Polish

Swahili: New Testament

Romans

8

1Przetoż teraz żadnego potępienia nie masz tym, który będąc w Chrystusie Jezusie nie według ciała chodzą, ale według Ducha.
1Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu kwa wale ambao katika maisha yao wameungana na Kristo.
2Albowiem zakon Ducha żywota, który jest w Chrystusie Jezusie, uwolnił mię od zakonu grzechu śmierci.
2Maana, sheria ya Roho iletayo uzima kwa kuungana na Kristo Yesu imenikomboa kutoka katika sheria ya dhambi na kifo.
3Bo co niemożnego było zakonowi, w czem on był słaby dla ciała, Bóg posławszy Syna swego w podobieóstwie grzesznego ciała i dla grzechu, potępił grzech w ciele,
3Mungu ametekeleza jambo lile ambalo Sheria haikuweza kutekeleza kwa sababu ya udhaifu w binadamu. Mungu alimtuma Mwanae akiwa mwenye mwili sawa na miili yetu sisi wenye dhambi, ili aikabili dhambi, na kwa mwili huo akaiangamiza dhambi.
4Aby ona sprawiedliwość zakonu była wypełniona w nas, którzy nie według ciała chodzimy, ale według Ducha.
4Mungu alifanya hivyo kusudi matakwa ya haki ya Sheria yatekelezwe kikamilifu ndani yetu sisi ambao tunaishi, si kwa nguvu za kibinadamu, bali kwa nguvu ya Roho.
5Albowiem, którzy są według ciała, o tem myślą, co jest cielesnego; ale którzy są według Ducha, myślą o tem, co jest duchowego.
5Maana, wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya mwili, hutawaliwa na fikira za mwili. Lakini wale wanaoishi kufuatana na matakwa ya Roho Mtakatifu, hutawaliwa na fikira za Roho.
6Gdyż zmysł ciała jest śmierć; ale zmysł ducha jest żywot i pokój,
6Fikira za mwili huleta kifo; fikira za Roho huleta uzima na amani.
7Przeto iż zmysł ciała jest nieprzyjacielem Bogu; bo się zakonowi Bożemu nie poddaje, gdyż też i nie może.
7Maana, mwenye kutawaliwa na fikira za mwili ni adui wa Mungu; haitii sheria ya Mungu, wala hawezi kuitii.
8Przetoż którzy są w ciele, Bogu się podobać nie mogą.
8Watu wanaotii matakwa ya mwili hawawezi kumpendeza Mungu.
9Lecz wy nie jesteście w ciele, ale w duchu, gdyż Duch Boży mieszka w was: a jeźli kto Ducha Chrystusowego nie ma, ten nie jest jego.
9Lakini ninyi hamuishi kufuatana na matakwa ya mwili, bali kufuatana na matakwa ya Roho, ikiwa Roho wa Mungu anaishi ndani yenu. Yeyote asiye na Roho wa Kristo, huyo si wake Kristo.
10Ale jeźli Chrystus w was jest, tedy ciało jest martwe dla grzechu, a duch jest żywy dla sprawiedliwości.
10Lakini kama Kristo yumo ndani yenu, ingawa miili yenu itakufa kwa sababu ya dhambi, kwenu Roho ndiye uhai kwa sababu mmekubaliwa kuwa waadilifu.
11A jeźli Duch tego, który Jezusa wzbudził z martwych, mieszka w was, ten który wzbudził Chrystusa z martwych, ożywi i śmiertelne ciała wasze przez Ducha swego, który w was mieszka.
11Ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Kristo kutoka wafu anaishi ndani yenu, basi huyo aliyemfufua Kristo kutoka wafu ataipa uzima miili yenu yenye hali ya kufa; atafanya hivyo kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12A tak, bracia! dłużnikami jesteśmy nie ciału, abyśmy według ciała żyli.
12Hivyo basi, ndugu zangu, tunalo jukumu, lakini si la kuishi kufuatana na maumbile ya kibinadamu.
13Albowiem jeźlibyście według ciała żyli, pomrzecie; ale jeźlibyście Duchem sprawy ciała umartwili, żyć będziecie.
13Kwa maana, kama mkiishi kufuatana na matakwa ya maumbile ya kibinadamu, hakika mtakufa. Lakini, kama kwa njia ya Roho mnayaua matendo yenu maovu, basi, mtaishi.
14Bo którzykolwiek Duchem Bożym prowadzeni bywają, ci są synami Bożymi.
14Wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu ni watoto wa Mungu.
15Gdyżeście nie wzięli ducha niewoli znowu ku bojaźni, aleście wzięli Ducha przysposobienia synowskiego, przez którego wołamy: Abba, to jest Ojcze!
15Kwa maana, Roho mliyempokea si Roho mwenye kuwafanya ninyi watumwa na kuwatia tena hofu; sivyo, bali mmempokea Roho mwenye kuwafanya ninyi watoto wa Mungu, na kwa nguvu ya huyo Roho, sisi tunaweza kumwita Mungu, "Aba," yaani "Baba!"
16Tenże duch poświadcza duchowi naszemu, iż jesteśmy dziećmi Bożymi.
16Naye Roho mwenyewe anajiunga na roho zetu na kuthibitisha kwamba sisi ni watoto wa Mungu.
17A jeźliż dziećmi, tedy i dziedzicami, dziedzicami wprawdzie Bożymi, a spółdziedzicami Chrystusowymi, jeźli tylko z nim cierpimy, abyśmy też z nim byli uwielbieni.
17Basi, kwa vile sisi ni watoto wa Mungu, tutapokea baraka zote Mungu alizowawekea watu wake, na tutashiriki urithi huo pamoja na Kristo; maana, tukiyashiriki mateso yake Kristo, tutaushiriki pia utukufu wake.
18Albowiem, (bracia!) mam za to, iż utrapienia teraźniejszego czasu nie są godne onej przyszłej chwały, która się ma objawić w nas.
18Naona kuwa mateso ya wakati huu wa sasa si kitu kamwe kama tukiyafananisha na ule utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19Bo troskliwe wyglądanie stworzenia oczekuje objawienia synów Bożych.
19Viumbe vyote vinatazamia kwa hamu Mungu awadhihirishe watoto wake.
20Gdyż stworzenie marności jest poddane, nie dobrowolnie, ale dla tego, który je poddał,
20Kwa maana, viumbe viliwekwa katika hali ya kutojiweza kabisa, si kwa hiari yao, ila vilifanywa hivyo kwa mapenzi ya Mungu. Hata hivyo yapo matumaini,
21Pod nadzieją, że i samo stworzenie będzie uwolnione z niewoli skażenia na wolność chwały dziatek Bożych.
21maana hivyo viumbe navyo vitaokolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu, vishiriki uhuru mtukufu wa watoto wa Mungu.
22Bo wiemy, iż wszystko stworzenie wespół wzdycha i wespół boleje aż dotąd.
22Kwa maana tunajua kwamba mpaka hivi sasa, viumbe vyote vinalia kwa maumivu kama ya kujifungua mtoto.
23A nie tylko ono stworzenie, ale i my, którzy mamy pierwiastki Ducha, i my sami w sobie wzdychamy, oczekując przysposobienia synowskiego, odkupienia ciała naszego.
23Wala si hivyo viumbe peke yake, bali hata sisi tulio na huyo Roho, aliye wa kwanza wa zawadi za Mungu; sisi pia tunalalamika ndani yetu, tukitazamia kufanywa watoto wa Mungu, nazo nafsi zenu zikombolewe.
24Albowiem nadziejąśmy zbawieni. A nadzieja widoma nie jest nadzieją; bo co kto widzi, przecz się tego spodziewa?
24Maana kwa matumaini hayo sisi tumekombolewa; lakini tumaini halina maana ikiwa tunakiona kile tunachotumainia. Maana ni nani anayetumaini kile ambacho tayari anakiona?
25Ale czego nie widzimy, tego się spodziewamy i tego przez cierpliwość oczekujemy.
25Kama tunakitumaini kile ambacho hatujakiona bado, basi, tunakingojea kwa uvumilivu.
26Także też i Duch dopomaga mdłościom naszym. Albowiem o co byśmy się modlić mieli, jako potrzeba, nie wiemy; ale tenże Duch przyczynia się za nami wzdychaniem niewymownem.
26Hali kadhalika, naye Roho anatusaidia katika udhaifu wetu. Maana hatujui inavyotupasa kuomba; lakini Roho mwenyewe anatuombea kwa Mungu kwa mlio wa huzuni usioelezeka.
27A ten, który się serc bada, wie, który jest zmysł Ducha, ponieważ według Boga przyczynia się za świętymi.
27Naye Mungu aonaye mpaka ndani ya mioyo ya watu, anajua fikira ya huyo Roho; kwani huyo Roho huwaombea watu wa Mungu kufuatana na mapenzi ya Mungu.
28A wiemy, iż tym, którzy miłują Boga, wszystkie rzeczy dopomagają ku dobremu, to jest tym, którzy według postanowienia Bożego powołani są.
28Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
29Albowiem, które on przejrzał, te też przenaznaczył, aby byli przypodobani obrazowi Syna jego, żeby on był pierworodnym między wieloma braćmi,
29Maana hao aliowachagua tangu mwanzo, ndio aliowateua wapate kufanana na Mwanae, ili Mwana awe wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30A które przenaznaczył, te też powołał; a które powołał, te też usprawiedliwił; a które usprawiedliwił, te też uwielbił.
30Basi, Mungu aliwaita wale aliokuwa amewateua; na hao aliowaita aliwakubali kuwa waadilifu; na hao aliowakubali kuwa waadilifu aliwashirikisha pia utukufu wake.
31Cóż tedy rzeczemy na to? Jeźli Bóg za nami, któż przeciwko nam?
31Kutokana na hayo, tuseme nini zaidi? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, nani awezaye kutupinga?
32Który ani własnemu Synowi nie przepuścił, ale go za nas wszystkich wydał: jakoż by wszystkiego z nim nie darował nam?
32Mungu hakumhurumia hata mwanae wa pekee, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote. Ikiwa amefanya hivyo, je, hatatujalia pia mema yote?
33Któż będzie skarżył na wybrane Boże? Bóg jest, który usprawiedliwia.
33Ni nani atakayewashtaki wateule wa Mungu? Mungu mwenyewe huwaondolea hatia!
34Któż jest, co by je potępił? Chrystus jest, który umarł, owszem i zmartwychwstał, który też jest na prawicy Bożej, który się też przyczynia za nami.
34Ni nani atakayewahukumu? Hakuna! Maana Kristo ndiye aliyekufa, tena alifufuka kutoka wafu na anakaa upande wa kulia wa Mungu. Yeye anatuombea!
35Któż nas odłączy od miłości Chrystusowej? czyli utrapienie? czyli ucisk? czyli prześladowanie? czyli głód? czyli nagość? czyli niebezpieczeóstwo? czyli miecz?
35Ni nani awezaye kututenga na mapendo ya Kristo? Je, ni taabu, au dhiki, au mateso, au njaa, au ukosefu wa nguo, au hatari, au kuuawa?
36Jako napisano: Dla ciebie cały dzieó zabijani bywamy, poczytaniśmy jako owce na rzeź naznaczone;
36Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Kwa ajili yako, twakikabili kifo kutwa kucha: tunatendewa kama kondoo wa kuchinjwa."
37Ale w tem wszystkiem przezwyciężamy przez tego, który nas umiłował.
37Lakini, katika mambo haya yote, tumepata ushindi mkubwa kwa msaada wake yeye aliyetupenda.
38Albowiem pewienem tego, iż ani śmierć, ani żywot, ani Aniołowie, ani księstwa, ani mocarstwa, ani teraźniejsze ani przyszłe rzeczy,
38Maana ninajua hakika kwamba hakuna kitu kiwezacho kututenganisha na upendo wake: wala kifo, wala uhai; wala malaika, au nguvu nyingine za mbinguni; wala yanayotokea sasa, wala yatakayotokea baadaye; wala mamlaka;
39Ani wysokość, ani głębokość, ani żadne insze stworzenie nie będzie nas mogło odłączyć od miłości Bożej, która jest w Jezusie Chrystusie, Panu naszym.
39Wala ulimwengu wa juu, wala wa chini kabisa. Hakuna kiumbe chochote kitakachoweza kututenga na upendo wa Mungu kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.