Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

12

1Sa antunchi chidinisailo but narodo, ai kadia de but narodo sas kai phirenas pe iek kavreske punrhe, O Jesus phendia leske disiplonge mai anglal, "Arakhen tume katar e drozhdi le Farizeanongi. Kodia si kodola kai chi keren so mothon.
1Wakati watu kwa maelfu walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu aliwaambia kwanza wanafunzi wake, "Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani unafiki.
2So godi si garado avela sikado; ai swako garaimos avela zhanglo.
2Kila kilichofunikwa kitafunuliwa, kila kilichofichika kitafichuliwa.
3Anda kodia, so godi mothona ando tuniariko avela ashundo ande vediara; ai so mothona ando khan andel sobi, avela phendo po chardako le kheresko.
3Kwa hiyo, kila mliyosema gizani, watu watayasikia katika mwanga, na kila mliyonong'ona faraghani milango imefungwa, yatatangazwa juu ya nyumba.
4"Me phenav tumenge, murhe vortacha, "Na daran katar kodole kai mudarel o stato, ai pala kodia nashti mai keren kanchi mai but.
4"Nawaambieni ninyi rafiki zangu: msiwaogope wale wanaoua mwili, wasiweze kufanya kitu kingine zaidi.
5Sikavava tumenge kastar trobul te daran: daran katar kodo kana si les e putiera te shudel tu ande iado. Me phenav tumenge, lestar daran.
5Nitawaonyesheni yule ambaye ni lazima kumwogopa: mwogopeni yule ambaye baada ya kuua ana uwezo wa kumtupa mtu katika moto wa Jehanamu. Naam, ninawaambieni, mwogopeni huyo.
6"Na bichin de panzhe chiriklian pa dui teliara? Numa chi iek anda lende nai bustardo angla Del.
6Inajulikana kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti kumi, au sivyo? Lakini mbele ya Mungu hasahauliki hata mmoja.
7Ai vi tumare bal sa jinde le. Na daran, tume mon mai but sar but chiriklia.
7Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope, basi, ninyi mna thamani zaidi kuliko shomoro wengi!
8"Phenav tumenge, kon godi phenela ke si murho anglal manush, i me phenava ke si murho anglal le angeluria le Devleske;
8"Nawaambieni kweli, kila mtu anayekiri hadharani kwamba yeye ni wangu, Mwana wa Mtu naye atakiri mbele ya malaika wa Mungu kwamba mtu huyo ni wake.
9Numa kon godi phenela ke nai murho anglal manush, i me phenava ke nai murho anglal le angeluria le Devleske.
9Lakini, mtu yeyote anayenikana mbele ya watu, naye atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
10"Ai kon godi dela duma nasul karing O Shav le Manushesko avela leske iertime; numa kon godi dela duma nasul karing o Swunto Duxo shoxar chi avela iertime.
10"Yeyote anayesema neno la kumpinga Mwana wa Mtu atasamehewa; lakini anayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11Kana ningerena tume angla le synagoguria ai le guvrnuria, ai le bare, na xan tume briga sar phenena vai so phenena:
11"Watakapowapeleka ninyi mbele ya masunagogi na mbele ya wakuu na watawala msiwe na wasiwasi juu ya jinsi mtakavyojitetea au jinsi mtakavyosema.
12Ke o Swunto Duxo sicharela tumen ande kado chaso so te phenen."
12Kwa maana wakati huo Roho Mtakatifu atawafundisheni kile mnachopaswa kusema."
13Vari kon phendia leske, "Gazda, phen murhe phraleske te xulavel mansa o barvalimos kai si ame."
13Mtu mmoja katika ule umati wa watu akamwambia, "Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane urithi aliotuachia baba."
14O Jesus phendia leske, "Tu manushale, kon thodian ma te kerav tumenge kris, ai te kerav o xulaimos?"
14Yesu akamjibu, "Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi mwamuzi au msuluhishi kati yenu?"
15Ai porme phendia lenge, "Arakhen tume zurales, te na avel tumenge drago zurales le barvalimata la phuviake, ke o traio le manushesko chi ashel anda pesko barvalimos, vi te avela defial barvalo."
15Basi, akawaambia wote, "Jihadharini na kila aina ya tamaa; maana uzima wa mtu hautegemei wingi wa vitu alivyo navyo."
16Ai phendia lenge aver paramichi, phenelas, ieke manusheske phuvia kai sas barvalo dine les but mishtimos.
16Kisha akawaambia mfano: "Kulikuwa na tajiri mmoja ambaye shamba lake lilizaa mavuno mengi.
17Ai wo gindilas ande peste, phenelas, 'So te kerav, kai nai ma dosta than te thav sa murhe fruti?'
17Tajiri huyo akafikiri moyoni mwake: Nitafanyaje nami sina mahali pa kuhifadhia mavuno yangu?
18Ai phendia, 'Zhanav so te kerav, peravava murhe shteli, ai kerav mai bare; ai thava sa murho jiv ai murho mishtimos andre.'
18Nitafanya hivi: nitabomoa ghala zangu na kujenga kubwa zaidi, na humo nitahifadhi mavuno yangu yote na mali yangu.
19Ai phenava murho duxoske, "Murho duxo, si tu but mishtimos garado pe but bersh; akana hodinis, xas, pes, ai raduisavo."
19Hapo nitaweza kuiambia roho yangu: sasa unayo akiba ya matumizi kwa miaka na miaka. Ponda mali, ule, unywe na kufurahi.
20Numa O Del phendia leske, "Prosto san, e riat cho duxo avela lino; ai so lashardian kaske ashela?"
20Lakini Mungu akamwambia: Mpumbavu wewe; leo usiku roho yako itachukuliwa. Na vitu vile vyote ulivyojilundikia vitakuwa vya nani?"
21Kadia si kodoleske kai chidel manjin peske, ai kai nai barvalo le Devlesko.
21Yesu akamaliza kwa kusema "Ndivyo ilivyo kwa mtu anayejilundikia mali kwa ajili yake mwenyewe, lakini si tajiri mbele ya Mungu."
22O Jesus phendia leske disiplonge, "Anda kodia phenav tumenge, na daran anda tumaro traio, anda so xana, anda tumaro stato, andal tsalia te vuriarven tume.
22Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Kwa sababu hiyo nawaambieni, msiwe na wasiwasi juu ya chakula mnachohitaji ili kuishi, wala juu ya mavazi mnayohitaji kwa ajili ya miili yenu.
23O traio mai baro sar o xabe, ai o stato mai but sar le tsalia.
23Kwa sababu uzima ni bora kuliko chakula, na mwili ni bora kuliko mavazi.
24Dikhen pel chiriklia, chi shuden sumuntsi ai chi chiden, ai chi garaven xaben andel banuria; ai O Del pravarel le! Chi mon tume mai but sar le chiriklia?
24Chukueni kwa mfano, kunguru: hawapandi, hawavuni wala hawana ghala yoyote. Hata hivyo, Mungu huwalisha. Ninyi mna thamani zaidi kuliko ndege!
25"Savo anda tumende te nekezhila sai lunzharel pesko traio xantsi?
25Ni nani kati yenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza urefu wa maisha yake?
26Te nashti kerena kanchi kai si tsinorhi diela, sostar nekezhin tume pa aver dieli?
26Basi, kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini kuwa na wasiwasi juu ya yale mengine?
27Dikhen sar barion le luluja, chi keren buchi, ai chi keren peske tsalia; ai inker mothav tumenge, chi o Solomon, ande sa pesko barvalimos nas kadia shukar huriardo sar iek luluji.
27Angalieni maua jinsi yanavyomea. Hayafanyi kazi wala hayafumi. Hata hivyo, nawahakikishieni kwamba hata Solomoni mwenyewe na fahari zake zote hakupata kuvikwa vizuri kama ua mojawapo.
28O Del huriarvel e char kai si pel kimpuria adies, ai kai terhara avela shudini ande iag. Sode mai but huriarvel tumen, tume kai si tume xantsi pachamos?
28Lakini, kama Mungu hulivika vizuri jani la shambani ambalo leo liko na kesho latupwa motoni, je, hatawafanyia ninyi zaidi? Enyi watu wenye imani haba!
29Ai tume, na roden so xana, ai so pena, ai na nekezhin tume.
29"Basi, msivurugike akili, mkihangaika daima juu ya mtakachokula au mtakachokunywa.
30Ke kodia roden le manush kai chi zhanen le Devles. Tumaro Dat kai si ando rhaio zhanel ke trobul tumen sa kadala dieli.
30Kwa maana hayo yote ndiyo yanayohangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo.
31Roden mai anglal e amperetsia le Devleski ai O Del dela tume sa kadal dieli opral.
31Shughulikieni kwanza Ufalme wa Mungu, na hayo yote mtapewa kwa ziada.
32Na daran, murhe bakriorha, ke tumaro Dat mangel te del tume e amperetsia.
32"Msiogope, enyi kundi dogo! Maana Baba yenu amependa kuwapeni Ufalme.
33Bichinen so si tume, ai den kal chorhe; keren tumenge manjin kai chi rimolpe, kai chi nandiol ando rhaio, kai o chor nashti den andre te choren ai e rhuzhina nashti rimol.
33Uzeni mali yenu mkawape maskini misaada. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, na jiwekeeni hazina mbinguni ambako haitapungua. Huko wezi hawakaribii, wala nondo hawaharibu.
34Ke kai si cho manjin, kotse si te avela cho ilo.
34Pale ilipo hazina yako, ndipo pia utakapokuwa moyo wako.
35"Aven gata ai huriardo, ai cho lampo del iag;
35"Muwe tayari! Jifungeni mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka;
36Ai te aven sar manush kai azhukeren penge gazdas te avel ka abiav; Kana avela ai kana marela, won sai phutren leske.
36muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka arusini, ili wamfungulie mara atakapobisha hodi.
37Raduime te aven le slugi, kana lengo gazda arakhela len gata kana avela palpale; chachimasa, phenav tumenge, thola peski prashtia, ai thola le te beshen tele kai skafidi, ai podaila le.
37Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia.
38O gazda sai avela mashkar la rachake vai mai pozno! Ai arakhela len gata. Raduime te aven le slugi.
38Heri yao watumishi hao ikiwa bwana wao atawakuta wanakesha hata ikiwa atarudi usiku wa manane au alfajiri.
39Te zhanen mishto, o gazda le kheresko te zhanelas kana o chor avel, wo lino sama sorho riat, ai chi meklino te phagavel lesko kher.
39Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe.
40Vi tume, aven gata. Ke O Shav le Manushesko avela ka chaso kai tume chi zhanena."
40Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia."
41O Petri phendia leske, "Devla, tu phenes kadia paramichi amenge vai savorhenge?"
41Petro akamwambia, "Bwana, mfano huo ni kwa ajili yetu tu, au ni kwa ajili ya watu wote?"
42Ai O Del phendia, "Kon si o chacho ai gojaver sluga, kai o gazda thodias te lel sama ande lesko kher te pravarel le lengo xaben pe vriama kai trobul?
42Bwana akajibu, "Ni nani basi, mtumishi aliye mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya watumishi wake ili awape chakula wakati ufaao?
43Raduime te avel kodia sluga, kai lesko gazda arakhela les ke kerel peski buchi kana avela palpale.
43Heri yake mtumishi huyo ikiwa bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44Chachimasa phenav tumenge, si te thol les baro pe so godi si les.
44Hakika atampa madaraka juu ya mali yake yote.
45"Numa kodia sluga te phenel peste, 'Murho gazda podail, chi avilo.' Ai marel le slugen, ai tholpe te xal, ai pel, ai te machol.
45Lakini, kama mtumishi huyo atafikiri moyoni mwake: na kusema: Bwana wangu amekawia sana kurudi halafu aanze kuwapiga watumishi wenzake, wa kiume au wa kike, na kula, kunywa na kulewa,
46O gazda kodola slugako si te avel andek dies kai wo chi azhukerel les, ai andek chaso kai wo chi zhanel, si te shinel les kotora, ai thol les kodolensa kai ankerdion so nai.
46bwana wake atarudi siku asiyoitazamia na saa asiyoijua; atamkatilia mbali na kumweka fungu moja na wasioamini.
47"Ai kodo sluga kai zhanel so mangel lesko gazda, ai chi kerdia kanch, ai chi kerdia so manglia lesko gazda, avela mardo butivar.
47Mtumishi ambaye anajua matakwa ya bwana wake lakini hajiweki tayari kufanya anavyotakiwa, atapigwa sana.
48Numa wo kai chi zhanel so mangel lesko gazda, ai kerdia le dieli bi malades, trobul te avel mardo, avela mardo mai xantsi. Ka kodo manush kai sas dino but trobul te del but; te si but dino kal manush, won phushen mai but lestar.
48Lakini yule afanyaye yanayostahili adhabu bila kujua, atapigwa kidogo. Aliyepewa vingi atatakiwa vingi; aliyekabidhiwa vingi zaidi atatakiwa kutoa vingi zaidi.
49"Avilem te shudav iag pe phuv; ai sode kamlemas te avel vunzhe dino iag?
49"Nimekuja kuwasha moto duniani, laiti ungekuwa umewaka tayari!
50Si iek bolimos kai me trobul te avav boldo; ai chi zhanav sar mai sigo te kerdiol kodo bolimos.
50Ninao ubatizo ambao inanipasa niupokee; jinsi gani ninavyohangaika mpaka ukamilike!
51Tume gindin ke avilem te anav e pacha pe phuv? Phenav tumenge, Nichi, avilem te hulavav.
51Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? Hata kidogo; si amani bali utengano.
52Ke dakanara panzh zhene ando iek kher hulade (chi aven iek fielo), trin chi malevana pala dui, ai dui chi malavena pala trin.
52Na tangu sasa, jamaa ya watu watano itagawanyika; watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53Xuladia o dat katar o shav, ai o shav katar o dat; ai e dei katar e shei, ai e shei katar e dei; ai e sakra katar e bori, ai e bori katar e sakra."
53Baba atakuwa dhidi ya mwanawe, mwana dhidi ya baba yake; mama dhidi ya bintiye, binti dhidi ya mama yake; mama mkwe dhidi ya mke wa mwanawe na huyo dhidi ya mama mkwe wake."
54Ai mai phendia le narodoske, "Kana dikhen iek nuvero kai avel anda Westo, tume strazo mothon, del breshind, ai kodia kerdiol.
54Yesu akayaambia tena makundi ya watu, "Mnapoona mawingu yakitokea upande wa magharibi, mara mwasema: Mvua itanyesha, na kweli hunyesha.
55Ai kana dikhen te phurdel e barval anda Souto, tume mothon, te avela tato, ai kodia kerdiol.
55Mnapoona upepo wa kusi unavuma, mwasema Kutakuwa na hali ya joto na ndivyo inavyokuwa.
56Tume manush kai ankerdion so chi san! Tume sai den po gor le dieli la phuviake ai le chereske, apo sostar te na haliaren le dieli kai si adies?
56Enyi wanafiki! Mnajua kutabiri hali ya hewa kwa kuangalia dunia na anga; kwa nini basi, hamwezi kujua maana ya nyakati hizi?
57Ai sostar, chi den po gor, anda tumende so si vorta?
57"Na kwa nini hamwezi kujiamulia wenyewe jambo jema la kufanya?
58Te thola vari kon dosh pe tute, ai te zhana andek than ka kher le forosko, zumav mai anglal te sai lashardios lesa pa drom, ke sai angerel tu anglai kris, ai e kris del tu kai zhandari ai zhandari thol tu ande temnitsa.
58Maana kama mshtaki wako anakupeleka mahakamani, ingekuwa afadhali kwako kupatana naye mkiwa bado njiani, ili asije akakupeleka mbele ya hakimu, naye hakimu akakutoa kwa polisi, nao wakakutia ndani.
59Phenav tuke, chi anklesa kotsar avri, mai anglal ke sar te pochines so godi kames.
59Hakika hutatoka huko nakwambia, mpaka utakapomaliza kulipa senti ya mwisho."