Paite

Swahili: New Testament

Luke

23

1Huan, mipi khempeuh a ding ua, Jesu Pilat kiangah a pita ua.
1Kisha, wote kwa jumla, wakasimama, wakampeleka Yesu mbele ya Pilato.
2Huan, Hiai miin ka chite uh a pimanga, Kaisar kiangah siah liau a kham, Kris, Kumpipa, a kichih, ka ja uh, chiin, a hekta ua.
2Wakaanza kumshtaki wakisema: "Tulimkuta mtu huyu akiwapotosha watu wetu, akipinga kulipa kodi kwa Kaisari na kujiita ati yeye ni Kristo, Mfalme."
3Huan, Pilatin, a kiangah, Judate kumpipa na hi hia? chiin, a donga. Hi e, chiin, a dawng a.
3Pilato akamwuliza Yesu, "Wewe ni Mfalme wa Wayahudi?" Yesu akamjibu, "Wewe umesema."
4Huan, Pilatin siampu liante leh mipite kiangah, Hiai mi tungah bangmah khelhna ka mu kei, a chi a.
4Pilato akawaambia makuhani wakuu na umati wa watu, "Sioni kosa lolote katika mtu huyu."
5Himahleh, amau, Galili gamah a pana, hiai mun phain, Judia gam kho tengah thuhilhin, mi tengteng a toknok gige ahi, chiin, a pang semsem ua.
5Lakini wao wakasisitiza wakisema: "Anawachochea watu kwa mafundisho yake katika nchi yote ya Yudea; alianza Galilaya, na sasa yuko hapa."
6Huan, Pilatin huai a jakin, huai mi tuh Galili gama mi a hih leh hih louh a donga.
6Pilato aliposikia hayo, akauliza, "Je, mtu huyu ni mwenyeji wa Galilaya?"
7Huchiin, Herod uka mi ahi chih a theih takin Herod kiangah a sawlta a; huai laiin amah leng Jerusalem khua ah a om a.
7Alipojua kwamba Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode, akampeleka kwa Herode, ambaye wakati huo alikuwa Yerusalemu.
8Herodin Jesu a muhin a kipak mahmah a; a tanchin a jak jiakin, tumasiah a pat muh a ut him ahi a, a thillamdang hih banghiam bek muh leng a lamen ahi.
8Herode alifurahi sana alipomwona Yesu. Alikuwa amekwisha sikia habari zake, na hivyo alikuwa anatazamia kwa muda mrefu kumwona kwa macho yake mwenyewe. Zaidi ya hayo, alikuwa anatumaini kumwona Yesu akitenda mwujiza.
9Huan thu tampi a donga; himahleh bangmahin a dawng tuan kei hi.
9Basi, akamwuliza maswali mengi kwa muda mrefu, lakini Yesu hakumjibu neno.
10Huan, siampu liante leh laigelhmiten dingin nakpi takin a hek ua.
10Makuhani wakuu na walimu wa Sheria wakajitokeza mbele, wakatoa mashtaka yao kwa nguvu sana.
11Huan, Herod leh a sepaihten Jesu a simmoh ua, nuihza bawlnan a zang uh, huan, puan thupi tak silh sakin Pilat kiangah a sawl nawnta hi.
11Basi, herode pamoja na maaskari wake, wakamwaibisha Yesu na kumfanyia mzaha; kisha wakamvika vazi la kifalme, wakamrudisha kwa Pilato.
12Huan, huai ni takin Herod leh Pilat a kihouthei ta uh; huai masiah jaw kihouthei lou hi ua.
12Herode na Pilato, ambao hapo awali walikuwa maadui, tangu siku hiyo wakawa marafiki.
13Huan, Pilatin siampu liante, heutute, mi tengteng a sam khawm a, a kiang uah,
13Basi, Pilato akaitisha mkutano wa makuhani wakuu, viongozi na watu,
14Mite a pimang, chiin, hiai mi ka kiangah na honpi uh ahi a; huan, ngai un, na ma ua ka etchet nungin na hekna thu uah hiai mi tungah bangmah khelhna ka mu kei ahi;
14akawaambia, "Mmemleta mtu huyu kwangu mkisema kwamba alikuwa anawapotosha watu. Sasa sikilizeni! Baada ya kuchunguza jambo hilo mbele yenu, sikumpata na kosa lolote kuhusu mashtaka yenu juu yake.
15Herodin leng a mu sam kei; i kiang uah a honsawl nawnta ahi; ngai un, sihna khop hial bangmah a hih kei hi.
15Wala si mimi tu, bali hata Herode hakuona kosa lolote, kwa maana amemrudisha kwangu. Ni dhahiri kwamba mtu huyu hakufanya chochote kinachostahili adhabu ya kifo.
16Huchiin ka vo dinga, ka pawt sak mai ding, a chi a.
16Hivyo, nitaamuru apigwe viboko, halafu nitamwachilia."
17(Ankuanglui nia mikhat amau laka a pawt sak teitei ding ahi ngala. )
17Kila sikukuu ya Pasaka, ilimlazimu Pilato kuwafungulia mfungwa mmoja.
18Himahleh, kituaktakin a kikou ua, Hiai mi hihmangthang inla, Barabba pen honpawt sak jawin, a chi ua.
18Lakini wote wakapiga kelele pamoja: "Mwondoe huyo, utufungulie Baraba!"
19Huai mi tuh khopia helna bang ahi hiam jiak leh, tual a thah jiaka suangkulha tang ahi.
19(Baraba alikuwa ametiwa ndani kwa kusababisha uasi katika mji na pia kwa sababu ya kuua.)
20Pilatin bel, Jesu khah a uta, a kiang uah thu a gen nawna.
20Pilato alitaka kumwachilia Yesu, hivyo akasema nao tena;
21Himahleh, a kikou ua, Kros ah kilhden in, kros ah kilhden in, a chi ua.
21lakini wao wakapiga kelele: "Msulubishe, msulubishe!"
22Huan, aman, a thum veina ah a kiang uah, Bang dingin maw? hiai min bang ahia ahihkhelh? sihna khop hial a tungah bangmah ka mu kei; huchiin ka vo dinga, ka khah mai ding, a chi a.
22Pilato akawaambia mara ya tatu, "Amefanya kosa gani? Sioni kosa lolote kwake linalomstahili auawe; kwa hiyo nitampiga viboko, halafu nimwachilie."
23Amau bel aw ngaihtakin kros a kilhden dingin a ngen teitei uh. Huan, a aw un a vau daita hi.
23Lakini wao wakazidi kupiga kelele kwa nguvu sana, kwamba Yesu ni lazima asulubiwe. Mwishowe, sauti zao zikashinda.
24Huan, Pilatin a nget bang ua hih dingin thu a hihpukta a.
24Basi, Pilato akaamua kwamba matakwa yao yatimizwe.
25Helna leh tualthah jiaka suangkulha tang a nget uh a khaha; Jesu bel a ut ut ua lohdingin a peta hi.
25Akamfungua kutoka gerezani yule waliyemtaka, ambaye alikuwa ametiwa gerezani kwa sababu ya uasi na kuua; akamtoa Yesu kwao, wamfanyie walivyotaka.
26Huan, a pi mang lai un, Simon Kurini khua a mi, gam lam a kipana hong a man ua, Jesu nunglama po dingin a tungah kros tuh a nga ta uhi.
26Walipokuwa wakimpeleka, walikutana na mtu mmoja, aitwaye Simoni wa Kurene, aliyekuwa anatoka shambani. Basi, walimkamata, wakamtwika ule msalaba auchukue nyuma ya Yesu.
27Huan, mi nazong leh numei amah kaha mau jeljul, mipi tampitakin a jui ua.
27Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao wakiwemo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia.
28Jesu bel amau lam a nga a, Jerusalem tanute aw, honkah kei un, noumau leh na tate uh dingin kap jaw un.
28Yesu akawageukia, akasema, "Enyi kina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu.
29Ngai un, a ni a hongtung dinga, huai niin, numei chingte, naupai ngei louhna gilte, naunek ngei louh nawite a hampha uh, a honchi ding uh.
29Maana, hakika siku zitakuja ambapo watasema: Heri yao wale walio tasa, ambao hawakupata kuzaa wala kunyonyesha watoto!
30Huai hun chiangin, miten, tangte kiangah, Hondelh un, a chi ding uh, mualte kiangah, Honkhuh un, a chi ding uhi.
30Wakati huo, ndipo watu wataanza kuiambia milima: Tuangukieni! na vilima, Tufunikeni!
31Sing a hinlaia bawn hichi banga a hih u leh; a keu chiangin bang a kilohta phet dia? a chi a.
31Kwa maana, kama watu wanautendea mti mbichi namna hiyo, itakuwaje kwa mti mkavu?"
32Huan, a kiangah mi dang nih, mi gilou, hihlup dingin a pi sam ua.
32Waliwachukua pia watu wengine wawili, wahalifu, wauawe pamoja naye.
33Huan, Lu Guh, a chih mun uh a tun un, huaiah kros ah a kilhden ua, mi giloute toh, a taklam ah khat, a vei lam ah khat.
33Walipofika mahali paitwapo, "Fuvu la Kichwa," ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili, mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto.
34Huan, Jesun, Pa, amau ngaidam in; a thil hih uh a theikei ua hi, a chi a. Huan a puansilhte kihawmin, ai a san uh.
34Yesu akasema, "Baba, uwasamehe kwa maana hawajui wanalofanya." Kisha wakagawana mavazi yake kwa kuyapigia kura.
35Huan, vantang honin dingin a en ua. Huchiin vaihawmmiten bel Midang bawn a hihdam jel aka; Pathian tel kris tuh a hih taktak leh amah leng kihihdam leh ake, chiin, a enghou ua.
35Watu wakawa wamesimama pale wakitazama. Nao viongozi wakamdhihaki wakisema: "Amewaokoa wengine; sasa na ajiokoe mwenyewe, kama yeye ndiye Kristo, mteule wa Mungu!"
36Huan, sepaihten leng amah nuihza bawlnan a nei ua, a kiangah a hong ua, zu thuk a pia ua,
36Askari nao walimdhihaki pia; walimwendea wakampa siki
37Judate kumpipa na hih taktak leh, kihihdam in, a chi ua.
37wakisema: "Kama kweli wewe ni Mfalme wa Wayahudi, jiokoe mwenyewe."
38Huan, a tung lamah, HIAI MI JUDATE KUMPIPA A HI, chiin, lai a kisuang hi.
38Vilevile maandishi haya yalikuwa yameandikwa na kuwekwa juu yake: "Huyu ndiye Mfalme wa Wayahudi."
39Huan, a mi gilou kilh khat un Jesu a taia, Kris na hi ka hia? kihihdam inla, kou leng honhihdam tanla, a chi a.
39Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia."
40Himahleh, khatpan tuh dawn kawmin, a taihilh a, Pathian na ngawn leng na kihta ka hia? kibang sapa hongawt uh.
40Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo.
41Ei jaw gawttuak him i hi; i thil hih man lel mu i hi a; hiai miin bel bangmah a hihkhial ngal keia, a chi a.
41Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya."
42Huan, aman, Jesu, thuneihna toh Kumpipa-a na hongpai chiangin hontheigige in, a chi a.
42Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako."
43Huan, aman, a kiangah, Chihtaktakin ka honhilh ahi, Tuniin ka kiangah Paradis ah na om sam ding, achia.
43Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
44Huan, dak gukna ding khawng ahi a, huai nungsiah dak kuana hun tanin gam pumpi a hongmial vekta a, ni vak a beita hi;
44Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likafunika nchi yote mpaka saa tisa,
45huan, Pathian biakin puanjak a lai ah a hong kekta hi.
45na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka vipande viwili.
46Huan, Jesu aw ngaihtakin a kikou a, Pa, na khutah ka kha ka honkem sak hi a chi a. Huan, huai a chih khitin a kha a khahta hi.
46Yesu akalia kwa sauti kubwa: "Baba, naiweka roho yangu mikononi mwako." Alipokwisha sema hayo, akakata roho.
47Huan, sepaih zaheupan thil omdan a muh in, Hiai mi pel louin mi dik ahi ngeingei, chiin, Pathian a phatta.
47Hapo, yule jemadari alipoona yaliyotukia akamsifu Mungu akisema: "Hakika huyu alikuwa mtu mwema."
48Huan, huai etnop tuh en dinga mipi hongkikhawm tengteng ten thil omdante a muh un a awm uh tumtumin a kik nawnta uhi.
48Watu wale wote waliokuwa wamekusanyika hapo kwa ajili ya tukio hilo, walipoona hayo yaliyotukia, walirudi makwao wakijipiga vifua kwa huzuni.
49Huan, amel theihte tengteng leh, numei Galili gama kipana honjuite, huai thilte enin gamla takah a ding uh.
49Marafiki zake wote pamoja na wale wanawake walioandamana naye kutoka Galilaya, walisimama kwa mbali kutazama tukio hilo.
50Huan, ngai un, mi khat amin Joseph, vaihawmmi, mi hoih tak, diktak, Judate khua khat Arimathai a kipan a oma,
50Kulikuwa na mtu mmoja jina lake Yosefu, mwenyeji wa kijiji kimoja cha Wayahudi kiitwacho Armathaya. Alikuwa mtu mwema anayeheshimika;
51A vaihawm uah leh a thil hih uah leng a kiawi kei him a. Pathian gam a lamen gige a.
51Alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu. Ingawa alikuwa mmoja wa Baraza kuu la Wayahudi, hakuwa amekubaliana nao katika kitendo chao.
52Huai mi tuh Pilat kiangah a hoha, Jesu luang a ngen a.
52Basi, yeye alikwenda kwa Pilato, akaomba apewe mwili wa Yesu.
53Huan a la khia a, puan mal ngatin a tuama, han, suang khuakkuak, kuamah sial ngei nai louhna ah, a siala.
53Kisha, akaushusha mwili huo kutoka msalabani, akauzungushia sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililokuwa limechongwa kwenye mwamba, ambalo halikuwa limetumika.
54Huan, huai ni tuh kiginni ahi a, Khawlni a honghi sinsinta hi.
54Siku hiyo ilikuwa Ijumaa, na maandalio ya siku ya Sabato yalikuwa yanaanza.
55Huan, numei, Galili gam akipana a kianga hongten a jui jel ua, han leh a luang sialdan a mu uh hi.Huan, a pai nawn ua, banghiam gim namtui khawng leh thau namtui khawng a bawl uhi.
55Wale wanawake walioandamana na Yesu kutoka Galilaya walimfuata Yosefu, wakaliona lile kaburi na jinsi mwili wake Yesu ulivyowekwa
56Huan, a pai nawn ua, banghiam gim namtui khawng leh thau namtui khawng a bawl uhi.
56Halafu, walirudi nyumbani, wakatayarisha manukato na marashi kuyapaka mwili wa Yesu. Siku ya Sabato walipumzika kama ilivyoamriwa na sheria.