1Ande kadia vriama uni manush kai sas kotse phende le manushen andai Galilee ai amisardia lengo rat le zheganensa kai mudarde sas angla Del.
1Wakati huo watu fulani walikuja, wakamweleza Yesu juu ya watu wa Galilaya ambao Pilato alikuwa amewaua wakati walipokuwa wanachinja wanyama wao wa tambiko.
2O Jesus phendia lenge, "Tume gindin ke kodola manush kai sas andai Galilee mai bezexale sas sar sa le kolaver manush andai Galilee, ke chinuisarde kadia?
2Naye Yesu akawaambia, "Mnadhani Wagalilaya hao walikuwa wahalifu zaidi kuliko Wagalilaya wengine, ati kwa sababu wameteseka hivyo?
3Me phenav tume, Nichi, te na keina tume anda tumare bezexa, xasavona savorhe.
3Nawaambieni hakika sivyo; lakini nanyi, hali kadhalika, msipotubu, mtaangamia kama wao.
4Ai kodola desh u oxto manush kai pelo pe lende o baro kher ande Siloam, ai mudarde le, tume gindin ke mai doshale sas sar sa o narodo kai si ando Jerusalem?
4Au wale kumi na wanane walioangukiwa na mnara kule Siloamu wakafa; mnadhani wao walikuwa wakosefu zaidi kuliko wengine wote walioishi Yerusalemu?
5Phenav tumenge, Nichi, Numa te na keina tume ande tumare bezexa, xasavona savorhe."
5Nawaambieni sivyo; lakini nanyi msipotubu, mtaangamia kama wao."
6Ai mai phendia lenge ek paramichi, "Iek manush sas les ek pruing le figenge ande leske rez, gelo te rodel figi pa late, chi arakhlia kanch.
6Kisha, Yesu akawaambia mfano huu: "Mtu mmoja alikuwa na mtini katika shamba lake. Mtu huyu akaenda akitaka kuchuma matunda yake, lakini akaukuta haujazaa hata tunda moja.
7Ai phendia kodoleske kai lel sama katar e rez, 'Dikh! De trin bersh si de sar avilem katse te rodav figi pe pruing le figenge, ai chi arakhlem kanch. Shin la, so mai mekhas te lel o than pe phuv intaiin?'
7Basi, akamwambia mfanyakazi wake: Angalia! Kwa miaka mitatu nimekuwa nikija kuchuma matunda ya mtini huu, nami nisiambulie kitu. Ukate! Kwa nini uitumie ardhi bure?
8O manush kai lelas sama katar e rez phendia leske, 'Devla! Mai mek la kado bersh. Pharhava e phuv ai thava so trobul;
8Lakini naye akamjibu: Bwana, tuuache tena mwaka huu; nitauzungushia mtaro na kuutilia mbolea.
9Ai amborim mai angle avela fruta, te na shinesa la.'"
9Kama ukizaa matunda mwaka ujao, vema; la sivyo, basi utaweza kuukata."
10O Jesus sicharelas ande synagogue andek dies savatone.
10Yesu alikuwa akifundisha katika sunagogi moja siku ya Sabato.
11Ai eta, kotse sas iek zhuvli kai sas bi vuzho ande late, ai nashti vortolas pe de desh u oxto bersh. Bangi sas andal zea, ai nashtilas te vortolpe.
11Na hapo palikuwa na mwanamke mmoja aliyekuwa mgonjwa kwa miaka kumi na minane kutokana na pepo aliyekuwa amempagaa. Kwa sababu hiyo, mwili wake ulikuwa umepindika vibaya hata asiweze kusimama wima.
12Ai kana O Jesus dikhlia la, phendia lake, "Zhuvlio, sastilian."
12Yesu alipomwona, alimwita, akamwambia, "Mama, umeponywa ugonjwa wako."
13Ai thodia lesko vas pe late; ai strazo vortosaili, ai naisisardia le Devles.
13Akamwekea mikono, na mara mwili wake ukawa wima tena, akawa anamtukuza Mungu.
14Numa o baro la synagogako xoliarikosas, ke O Jesus sastiardias po Savatone, ai o baro phendia la narodoske, "Shov dies si te kerelpe buchi, aven te sastion kadala diesa, ai na Savatone.
14Lakini mkuu wa sunagogi alikasirika kwa sababu Yesu alikuwa amemponya siku ya Sabato. Hivyo akawaambia wale watu walikusanyika pale, "Mnazo siku sita za kufanya kazi. Basi, fikeni siku hizo mkaponywe magonjwa yenu; lakini msije siku ya Sabato."
15Devla phendia leske, "Tu manush kai ankerdiol so chi san! Savo anda tumende Savatone chi phutrel andal shtali peske gurumlia vai peske magares, te angerel le te pen?
15Hapo Bwana akamjibu, "Enyi wanafiki! Nani kati yenu hangemfungua ng'ombe au punda wake kutoka zizini ampeleke kunywa maji, hata kama siku hiyo ni ya Sabato?
16Ai e zhuvli kai si e shei la Abrahamoski, ai kai o beng ankerelas la de desh u oxto bersh, chi trobulas te sastiarav la Savatone?"
16Sasa, hapa yupo binti wa Abrahamu ambaye Shetani alimfanya kilema kwa muda wa miaka kumi na minane. Je, haikuwa vizuri kumfungulia vifungo vyake siku ya Sabato?"
17Sar delas duma, sa kodola manush kai sas leske duzhmaia, lazhaile sas; ai sa le manush raduimesas andal bucha shukar kai kerelas O Jesus.
17Alipokwisha sema hayo, wapinzani wake waliona aibu lakini watu wengine wote wakajaa furaha kwa sababu ya mambo yote aliyotenda.
18Porme O Jesus phendia, "Pe soste miazol e amperetsia le Devleski? Ai pe soste sai miazol?
18Yesu akauliza: "Ufalme wa Mungu unafanana na nini? Nitaulinganisha na nini?
19Si sar iek sumuntsa garchitsaki, kai iek manush lia, ai shudia ande peski niva; bariol, ai kerdiol ek baro khash; ai le chiriklia anda cheri beshle pel krenzhi."
19NI kama mbegu ya haradali aliyotwaa mtu mmoja na kuipanda shambani mwake; ikaota hata ikawa mti. Ndege wa angani wakajenga viota vyao katika matawi yake."
20Ai mai phendia,
20Tena akauliza: "Nitaulinganisha Ufalme wa Mungu na nini?
21"Pe soste miazol e amperetsia le Devleski? Si sar o drozhdi, kai ek zhuvli lias ai thodias ande trin musuri arho te puchilo sa o arho.
21Ni kama chachu aliyoitwaa mama mmoja na kuichanganya pamoja na unga debe moja kisha unga wote ukaumuka wote."
22Jesus nakhelas andel foruria ai andel gava, sicharelas, ai zhalas karing o Jerusalem.
22Yesu alindelea na safari yake kwenda Yerusalemu huku akipitia mijini na vijijini, akihubiri.
23Vari kon phendia leske, "Devla, ferdi xantsi manush si kai avela skepime?" Ai O Jesus phendia lenge,
23Mtu mmoja akamwuliza, "Je, Mwalimu, watu watakaookoka ni wachache?"
24"Thon zor te zhan pa e tang vurota; ke me phenav tumenge, but zumavena te zhan andre, numa nashtina.
24Yesu akawaambia, "Jitahidini kuingia kwa kupitia mlango mwembamba; maana nawaambieni, wengi watajaribu kuingia lakini hawataweza.
25Kana o gazda le kheresko wushtela, ai phandavela o wudar, ai tumen beshen avri, ai chinaiina te maren anda o wudar, ai phenenas, 'Devla, Devla, phuter amenge,' ai wo phenela tumenge, 'Chi zhanav katar san.'
25"Wakati utakuja ambapo mwenye nyumba atainuka na kufunga mlango. Ninyi mtasimama nje na kuanza kupiga hodi mkisema: Bwana, tufungulie mlango. Lakini yeye atawajibu: Sijui mmetoka wapi.
26Antunchi phenena, 'Xaliam ai piliam tusa, ai tu phendian cho zakono pe amare droma.'
26Nanyi mtaanza kumwambia: Sisi ndio wale tuliokula na kunywa pamoja nawe; na wewe ulifundisha katika vijiji vyetu.
27Ai wo phenela lenge, 'Phenav tumenge, chi zhanav katar san; zhantar mandar, sa tume bucharia le bezexeske.'
27Lakini yeye atasema: Sijui ninyi mmetoka wapi; ondokeni mbele yangu, enyi nyote watenda maovu.
28Kotse kai roven ai kai chiden dandendar, kana dikhen la Abramos, ai o Isaak, ai o Iakov, ai sa le profeton, ande amperetsia le Devleski, ai tume avena shudine avri.
28Ndipo mtakuwa na kulia na kusaga meno, wakati mtakapowaona Abrahamu, Isaka na Yakobo, na manabii wote wapo katika Ufalme wa Mungu, lakini ninyi wenyewe mmetupwa nje!
29Avena andai Easto, ai andai Westo, ai andai Norto, ai andai Southo ai thonpe kai skafidi ande amperetsia le Devleski.
29Watu watakuja kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini, watakuja na kukaa kwenye karamu katika Ufalme wa Mungu.
30Ashun! Uni kai si palune aven anglune, ai uni kai si anglune aven palune."
30Naam, wale walio wa mwisho watakuwa wa kwanza; na wale walio wa kwanza watakuwa wa mwisho."
31Sa kodo dies uni Farizeanuria avile, phenenas leske, "Zhatar katsar, ke o Herod mangel te mudarel tu."
31Wakati huohuo, Mafarisayo na watu wengine walimwendea Yesu wakamwambia, "Ondoka hapa uende mahali pengine, kwa maana Herode anataka kukuua."
32Ai wo phendia lenge, "Zhan, ai phenen kodola zhigeniaki, 'Dikh! Goniv le bengen ai sastiarav adies ai terhera, ai o trito dies getova murhi buchi.'
32Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie huyo mbweha hivi: Leo na kesho ninafukuza pepo na kuponya wagonjwa, na siku ya tatu nitakamilisha kazi yangu.
33Numa trobul te phirav adies, ai terhara, ai kolaver dies, ke chi maladiol kai ek profeto xasavol andai Jerusalem.
33Hata hivyo, kwa leo, kesho na kesho kutwa, ni lazima niendelee na safari yangu, kwa sababu si sawa nabii auawe nje ya Yerusalemu.
34Jerusalem! Jerusalem! Kai mudaren le profeton, ai kai shuden baxensa kodola kai si tumenge tradine! Sodivar manglem te chidav che shaven, sar ek kaini kai chidel peske puion tela peske phaka. Numa tume chi manglian.
34"Yerusalemu! We Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako pamoja kama kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa yake, Lakini wewe umekataa.
35Dikh! Tumaro kher avela tumenge meklo; numa phenav tumenge, chi mai dikhena ma zhi kai chi mothona, Raduime kodo kai avel anda anav le Devlesko.'"
35Haya, utaachiwa mwenyewe nyumba yako. Naam, hakika nawaambieni, hamtaniona mpaka wakati utakapofika mseme: Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana."