Romani: New Testament

Swahili: New Testament

Luke

7

1Kana O Jesus getosardia sa pesko divano angla narodo, gelo ando Capernaum.
1Baada ya kusema yale aliyotaka watu wasikie, Yesu alikwenda Kafarnaumu.
2Iek manush kai poronchilas pe iek shel ketani sas les iek sluga kai sas leske drago; ai kudia sluga sas naswalo, merimasko.
2Huko kulikuwa na jemadari mmoja Mroma ambaye alikuwa na mtumishi wake aliyempenda sana. Huyu mtumishi alikuwa mgonjwa karibu kufa.
3Kodo manush kana ashundia pa Jesus, tradia phure Zhidovon leste te phushel les te avel te sastiarel lesko sluga.
3Yule jemadari aliposikia habari za Yesu, aliwatuma wazee fulani Wayahudi waende kumwomba aje amponye mtumishi wake.
4Avile ka Jesus, ai phushenas les, phenenas, " Kodo manush si respektime ai trobul te avela sasto.
4Walipofika kwa Yesu, walimsihi sana, wakasema: "Huyu anastahili afanyiwe jambo hilo,
5Ke kodo manush drago leske amaro narodo, ai wo kerdia amare synagogue."
5maana analipenda taifa letu, na ndiye aliyetujengea lile sunagogi."
6O Jesus gelo lensa, nas dur katar lesko kher, kana kodo manush kai poronchilas peske ketani, tradia peske vortachen te mothon le Devleski, "Na nashen pala mande, ke chi sim dosta vorta te aves mande khere.
6Basi, Yesu akaenda pamoja nao. Alipokuwa karibu kufika nyumbani kwa yule jemadari Mroma, yule jemadari aliwatuma marafiki zake wamwambie Yesu: "Bwana, usijisumbue zaidi, maana mimi sistahili uingie nyumbani mwangu.
7Sa anda kodia chi haliardema dosta vorta te zhav me karing tute, numa phen iek vorba, ai murho sluga avela sasto.
7Ndio maana sikujiona nastahili hata kuja kwako; amuru tu, na mtumishi wangu atapona.
8Ke me kai trobul te kerav so mothon kodola kai si mai bare mandar, si ma ketani te lel murho vas, ai phenav iekeske, "Zha', ai kodo zhal; ai kolavreske mothav, 'Aidi', ai avel; ai murha slugaki mothav, 'Ker kadia', ai wo kerel.
8Mimi pia ni mtu niliye chini ya mamlaka, na ninao askari chini yangu. Namwambia mmoja, Nenda!, naye huenda; namwambia mwingine, Njoo! naye huja; na nikimwambia mtumishi wangu, Fanya hiki!, hufanya."
9Kana O Jesus ashundia kadala vorbi, chudisailo ai boldinisailo karing o narodo kai lelas pala leste, ai phendia, "Me mothav tumenge, chi anda Israel chi arakhlem kasavestar pachamos,"
9Yesu aliposikia hayo, alishangaa; halafu akauelekea ule umati wa watu uliokuwa unamfuata, akasema, "Sijaona imani kubwa namna hii hata katika Israeli."
10Kana aresle khere le manush kai sas tradine katar kodo manush karing O Jesus, arakhle sasto o sluga kai sas naswalo.
10Wale watu walipowasili nyumbani walimkuta yule mtumishi hajambo kabisa.
11O kolaver dies O Jesus gelo andek gav kai bushol Nain; leske disipluria ai but narodo zhanas lesa.
11Baadaye kidogo Yesu alikwenda katika mji mmoja uitwao Naini, na wafuasi wake pamoja na kundi kubwa la watu waliandamana naye.
12Kana areslo pasha o wudar le forosko, manush zhanas te gropon mules, iek zhuvli kai sas la ferdi iek shav, phivli sas, ai but narodo sas lasa kodo le gavesko.
12Basi, alipokuwa anakaribia lango la mji, walitokea watu wamebeba maiti ya kijana mmoja, mtoto wa pekee wa mama mjane. Watu wengi wa mji ule walikuwa pamoja na huyo mama.
13Kana O Del dikhlia la, pelia leski mila anda late, ai phendia lake, "Na rov!"
13Bwana alipomwona mama huyo, alimwonea huruma, akamwambia, "Usilie."
14Pashilo ai azbadia o khash kai sas o mulo andre; kodola manush kai ingerenas o khash terdile. O Jesus phendia. "Terno manush, me phenav tuke, Vushti opre!"
14Kisha akaenda, akaligusa lile jeneza, na wale waliokuwa wanalichukua wakasimama. Halafu akasema, "Kijana! Nakuamuru, amka!"
15O mulo vushtilo opre ai beshlo tele ai delas duma, ai O Jesus del les palpale ka peski dei.
15Yule aliyekufa akaketi, akaanza kuongea. Na Yesu akamkabidhi kwa mama yake.
16Savorhe daraile, ai luvudinas le Devles, ai mothonas, "Iek baro profeto si mashkar amende! O Del avilo te skepil pesko narodo!"
16Watu wote walishikwa na hofu, wakawa wanamtukuza Mungu wakisema: "Nabii mkuu ametokea kati yetu. Mungu amekuja kuwakomboa watu wake."
17E viasta pa Jesus geli ande sa e Judea, ai sa le foruria kai sas pashe.
17Habari hizo zikaenea kote katika Uyahudi na katika nchi za jirani.
18Le Iovanoske disipluria phende leske pa kadala dieli.
18Wanafunzi wa Yohane walimpa habari Yohane juu ya mambo hayo yote. Naye Yohane, baada ya kuwaita wawili kati ya wanafunzi wake,
19O Iovano akhardia duien andal slugi ai tradia le karing O Jesus, te phushen lestar, "Tu san kodo kai trobulas te avel, vai trobul te azhukeras avres?"
19aliwatuma kwa Bwana wamwulize: "Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
20Kana aresle ka Jesus, phende, "O Iovano o baptisto tradia amen karing tute, te mothos, "Tu san kodo kai trobul te avel, vai trobul te azhukeras avres?"
20Wale wanafunzi walipomfikia Yesu wakamwambia, "Yohane Mbatizaji ametutuma kwako tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
21Ande kadia vriama O Jesus sastiardia bute manushen kai sas naswale, bange, kodola kai sas beng ande lende, ai phuterdia le iakha bute korhen.
21Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena.
22O Jesus dia atweto ka le Iovanoske disipluria, "Zhan palpale! Mothon le Iovanoske so dikhlian ai so ashundian! Le korhe dikhen, le bange phiren, le lepra vuzhile, le kashuke ashunen, le mule vushten, e lashi viasta si phendi le chorhe manushenge.
22Basi, Yesu akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini wanahubiriwa Habari njema.
23Raduime te avel kodo kai chi rimol leske kanch!"
23Heri mtu yule ambaye hana mashaka nami!"
24Kana kodola kai tradia sas o Iovano geletar, O Jesus phendia le narodoske pai Iovano, "So gelian tume te dikhen ande pusta? Iek sulum kai mishtil katar e barval?
24Hapo wajumbe wa Yohane walipokwisha kwenda zao, Yesu alianza kuyaambia makundi ya watu juu ya Yohane: "Mlikwenda kule jangwani, hivi mlitaka kuona kitu gani? Mlitaka kuona unyasi unaotikiswa na upepo?
25Numa so gelian te dikhen? Iek manush kai si vuriardo ande shukar tsalia? Eta, kodola kai si le shukar tsalia, ai kai traiin ando mishtimos, kodola traiin andel khera le amperatonge!
25Basi, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona mtu aliyevalia mavazi maridadi? La hasha! Wanaovaa mavazi maridadi na kuishi maisha ya anasa, hukaa katika majumba ya wafalme!
26So gelian tume te dikhen? Iek profeto? E, me phenav tumenge, dikhliam mai but sar iek profeto.
26Basi, niambieni, mlikwenda kuona nini? Mlikwenda kumwona nabii? Naam, hakika ni zaidi ya nabii.
27O Iovano si kodo kai si ramome, "Eta, tradav murha sluga kai anel e viasta angle tute, te lasharel o drom angla tute."
27Huyu Yohane ndiye anayesemwa katika Maandiko Matakatifu: Hapa ni mtumishi wangu, asema Bwana; ninamtuma akutangulie, akutayarishie njia."
28Me phenav tumenge, "Mashkar kodole kai arakhadile katar e zhuvli nai mai bare de sar o Iovano o baptisto, inker o mai tsinorho ando rhaio le Devlesko mai baro lestar."
28Yesu akamalizia kwa kusema, "Nawaambieni, kati ya binadamu wote hakuna aliye mkubwa zaidi kuliko Yohane Mbatizaji. Hata hivyo, yule aliye mdogo kabisa katika ufalme wa Mungu ni mkubwa zaidi kuliko yeye."
29Ai sa o narodo kai ashundia les, ai vi le manush kai chiden e taksa, phende ke vorta so phenel O Del, ai mekle te bolel o Iovano.
29Waliposikia hayo watu wote na watoza ushuru waliusifu wema wa Mungu; hao ndio wale waliokuwa wameupokea ubatizo wa Yohane.
30Numa le Farizeanuria ai le ablokatura chi bolenas pe lestar, phende ke nas vorta so mothol O Del.
30Lakini Mafarisayo na walimu wa Sheria walikataa mpango wa Mungu uliowahusu wakakataa kubatizwa na Yohane.
31"No pala kaste malaven kadala manush kadala vriamake, ai pe kaste miazon.
31Yesu akaendelea kusema, "Basi, nitawafananisha watu wa kizazi hiki na kitu gani? Ni watu wa namna gani?
32Won miazon sar glate kai beshen ando bazari, ai kai den duma iek kavresa ai mothon, 'Jilabadiam ande tuturaza, ai tume chi kheldian ai jilabadian jilia miloso ai tume chi ruian.'
32Ni kama vijana waliokuwa wamekaa sokoni na kuambiana, kikundi kimoja na kingine: Tumewapigieni ngoma, lakini hamkucheza! Tumeomboleza, lakini hamkulia!
33O Iovano o baptisto avilo ai chi xal o manrho ai chi pel mol; ai tume mothon 'o beng si ande leste.'
33Kwa maana Yohane alikuja, yeye alifunga na hakunywa divai, nanyi mkasema: Amepagawa na pepo!
34O Shav le Manushesko avilo, ai xalas ai pelas; ai tume phende, "Dikh, kado manush xal but ai pel but, ek vortakolo le manushensa kai chiden e taksa ai le bezexalensa!"
34Akaja Mwana wa Mtu; anakula na kunywa, mkasema: Mwangalieni mlafi huyu na mlevi; rafiki ya watoza ushuru na wenye dhambi!
35Numa o chachimos sikadilo katar le glate.
35Hata hivyo, hekima ya Mungu imethibitishwa kuwa njema na wote wale wanaoikubali."
36Iek Farisi mangliape katar O Jesus te xal lesa. O Jesus gelo ando kher le manushengo ai thodiape kai skafidi te xal.
36Mfarisayo mmoja alimwalika Yesu kula chakula nyumbani kwake. Akaingia nyumbani mwa huyo Mfarisayo, akakaa kula chakula.
37Sas iek zhuvli bezexali kai sas ando gav, kana ashundia ke O Jesus sas pa e skafidi ando kher le Farizeanongo, andini iek botela pherdo duxi.
37Basi, katika mji ule kulikuwa na mama mmoja aliyekuwa anaishi maisha mabaya. Alipopata habari kwamba Yesu yuko nyumbani kwa huyo Mfarisayo, alichukua chupa ya alabasta yenye marashi.
38Ai beshelas pashal punrhe le Jesusoske, ai rovelas; ai lake asua chindarde le punrhe le Jesusoske, ai porme koslia leske balensa ai chumidia leske punrhe, ai thodia duxi pe lende.
38Akaja, akasimama karibu na miguu yake Yesu, akilia, na machozi yake yakamdondokea Yesu miguuni. Huyo mwanamke akaipangusa miguu ya Yesu kwa nywele zake. Kisha akaibusu na kuipaka yale marashi.
39O Farisi kai akhardiasas le Jesusos ando pesko kher ai dikhlia so kerdilia, motholas ande peste, "Kado manush te avilino profeto, zhanglino so si kodia zhuvli kai azbal les; wo zhanglino ke bezexalila."
39Yule Mfarisayo aliyemwalika Yesu alipoona hayo, akawaza moyoni mwake, "Kama mtu huyu angekuwa kweli nabii angejua huyu mwanamke ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi."
40O Jesus phendia leske, "Simon, si ma vari so te mothav tuke." O Simon phendia, "De duma, Gazda."
40Yesu akamwambia huyo Mfarisayo, "Simoni, ninacho kitu cha kukwambia." Naye Simoni akamwambia, "Ndio Mwalimu, sema." Yesu akasema,
41Dui manush sas kai kamenas leske love, iek kamelas leske pansh shela teliara ai o kolaver panvardesh teliara.
41"Watu wawili walikuwa wamemkopa mtu fedha: mmoja alikuwa amekopa dinari mia tano, na mwingine hamsini.
42Sar nas le love te pochinen, wo chi mai manglia peske love lendar. No O Jesus phushel, "Savo andal dui avela lenge drago kodo manush?"
42Waliposhindwa kulipa madeni yao, huyo mtu aliwasamehe wote wawili. Sasa ni yupi kati ya hao wawili atampenda zaidi huyo bwana?"
43O Simon dia atweto, "Me gindiv ke kuko kai diasas les mai but." O Jesus phendia leske, "Vorta phendian."
43Simoni akamjibu, "Ni dhahiri kwamba yule aliyesamehewa deni kubwa zaidi atampenda zaidi yule bwana." Yesu akamwambia, "Sawa."
44Porme dikhlia pe zhuvli, ai phendia le Simonoske, "Dikhes kacha zhuvli? Avilem ande cho kher; ai chi dian ma vov si pai te xalavel murhe punrhe numa woi chindiatar le peske asuensa ai koslia le balensa.
44Halafu akamgeukia yule mwanamke na kumwambia Simoni, "Unamwona huyu mwanamke, sivyo? Basi, mimi nilipoingia hapa nyumbani kwako hukunipa maji ya kunawa miguu yangu; lakini mwanamke huyu ameniosha miguu yangu kwa machozi yake na kunipangusa kwa nywele zake.
45Chi chumidian ma, numa woi de sar avilem ando kher, sa murhe punrhe chumidel.
45Wewe hukunisalimu kwa kunibusu, lakini huyu mwanamke tangu nilipoingia hapa amekuwa akiibusu miguu yangu.
46Chi shordian vov si vuloi pe murho shero, numa woi shordia duxi pe murhe punrhe.
46Wewe hukunionyesha ukarimu wako kwa kunipaka mafuta kichwani, lakini huyu mwanamke amefanya hivyo kwa kunipaka mafuta miguu yangu.
47Anda kodia mothav tuke, lake but bezexa iertimele, ke drago simas lake. Numa kodoles ke kai iertin xantsi, kodo volil xantsi."
47Kwa hiyo nakwambia amesamehewa dhambi zake nyingi kwa kuwa ameonyesha upendo mkubwa. Mwenye kusamehe kidogo, hupenda kidogo."
48Ai O Jesus mothol la zhuvliake, "Che bezexa iertimele!"
48Basi, Yesu akamwambia yule mwanamke, "Umesamehewa dhambi zako."
49Kodola kai sas kai skafidi lesa mothon ande pende, "Kon si kado kai iertil vi le bezexa?"
49Na hapo wale waliokuwa pamoja naye mezani wakaulizana, "Ni mtu wa namna gani huyu awezaye kusamehe dhambi?"
50Numa O Jesus phendia la zhuvliake, "Cho pachamos skepisardia tu, zha pachasa."
50Naye Yesu akamwambia yule mwanamke, "Imani yako imekuokoa; nenda kwa amani."