1Bądźcie naśladowcami moimi, jakom i ja Chrystusowy;
1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
2A chwalę was, bracia! iż pamiętacie wszystkie moje nauki, a jakom wam podał, podania trzymacie.
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
3A chcę, abyście wiedzieli, iż każdego męża głową jest Chrystus, a głową niewiasty mąż, a głową Chrystusową Bóg.
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
4Każdy mąż, gdy się modli albo prorokuje z przykrytą głową, szpeci głowę swoję.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
5I każda niewiasta, gdy się modli albo prorokuje, nie nakrywszy głowy swojej, szpeci głowę swoję; boć to jedno, a toż samo jest, jakoby ogolona była.
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
6Albowiem jeźli się nie nakrywa niewiasta, niechże się też strzyże; a jeźli szpetna rzecz jest niewieście, strzyc się albo golić, niechże się nakrywa.
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
7Albowiem mąż nie ma nakrywać głowy, gdyż jest wyobrażeniem i chwałą Bożą; ale niewiasta jest chwałą mężową.
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
8Bo mąż nie jest z niewiasty, ale niewiasta z męża.
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
9Albowiem mąż nie jest stworzony dla niewiasty, ale niewiasta dla męża.
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
10A przetoż niewiasta powinna mieć władzę na głowie dla Aniołów.
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
11A wszakże mąż nie jest bez niewiasty, ani niewiasta nie jest bez męża w Panu.
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
12Albowiem jako niewiasta z męża jest, tak też mąż przez niewiastę; jednak wszystkie rzeczy są z Boga.
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
13Sami u siebie rozsądźcie, przystoili niewieście bez nakrycia modlić się Bogu?
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
14Azaż was i samo przyrodzenie nie uczy, iż mężowi, gdyby włosy zapuszczał, jest mu ku zelżywości?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
15Ale niewiasta, jeźli zapuszcza włosy, jest jej ku poczciwości, przeto iż jej włosy dane są za przykrycie.
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
16A jeźliby się kto zdał być swarliwym, my takiego obyczaju nie mamy, ani zbory Boże.
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
17A to opowiadając nie chwalę, że się nie ku lepszemu, ale ku gorszemu schodzicie.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
18Albowiem najprzód, gdy się wy schodzicie we zborze, słyszę, iż rozerwania bywają między wami, i poniekąd wierzę.
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
19Bo muszą być kacerstwa między wami, aby ci, którzy są doświadczeni, byli jawnymi między wami.
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
20Gdy się wy tedy wespół schodzicie, nie jest to używać wieczerzy Paóskiej.
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
21Albowiem każdy wieczerzę swoję pierwej zjada i jeden łaknie, a drugi jest pijany.
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
22Azaż domów nie macie do jedzenia i do picia? Albo zborem Bożym gardzicie i zawstydzacie tych, którzy nie mają? Cóż wam rzekę? Pochwalęż was? W tem nie chwalę.
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
23Albowiem jam wziął od Pana, com też wam podał, iż Pan Jezus tej nocy, której był wydan, wziął chleb,
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
24A podziękowawszy, złamał i rzekł: Bierzcie, jedzcie; to jest ciało moje, które za was bywa łamane; to czyócie na pamiątkę moję.
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
25Także i kielich, gdy było po wieczerzy mówiąc: Ten kielich jest nowy testament we krwi mojej; to czyócie, ilekroć pić będziecie, na pamiątkę moję
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
26Albowiem ilekroć byście jedli ten chleb i ten kielich byście pili, śmierć Paóską opowiadajcie, ażby przyszedł.
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
27A tak, kto by jadł ten chleb, albo pił ten kielich Paóski niegodnie, będzie winien ciała i krwi Paóskiej.
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
28Niechże tedy człowiek samego siebie doświadczy, a tak niech je z chleba tego i z kielicha tego niechaj pije.
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
29Albowiem kto je i pije niegodnie, sąd sobie samemu je i pije, nie rozsądzając ciała Paóskiego.
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
30Dlatego między wami wiele jest słabych i chorych, i niemało ich zasnęło.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
31Bo gdybyśmy się sami rozsądzali, nie bylibyśmy sądzeni.
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
32Lecz gdy sądzeni bywamy, od Pana bywamy ćwiczeni, abyśmy z światem nie byli potępieni.
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
33Ale tak, bracia moi! gdy się schodzicie ku jedzeniu, oczekiwajcie jedni drugich.
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
34A jeźli kto łaknie, niechże je w domu, abyście się na sąd nie schodzili. A inne rzeczy, gdy przyjdę, postanowię.
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.