Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

19

1O Jesus gelo ando Jericho, nakhlo anda foro.
1Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
2Sas iek manush barvalo kai busholas Zacchaeus. Wo sas o baro mashkar le manush kai chidenas e taksa,
2Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
3ai kado manush rodelas te zhanel kon si O Jesus; numa nashtilas katar o but narodo, ke tsinorho sas.
3Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
4Nashlo angle, ai anklisto pe ek khash kai busholas Sicamore te dikhel les; ke O Jesus sas te nakhel kotsar.
4Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
5Kana O Jesus areslo pe kodo than, vazdia le iakha opre, dikhlia les, ai phendia leske, "Zacchaeus, huli tele mai sigo, ke trobul adies te beshav ande cho kher."
5Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, "Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako."
6O Zacchaeus hulisto sigo tele, ai premisardia les peste raduimasa.
6Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
7Ai kana le manush dikhle so kerdilia, denas pe duma, phenenas, "O Jesus zhal te beshel le manusha kai si bezexalo."
7Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, "Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi."
8O Zacchaeus angla Jesus sa, ai phendia le Devleske, "Ashun Devla! Dav dopash anda murho barvalimos kal chorhe; ai te lem katar vari kon ande vari soste, dava les shtarvar mai but."
8Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
9O Jesus phendia leske, "O skepimos avilo adies ande kado kher, ke vi kako si iek shav le Abrahamosko.
9Yesu akamwambia, "Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
10Ke O Shav le Manushesko avilo te rodel ai te skepil kon sas xasardo."
10Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea."
11Sar le manush ashunenas, O Jesus phendia lenge ek paramichi, ke pasha Jerusalem sas, ai ke gindinaspe ke e amperetsia le Devleski sas te sikadiol strazo.
11Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
12No O Jesus phendia, "Iek manush barvalo gelotar ande them dur te keren anda leste amperato ai te avel palpale.
12Hivyo akawaambia, "Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
13Ai akhardia peske desh slugen, ai dia sakones iek galbano sumnakuno, ai phendia lenge, "Keren buchi kadale sumnakasa zhi kai avav."
13Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
14Numa le manush kodole manusheske gretsosarde les, ai trade vari kas te phenen leske, "Chi mangas kado manush te avela amaro amperato."
14Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
15Kotse kai gelo kerde amperato anda leste, ai kana avilo palpale ande pesko them, wo akhardia le slugen kai dias len o sumnakai, wo manglia te zhanel sode mai but swako sluga sas les pala leski buchi.
15"Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
16O pervo avilo ai phendia, "Gazda, nirisardem aver desh galbi le galbanosa kai dian ma.
16Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
17Ai o gazda phendia leske, "Mishto kerdian, lasho sluga; kai sanas lasho ande xantsi buchi, dava tu desh foruria te poronchis pe lende."
17Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
18O duito avilo ai phendia leske, "Gazda, nirisardem aver pansh galbi le galbanosa kai dian ma."
18Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
19O gazda phendia leske, "Vi tu poronchisa pe pansh foruria."
19Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
20Aver avilo phenelas, "Gazda, Dikh! Katse si cho galbano kai dian ma, garadem les ande poxtan.
20"Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
21Ke darailem tutar, ke tu san manush zurale ilesko: tu les so chi dian, ai chides so chi bariardian."
21kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
22O amperato phendia leske, "Dav tu kris pala che vorbi, tu san chorho sluga, tu zhanesas ke sim manush zurale ilesko, lav so chi dem, ai chidav so chi bariardem.
22Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
23Apo, "Sostar chi thodian murhe love ande banka? Saxke, kana avilemas khere sas te bution?"
23Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
24Porme phendia kodolenge kai sas kotse, "Len lestar o galbano, ai den les ka kako kai si les desh."
24Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
25Le kolaver phendia leske, "Gazda, si les vunzhe desh galbi!"
25Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
26O Jesus phendia, "Me phenav tumenge, avela dino ka kuko kai si les; numa ka kuko kai nai, avela lino lestar vi so si les.
26Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
27Numa le manush kai chi mai le te avav lengo amperato, anen le katse, ai mudaren le angla mande."
27Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu."
28Kana phendia kodia paramichi, O Jesus gelotar angla manush te zhal ande Jerusalem.
28Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
29Kana pashilo pashai Bethphage ai Bethani karing e plai kai busholas E Plai le Maslinengi, O Jesus tradia dui anda peske disiplonge, phenelas,
29Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
30"Zhan ando gav kai si angla amende; ai kana aresena, arakhena kotse ieke magares kai si phanglo, pe kodo magari inker chi iek manush chi beshlo; phutren les, ai anen les katse.
30akawaambia: "Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
31Te phushela tumen vari kon, "Sostar phutren le magares?" Tume phenen leske, "Ke trobul le Devles."
31Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye."
32Le disipluria kai sas tradino gele, ai arakhle sa le dieli sar O Jesus phendiasas lenge.
32Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
33Kana phutrenas le magares, o gazda phendia lenge, "Sostar phutren le magares?"
33Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, "Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?"
34Ai won phende, "Ke trobul le Devles."
34Nao wakawajibu, "Bwana anamhitaji."
35Angerde le magares ka Jesus; ai thode pe penge raxamia po magari, ai thode le Jesusos te beshel opral.
35Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
36Sar phirelas, won shudenas penge raxamia po drom.
36Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
37Ai kana pasholas pashai Jerusalem, karing e plaiing kai xulelas e plaiing kai bushol E Plaiing le Maslinenge, sa le disipluria raduime sas, ai dine naisimos ka Del pala sa le mirakluria kai dikhle; phenenas,
37Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
38"Raduime te avel o amperato kai avel ando anav le Devlesko! Pacha ando rhaio, ai o barimos te avel ando rhaio."
38wakawa wanasema: "Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!"
39Ai uni Farizeanonge kai sas mashkar o narodo, phende le Jesusoske, "Gazda, phen che disiplonge te terdion."
39Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, "Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!"
40Ai O Jesus phendia lenge, "Me phenav tumenge, te terdiona won te tsipin, le bax si te tsipin."
40Yesu akawajibu, "Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti."
41Ai kana pasholas pasha foro, O Jesus dikhelas pe Jerusalem ai rovelas,
41Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
42ai phenelas, "Te zhanglianas ande kado dies le dieli kai si cha pachake! Numa akana garade le angla che iakha.
42akisema: "Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
43Uni diesa avela pe tute kana che duzhmaia avena kruglom tutar, phandavena tu, ai chidena tu pa sako rik.
43Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
44Phagavena tu ai sa le manushen mashkar tute; ai chi mekena pe tute te ashel bax pe baxeste ke chi zhanglian e vriama kana O Del avilo te skepil tu."
44Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa."
45O Jesus avilo ande tampla, ai gonisardia sa kodolen kai bichinenas ai chinenas,
45Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
46ai phenel lenge, "Ramome, 'Murho kher si o kher le rhugimasko; numa tume kerdian anda leste kher chorengo.'"
46akisema, "Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi."
47O Jesus sicharelas swako dies ande tampla, ai le bare rasha, ai le Gramnoturia, ai le bare le narodoske rodenas te mudaren le Jesusos.
47Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
48Numa chi zhanenas sar te keren; ke sa le manush drago lenge te ashunen leste.
48lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.