1Przeto nie mogąc dłużej znosić, upodobało się nam, abyśmy sami w Atenach zostali.
1Mwishowe hatukuweza kuvumilia zaidi. Basi, tuliamua kubaki kule Athene peke yetu,
2I posłaliśmy Tymoteusza, brata naszego i sługę Bożego, i pomocnika naszego w Ewangielii Chrystusowej, aby was utwierdził i napominał z strony wiary waszej.
2na kumtuma kwenu ndugu yetu Timotheo, ambaye ni mfanyakazi mwenzetu kwa ajili ya Mungu katika kuhubiri Habari Njema ya Kristo. Tulimtuma ili awaimarisheni na kuwafarijini,
3Aby się żaden nie poruszał w tych uciskach; gdyż sami wiecie, żeśmy na to wystawieni.
3kusudi imani ya mtu yeyote miongoni mwenu isije ikafifia kwa sababu ya taabu hizo. Ninyi mnajua kwamba tunapaswa kupata mateso.
4Albowiem gdyśmy byli u was, opowiadaliśmy wam, żeśmy mieli być uciśnieni, jakoż się też to stało, i wiecie o tem.
4Maana, tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwaambieni kwamba tutateswa; na kama mjuavyo ndivyo ilivyotukia.
5Dlatego i ja, nie mogąc tego dłużej znosić, posłałem go, abym się dowiedział o wierze waszej, by was snać nie kusił ten, co kusi, a nie była daremna praca nasza.
5Ndio maana nilimtuma Timotheo kwenu. Sikuweza kungoja zaidi, na hivyo nilimtuma nipate habari za imani yenu. Isije ikawa labda Mshawishi aliwajaribuni na kazi yote tuliyofanya miongoni mwenu imepotea bure!
6Lecz teraz Tymoteusz od was do nas przyszedł i zwiastował nam wesołą nowinę o wierze i miłości waszej, a iż nas zawsze dobrze wspominacie, żądając nas widzieć, tak jako i my was.
6Sasa Timotheo amekwisha rudi, naye ametupa habari za kufurahisha kuhusu imani na upendo wenu. Ametuarifu kwamba mnatukumbuka daima, na kwamba mna hamu ya kutuona sisi kama nasi tulivyo na hamu ya kuwaoneni.
7Dlatego pocieszeni jesteśmy, bracia! z was w każdym utrapieniu i potrzebie naszej przez wiarę waszę;
7Basi, habari za imani yenu zimetutia moyo katika taabu na mateso yetu yote,
8Bo teraz my żyjemy, jeźli wy stoicie w Panu.
8kwani sasa tunaishi kweli ikiwa ninyi mnasimama imara katika kuungana na Bwana.
9Albowiem jakież dziękowanie możemy Bogu oddać za was za wszelkie wesele, którem się weselimy dla was przed Bogiem naszym?
9Sasa twaweza kumshukuru Mungu wetu kwa ajili yenu. Tunamshukuru kwa furaha tuliyo nayo mbele yake kwa sababu yenu.
10W nocy i we dnie bardzo się gorliwie modląc, abyśmy oglądali oblicze wasze i dopełnili niedostatków wiary waszej.
10Tunazidi kumwomba Mungu usiku na mchana kwa moyo wetu wote ili atupatie fursa ya kuwaoneni uso kwa uso ili tuweze kurekebisha chochote kilichopungua katika imani yenu.
11Lecz sam Bóg i Ojciec nasz, i Pan nasz, Jezus Chrystus, niech wyprostuje drogę naszę do was;
11Tunamwomba Mungu, Baba yetu mwenyewe, na Bwana wetu Yesu atutayarishie njia ya kuja kwenu.
12A was Pan niech pomnoży i obfitującymi uczyni w miłości jednego ku drugiemu, i ku wszystkim, jako i nas ku wam,
12Bwana awawezeshe ninyi kupendana na kuwapenda watu wote zaidi na zaidi, kama vile sisi tunavyowapenda ninyi.
13Aby utwierdzone były serca wasze nienaganione w świętobliwości przed Bogiem i Ojcem naszym, na przyjście Pana naszego, Jezusa Chrystusa, ze wszystkimi świętymi jego.
13Hivyo ataiimarisha mioyo yenu, nanyi mtakuwa wakamilifu na watakatifu mbele ya Mungu na Baba yetu wakati Bwana wetu Yesu atakapokuja pamoja na wote walio wake.