chukua mkeka wako, tembea."
12Huan, amau a kiangah, Na awngphah la inla, khein paita in, na kianga chipa kua ahia? a chi ua, a dong ua.
12Nao wakamwuliza, "Huyo mtu aliyekwambia: Chukua mkeka wako, tembea, ni nani?"
13Himahleh, a dampan tuh kua ahia a hih a theikei a, huaia mipi a om jiak un Jesu a paimangta ngala.
13Lakini yeye hakumjua huyo mtu aliyemponya, maana Yesu alikuwa amekwisha ondoka mahali hapo, kwani palikuwa na umati mkubwa wa watu.
14Adenchiangin Jesun amah Pathian biakin ah a mu a, a kiangah, Ngaiin, na damta hi, khial nawnta ken, huchilou injaw thil hoihlou sem na tungah a hongom kha ding hi, a chi a.
14Basi, baadaye Yesu alimkuta huyo aliyeponywa Hekaluni, akamwambia, "Sasa umepona; usitende dhambi tena, usije ukapatwa na jambo baya zaidi."
15Huan, huai mi tuh a vapai khia a, Judate kiangah a hihdampa Jesu ahi chih a hilh a.
15Huyo mtu akaenda, akawaambia viongozi wa Wayahudi kwamba Yesu ndiye aliyemponya.
16Huchiin, Khawlnia huai thil a hih jiakin Judaten Jesu a engbawl ua.
16Kwa vile Yesu alifanya jambo hilo siku ya Sabato, Wayahudi walianza kumdhulumu.
17Himahleh, Jesun amau a houpiha, a kiang uah, Ka Pan tutan phain leng na asem jel hi, ken leng ka sem jel, a chi a.
17Basi, Yesu akawaambia, "Baba yangu anafanya kazi daima, nami pia nafanya kazi."
18Huchiin, Judaten hihlup a tum semsem ua, Khawlni a tanlouh jiak kia leng ahi keia, Pathian amah Paa a bawl a, Pathian toh ki kima a kibawl jiakin leng ahi.
18Kwa sababu ya maneno haya, viongozi wa Wayahudi walizidi kutafuta njia ya kumwua Yesu: si kwa kuwa aliivunja Sheria ya Sabato tu, bali pia kwa kuwa alisema kwamba Mungu ni Baba yake, na hivyo akajifanya sawa na Mungu.
19Huan, Jesun a kiang uah, Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Tapain amahin bangmah a hih theikei, Pa thil hih a muh kia lou ngal; thil a hih peuhmah, Tapain leng a hih sam jel ahi.
19Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mwana hawezi kufanya kitu peke yake; anaweza tu kufanya kile anachomwona Baba akikifanya. Maana kile anachofanya Baba, Mwana hukifanya vilevile.
20Pain Tapa a ita, a thilhih peuhmah a kiangah a musak a; hiaite sanga thilhih thupijaw a kiangah a musak ding, lamdang na sak ding un.
20Baba ampenda Mwana, na humwonyesha kila kitu anachokifanya yeye mwenyewe, tena atamwonyesha mambo makuu kuliko haya, nanyi mtastaajabu.
21Pain misite a a kithou a, hinna a piak bangin, Tapa inleng a utnana kiangah hinna a pia.
21Kama vile Baba huwafufua wafu na kuwapa uzima, vivyo hivyo naye Mwana huwapa uzima wale anaopenda.
22Pain kuamah vai a hawm sak ngei kei, vai tengteng Tapa a hawm sak zota;
22Baba hamhukumu mtu yeyote; shughuli yote ya hukumu amemkabidhi Mwana,
23mi tengtengin Pa zahna apiak bang un, Tapa leng zahna a piakna dingun. Kuapeuhmah Tapa zah lou ten jaw, Pa a sawlpa leng a zah kei uhi.
23ili watu wote wamheshimu Mwana kama vile wanavyomheshimu Baba. Asiyemheshimu Mwana hamheshimu Baba ambaye amemtuma.
24Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, Kuapeuh ka thu ja a, honsawlpa gingtain, khantawna hinna a nei; siamlouhin a om keia, sihnaa kipan a pawta, hinna ah a lut zota ahi.
24"Kweli nawaambieni, anayesikia neno langu, na kumwamini yule aliyenituma, anao uzima wa milele. Hatahukumiwa kamwe, bali amekwisha pita kutoka kifo na kuingia katika uzima.
25Chihtaktakin, chihtaktakin kon hilh ahi, A hun a tung dekta, tuin leng a tung lellelta, huaihun chiangin misiten Pathian Tapa aw a za ding ua, a za peuhmah a hing ding uh.
25Kweli nawaambieni, wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo wafu wataisikia sauti ya Mwana wa Mungu, nao watakaoisikia, wataishi.
26Pain amaha hinna a nei bangin, Tapa leng amaha hinna neidingin a peta hi.
26Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo pia alivyomjalia Mwanawe kuwa asili ya uhai.
27Huan, Mihing Tapa a hih jiakin, a kiangah thukhenvaihawmna thu a pia hi.
27Tena amempa mamlaka ya kuhukumu kwa sababu yeye ni Mwana wa Mtu.
28Hiai khawng lamdang sa kei un, a hun a tung dekta, huai hun chiangin han a om tengtengin a aw a za ding ua, a pawt vek ding uh;
28Msistaajabie jambo hili; maana wakati unakuja ambapo wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake,
29thil hoih hihte tuh hinna tangin a thou nawn ding ua, thil gilou hihte tuh siam louh tangin a thou nawn ding uh.
29nao watafufuka: wale waliotenda mema watafufuka na kuishi, na wale waliotenda maovu watafufuka na kuhukumiwa.
30Keimahin bangmah ka hih theikei; bila kajak bangbangin vai ka hawm jel; ka vaihawm tuh a dik ahi, keimah thu thuin om ka tum keia, honsawlpa thuthu ja ua om ka tup jel jiakin.
30"Mimi siwezi kufanya kitu kwa uwezo wangu mwenyewe. Mimi nina hukumu kama ninavyosikia kutoka kwa Baba, nayo hukumu yangu ni ya haki. Nia yangu si kufanya nipendavyo mwenyewe, bali apendavyo yule aliyenituma.
31Keimah tanchin theisak leng, ka thu theihsak a dik kei ding;
31Nikijishuhudia mimi mwenyewe, ushahidi wangu hauwezi kukubaliwa kuwa wa kweli.
32ka tanchin theisak mi dang ahi, aman ka tanchin a theihsak tuh a dik chih ka thei hi.
32Lakini yuko mwingine ambaye hutoa ushahidi juu yangu, nami najua kwamba yote anayosema juu yangu ni ya kweli.
33Nou Johan kiangah mi na sawl ua, huan, aman, thutak tanchin honna theisak hi.
33Ninyi mlituma ujumbe kwa Yohane naye aliushuhudia ukweli.
34Thu theihsak ka san tuh mihing akipan ahi chihna ahi keia; himahleh na hinna ding un hiai thu tuh ka gen ahi.
34Si kwamba mimi nautegemea ushahidi wa wanadamu, lakini nasema mambo haya ili mpate kuokolewa.
35Huai Johan tuh khawnvak kuangtak leh vak tak ahi, a vakah nuamsak tak dih na ut uh.
35Yohane alikuwa kama taa iliyokuwa ikiwaka na kuangaza, nanyi mlikuwa tayari kufurahia mwanga huo kwa kitambo.
36Himahleh, theihsakna ka neihjaw Johan theihsakna thu sangin a thupi jaw ahi: Pain thil hih zoh dinga a honpiak, ka thil hih ngeiin Pain honsawl chih ka tanchin a theisak hi.
36Lakini mimi nina ushahidi juu yangu ambao ni mkuu zaidi kuliko ule wa Yohane. Kwa maana kazi ninazofanya, kazi alizonipa Baba nizifanye, ndizo zinazonishuhudia kwamba Baba ndiye aliyenituma.
37Pa honsawlpan leng ka tanchin a theisakta. Nou chiklai mahin a aw na za ngei kei ua, a mel leng na mu ngei sam kei uh.
37Naye Baba aliyenituma hunishuhudia. Ninyi hamjapata kamwe kusikia sauti yake, wala kuuona uso wake,
38A thu leng noumau ah na pai kei uh, a sawlpa na gintak louh jiakun.
38na ujumbe wake haukai ndani yenu maana hamkumwamini yule aliyemtuma.
39Laisiangthou na phat sim ua, a sunga khantawna hinna oma na gintak jiakun: huai laisiangthou tuh ka tanchin theihpihna lah ahi ngala.
39Ninyi huyachunguza Maandiko Matakatifu mkidhani kwamba ndani yake mtapata uzima wa milele; na kumbe maandiko hayohayo yananishuhudia!
40Himahleh, hinna nei dingin ka kiangah na hong nuam ngal kei uh.
40Hata hivyo, ninyi hamtaki kuja kwangu ili mpate uzima.
41Mihing pahtawina ka sang kei.
41"Shabaha yangu si kupata sifa kutoka kwa watu.
42Himahleh nou kon thei hi, Pathian itna noumau ah na neikei uhi.
42Lakini nawajua ninyi, najua kwamba upendo kwa Mungu haumo mioyoni mwenu.
43Ka Pa minin ka honga, nouten non kipahpih kei uh: mi dang amah minin hong leh, amah na kipahpih ding uhi.
43Mimi nimekuja kwa mamlaka ya Baba yangu, lakini hamnipokei; bali mtu mwingine akija kwa mamlaka yake mwenyewe, mtampokea.
44Nou kipahtawi tuahna paktate aw, bangchin na gingta thei ding ua? Pathian tak kiaa pawt pahtawina lah na zong kei ua.
44Mwawezaje kuamini, hali ninyi mnapenda kupokea sifa kutoka kwenu ninyi wenyewe, wala hamtafuti sifa kutoka kwake yeye aliye peke yake Mungu?
45Ken Pa kianga nou kon hek ding gingta kei un: nou honhek khat a om, na muan uh Mosi ngei.
45Msifikiri kwamba mimi nitawashtaki kwa Baba. Mose ambaye ninyi mmemtumainia ndiye atakayewashtaki.
46Mosi na gingta hile-uchin kei leng hongingta ta ding hi uchina; aman ka tanchin ahi a gelh.Himahleh, a thu gelh lah na gingta ngal kei ua, bangchin ka thu na gingta ding ua? a chi a.
46Kama kweli mngemwamini Mose, mngeniamini na mimi pia; maana Mose aliandika juu yangu.
47Himahleh, a thu gelh lah na gingta ngal kei ua, bangchin ka thu na gingta ding ua? a chi a.
47Lakini hamuyaamini yale aliyoandika, mtawezaje basi, kuamini maneno yangu?"