1Theophilus, dem duma ande murhi pervo klishka pa sa le dieli kai O Jesus nachinaisardia te kerel ai te sicharel de anda gor,
1Ndugu Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2zhi ka dies kai gelotar ando rhaio, ai kai dia ordina katar O Swunto Duxo le apostlonge kai alosardiasas;
2mpaka siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3pala peske martia sikadilo lenge zhuvindo, ai sikadia lenge butivar ke zhuvindolo ke beshlo lensa shtarvardesh dies, ai delas duma lensa pal dieli le amperetsia le Devleski.
3Kwa muda wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya ufalme wa Mungu.
4Andek dies kai sas lensa O Jesus phendia lenge, "Te na zhan anda Jerusalem, numa te azhukeren so lesko Dat shinadiasas lenge. Tume ashundian tumenge pe kadia.
4Wakati walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5Ke o Iovano boldia ando paiesa, numa tume pa xantsi dies avena bolde le Swuntone Duxosa."
5Kwani Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa Roho Mtakatifu."
6Kana le disipluria ai O Jesus sas andek than, won pushle les, "Devla, Kana si kadia vriama kai anesa palpale e amperetsia ka Israel?"
6Basi, mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7O Jesus phendia lenge, "Nai tumendar te zhanen e vriama vai le diesa, ke ferdi O Dat si les e putiera te phenel kana kerdiol.
7Lakini Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8Numa tume avena pherde putierasa kana O Swunto Duxo avela pe tumende, ai avena murhe marturia ande Jerusalem, ai ande sa Judea, ai Samaria, ai pe sa e lumia."
8Lakini wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9Kana phendia kodo divano, O Jesus gelotar ando rhaio, andek nuvero angla lenge iakha.
9Baada ya kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha wasimwone tena.
10Ai sar dikhenas po cheri sar zhaltar O Jesus, eta, dui manush kai sas vuliarde ando parno sikadile lenge;
10Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11ai phende lenge, "Tume kai san anda Galilee, sostar dikhen po cheri? O Jesus kai sas lino tumendar ando rhaio avela palpale sakadia sar tume dikhlian les te zhaltar ando rhaio."
11wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12Antunchi gele palpale ando Jerusalem anda E Plaiin le Maslinenge kai si pashai Jerusalem sar lel iek dies le Savatosko te zhal.
12Kisha mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita moja kutoka mjini.
13Kana aresle, gele andek soba opre kai beshenas o Petri, o Iakov, ai o Iovano, ai o Andre, o Filip, ai o Thomas, o Bartholomew, ai o Mate, o Iakov o shav le Alphaeusosko, ai o Simon (o zealot), ai o Judas o shav le Iakovosko.
13Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14Ai savo andek than rhuginas pe chachimasa, le zhuvliansa, ai e Maria e dei le Jesusoski, ai leske phral.
14Hawa wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria mama yake Yesu, na ndugu zake.
15Ai andek dies ande kodia vriama o Petri wushtilo opre mashkar le disiplonge, ai phendia, won sas chidine andek than sas iek shel ai bish,
15Siku chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16"Murhe phral, o ramomos trobulas te kerdiol, so O Swunto Duxo ande Vorba le Devleski phendiasas mai anglal katar o mui le Davidosko pa Judas, kai dia O Jesus ando lengo vas te astaren les.
16akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17O Judas sas mashkar amende, ke alosardiasas te kerel buchi amensa.
17Yuda alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18Le lovensa kai dine les te purhisar O Jesus. O Judas chindia peske iek kimpo, ai amboldia pe o shero pervo, ai lesko stato pharhadilo mashkaral, ai sa lesko porha ankliste avri.
18("Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika nje.
19Sa o narodo anda Jerusalem ashunde so kerdilia, ai akharde kodole kimpos ande penge shib Acel'dama kodia znachil, O Kimpo le Ratesko.
19Kila mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao, wakaliita lile shamba Hekeli Dama, maana yake, Shamba la Damu.)
20Ke te si ramome andel Psalms, te kerdiol lesko kher sar iek pusta, ai "Te na beshel khonik ande kodo kher; ai aver manush te lel lesko than te kerel buchi."
20Basi, imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote asiishi ndani yake. Tena imeandikwa: Mtu mwingine achukue nafasi yake katika huduma hiyo.
21"Trobul o manush te avel pala amende te avel marturo anda zhuvindimos le Jesusosko. Kodo manush trobul te avel iek ando kodola kai sas mashkar amende sagda kai O Jesus phirdia amensa,
21Kwa hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana Yesu.
22de katar e vriama kai o Iovano boldia les ai zhi ka dies kai O Jesus gelotar mashkar amendar ando rhaio.
22Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
23Andine le duien manushen, o Josef kai busholas Barsabbas, ai vi akharenas les Justus, ai o Matthias.
23Basi, wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia Yusto), na wa pili Mathia.
24Ai rhugisaile ai phende, "Devla, tu kai zhanes sa le ile, savo anda kakala dui manush alosardian,
24Kisha wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25te len o than ande kadia buchi sar ek Apostle, o than kai o Judas meklia te zhal ka pesko than ke kerdia bezex."
25ili achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26Antunchi kerde vari so te alon iekes andel dui, ai o Matthias sas alome; ai thodinosas andel desh u iek disiplonsa.
26Hapo, wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale mitume wengine kumi na mmoja.