Paite

Swahili: New Testament

Romans

8

1Huaijiakin, tun jaw Kris Jesu a omte adingin, siamlouh tansakna himhim a omta kei hi.
1Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
2Kris Jesu a Hinna Kha dan in khelhna leh sihna dan akipan honsuakta sakta ngala.
2Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
3Sa jiaka dan a hat louh a, ahihtheih vual louh tuh, Pathianin, amah Tapa ngei, khelhna sa gilou bang puin, khelhna thoihna dia honsawlin, sa a khelhna om tuh siamlouh a tangsakta ahi,
3Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
4Sa dan juilou a Kha dan jui zote eimaha danin a ngiat diktatna tuh tangtuna a om theihna dingin.
4Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
5Sa dana omten sa lam thilte a lunggulh nak uh; Kha dana omten bel Kha lam thilte a lunggulh nak uhi.
5Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
6Sa lam thilte deih jaw sihna ahi ngala, Kha lam thil deih bel hinna leh khamuanna ahi;
6Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
7Sa deihdan jaw Pathian douna a hih jiakin. Huai tuh Pathian danin a om ngal keia, om leng a om theikei himhim ahi.
7Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
8Huchiin, saa omten Pathian a kipaksak theikei uh.
8Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9Himahleh, Pathian Kha noumaua a om taktak leh, saa om na hi kei ua, Khaa om na hi jaw uhi. Ahihhangin kuapeuh Kris Kha neilou jaw amaha ahi kei.
9Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
10Kris noumaua om ngal leh, khelhna jiakin pumpi a si ahi; kha tuh dikna jiakin a hing ahi.
10Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
11Himahleh misi laka kipan Jesu kaithou nawnpa Kha nou maua a om leh, misi laka kipan Kris Jesu kaithou nawnpan, noumaua om a Kha pansanin na pumpi sitheite uh a hihhing sam ding hi.
11Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12Huaijiakin, unaute aw, bat i nei; sa dana om dingin sa lakah bel ahi kei;
12Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
13Sa dana na om u leh, na si mahmah ding uhi; ahihhangin pumpi thilhihte Kha a na hihlup jel u leh na hing ding uhi.
13Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
14Pathian Kha pia om peuhmah te jaw, Pathian tate ahi ngal ua.
14Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
15Laua om nawn dingin sikha hihna kha na tang uh ahi ngal keia; ta hihna kha na tang uh ahi jaw. Abba! Pa! chia, i kikou chiangin,
15Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, "Aba," yaani "Baba!"
16Kha mahmahin, eimah kha toh, Pathian tate i hi chih hontheisak hi;
16Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
17Huan, tate i hih leh, gou luahpihte i hi hi; Pathian gouluahte, Kris luahpihte i hi a; a kianga pahtawia i om sam theihna dinga amah i thuakpih taktak leh.
17Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
18Tulai a thuaknate peuh denchianga i tunga thupina hihlat ding toh tehpihthamin kasep kei.
18Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19Thilsiam tengteng ten, lamen mahmah in, Pathian tate honglatna a ngaklah mahmah ngal ua.
19Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
20Thilsiam tengtengte thil thulimlou thuthua om sakin a omta uh; a ut ua om ahi kei ua, lametnaa a omsakpa jiak ahi jaw hi;
20Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
21Thilsiam tengteng leng siatna sikhaa kipan suahtaksakin a om ding ua, Pathian tate noplenna thupia lut ding ahi ngal ua.
21maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
22Thilsiam tengteng tu tanin thum leh nauveina thuakin a om uh chih i thei ngal ua.
22Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
23Thilsiamte kia hilou-in, eite ngei, Kha gahmasa tengte leng, ta hihna kilatna, i pumpi tatna ngakin i lungsimin i mau sam ngal ua.
23Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
24Hiai lametnaa hotdam i hi ngal ua. Himahleh muh theih gige lametna jaw lametna ahi kei. Kuan a muh theih gige a lamena?
24Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
25I muh louhpen i lamet lebel i ngak teitei hi.
25Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
26Huchimahbangin, Khain i hatlouhna ah hon huh jel; bangchia thum ding ahia chih i thei ngal kei ua; himahleh Khain mauna gen vuallouhin honthum sak jel hi.
26Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
27Huan, Pathian deihlam bang jelin misiangthoute a thum sak jel jiakin, lungtang Enpan Kha deihlam a thei jel ahi.
27Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
28Huan, Pathian itte, aman a seh banga a sapte adin, a hoihna ding un bangkimin a sep sak chiat chih i thei hi:
28Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
29A theih kholhte amah Tapa bang taka om dingin a sep khol ngala, a Tapa tuh unau tampite laka ta masapen a honghih theihna dingin.
29Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30Huan, a seh kholhte tuh a sam laia; huan a sapte tuh siam a tangsak laia; huan, siam a tansakte tuh a pahtawi lai hi.
30Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
31Huai thu ah bang i gen dia leh? Pathian ei lama a pan leh kuan ahia hondou thei ding?
31Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
32Amah Tapa ngei leng hawi loua, i vek ua dinga pepan thil tengteng leng a thawnin a honpe tawk kei dia hia?
32Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
33Pathian mi telte kuan ahia hek ding? Siamtangsakpapen Pathian ahi ngala.
33Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
34Kuan ahia siamlouh tangsak ding? Si pen Kris Jesu ahi ngala; ahi, thou nawn zotaa, Pathian taklama oma hon-gensakpa ahi.
34Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
35Kris itna akipan kuan ahia honkhen ding? Gimthuaknain hia, lungngaihnain hia, sawina in hia, tamin hia, vuaktanna in hia, lauhhuaina in hia, temsauin hia honkhen ding?
35Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
36Nangmah jiakin ni tumin thahin ka om uh; belam goh dingte banga sim ka hi uh, chih gelh bangin.
36Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa."
37Khen lou hial ding, huaite tengtengah, honitna jiakin, vualtungtuangte sanga tungtuang jaw i hi hi.
37Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
38Sihna hiam, hinna hiam, angelten hiam. Lalnate hiam. Thilomlelte hiam, thilhongomdingte hiam, thilhihtheihna hiam,Sanna hiam, thukna hiam, thilsiam dangte himhim hiamin leng, i Toupa Kris Jesua om Pathian itna akipan, honkhen theikei ding chih diktakin ka thei ngala.
38Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
39Sanna hiam, thukna hiam, thilsiam dangte himhim hiamin leng, i Toupa Kris Jesua om Pathian itna akipan, honkhen theikei ding chih diktakin ka thei ngala.
39Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.