Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

6

1Andek dies Savatone O Jesus nakhelas andel kimpuria le jiveske, leske disipluria lenas jiv, phagenas le jiv ande penge vas, ai xale.
1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
2Uni Farizeanuria phende lenge, "Sostar keren so nai slobodo te keren Savatone?"
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
3O Jesus dia le atweto, "Pate chi jindian so kerdia o David, kana wo ai kodola kai sas lesa bokhale sas.
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
4Gelo ando kher le Devlesko, ai lia le manrhe (Shewbread), ai xalia ai dia kodolen kai sas lesa, ai nai slobodo te keren kadia de ferdi le rashange te xan kodo manrho?"
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
5Ai mai phendia lenge, "Ke O Shav le Manushesko si o Gazda po Savato."
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
6Aver dies pale Savatone O Jesus gelo ande synagogue ai sicharelas; ai kotse sas o manush kai o vas o chacho kodole le manushesko sas shuko.
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
7Le Gramnoturia ai le Farizeanuria mangenas te thon dosh pe leste. Lenas sama po Jesus te sastiarela vari kas Savatone.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
8Numa O Jesus zhanelas lenge ginduria, ai phendia le manusheske kai sas lesko vas shuko, "Vushti opre, ai besh kata mashkaral." Vushtilo opre.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
9Antunchi O Jesus phendia lenge, "Phushav tume, So si slobodo adies Savatosko te kerel mishtimos vai te kerel nasulimos; te sai skepis le manushes vai te mudares le manushes?"
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
10Wo dikhlia pe lende, ai phendia le manusheske, "Lunzhar cho vas," ai kodo manush lunzhardia pesko vas ai lesko vas sastilo.
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
11Savorhe xolaile ai denas pe duma mashkar pende so te keren le Jesusosko.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
12Ande kodia vriama O Jesus gelo po plai te rhugilpe, ai sa e riat nakhlo te rhugilpe ka Del.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
13Kana phuterdiol o dies O Jesus akhardia peske disiplon; ai alosardia desh u dui, ai akhardia le Apostles.
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
14Ai dia le anav, iek busholas o Simon kai akhardo sas o Petri ai lesko phral Andre, o Iakov ai o Iovano, o Philip ai o Bartholomew,
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
15Mate ai o Thomas, Iakov o shav le Alphaeusosko, ai o Simon akharenas les Zelotes.
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
16O Judas o shav le Iakovosko, ai Judas Iscariot, kodo kai purhisardia O Jesus.
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
17Ai avilo tele lensa katar e plaiing, ai terdilo pek than kai sas but narodo anda leske disipluria. Sas but narodo anda Judea ai anda Jerusalem, ai anda le gava Tire ai Sidon pasha pai, won avile te ashunen les, ai te aven saste anda penge naswalimos.
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
18Kodola kai sas chinuime katar o bi vuzho sastionas,
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
19ai sa o narodo rodelas te azbal le Jesusos, ke putiera anklelas angla leste, ai sastiarelas le savorhen.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
20Antunchi O Jesus vazdia le iakha pe peske disipluria, ai phendia "Raduime te aven tume kai san chorhe; ke o rhaio le Devlesko tumaro si.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
21Raduime te aven tume kai san bokhale akana; ke avela tume dino but.
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
22Raduime te aven tume kai roven akana; ke asana. Raduime te aven gretsona tume le manush, kana gonina tume, kana chinuina tume, ai kana shudena tumaro anav sar kanch pa O Shav le Manushesko.
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
23Raduin tume kodo dies, ai xoten raduimastar ke tumari podarka avela bari ando rhaio, ke kadia kerenas lenge dada le profetonsa.
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
24"Numa nasul avela tumenge kai san barvale, ke si tume swako fielo.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
25Nasul avela tumenge kai si tume but xabe, ke avena bokhale. Nasul avela tumenge kai asan akana, ke nekezhis ai roves.
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
26Nasul avela, kana sa le manush phenena mishtimos pa tumende! Ke kadia kerenas lenge dada le profetonsa.
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
27"Numa me phenav tumenge kai ashunen ma te aven tumenge drago tumare duzhmaia, keren mishtimos kodolenge kai san lenge griatsia.
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
28Swuntson kodolen kai den tume armaia, rhugin kodolenge kai chi keren tumensa mishto.
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
29Te dela tu vari kon iek palma pai buka, de les vi le kolaver; te lela vari kon chi raxami, mek les te lel vi chi bunda.
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
30De kodoles kai mangel vari so tutar, ai te lel vari so tutar na manges palpale katar kodo kai dian les.
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
31So mangen tume te keren le kolaver tumenge, keren vi tume lenge.
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
32"Te aven tumenge drago kodola kai san vi tume lenge drago, che mishtimos keren? Vi le bezexale drago lenge kodola kai si vi won lenge drago.
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
33Te kerena mishtimos kodolenge kai keren tumenge mishtimos, che mishtimos keren? Vi le bezexale keren kadia.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
34Ai te dena le kodolen kai tume zhanen ke vi won dena tumen, che mishtimos keren? Vi le bezexale den kal bezexale saxke te keren vi le sakadia.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
35Numa te aven tumenge drago tumare duzhmaia, ai keren mishtimos lenge; den bi te azhukeren palpale. Ai tumari podarka avela bari ai aven shave le Devleski; ke O Del lasholo kodolensa kai chi naisin leske, ai vi kodolensa kai nai lashe.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
36Aven lasho sar tumaro Dat, lasholo.
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
37"Na keren kris pe kanikaste, ai chi avel chi pe tumende kris; na thon dosh ai chi tume chi aven doshale; iertin ai vi tume aven iertime;
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
38Den, ai avela vi tumen dino; ai si tume dosta, ai vi mai but, sar den ka kolaver, avena palpale tumen mai but sar dian.
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
39Ai O Jesus phendia lenge aver paramichi, "Sar sai iek korho manush angerel avre korhes. Vi le dui peren ande gropa.
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
40O disiplo nai mai baro katar pesko gazda, numa swako disiplo kai phirela vorta avela sar pesko gazda.
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
41Sostar dikhes e sulum kai si ande iakh che phraleski, kana tut si tu khash ande chiri iakh?
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
42Vai sar sai mothos che phraleske, 'Phrala, mek ma te lav e sulum kai si tu ande iakh,' kana tu chi dikhes o khash kai si ande chiri iakh? O manush kai ankerdiol so chi san! Le avri mai anglal o khash kai si ande chiri iakh, ai antunchi dikhesa sar te ankalaves e sulum kai si ande iakh che phraleski.
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
43E lashi khash nashti bariol fruta chorhi, ai chi e chorhi khash chi bariol fruta lashi.
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
44Ke palai fruta dikhes te si e khash chorhi vai lashi. Le manush nashti chidenpe figi katar kanrhe, vai stuguro katar kanrhe.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
45O manush o lasho, ankalavel lashe dieli anda lashimos ka si les anda ilo, ai o manush o chorho ankalavel chorhe dieli andal chorhe dieli kai si les garade, ke o manush mothol anda mui so si les ando ilo."
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
46" Sostar akharen ma, Devla, ai chi keren so mothav tumenge?
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
47Sikavava tumenge pe kaste miazol, swako manush kai avel mande ashunel murhe vorbi ai kerel le.
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
48Kodo manush si sar iek manush kai kerel iek kher, kerdia bari gropa, ai kerdia bax, fundania po bax, o pai kai xhal dia opral, o pai avilo po kher, ai o kher chi mishtisailo, ke kodo kher mishto kerdo sas.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
49Numa kodo kai ashunel ai chi kerel so mothav, wo si sar iek manush kai kerdia iek kher pe phuv, bi fundaniako, o pai avilo pe kodo kher ai kodo kher pelo, ai chi mai arashilia kanch.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"