Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

18

1O Jesus mai phendia lenge ek paramichi, te sikavel ke trobul sa data te rhugis tu, ai na aterdios;
1Basi, Yesu aliwasimulia mfano kuonyesha kwamba ni lazima kusali daima bila kukata tamaa.
2phenelas, "Sas andek foro iek ablakato, kai chi daralas katar O Del, ai vi chi respektisardia le manushen.
2Alisema: "Katika mji mmoja kulikuwa na hakimu ambaye hakuwa anamcha Mungu wala kumjali binadamu.
3Ai sas ek phivli ande kudo foro; woi avelas leste, phenelas, "Ker mange kris pek manush kai rodel mange nasul."
3Katika mji huohuo, kulikuwa pia na mama mmoja mjane, ambaye alimwendea huyo hakimu mara nyingi akimwomba amtetee apate haki yake kutoka kwa adui yake.
4Ai but vriama chi manglia te kerel lake so mangelas, numa antunchi phendia wo ande peste, "Chi darav katar O Del, ai chi respektiv le manush.
4Kwa muda mrefu huyo hakimu hakupenda kumtetea huyo mjane; lakini, mwishowe akajisemea: Ingawa mimi simchi Mungu wala simjali binadamu,
5Numa ke kodia phivli dziliarel ma, kerava lake so mangel, saxke te na mai avel te dziliarel ma."
5lakini kwa vile huyu mjane ananisumbua, nitamtetea; la sivyo ataendelea kufika hapa, na mwisho atanichosha kabisa!"
6O Devla mai phendia, "Ashunen so phendia o chorho ablakato.
6Basi, Bwana akaendelea kusema, "Sikieni jinsi alivyosema huyo hakimu mbaya.
7O Del sar te na kerel vorta peske manushenge kai mangenas lestar kuriat ai kujes? Azhukerel lungo vriama te zhutil le?
7Je, ndio kusema Mungu hatawatetea wale aliowachagua, ambao wanamlilia mchana na usiku? Je, atakawia kuwasikiliza?
8Phenav tumenge, kerela lenge sigo kris, numa kana O Shav le Manushesko avela, arakhela pachamos pe phuv?"
8Nawaambieni atawatetea upesi. Hata hivyo, je, kutakuwako na imani duniani wakati Mwana wa Mtu atakapokuja?"
9O Jesus phendia kacha paramichi pal manush kai pachanpe ande pende, ai vurhitsisardia sa le kolaver.
9Halafu Yesu aliwaambia pia mfano wa wale ambao walijiona kuwa wema na kuwadharau wengine.
10"Dui manush gele ande tamplo te rhuginpe; iek sas Farisi, ai o kaver sas manush kai chidelas e taksa.
10"Watu wawili walipanda kwenda Hekaluni kusali: mmoja Mfarisayo, na mwingine mtoza ushuru.
11O Farisi ande punrhende rhugilaspe ande peste, "O Devla, naisiv tuke, ke chi sim sar le kolaver manush, kai si chor, nai chacho, kai keren kurvia, ai vi sar o manush kai chidelas e taksa.
11Huyo Mfarisayo akasimama, akasali kimoyomoyo: Ee Mungu, nakushukuru kwa vile mimi si kama watu wengine: walafi, wadanganyifu au wazinzi. Nakushukuru kwamba mimi si kama huyu mtoza ushuru.
12Postiv duvar ando kurko, dav desh anda ek shel partia."
12Nafunga mara mbili kwa juma, natoa zaka sehemu ya kumi ya pato langu.
13O manush kai chidelas e taksa, beshelas mai dur, chi tromalas te vazdel le iakha karing o cheri, numa marelaspe ande kolin, ai phendia, "O Devla te avel tuke mila anda mande kai sim bezexalo."
13Lakini yule mtoza ushuru, akiwa amesimama kwa mbali bila hata kuinua macho yake mbinguni, ila tu akijipiga kifua kwa huzuni, alisema: Ee Mungu, unionee huruma mimi mwenye dhambi.
14Phenav tumenge, "Kado manush gelo peste khere iertime mai sigo ke sar o kolaver; ke kon godi vazdelape avela meklo tele; ai kodo kai mekelape tele avela vazdino."
14Nawaambieni, huyu mtoza ushuru alirudi nyumbani akiwa amesamehewa. Lakini yule mwingine, sivyo. Kwa maana kila anayejikweza atashushwa, na kila anayejishusha atakwezwa."
15Andine ka Jesus le tsinorhe glaten, te thol peske vas pe lende; numa kana le disipluria dikhle, dine le trad.
15Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awawekee mikono yake. Wanafunzi walipowaona, wakawazuia kwa maneno makali.
16Numa O Jesus akhardia le glaten peste, "Mek te aven le glate mande, ai na aterdiaren le, ke e amperetsia le Devleski si kodolenge kai miazon sar lende.
16Lakini Yesu akawaita kwake akisema: "Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana Ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu kama hawa.
17Phenav tumenge o chachimos, kako kai chi primila e amperetsia le Devleski sar ek glata nashti zhala andre."
17Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo, hataingia katika Ufalme huo."
18Iek manush la Krisako phushlia le Jesusos, "Lasho Gazda, so trobul te kerav te avel ma traio kai chi mai getol pe?"
18Kiongozi mmoja, Myahudi, alimwuliza Yesu, "Mwalimu mwema, nifanye nini ili niweze kuupata uzima wa milele?"
19O Jesus phendia leske, "Sostar mothos mange lasho? Ke nai khonik lasho. O Del ferdi lasho."
19Yesu akamwambia, "Mbona waniita mwema? Hakuna aliye mwema ila Mungu peke yake.
20Zhanes le zakonuria, "Na ker kurvia, na mudar, na chor, na xoxav, preznaisar che dades ai cha da."
20Unazijua amri: Usizini; usiue; usiibe; usitoe ushahidi wa uongo; waheshimu baba yako na mama yako."
21O manush phendia, "Sa kadala zakonuria ankerdem de sar sim tsinorho."
21Yeye akasema, "Hayo yote nimeyazingatia tangu ujana wangu."
22Kana O Jesus ashundia kodia, phendia leske, "Mai trobul te keres iek diela. Bichin sa so si tu, ai de kal chorhe, ai avela tu manjin ando rhaio; antunchi aidi pala mande."
22Yesu aliposikia hayo akamwambia, "Unatakiwa bado kufanya kitu kimoja: uza kila ulicho nacho, wagawie maskini, na hivyo utakuwa na hazina yako mbinguni; halafu njoo unifuate."
23Kana kodo manush ashundia kodia, nekezhisailo; ke defial barvalo sas.
23Lakini huyo mtu aliposikia hayo, alihuzunika sana kwa sababu alikuwa tajiri sana.
24Kana O Jesus dikhlia ke tristosailo, phendia, "Trutno kodolenge kai si le barvalimos te zhan ande amperetsia le Devleski.
24Yesu alipoona akihuzunika hivyo, akasema, "Jinsi gani ilivyo vigumu kwa matajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu!
25Ke mai vushoro te nakhel iek gemula andai iakh la suviaki, de sar iek barvalo manush te zhal ande amperetsia le Devleski.
25Naam, ni rahisi zaidi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano, kuliko tajiri kuingia katika Ufalme wa Mungu."
26Le manush kai ashunenas leste phende, "Apo, kon sai avela skepime?"
26Wale watu waliposikia hayo, wakasema, "Nani basi, atakayeokolewa?"
27O Jesus phendia, "Le manush anda pende nashtin, numa le Devlesa vari so sai kerdiol."
27Yesu akajibu, "Yasiyowezekana kwa binadamu, yanawezekana kwa Mungu."
28Antunchi o Petri phendia, "Dikh! Ame mekliam swako fielo ai liam ame pala tute." O Jesus phendia lenge,
28Naye Petro akamwuliza, "Na sisi je? Tumeacha vitu vyote tukakufuata!"
29"Phenav tumenge o chachimos, Kon godi mekela kher, rhomni, vai phralen, dades, vai da, vai glaten pala e amperetsia le Devleski,
29Yesu akawaambia, "Kweli nawaambieni, mtu yeyote aliyeacha nyumba au mke au kaka au wazazi au watoto kwa ajili ya Ufalme wa Mungu,
30avela les mai but pe kadia phuv, ai ande kolaver traio kai chi mai getolpe."
30atapokea mengi zaidi wakati huu wa sasa, na kupokea uzima wa milele wakati ujao."
31Antunchi O Jesus lia le desh u do disiplon rigate, ai phendia lenge, "Ashun, ame zhas ando Jerusalem, ai so godi sas ramome katar le profeturia pa Shav le Manushesko kerdiola.
31Yesu aliwachukua kando wale kumi na wawili, akawaambia, "Sikilizeni! Tunakwenda Yerusalemu na huko kila kitu kilichoandikwa na manabii kuhusu Mwana wa Mtu kitakamilishwa.
32Dena les kal manush kai Nai Zhiduvuria te marena mui lestar, ai chinuina les, ai chungardena pe leste, ai marena les le bichosa, ai mudarena les,
32Kwa maana atakabidhiwa kwa watu wa mataifa nao watamtendea vibaya na kumtemea mate.
33ai o trito dies si te zhuvindil."
33Watampiga mijeledi, watamuua; lakini siku ya tatu atafufuka."
34Numa le disipluria chi haliarde so phendia lenge; ai kadala vorbi garadesas lendar, won chi haliarenas sar divinilas O Jesus.
34Lakini wao hawakuelewa hata kidogo jambo hilo; walikuwa wamefichwa maana ya maneno hayo, na hawakutambua yaliyosemwa.
35Kana O Jesus pasholas pasha Jericho, iek korho beshelas tele pasha drom, ai mangelas kristaradia:
35Wakati Yesu alipokaribia Yeriko, kulikuwa na mtu mmoja kipofu ameketi njiani akiomba.
36Kai ashundia le manushen sar nakhen, phushelas, "So si?"
36Aliposikia umati wa watu ukipita aliuliza, "Kuna nini?"
37Phende leske, O Jesus anda Nazareth nakhel katsar.
37Wakamwambia, "Yesu wa Nazareti anapita."
38Numa wo tsipisardia, phenelas, "Jesus, tu Shav le Davidosko! Av tuke mila anda mande!"
38Naye akapaza sauti akisema, "Yesu, Mwana wa Daudi, nihurumie!"
39Le manush kai sas anglal tsipinas pe leste te ashel, numa wo tsipilas mai zurales, "Tu Shav le Davidosko! Av tuke mila anda mande."
39Wale watu waliotangulia wakamkemea wakimwambia anyamaze; lakini yeye akazidi kupaza sauti: "Mwana wa Daudi, nihurumie;"
40O Jesus aterdilo, ai phendia o korho te anen leste; ai kana andine les, phushlia les, phenelas,
40Yesu alisimama, akaamuru wamlete mbele yake. Yule kipofu alipofika karibu, Yesu akamwuliza,
41"So manges te kerav tuke?" Wo phendia, "Devla, Phuter murhe iakha te dikhav."
41"Unataka nikufanyie nini?" Naye akamjibu, "Bwana, naomba nipate kuona tena."
42O Jesus phendia leske, "Antunchi dikhes! Cho pachamos sastiardian tu."
42Yesu akamwambia, "Ona! Imani yako imekuponya."
43Ai strazo dikhlia, ai liape pala Jesus, ai luvudilaspe ka Del; ai sa o narodo kana dikhle so kerdilia luvudinaspa ka Del.
43Na mara yule aliyekuwa kipofu akapata kuona, akamfuata Yesu akimtukuza Mungu. Watu wote walipoona hayo, wakamsifu Mungu.