1Huan Sardi khuaa saptuamte angel kiangah hichi bangin gelh in: Pathian Kha sagih leh aksi sagih neipan hiai thilte a gen hi: Na thilhihte ka thei, si napiin hing min na pua.
1"Kwa malaika wa kanisa la Sarde andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye na roho saba za Mungu na nyota saba. Nayajua mambo yako yote; najua unajulikana kuwa na uhai kumbe umekufa!
2Kivengin, thil om sunte, si dia kisate, tungding nawn in; ka Pathian maah na thilhihte bangmah zohsa himhim ka mu kei hi.
2Amka! Imarisha chochote chema kilichokubakia kabla nacho hakijatoweka kabisa. Maana, mpaka sasa, sijayaona matendo yako kuwa ni makamilifu mbele ya Mungu wangu.
3Huaijiakin, na muhdan leh na jakdan thei gige in; kem inla, kisik in. Huchia na kiven keileh, guta bangin ka hongpai dia, bangchik hunin ahia nang kon phawn ding chih na theikei ding.
3Kumbuka, basi, yale uliyofundishwa na jinsi ulivyoyasikia, uyatii na ubadili nia yako mbaya. Usipokesha nitakujia ghafla kama mwizi, na wala hutaijua saa nitakapokujia.
4Himahleh, Sardi khua ah min tawm chik, apuante uh nin sak lou na neia; amau tuh puan ngou silhin kei toh ka vak khawm ding uh, huchi kilawm him a hih jiak un.
4Lakini wako wachache huko Sarde ambao hawakuyachafua mavazi yao. Hao wanastahili kutembea pamoja nami wakiwa wamevaa mavazi meupe.
5A vualzoupa tuh, huchibangin puan ngou-in a kijem dia, huan bangchi mahin hinna laibu akipat a min ka hihmang kei ding, huan ka Pa ma leh angelte maah a min ka pauhial ding.
5"Wale wanaoshinda, watavikwa mavazi meupe kama hao. Nami sitayafuta majina yao kutoka katika kitabu cha uzima; tena nitawakiri kwamba ni wangu mbele ya Baba yangu na mbele ya malaika wake.
6Saptuam kiang Kha thugen tuh bil nei peuhin ja uhen, a chi, chiin.
6"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
7Philadelphia khuaa saptuamte angel kiangah kichi bangin gelh in; Huai siangthoupa, huai dikpa, huai David tahbi neipa, huai hon tuh kuamahin a khak theih louhpa leh huai khak tuh kuamahin a hon theih louhpan hiai thilte a gen hi:
7"Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
8Na thilhihte ka thei, ngai in, na maah kuamah khak theih louh kong honsain ka koih; huan thilhihtheihna neuchik na neia, huan ka thu na kemta a, huan ka min na pai keia.
8Nayajua mambo yako yote! Sasa, nimefungua mbele yako mlango ambao hakuna mtu awezaye kuufunga; najua kwamba ingawa huna nguvu sana, hata hivyo, umezishika amri zangu, umelitii neno langu wala hukulikana jina langu.
9Ngaiin, juau lel gena, hi lou napia, huai Judate hia kigente, Setan omkhawmnaa te tuh ka honpia hi, ngaiin, amau ka honpai sak dia, na khe bul ah ka kun sak ding, kon itdan a theihna ding un.
9Sikiliza! Nitawapeleka kwako watu wa kundi lake Shetani, watu ambao hujisema kuwa ni Wayahudi, kumbe ni wadanganyifu. Naam, nitawapeleka kwako na kuwafanya wapige magoti mbele yako wapate kujua kwamba kweli nakupenda wewe.
10Ka dohzohna thu na kep jiakin, zeeta na om chiangin ken leng ka honkem ding, huai hun tuh khovel pumpi tunga hongtung ding ahi, leitunga teng tengteng leng zeet dingin.
10Kwa kuwa wewe umezingatia agizo langu la kuwa na uvumilivu, nami pia nitakutegemeza salama wakati ule wa dhiki inayoujia ulimwengu mzima kuwajaribu wote wanaoishi duniani.
11Ka hong pai pah dia: kuamah in na lallukhu a lak louh na dingin, na neihpen tuh kem kinken in.
11Naja kwako upesi! Linda, basi, ulicho nacho sasa, ili usije ukanyang'anywa na mtu yeyote taji yako ya ushindi.
12A vual zoupa tuh, ka Pathian biakin ah khuamin ka pang sak dia, huan huaiah kipanin a pai khe nawn kei ding, amah tungah tuh ka Pathian min bang, ka Pathian khopi Jerusalem thak, ka Pathian akipana vana hongpai khe suk in bang leh, keimah min thak bang ka gelh ding.
12"Wale wanaoshinda nitawafanya wawe minara katika Hekalu la Mungu wangu, na hawatatoka humo kamwe. Pia nitaandika juu yao jina la Mungu wangu na jina la mji wa Mungu wangu, yaani Yerusalemu mpya, mji ambao utashuka kutoka juu mbinguni kwa Mungu wangu. Tena nitaandika juu yao jina langu jipya.
13Saptuamte kianga Kha thugen tuh bil nei peihin ja uhen, a chi, chiin.
13"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!
14Huan Leodisia khuaa saptuamte angel kiangah hichibangin gelh in: Theihpihpa ginom leh dik, Pathian thilsam bul Amenin hiai thilte a gen:
14"Kwa malaika wa kanisa la Laodikea andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aitwaye Amina. Yeye ni shahidi mwaminifu na wa kweli, ambaye ni chanzo cha viumbe vyote alivyoumba Mungu.
15Na thilhihte ka thei, lum la lum lou vot la vot louin na om a: na lum leh lum inla, na vot leh vot vanglak lechin!
15Nayajua mambo yako yote! Najua kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungekuwa kimojawapo: baridi au moto.
16Lum la lum lou, vot lah vot lou a, na om pelhpulh jiakin, ka kam akipanin kon se khe ding.
16Basi, kwa kuwa hali yako ni vuguvugu, si baridi wala si moto, nitakutapika!
17Mi genthei nuamsa lou, jawng, mitdel leh vuaktang na hihlam kithei loua, ka hausa, hausaknate ka neita, bangmah ka kitasam kei na chih jiakin:
17Wewe unajisema, Mimi ni tajiri; ninajitosheleza, sina haja ya kitu chochote. Kumbe, hujui kwamba wewe ni mnyonge, unahitaji kuhurumiwa, maskini, kipofu tena uko uchi!
18Kei akipatin dangkaeng meia hihsiangthou lei dingin kon thuhilh, na honghauhsak theihna dingin; puan ngoute bang na honsilha, na vuaktang zumhuaina a dawk louhna ding in; huan na muh theihna dingin na mita nuh ding mitlou leng leiin.
18Nakushauri ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto upate kuwa tajiri kweli. Tena afadhali ununue pia vazi jeupe, uvae na kufunika aibu ya uchi wako. Nunua pia mafuta ukapake machoni pako upate kuona.
19Ka itte tuh ka thuhilhin, ka sawia; huai jiakin phatuamngai inla, kisik in.
19Mimi ndiye mwenye kumwonya na kumrudi yeyote ninayempenda. Kwa hiyo kaza moyo, achana na dhambi zako.
20Ngaiin, kongkhaka dingin ka kiu hi: min ka aw a jaka kong a hon leh, a kiangah ka lut dia amah toh nitakan ka ne dia, aman leng kei toh a ne ding.
20Sikiliza! Mimi nasimama mlangoni na kubisha hodi. Mtu akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia nyumbani kwake na kula chakula pamoja naye, naye atakula pamoja nami.
21A vualzoupa tuh ka laltutphah tungah ka kiangah ka tu sak ding, kei leng ka vualzou a, laltutphah tunga ka Pa toh ka tut bangin.Saptuamte kianga Kha thugen tuh bil nei peuhin ja uhen, a chi, chiin, a chi.
21"Wale wanaoshinda nitawaketisha pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi mwenyewe nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
22Saptuamte kianga Kha thugen tuh bil nei peuhin ja uhen, a chi, chiin, a chi.
22"Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!"