Romani: New Testament

Swahili: New Testament

John

6

1Pala kodia, O Jesus gelotar inchal o pai kai busholas Galilee (vai Tiberias).
1Baada ya hayo, Yesu alivuka ziwa Galilaya (au Ziwa Tiberia).
2But narodo lelaspe pala leste, ke le manush dikhenas le mirakluria kai kerelas, ai sastiarelas le naswalen.
2Umati mkubwa wa watu ulimfuata kwa sababu watu hao walikuwa wameona ishara alizokuwa akifanya kwa kuwaponya wagonjwa.
3O Jesus anklisto po plai ai beshlo tele kotse peske disiplonsa.
3Yesu alipanda mlimani, akaketi pamoja na wanafunzi wake.
4Ai O Dies O Baro le Zhidovongo pasholas.
4Sikukuu ya Wayahudi iitwayo Pasaka ilikuwa imekaribia.
5O Jesus vazdia le iakha, ai dikhlia ek baro narodo avel leste, wo phendia le Filiposke, "Kai sai chinasa dosta xabe te pravaras sa kadale narodos?"
5Basi, Yesu na alipotazama na kuona umati wa watu ukija kwake, alimwambia Filipo, "Tununue wapi mikate ili watu hawa wapate kula?"
6Wo phendia kadia te zumavel les, numa O Jesus zhanglia so kerelas.
6(Alisema hivyo kwa kumjaribu Filipo, kwani alijua mwenyewe atakalofanya.)
7O Filip phendia leske, "Dui shela teliara rupunen chi avela ame dosta te chinas manrho te das xantsi kotororho swakones.
7Filipo akamjibu, "Mikate ya denari mia mbili za fedha haiwatoshi watu hawa hata kama ila mmoja atapata kipande kidogo tu!"
8Iek anda leske disipluria, o Andre, o phral le Simonosko Petri, phenel leske,
8Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
9"Si katse iek raklorho, kai si les panzh manrhe, ai dui tsinorhe mashe. Numa so si kadala pe kado but narodo?"
9"Yupo hapa mtoto mmoja aliye na mikate mitano ya shayiri na samaki wawili; lakini hivi vyatosha nini kwa watu wengi kama hawa?"
10O Jesus phendia lenge, "Antunchi keren te beshen savorhe tele. Kotse sas but char. Le manush beshle tele. Won sas pashte panzh mi mursh.
10Yesu akasema, "Waketisheni watu." Palikuwa na nyasi tele mahali hapo. Basi, watu wakaketi, jumla yapata wanaume elfu tano.
11O Jesus lia le manrhe, naisisardia le Devles, ai O Jesus dia le kal disipluria, ai leske disipluria dia le ka narodo kai beshelas tele, ai sakadia le masheske, ai sas le sode won mangle.
11Yesu akaitwaa ile mikate, akamshukuru Mungu, akawagawia watu waliokuwa wameketi; akafanya vivyo hivyo na wale samaki, kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
12Kana xale dosta savorhe, wo phenel peske disiplonge, "Chiden le kotora kai ashshile; te na xasavol kanchi."
12Watu waliposhiba Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kusanyeni vipande vilivyobaki visipotee."
13Le disipluria chide le desh u dui shkonitsi pherdesas le kotorensa kay ashshile katar le panzh manrhe kana savorhe xale.
13Basi, wakakusanya vipande vya mikate ya shayiri walivyobakiza wale watu waliokula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
14Le zhene kai dikhle o miraklo kai kerdia O Jesus, phende "Kado si o chacho profeto kai trobulas te avel ande lumia!"
14Watu walipoiona ishara hiyo aliyoifanya Yesu, wakasema, "Hakika huyu ndiye nabii anayekuja ulimwenguni."
15Ai O Jesus zhanelas ke si te aven te len les pe zor, te keren les amperato, gelotar po plai kokorho.
15Yesu akajua ya kuwa watu walitaka kumchukua wamfanye mfalme, akaondoka tena, akaenda mlimani peke yake.
16Kana e riat avili, leske disipluria gele karing e maria.
16Ilipokuwa jioni wanafunzi wake waliteremka hadi ziwani,
17Ankliste ande ek chuno, ai thodepe te nakhen o pai palpale karing o Capernaum. Akana sas tumiariko, ai O Jesus inker chi avilo lende.
17wakapanda mashua ili wavuke kwenda Kafarnaumu. Giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa hajawafikia bado.
18Ai e maria buntuime sas ke barval phurdelas zurales.
18Ziwa likaanza kuchafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
19Kana kerdesas trin vai shtar maili vai pansh vai shov kilometre po pai ando chuno. Won dikhle O Jesus phirelas pe maria, ai pasholas lende ando chuno; ai won daraile.
19Wanafunzi walipokuwa wamekwenda umbali wa kilomita tano au sita, walimwona Yesu akitembea juu ya maji, anakaribia mashua; wakaogopa sana.
20Numa O Jesus phendia lenge, "Me sim, na daran."
20Yesu akawaambia, "Ni mimi, msiogope!"
21Mangenas te len les ande pengo chuno; ai strazo o chuno areslo karing e phuv kai trobulas te zhan.
21Walifurahi kumchukua Yesu katika mashua; na mara mashua ikawasili nchi kavu walipokuwa wanakwenda.
22Pe terharin, kana o narodo kai beshle pe kolaver rig la mariako, dikhle ke sas kotse ferdi iek chuno. Won zhangle ke O Jesus chi anklisto ando chuno peske disiplonsa, numa geletar korkorho.
22Kesho yake umati wa watu wale waliobaki upande wa pili wa ziwa walitambua kwamba kulikuwa na mashua moja tu pale, na Yesu hakuingia katika mashua pamoja na wanafunzi wake, ila wanafunzi hao walikuwa wamekwenda zao peke yao.
23Numa aver chunuria avile andai Tiberias, areslesas pasha o than kai xalesas o manrho, kana O Jesus naisisardiasas le Devles.
23Mashua nyingine kutoka Tiberia zilifika mahali hapo watu walipokula ile mikate, Bwana alipokwisha mshukuru Mungu.
24Kana o narodo dikhle ke O Jesus nas kotse, ai chi leske disipluria. Won ankliste ande lenge chunuria, ai gele ando Capernaum te roden les.
24Basi, hao watu walipogundua kwamba Yesu na wanafunzi wake hawakuwapo mahali hapo, walipanda mashua, wakaenda Kafarnaumu wakimtafuta.
25Kana o narodo arakhle O Jesus pe kolaver rig la mariako, won phende leske, "Gazda, kana avilian tu katse?"
25Wale watu walipomkuta Yesu ng'ambo ya pili wa ziwa walimwuliza, "Mwalimu, ulifika lini hapa?"
26O Jesus phendia lenge, "Chachimasa, chachimasa, phenav tumege: roden ma, ke xalian o manrho ai chaililian, ai na ke dikhlian le mirakluria.
26Yesu akawajibu, "Kweli nawaambieni, mnanitafuta si kwa kuwa mmeona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
27Na keren buchi le xabeneski kai rimolpe, numa keren buchi le xabeneski kai beshel but vriama ai kai kerel te avel o traio kai chi mai getolpe. Ai ke O Shav le Manushesko dela tumenge; ke O Del, O Dat, thodia pe leste o semno leska putierako."
27Msikishughulikie chakula kiharibikacho; kishugulikieni chakula kidumucho kwa ajili ya uzima wa milele. Mwana wa Mtu ambaye Baba amemthibitisha atawapeni chakula hicho."
28Antunchi won phende leske, "So trobul te keras, te keras e buchi maladi angla Del?"
28Wao wakamwuliza, "Tufanye nini ili tuweze kuzitenda kazi za Mungu?"
29O Jesus phendia lenge, "Kadia si e buchi le Devleski, te pachan tume ande kodo kai wo tradia."
29Yesu akawajibu, "Hii ndiyo kazi anayotaka Mungu muifanye: kumwamini yule aliyemtuma."
30Phen leske, "Che semno la putierako sikaves tu, kashte te dikhas, vai pachas ame ande tute? So keres tu?"
30Hapo wakamwambia, "Utafanya ishara gani ili tuione tupate kukuamini? Utafanya kitu gani?
31Amare dada xale o manrho ande pusta; sar si ramome, wo dia le manrho anda cheri te xan."
31Wazee wetu walikula mana kule jangwani, kama yasemavyo Maandiko: Aliwalisha mkate kutoka mbinguni."
32O Jesus phenel lenge, "Chachimasa, chachimasa, phenav tumenge, O Moses chi dia tume o manrho anda cheri; numa murho Dat del tumen o chacho manrho anda cheri.
32Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, Mose hakuwapeni mkate kutoka mbinguni; Baba yangu ndiye awapaye ninyi mkate halisi kutoka mbinguni.
33Ke o manrho kai del O Del, kodo si kai hulel anda rhaio, ai del traio la lumiako."
33Maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na aupaye ulimwengu uzima."
34Won phenen leske, "Gazda, de ame kodo manrho sagda."
34Basi, wakamwambia, "Mheshimiwa, tupe daima mkate huo."
35O Jesus phendia lenge, "Me sim o manrho le traiosko; kodo kai avela mande shoxar chi avela bokhalo; kodo kai pachal ande mande shoxar chi avela trushalo."
35Yesu akawaambia, "Mimi ndimi mkate wa uzima. Anayekuja kwangu hataona njaa; anayeniamini hataona kiu kamwe.
36Numa phendem tumenge, "Tume dikhlian ma numa chi pachan ma.
36Lakini niliwaambieni kwamba ingawa mmeniona hamniamini.
37So godi murho Dat del ma avela mande. Ai kodales kai avela mande shoxar chi dava avri.
37Wote anaonipa Baba watakuja kwangu; nami sitamtupa nje yeyote anayekuja kwangu,
38Ke hulistem anda rhaio, te kerav e voia kodoleski kai tradia ma, ai na murhi voia.
38kwani nimeshuka kutoka mbinguni si kwa ajili ya kufanya matakwa yangu, ila kutimiza matakwa ya yule aliyenituma.
39Ai kadia si e voia le Dadeski kai tradia ma; te na xasarav chi iek anda kodola kai dia ma, numa te vushtiavav le savorhen ka traio ka mai paluno dies.
39Na matakwa ya yule aliyenituma ndiyo haya: nisimpoteze hata mmoja kati ya wale alionipa, ila niwafufue wote Siku ya mwisho.
40Ai kadia si leski voia, ke kon godi dikhela le Shaves, ai pachalape ande leste, avela les o traio kai chi mai getolpe; ai vushtiavava le ka traio ka paluno dies.
40Maana anachotaka Baba yangu ndicho hiki: kila amwonaye Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele; nami nitamfufua Siku ya mwisho."
41Le Zhiduvuria line xoli po Jesus, ke phendia lenge, "Me sim o manrho kai hulisto anda rhaio."
41Basi, Wayahudi wakaanza kunung'unika kwa kuwa alisema: "Mimi ni mkate ulioshuka kutoka mbinguni."
42Pate won phende, "Nai wo O Jesus, o shav le Josefesko, ai zhanas leske dades ai leska da? Sar sai mothol ke hulisto anda rhaio?"
42Wakasema, "Je, huyu si mwana wa Yosefu? Tunawajua baba yake na mama yake! Basi, anawezaje kusema kwamba ameshuka kutoka mbinguni?"
43O Jesus phendia lenge, "Na xoliavon mashkar tumende.
43Yesu akawaambia, "Acheni kunung'unika ninyi kwa ninyi.
44Khonik nashtil te avel mande, te na avela O Dat kai tradia ma te tsirdel les mande; ai vushtiavava les anda merimos ka traio le rhaiosko ka paluno dies.
44Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, Baba aliyenituma asipomvuta kwangu; nami nitamfufua mtu huyo Siku ya mwisho.
45Le profeturia ramosarde, "Savorhe avena sicharde katar O Del." Savo godi manush ashunela le Dades ai lelape pala lesko sicharimos avela mande.
45Manabii wameandika: Watu wote watafundishwa na Mungu. Kila mtu anayemsikia Baba na kujifunza kutoka kwake, huja kwangu.
46Khonik chi dikhlia le Dades; kodo kai avilo katar O Del, si kodo kai dikhlia le Dades.
46Hii haina maana kwamba yupo mtu aliyemwona Baba, isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
47Chachimasa, chachimasa, phenav tumenge: kodo kai pachalpe ande mande avela les o traio kai chi mai getolpe.
47Kweli, nawaambieni, anayeamini anao uzima wa milele.
48Me sim o manrho le traiosko.
48Mimi ni mkate wa uzima.
49Tumare dada xale o manrho ande pusta, numa mule.
49Wazee wenu walikula mana kule jangwani, lakini walikufa.
50Numa o manrho kai hulel anda rhaio kadia lo ke savo kai xala les chi merela.
50Huu ndio mkate kutoka mbinguni; mkate ambao anayekula hatakufa.
51Me sim o manrho o zhuvindo kai hulisto anda rhaio. Te si vari kon kai xala anda kadia manrho, traiila sagda. Ai o manrho kai dava si murho stato, ai dava les te avel o traio la lumiako."
51Mimi ni mkate hai ulioshuka kutoka mbinguni. Mtu yeyote akila mkate huu ataishi milele. Na mkate nitakaompa ni mwili wangu ninaoutoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu."
52Pe kadia le Zhiduvuria denas pe duma mashkar pende, phenenas, "Sar sai wo del amen pesko stato te xa?"
52Ndipo Wayahudi wakaanza kubishana kati yao:
53O Jesus phendia lenge, "Chachimasa, chachimasa, phenav tumenge, te na xana o stato katar O Shav le Manushesko, ai te na pena lesko rat, chi avela tumen o traio ande tumende.
53Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, msipokula mwili wa Mwana wa Mtu na kunywa damu yake, hamtakuwa na uzima ndani yenu.
54Savo kai xala murho stato, ai pela murho rat avela les o traio le rhaiosko, ai vushtiavava les ka traio le rhaiosko o paluno dies.
54Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anao uzima wa milele nami nitamfufua siku ya mwisho.
55Ke murho stato si chacho pravarimos, ai murho rat si chacho pimos.
55Maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
56Savo kai xal murho stato ai pel murho rat traiil ande mande ai traiiv ande leste.
56Aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, akaa ndani yangu, nami nakaa ndani yake.
57O Dat kai tradia ma zhuvindo lo, ai traiiv anda leste sakadia, kodo kai xal murho stato traiila anda mande.
57Baba aliye hai alinituma, nami naishi kwa sababu yake; vivyo hivyo anilaye mimi ataishi pia kwa sababu yangu.
58Kado si o manrho kai hulisto anda rhaio; nai sar tumare phurane dada kai xale o manrho ande pusta, ai mule. Kon xala kado manrho traiila sa data.
58Basi, huu ndio mkate ulioshuka kutoka mbinguni; si kama mana waliyokula babu zetu, wakafa. Aulaye mkate huu ataishi milele."
59O Jesus phendia kadala vorbi kana sicharelas ande synagogue ando Capernaum.
59Yesu alisema hayo alipokuwa akifundisha katika sunagogi kule Kafarnaumu.
60But anda peske disipluria, kana ashunde kadia, phende, "Kadala vorbi si trutno. Kon sai ashunel le?"
60Basi, wengi wa wafuasi wake waliposikia hayo, wakasema, "Haya ni mambo magumu! Nani awezaye kuyasikiliza?"
61O Jesus haliardia ande peste ke leske disipluria denas pe duma mashkar pende pa kado divano, anda kodia phendia lenge, "Dukhavel tumen so ashundian?"
61Yesu alijua bila kuambiwa na mtu kwamba wanafunzi wake walikuwa wananung'unika juu ya jambo hilo, akawauliza, "Je, jambo hili linawafanya muwe na mashaka?
62So keren tume kana dikhena ke O Shav le Manushesko anklel kotse kai sas mai anglal?
62Itakuwaje basi, mtakapomwona Mwana wa Mtu akipanda kwenda kule alikokuwa kwanza?
63Le Devlesko Duxo del o traio: o stato chi mol kanchi. Le vorbi kai phendem tumenge, won si duxo ai traio.
63Roho ndiye atiaye uzima; binadamu peke yake hawezi. Maneno niliyowaambieni ni Roho, ni uzima.
64Numa si mashkar tumende uni kai chi pachan." Ke O Jesus zhanglia de mai anglal kon si kodola kai chi pachanpe, ai kon si kodo kai purhila les.
64Hata hivyo, wako baadhi yenu wasioamini." (Yesu alisema hivyo kwani alijua tangu mwanzo ni kina nani wasioamini, na pia ni nani atakayemsaliti.)
65Wo phendia, "Sostar phendem tumenge, ke khonik nashtil te avel mande te na tsirdela les O Del mande."
65Kisha akasema, "Ndiyo maana niliwaambieni kwamba hakuna awezaye kuja kwangu asipowezeshwa na Baba yangu."
66Ai de katar kodia vriama but anda leske disipluria geletar, ai chi mai zhanas lesa.
66Kutokana na hayo, wengi wa wafuasi wake walirudi nyuma wasiandamane naye tena.
67Ai O Jesus phendia le desh u dui disiplonge, "Ai tume, chi mangen vi tume te zhantar?"
67Basi, Yesu akawauliza wale kumi na wawili, "Je, nanyi pia mwataka kwenda zenu?"
68Ai O Simon Petri phendia leske, "Devla, kaste te zhasas ame? Si tu le vorbi kai den o traio le rhaiosko.
68Simoni Petro akamjibu, "Bwana, tutakwenda kwa nani? Wewe unayo maneno yaletayo uzima wa milele.
69Ai akana pachas ai zhanas kai tu san O Kristo, O Swunto Shav le Devlesko.
69Sisi tunaamini, na tunajua kwamba wewe ndiwe yule Mtakatifu wa Mungu."
70O Jesus phendia lenge, "Pate chi alosardem tumen me, le desh u duien? Ai iek anda tumende si iek beng!"
70Yesu akawaambia, "Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Hata hivyo, mmoja wenu ni Ibilisi!"
71Wo delas duma pa Judas Iscariot o shav le Simonosko. Ke wo sas kai trobulas te purhil les, iek andal desh u dui.
71Yesu alisema hayo juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskarioti; maana huyu alikuwa ndiye atakayemsaliti, ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili.