1Pala kodia O Jesus phiradia ande Galilee; ke chi mangel te phirel ande Judea, ke le Zhiduvuria rodenas te mudaren les.
1Baada ya hayo, Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya. Hakutaka kutembea mkoani Yudea kwa sababu viongozi wa Wayahudi walikuwa wanataka kumwua.
2Ai O Dies O Baro le Zhidovongo le Tabernacles pasholas.
2Sikukuu ya Vibanda ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
3Leske phral phende leske, "Zhatar katse, ai zha ando Judea, kashte che disipluria te sai dikhen le mirakluria kai tu keres.
3Basi ndugu zake wakamwambia, "Ondoka hapa uende Yudea ili wanafunzi wako wazione kazi unazozifanya.
4Khonik chi garavel so kerel te mangel te sikadiol. Te keres kadalendar dieli, sikav tu ka sa la lumiake!"
4Mtu hafanyi mambo kwa siri kama anataka kujulikana kwa watu. Maadam unafanya mambo haya, basi, jidhihirishe kwa ulimwengu."
5Ke chi leske chache phral chi pachanaspe ande leste.
5(Hata ndugu zake hawakumwamini!)
6O Jesus phendia lenge, "Murhi vriama chi avili inker; numa tumari vriama sagda gata la.
6Basi, Yesu akawaambia, "Wakati wangu ufaao haujafika bado. Lakini kwenu ninyi kila wakati unafaa.
7E lumia nashti gretsol tumen, numa gretsol man, ke phenav pa late, ke laki buchi so kerel si nasul.
7Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi, lakini mimi wanichukia kwa sababu mimi nauambia wazi kwamba matendo yake ni maovu.
8Zhantar tume ka Dies O Baro le Zhidovongo, me chi zhav ka kado Dies O Baro le Zhidovongo inker, ke murhi vriama chi avili inker.
8Ninyi nendeni kwenye sikukuu hiyo. Mimi siendi kwenye sikukuu hiyo, maana saa yangu ifaayo haijafika."
9Wo phendia lenge kadala vorbi ai beshlo ando Galilee.
9Alisema hayo kisha akabaki huko Galilaya.
10Kana leske phral gele ka Dies O Baro le Zhidovongo, antunchi O Jesus gelo, vi wo numa na angle narodo, numa sar chordanes.
10Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri.
11Le Zhiduvuria rodenas les ka O Dies O Baro le Zhidovongo. Ai phende, "Kai lo?"
11Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; Wakauliza: "Yuko wapi?"
12But manush denas duma pala leste ando narodo. Uni phende, "Wo si iek manush o lasho." Aver phenenas, "Nichi." Wo atsavel le manushen."
12Kulikuwa na minong'ono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, "Ni mtu mwema." Wengine walisema, "La! Anawapotosha watu."
13Numa khonik chi delas duma pa leste angla manush, ke daranas katar le Zhiduvuria.
13Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema, habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi.
14Karing mashkar O Dies O Baro le Zhidovongo O Jesus gelo ande tampla, ai sicharelas.
14Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda Hekaluni, akaanza kufundisha.
15Le Zhiduvuria chudinaspe, ai phenenas, "Sar wo zhanel kadia but kana shoxar chi sichilo."
15Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema "Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?"
16O Jesus phenel lenge, "O sicharimos kai dav nai murho, numa avel katar O Del kai tradia ma.
16Hapo Yesu akawajibu, "Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma.
17Te vari kon te kerel so mangel O Del, zhanela ke so sicharav avel katar O Del, vai te dava duma anda mande.
17Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe.
18Kon del duma pestar rodel pesko barimos: numa kodo kai rodel o barimos kodolesko kai tradia les, kodo si chacho, ai nai xoxaimos ande leste.
18Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote.
19O Moses dia tume o zakono? Numa khonik anda tumende chi keren o zakono. Sostar roden tume te mudaren ma?"
19Je, Mose hakuwapeni Sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika Sheria. Kwa nini mnataka kuniua?"
20Le manush phende leske, "Tut si tu iek beng ande tute! Kon rodel te mudarel tu?""
20Hapo watu wakamjibu, "Una wazimu wewe! Nani anataka kukuua?"
21O Jesus phenel lenge, "Kerdem iek diela, ai savorhe chudisailian.
21Yesu akawajibu, "Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia.
22Ke o Moses dia tumen o zakono te shinen pe murshen (na ke avel katar o Moses, numa katar tumare phure), ai tume shinen ieke manushes po dies O Savatone.
22Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa ninyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato.
23Te sai shinen ieke manushes po dies O Savatone, te phagen o zakono le Mosesosko. Sostar xoliavon pe mande, ke sastiardem ieke manushes sa antrego po dies O Savatone?
23Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi Sheria ya Mose isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato?
24Aterdion te keren kris pala so dikhen avrial po manush, aven vorta ai chache ande tumare kris kana keren la."
24Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki."
25Uni manush anda o Jerusalem phende, "Pate nai kado o manush kai rodas te mudaras les?
25Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, "Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu?
26Dikh! Del duma angla savorhenge, ai khonik chi phenel leske kanchi! Amborim ke le bare kai poronchin zhanen ke wo si O Kristo?
26Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo?
27Numa kana O Kristo avela, khonik chi zhanela katar avel, numa ame zhanas katar avel kado manush."
27Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!"
28Sar O Jesus sicharelas ande tampla, tsipisardia, "Tume zhanen ma, ai zhanen katar sim: ai chi avilem anda mande, numa kodo kai tradia ma wo si chacho, ai tume chi zhanen les.
28Basi, Yesu alipokuwa anafundisha Hekaluni alipaaza sauti na kusema, "Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui.
29Numa me zhanav les; ke avav lestar, ai wo tradia ma."
29Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma."
30Antunchi rodenas sar te len les; numa khonik chi thode o vas pe leste, ke lesko chaso chi avilo inker.
30Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado.
31Numa but mashkar o narodo pachanaspe ande leste, ai phende, "Kana O Kristo avela, sai kerela mai but mirakluria sar kerdia kado?"
31Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, "Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?"
32Le Farizeanuria ashunde ke o narodo mothon kodala dieli pa Jesus; ai le Farizeanuria ai le bare rasha trade penge zhandari te len les.
32Mafarisayo waliwasikia watu wakinong'ona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni.
33O Jesus phendia lenge, "Me beshav tumensa mai xantsi vriama, ai porme zhavtar karing kodo kai tradia ma.
33Yesu akasema, "Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma.
34Tume rodena ma, numa chi arakhena ma, ke nashti avena kai zhava."
34Mtanitafuta lakini hamtaniona, maana pale nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika."
35Le Zhiduvuria phenen mashkar pende, "Kai wo zhala kai chi arakhasa les? Zhala karing le foruria kai si ande Gretsia, ai sicharel le Grekone?
35Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, "Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki?
36So si kadala vorbi kai phendia, Tume rodena ma, numa chi arakhena ma, ke nashti aven kai me zhava. So znachil?"
36Ana maana gani anaposema: Mtanitafuta lakini hamtanipata, na mahali nitakapokuwa ninyi hamwezi kufika?"
37O paluno Dies O Baro le Zhidovongo sas o mai baro, ai O Jesus beshelas ande punrhende ai tsipisardia, phenelas, "Te si vari kon trushalo, mek te avel mande, ai pel
37Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalum. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, "Aliye na kiu na aje kwangu anywe.
38"Kon pachalape ande mande, sar E Vorba le Devleski phenel, pai zhuvindo hulela anda lesko ilo."
38Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: Anayeniamini mimi, mito ya maji yenye uzima itatiririka kutoka moyoni mwake!"
39O Jesus phendia pa Swunto Duxo, kodala kai pachanpe ande leste premina: ke O Swunto Duxo nai dino inker, ke O Jesus nas vazdino ando rhaio inker.
39(Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado.)
40Kana but le manusheske ashunde leske vorbi, phenenas, "Chaches, kado manush si o profeto."
40Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, "Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!"
41Aver phende, "Wo si O Kristo!" Numa aver phende, "Pate, sai Kristo avel andai Galilee!
41Wengine wakasema, "Huyu ndiye Kristo!" Lakini wengine walisema, "Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya?
42Pate o ramomos chi phendia, ke O Kristo si te avel ande vitsa le Davidoski, ai anda foro kai bushol Bethlehem, kai beshlo o David?"
42Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!"
43Anda kodia chi haliarenas mashkar pende iek fialo pala Jesus.
43Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu.
44Uni mangenas te len les, numa khonik chi thode o vas pe leste.
44Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata.
45Le zhandari gele palpale ka le bare rasha ai le Farizeanuria, ai phende lenge, "Sostar tume chi andian les?"
45Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, "Kwa nini hamkumleta?"
46Le zhandari phende lenge, "Chi iek manush chi dia duma sar kado manush!"
46Walinzi wakawajibu, "Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!"
47Le Farizeanuria phushle len, "Vi tume atsardian pala leste.
47Mafarisayo wakawauliza, "Je, nanyi pia mmedanganyika?
48Pate si vari kon andal le bare kai poronchin, vai iek andal Farizeanuria kai pachanpe ande leste?
48Je, mmekwisha mwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini?
49Numa kodo narodo kai chi zhanen o zakono o Mosesosko, si armandine."
49Lakini umati huu haujui Sheria ya Mose; umelaaniwa!"
50O Nicodemus sas iek baro mashkar lende; wo gelosas mai anglal te dikhel O Jesus, phendia lenge,
50Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia,
51"Amaro zakono chi kerel kris po manush mai anglal sar te ashunas les, ai te zhanas so kerdia."
51"Je, Sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?"
52Won phende leske, "Vi tu san anda Galilee? Sichos o ramomos le Devlesko ai dikhesa, ke chi iek profeto avel anda Galilee.
52Nao wakamjibu, "Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!"
53Antunchi swako gelo peske khere.
53Basi, wote wakaondoka, kila mtu akaenda zake;