1Huan, ni bangzah hiam nungin Kapernaum khuaa a honglut nawn leh, in ah a om chih thu a hongthangta a.
1Baada ya siku kadhaa, Yesu alirudi Kafarnaumu, watu wakapata habari kwamba alikuwa nyumbani.
2Huchiin, kongkhak kim a leng omna ding himhim omlou khop hialin mi tampi a hongkhawmta ua; huan a kiang uah thu a genta a.
2Basi, wakaja watu wengi sana hata nafasi yoyote ikakosekana mlangoni. Yesu alikuwa akiwahubiria ujumbe wake,
3Huan, mijaw khat, mi li jawn, a kiangah a honpi ua.
3wakati mtu mmoja aliyepooza alipoletwa kwake akiwa amechukuliwa na watu wanne.
4Huan, mipi jiaka a kiang naia a hongtheih louh jiakun a omna in tung uh a hong ua; huan, a laihong khit un a a lupna tuh a tunga mijaw lum kawmin a khai khe suk ua.
4Kwa sababu ya huo umati wa watu, hawakuweza kumpeleka karibu na Yesu. Basi, wakatoboa sehemu ya dari iliyokuwa juu ya mahali alipokuwa Yesu. Walipokwisha pata nafasi, wakamteremsha huyo mtu akiwa amelala juu ya mkeka.
5Huchiin, Jesun a gin dan uh a na muhin, mijaw kiangah, Ka ta, na khelhnate ngaihdam a hita, a chi a.
5Yesu alipoona imani yao, akamwambia huyo mtu aliyepooza, "Mwanangu, umesamehewa dhambi zako."
6Huan, laigelhmi khenkhatte huai laiah a tu ua.
6Baadhi ya walimu wa Sheria waliokuwa wameketi hapo wakawaza mioyoni mwao,
7Hiai min bangdia hichi bang thu gen ahia? Pathian a gnsia hi; mi khat, Pathian kia loungal, kuan ahia khelhnate ngaidam thei? chiin, a lungtang un a ngaihtuah ua.
7"Anathubutuje kusema hivyo? Anamkufuru Mungu! Hakuna mtu awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake."
8Huan, Jesun, a lungtang un huchibangin a ngaihtuah uh chih a lungsimin ana thei paha, a king uah, Huai thu bang dia na lungtang ua ngaihtuah na hi ua?
8Yesu alitambua mara mawazo yao, akawaambia, "Mbona mnawaza hivyo mioyoni mwenu?
9Mijaw kiangah, Na khelhnate ngaihdam a hita, chih leh, Na lupna la inla, kein paita in, chih a koi ahia a gen nuam jaw?
9Ni lipi lililo rahisi zaidi: kumwambia mtu huyu aliyepooza, Umesamehewa dhambi zako, au kumwambia, Inuka! Chukua mkeka wako utembee?
10Abang abang hileh, leitung ah Mihing Tapain khelhnate ngaihdam theihna a nei chih na theihna dingun, mijaw kiang ah
10Basi, nataka mjue kwamba Mwana wa Mtu anayo mamlaka ya kuwasamehe watu dhambi duniani." Hapo akamwambia huyo mtu aliyepooza,
11Thou inla, na lupna la inla, na in ah pai in, ka honchi, a chi a.
11"Nakwambia simama, chukua mkeka wako uende nyumbani!"
12Huchiin amah tuh a thou, a lupna a la paha, a vek ua mitmuhin a pai kheta a; huchiin a vek un lamdang a sa mahmah uh, Hichi bang himhim i mu ngei kei, chiin, Pathian a phat uh.
12Mara, watu wote wakiwa wanamtazama, huyo mtu akainuka, akauchukua mkeka wake, akaenda zake. Watu wote wakashangaa na kumtukuza Mungu wakisema, "Hatujapata kamwe kuona jambo kama hili."
13Huan, a awt nawna dil geiah a paita a, huan, mipi tengteng a kiangah a vahoh ua, thu a nahilha.
13Yesu alikwenda tena kando ya ziwa. Umati wa watu ukamwendea, naye akaanza kuwafundisha.
14Huan, a pai kawmin, Levi, Alphai tapa,. siahpiakna muna tu a mu a, a kingah, Honjui in, a chi a. Huan a thu a a juita a.
14Alipokuwa akipita, akamwona Lawi mwana wa Alfayo, ameketi katika ofisi ya ushuru. Yesu akamwambia, "Nifuate!" Lawi akasimama, akamfuata.
15Huan, hichi ahi a, Jesun Levi in ah an a um a, siahkhonmite leh mi khialte tampiiin Jesu leh a nungjuite tuh a umpih chiat ua, amah juite tampi ahi ngal ua.
15Baadaye, Yesu alikuwa amekaa mezani, nyumbani kwa Lawi, kula chakula. Watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wamemfuata Yesu na wengi wao wakawa wamekaa mezani pamoja naye na wanafunzi wake.
16Huan, Pahrisaite laka laigelhmiten Jesun mi khialte leh siahkhonmite kianga a nek a muh un, a nungjuite kingah, Bang chi dan ahia siahkhonmite leh mi khialte kainga a neka a dawn? a chi ua.
16Basi, baadhi ya walimu wa Sheria ambao walikuwa Mafarisayo walipomwona Yesu akila pamoja na watu wenye dhambi na watoza ushuru, wakawauliza wanafunzi wake, "Kwa nini anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?"
17Huan, Jesun huai a ja a, a kiang uah, Mi hatten daktor a kiphamoh kei ua, mi damlouten a kiphamoh jaw uh; mi diktatte sam dinga hong ka hi keia, mi khialte sam dinga hong ka hi keia, mi khialte sam dinga hong ka hi jaw, a chi a.
17Yesu alipowasikia, akawaambia, "Watu wenye afya hawahitaji daktari; wanaomhitaji ni wale walio wagonjwa. Sikuja kuwaita watu wema, ila wenye dhambi."
18Huan, Johan nungjuite leh Pharisaiten an a ngawl ua; huan mi a hong ua, Jesu kiangah, Bang dia Johan nungjuite leh Pharisaite, nungjuiten an ngawl ua, na nungjuiten a ngolh sam louh uh? a chi ua.
18Wakati mmoja wanafunzi wa Yohane na wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wanafunga. Basi, watu wakaja, wakamwuliza Yesu, "Kwa nini wanafunzi wa Yohane na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?"
19Jesun a kiang uah, Mou pite kianga a pasal ding a om laiteng mou piten an a ngawl thei ua hia? A pasal ding a kiang ua a om laiteng a ngawl theikei ding uh.
19Yesu akajibu, "Walioalikwa harusini wanawezaje kufunga kama bwana harusi yupo pamoja nao? Wakati wote wawapo pamoja na bwana harusi hawawezi kufunga.
20Himahleh, a pasal ding a kiang ua kipana pi mang nite a hongtung dinga, huai ni chiangin jaw a ngawl ding uh.
20Lakini wakati utafika ambapo bwana harusi ataondolewa kati yao; wakati huo ndipo watakapofunga.
21Kuamahin puan lui puan tuikhai nai louh themin a thuap ngei kei uh; thuap le uh, a thuap bit na dingin a kai kek dinga, a thakin a lui a kai kek dinga, a hongkek semsem ding.
21"Hakuna mtu anayekata kiraka kutoka katika nguo mpya na kukishonea katika nguo kuukuu. Kama akifanya hivyo, hicho kiraka kipya kitararuka kutoka hilo vazi kuukuu, nalo litaharibika zaidi.
22Huan, kuamah-in uain thak, savun uain thawl lui ah a thun ngei kei uh; thun le uh, uain in savun thawl a phu kham dinga, uain a mangthang ding, savun thawl mah leng; uain thak tuh savun uain thawl thak ah a thun zonak uh, a chi a.
22Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai itavipasua hivyo viriba, nayo divai pamoja na hivyo viriba vitaharibika. Divai mpya hutiwa katika viriba vipya!"
23Huan, hichia hi a, Jesu tuh Khawl niin buh lei khawngah a pai suaka, huan a nungjuiten a pai kawm un buhvuite a khiakta ua.
23Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano. Walipokuwa wanatembea, wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano.
24Huan, Pharisaiten, a kiang ah, En dih, bang dia Khawlni a hihsianglou hih ahi ua? a chi ua.
24Mafarisayo wakawaambia, "Tazama! Kwa nini wanafanya jambo ambalo si halali kufanya wakati wa Sabato?"
25Huan, aman tuh a kiang uah, David leh a lawmte a taksap ua a gilkial lai ua a thil hih uh na sim kei ua hia
25Yesu akawajibu, "Je, hamjapata kusoma juu ya kile alichofanya Daudi wakati alipohitaji chakula? Yeye pamoja na wenzake waliona njaa,
26Huchia Abiathar Siampu Lianpen a hih laia, Pathian in a a luta, siampute kia loungalin a nek sianglouh tanghoukoih a neka, a lawmte kianga a paik sam thu, a chi a.
26naye akaingia ndani ya Nyumba ya Mungu, akala ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu. Jambo hili lilifanyika wakati Abiathari alikuwa Kuhani Mkuu. Na ni makuhani tu peke yao waliokuwa wameruhusiwa kula mikate hiyo. Lakini Daudi aliila, tena akawapa na wenzake."
27Huan, amah mahin, a kiang uah, Khawlni jaw mihing a dia bawl ahi, mihing bel Khawlni adia bawl ahi kei.Huchiin Mihing Tapa jaw Khawlni tungah nangawn Toupa ahi, a chi a.
27Basi, Yesu akawaambia, "Sabato iliwekwa kwa ajili ya binadamu na si binadamu kwa ajili ya Sabato!
28Huchiin Mihing Tapa jaw Khawlni tungah nangawn Toupa ahi, a chi a.
28Kwa hiyo, Mwana wa Mtu ni Bwana hata wa Sabato."