1Panvardesh dies kai sas Pentecost savorhe sas ande iek than.
1Siku ya Pentekoste ilipofika, waumini wote walikuwa wamekusanyika pamoja.
2Ai strazo avilo ek bunto sar ek zurali barval phurdelas, ai pherdilo sa o kher kai beshenas tele.
2Ghafla, sauti ikasikika kutoka angani; sauti iliyokuwa kama ya upepo mkali, ikajaza ile nyumba yote walimokuwa wamekaa.
3Antunchi sikadilia lenge shiba kai miazonas sar parha iagaki, ai kodola shiba huladile, ai thodepe iek po iek pe lende.
3Kisha, vikatokea vitu vilivyoonekana kama ndimi za moto, vikagawanyika na kutua juu ya kila mmoja wao.
4Ai savorhe pherdile le Swuntone Duxosa, ai nachinaisarde te den duma aver shiba, sar O Swunto Duxo dia le le vorbi te phenen.
4Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema lugha mbalimbali kadiri Roho alivyowawezesha.
5Sas ando Jerusalem Zhiduvuria, manush kai pachanaspe zurales ando zakono, anda sa le thema la lumiake.
5Na huko Yerusalemu walikuwako Wayahudi, watu wamchao Mungu, waliotoka katika kila nchi duniani.
6Pala bunto kai kerdiliasas, but narodo chidinisailia, ai savorhe chudisaile, ke swako anda lende ashunelas le manushen kai pachanaspe sar denas duma ande penge shib.
6Waliposikia sauti hiyo, kundi kubwa la watu lilikusanyika. Wote walishtuka sana kwani kila mmoja wao aliwasikia hao waumini wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7Savorhe chudisaile ai shodo sas lenge, ai mothonas iek kavreske, "Eta, kodola manush kai den duma si andal Galileanuria?
7Walistaajabu na kushangaa, wakisema, "Je, hawa wote tunaowasikia wakisema hivi, si wenyeji wa Galilaya?
8Ai sarta sai dashtil pe, ke swako anda amende ashunel le, sar den duma ande penge shib.
8Imekuwaje, basi, kwamba kila mmoja wetu anawasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe?
9Si mashkar amende manush anda them kai bushol Parthians, ai Medes, ai Elamites, ai anda Mesopotamia, ai andai Judea, ai andai Cappodocia, ai andai Pontus ai Asia,
9Baadhi yetu ni Waparthi, Wamedi na Waelami; wengine ni wenyeji wa Mesopotamia, Yudea, Kapadokia, Ponto na Asia,
10ai andai le Phrigia, ai Pamphilia, andai Egypt, ai uni thana andai Libya pashai Cyrene, ai kodola kai avile andai e Roma,
10Frugia na Pamfulia, Misri na sehemu za Libya karibu na Kurene; wengine wetu ni wageni kutoka Roma,
11Zhiduvuria ai aver manush kai kerdile sar lende. Le Cretia ai le Arapuria, sar ashunas le kai den duma ande amare shiba pal lashimata le Devleski!"
11Wayahudi na watu walioongokea dini ya Kiyahudi; wengine wametoka Krete na Arabia. Sisi sote tunasikia wakisema kwa lugha zetu wenyewe mambo makuu ya Mungu."
12Savorhe chidisaile, ai chi zhanenas so te gindinpe, won mothonas iek kavreske, "So si so mothon?"
12Wote walishangaa na kufadhaika huku wakiulizana, "Hii ina maana gani?"
13Numa uni marenas mui ai mothonas, "Pherdo mol le."
13Lakini wengine wakawadhihaki wakisema, "Watu hawa wamelewa divai mpya!"
14Antunchi o Petri sikadilo peske desh u ieke disiplonsa, ai vazdia o glaso ai phendia lenge, "Tume manush kai san Zhiduvuria, ai tume savorhe kai avilian ande Jerusalem, te zhanen iek diela ai thon khan ka murhe vorbi."
14Lakini Petro alisimama pamoja na wale kumi na mmoja akaanza kuwahutubia watu kwa sauti kubwa: "Ndugu Wayahudi nanyi nyote mnaokaa hapa Yerusalemu, sikilizeni kwa makini maneno yangu.
15Kakala manush nai mate sar tume mothon, ke akana si inia chasuria diminiatsi.
15Watu hawa hawakulewa kama mnavyodhani; mbona ni saa tatu tu asubuhi?
16Numa akana si katse kai phendia sas o profeto Joel.
16Ukweli ni kwamba jambo hili ni lile alilosema nabii Yoeli:
17Andel paluno dies O Del phenel, shorava murho Swunto Duxo po swako manush; tumare shave ai tumare sheia profesisaren, ai tumare terne avela le vizione, ai tumare phure dikhena sune;
17Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
18ai pe murhe slugi, le mursh ai le zhuvlian, kodola duesa shorava murho Swunto Duxo, ai won den profesi.
18Naam, hata watumishi wangu, wanaume kwa wanawake, nitawamiminia Roho wangu, siku zile, nao watautangaza ujumbe wangu.
19Kerava bare dieli opre ando cheri, ai mirakluria tele pe phuv, rat, iag, ai tsu.
19Nitatenda miujiza juu angani, na ishara chini duniani; kutakuwa na damu, moto na moshi mzito;
20O kham parhudiola ai kerdiola tuniariko, ai o shunuto pherdiola rat, mai anglal sar o dies kai avela O Kristo, kodo dies baro ai luvudime.
20jua litatiwa giza, na mwezi utakuwa mwekundu kama damu, kabla ya kutokea ile siku kuu na tukufu ya Bwana.
21Antunchi kon godi tsipila po anav le Devlesko avela skepime.
21Hapo, yeyote atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa.
22Tume manush kai san ande Israel, ashunen kadala vorbi. O Jesus andai Nazareth, kado manush kai leske O Del sas marturo angla tumende, ai katar le mirakluria ai le bare bucha kai kerdia lestar mashkar tumende; sar tume zhanen.
22"Wananchi wa Israeli, sikilizeni maneno haya! Yesu wa Nazareti alikuwa mtu ambaye mamlaka yake ya kimungu yalithibitishwa kwenu kwa miujiza, maajabu na ishara Mungu alizofanya kati yenu kwa njia yake, kama mnavyojua.
23Kado manush sas tume dino te manglia O Del, ai kai manglia wo mai anglal tume karfosardian les, mudardian les, katar le manush le bezexa le.
23Kufuatana na mpango wake mwenyewe Mungu alikwisha amua kwamba Yesu angetiwa mikononi mwenu; nanyi mkamuua kwa kuwaachia watu wabaya wamsulubishe.
24O Del zhuvindisardia les, skepisardia les andai martia, ke nashtilas e martia te ankerel les.
24Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu akamwokoa katika maumivu ya kifo kwa maana haingewezekana kabisa kifo kimfunge.
25Ke o David mothol pa peste: "Dikhem le Devles sagda sar beshelas angla mande: ke wo si pe murhi rig e chachi, saxke te na izdral.
25Maana Daudi alisema juu yake hivi: Nilimwona Bwana mbele yangu daima; yuko nami upande wangu wa kulia, na hivyo sitatikisika.
26Ai inker murho ilo raduimelo, ai murhi shib pherdo raduimos la; ai vi murho stato merela raduimasa.
26Kwa hiyo, moyo wangu ulifurahi; tena nilipiga vigelegele vya furaha. Mwili wangu utakaa katika tumaini;
27Ke chi mekes murho traio mashkar le mule, ai chi mekesa kodoles kai si chiro te dikhel o chorhimos.
27kwa kuwa hutaiacha roho yangu katika kuzimu, wala kumruhusu mtakatifu wako aoze.
28Sikadian mange le droma le traioske; pheres ma raduimos ke pasha mande san.
28Umenionyesha njia za kuufikia uzima, kuwako kwako kwanijaza furaha!
29Murhe phral, slobodo mange te dav tumensa duma vorta pa David amaro dat, mulo ai groposarde les, ai lesko gropo inker adies mashkar amende lo.
29"Ndugu zangu, napenda kuwaambieni waziwazi juu ya mambo yaliyompata Daudi, babu yetu. Yeye alikufa, akazikwa, tena kaburi lake liko papa hapa petu mpaka leo.
30Sar wo sas profeto, ai zhanelas ke O Del shinadia ai solaxadia te iek andel leske manush avela amperato.
30Lakini kwa vile Daudi alikuwa nabii, alijua kuwa Mungu alimwapia kiapo kwamba atamtawaza mmoja wa uzawa wake kuwa mfalme mahali pake.
31Pa zhuvindimos le Kristosko phendia, ai mothodia ke chi mekela les mashkar le mule, ai lesko stato chi dikhela o chorhimos.
31Daudi aliona kabla mambo yatakayofanywa na Mungu na hivyo akasema juu ya ufufuo wa Kristo wakati aliposema: Hakuachwa kuzimu, mwili wake haukuoza.
32Kodo Jesus si kai O Del zhuvindisardia, ai savorhe marturia sam.
32Basi, Mungu alimfufua huyo Yesu na sisi sote ni mashahidi wa tukio hilo.
33Vazdino katar o chachimos le Devlesko, lia katar O Dat O Swunto Duxo kai sas shinado, ai shordia pesko Swunto Duxo, sar dikhen ai ashunen.
33Yesu aliinuliwa juu mpaka upande wa kulia wa Mungu, akapokea kutoka kwa Baba ile zawadi aliyoahidi yaani Roho Mtakatifu; na mnachoona sasa na kusikia ni mmiminiko wa huyo Roho.
34Ke o David chi gelo ando cheri, numa wo mothol, "O Del phendia murhe Devleske, besh pe murhi rik e chachi,
34Maana Daudi mwenyewe, hakupanda mpaka mbinguni; ila yeye alisema: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia,
35zhi kai kerav skeri anda che duzhmaia.
35hadi nitakapowafanya adui zako kibao cha kukanyagia miguu yako.
36Ai ke sa o kher le Israelongo te zhanel chachimasa, ke O Del kerdia Kristo kodo Jesus, kai tume karfosardian.
36"Watu wote wa Israeli wanapaswa kufahamu kwa hakika kwamba huyo Yesu mliyemsulubisha ninyi, ndiye huyo ambaye Mungu amemfanya kuwa Bwana na Kristo."
37Kana ashunde kado divano, lengo ilo sas azbado, ai phende le Petreske ai kolaver apostlonge, "Murhe phral, so keras?"
37Basi, watu waliposikia hayo, walichomwa moyo, wakawauliza Petro na wale mitume wenzake: "Ndugu zetu, tufanye nini?"
38O Petri phendia lenge, "Kein tume anda tumare bezexa, ai swako anda tumende te avel boldo ando anav le Jesus Kristosko pala iertimos tumare bezexengo, ai avela dino O Swunto Duxo.
38Petro akajibu, "Tubuni na kila mmoja wenu abatizwe kwa jina la Yesu Kristo ili mpate kuondolewa dhambi zenu na kupokea ile zawadi ya Roho Mtakatifu.
39Ke so sas shinado katar O Del tumenge si, ai tumare shavengo, ai sa kodolenge kai si dur, sode avena, sode O Del akharela len.
39Maana, ahadi ile ilikuwa kwa ajili yenu, kwa ajili ya watoto wenu, kwa ajili ya wote wanaokaa mbali; na kwa ajili ya kila mtu ambaye Bwana Mungu wetu atamwita kwake."
40Ai mai avre vorbensa motholas lenge te zuralel le, skepin tume anda kado narodo kai si bezexalo.
40Kwa maneno mengine mengi, Petro alisisitiza na kuwahimiza watu akisema, "Jiokoeni katika kizazi hiki kiovu."
41Le manush kai premisarde leski vorba boldia len, ai ande kado dies pherdile trin mi shave Devleske.
41Wengi waliyakubali maneno yake, wakabatizwa. Watu wapatao elfu tatu wakaongezeka katika kile kikundi siku hiyo.
42Ai zhanas angle kadia ando sicharimos le apostlongo ai te chidenpe opral andek than te xan o manrho, ai te rhuginpe.
42Hawa wote waliendelea kujifunza kutoka kwa mitume, kuishi pamoja kidugu, kumega mkate na kusali.
43Dar kerdiolas ando narodo, ke le apostluria kerenas but mirakluria ai but semnuria.
43Miujiza na maajabu mengi yalifanyika kwa njia ya mitume hata kila mtu akajawa na hofu.
44Sa kodola kai pachanaspe ando Del sas ande iek than, ai kerenas buchi andek than.
44Waumini wote waliendelea kuwa kitu kimoja na mali zao waligawana pamoja.
45Bichinenas penge khera ai pengo mishtimos kai sas le, ai hulavenas le love pe savorhende.
45Walikuwa wakiuza mali na vitu vyao kisha wakagawana fedha kadiri ya mahitaji ya kila mmoja.
46Savorhe sas swako dies andek than ande khangeri, ai phagenas o manrho andel khera, ai xanas penge xabe raduimasa, ai prostovanes ande pengo ilo.
46Waliendelea kukutana pamoja kila siku Hekaluni. Lakini wakati wa kumega mkate, walikutana katika nyumba zao na wakakishiriki chakula hicho kwa furaha na moyo mkunjufu.
47Naisinas le Devles, ai arakhenas mishtimos mashkar sa o narodo. Ai O Del tholas ande khangeri swako dies aver manush kai sas skepime.
47Walimtukuza Mungu, wakapendwa na watu wote. Kila siku Bwana aliwaongezea idadi ya watu waliokuwa wakiokolewa.