Polish

Swahili: New Testament

Romans

6

1Cóż tedy rzeczemy? Zostaniemyż w grzechu, aby łaska obfitowała?
1Tuseme nini basi? Je, twendelee kubaki katika dhambi ili neema ya Mungu iongezeke?
2Nie daj tego Boże! albowiem którzyśmy umarli grzechowi, jakoż jeszcze w nim żyć będziemy?
2Hata kidogo! Kuhusu dhambi sisi tumekufa--tutaendeleaje kuishi tena katika dhambi?
3Azaż nie wiecie, iż którzykolwiek ochrzczeni jesteśmy w Chrystusa Jezusa, w śmierć jego ochrzczeni jesteśmy?
3Maana, mnajua kwamba sisi tuliobatizwa tukaungana na Kristo Yesu, tulibatizwa na kuungana na kifo chake.
4Pogrzebieniśmy tedy z nim przez chrzest w śmierć, aby jako Chrystus wzbudzony jest z martwych przez chwałę ojcowską, tak żebyśmy i my w nowości żywota chodzili.
4Tulipobatizwa tuliungana na kifo chake, tukazikwa pamoja naye, ili kama vile Kristo alivyofufuliwa kutoka wafu kwa kitendo kitukufu cha Baba, sisi pia tuweze kuishi maisha mapya.
5Bo jeźliżeśmy z nim wszczepieni w podobieóstwo śmierci jego, tedy też i w podobieóstwo zmartwychwstania wszczepieni z nim będziemy.
5Maana, kama sisi tumeungana naye katika kufa kama yeye, vivyo hivyo tutaungana naye kwa kufufuliwa kutoka wafu kama yeye.
6To wiedząc, że stary nasz człowiek pospołu jest z nim ukrzyżowany, aby ciało grzechu było zniszczone, żebyśmy już więcej nie służyli grzechowi;
6Tunajua kwamba utu wetu wa kale ulisulubiwa pamoja na Kristo, ili hali ya dhambi iharibiwe, tusiwe tena watumwa wa dhambi.
7Bo ktoć umarł, usprawiedliwiony jest od grzechu.
7Kwa maana, mtu aliyekufa, amenasuliwa kutoka katika nguvu ya dhambi.
8Jeźliśmy tedy z Chrystusem umarli, wierzymy, iż też z nim żyć będziemy,
8Basi, ikiwa tumekufa pamoja na Kristo, tunaamini kwamba tutaishi pia pamoja naye.
9Wiedząc, że Chrystus powstawszy z martwych, więcej nie umiera i śmierć mu więcej nie panuje.
9Maana, tunajua kwamba Kristo amekwisha fufuliwa kutoka wafu na hafi tena; kifo hakimtawali tena.
10Bo iż umarł, grzechowi raz umarł, a iż żyje, żyje Bogu.
10Hivyo, kwa kuwa alikufa--mara moja tu--dhambi haina nguvu tena juu yake; na sasa anaishi maisha yake katika umoja na Mungu.
11Tak też i wy rozumiejcie, żeście wy umarłymi grzechowi, aleście żywymi Bogu w Chrystusie Jezusie, Panu naszym.
11Hali kadhalika nanyi lazima mjione kuwa mmekufa kuhusu dhambi, lakini kama mnaoishi katika umoja na Mungu kwa njia ya Kristo Yesu.
12Niechże tedy nie króluje grzech w śmiertelnem ciele waszem, żebyście mu posłuszni byli w pożądliwościach jego.
12Kwa hiyo, dhambi isiitawale tena miili yenu ambayo hufa, na hivyo kuzitii tamaa zake.
13Ani stawiajcie członków waszych orężem niesprawiedliwości grzechowi: ale stawiajcie siebie samych Bogu, jako z umarłych żywi, i członki wasze orężem sprawiedliwości Bogu.
13Wala msitoe hata sehemu moja ya miili yenu iwe chombo cha kutenda uovu na dhambi. Badala yake, jitoleeni ninyi wenyewe kwa Mungu kama watu waliofufuliwa kutoka wafu; toeni nafsi zenu zote kwa Mungu kwa ajili ya uadilifu.
14Albowiem grzech panować nad wami nie będzie; bo jesteście nie pod zakonem, ale pod łaską.
14Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
15Cóż tedy? Będziemyż grzeszyli, żeśmy nie pod zakonem, ale pod łaską? Nie daj tego Boże!
15Basi, tuseme nini? Je, tutende dhambi ati kwa sababu hatuko chini ya Sheria bali chini ya neema? Hata kidogo!
16Azaż nie wiecie, że komu się stawiacie za sługi ku posłuszeóstwu, tegoście sługami, komuście posłuszni; bądź grzechowi ku śmierci, bądź posłuszeóstwu ku sprawiedliwości?
16Mnajua kwamba mkijitolea ninyi wenyewe kama watumwa na kumtii fulani, mnakuwa kweli watumwa wake mtu huyo--au watumwa wa dhambi, na matokeo yake ni kifo, au wa utii, na matokeo yake ni kukubaliwa kuwa waadilifu.
17Ale chwała Bogu, że bywszy sługami grzechu, usłuchaliście z serca sposobu onej nauki, którejście się poddali.
17Ingawa mlikuwa watumwa wa dhambi zamani, sasa lakini--namshukuru Mungu--mmetii kwa moyo wote yale maazimio na mafundisho mliyopokea.
18A będąc uwolnieni od grzechu, staliście się niewolnikami sprawiedliwości.
18Mlikombolewa kutoka utumwa wa dhambi, mkawa watumwa wa uadilifu.
19Po ludzku mówię dla mdłości ciała waszego. Albowiem jakoście stawiali członki wasze na służbę nieczystości i nieprawości ku czynieniu nieprawości: tak teraz stawiajcie członki wasze na służbę sprawiedliwości ku poświęceniu.
19(Hapa natumia lugha ya kawaida ya watu kwa sababu ya udhaifu wenu wenyewe.) Kama vile wakati fulani mlivyojitolea ninyi wenyewe kutumikia uchafu na uhalifu kwa ajili ya uovu, vivyo hivyo sasa jitoleeni nafsi zenu wenyewe kutumikia uadilifu kwa ajili ya utakatifu.
20Bo pókiście byli sługami grzechu, byliście wolnymi od sprawiedliwości:
20Mlipokuwa watumwa wa dhambi, mlikuwa huru mbali na uadilifu.
21Jakiżeście tedy naonczas pożytek mieli onych rzeczy, za które się teraz wstydzicie? Bo koniec onych jest śmierć.
21Sasa, mlipata faida gani siku zile kutokana na mambo yale ambayo mnayaonea aibu sasa? Maana, matokeo ya mambo haya ni kifo!
22Lecz teraz, będąc uwolnieni od grzechu, a zniewoleni Bogu, macie pożytek swój ku poświęceniu, a koniec żywot wieczny.
22Lakini sasa, mmekwisha kombolewa kutoka utumwa wa dhambi na mmekuwa watumishi wa Mungu; faida mliyo nayo sasa ni utakatifu, na matokeo yake ni uzima wa milele.
23Albowiem zapłata za grzech jest śmierć; ale dar z łaski Bożej jest żywot wieczny, w Chrystusie Jezusie, Panu naszym.
23Kwa maana mshahara wa dhambi ni kifo; lakini zawadi anayotoa Mungu ni uzima wa milele katika kuungana na Kristo Yesu, Bwana wetu.