1Porme O Jesus zhalas foro forestar, ai gav gavestar ai motholas e lashi viasta pa rhaio le Devlesko;
1Baada ya hayo, Yesu alipitia katika miji na vijiji akitangaza Habari Njema za Ufalme wa Mungu. Wale kumi na wawili waliandamana naye.
2ai xantsi zhuvlia kai sastilesas anda chorhe duxuria ai andal naswalimata: e Maria, kai akharenas la Magalena, ai anklistesas anda late le efta bengen;
2Pia wanawake kadhaa ambao Yesu alikuwa amewatoa pepo wabaya na kuwaponya magonjwa, waliandamana naye. Hao ndio akina Maria (aitwaye Magdalene), ambaye alitolewa pepo wabaya saba;
3Joanna, e rhomni le Chazasosli, kai lele sama katar o amperato Herod; ai Susanna; ai but aver zhuvli kai zhutisarde le Jesososke penge mishtimasa.
3Yoana, mke wa Kuza, mfanyakazi mkuu wa Herode; Susana na wengine kadhaa. Hao wanawake walikuwa wakiwatumikia kwa mali yao wenyewe.
4But manush avenas ai avenas anda foro forestar ka Jesus, ai kana o narodo chidinisailo, O Jesus phendia lenge ek paramichi.
4Kundi kubwa la watu lilikuwa linakusanyika, na watu walikuwa wanamjia Yesu kutoka kila mji. Naye akawaambia mfano huu:
5"Iek manush gelo te shudel peske sumuntsi; kana shudelas sumuntsi, uni pelia andal sumuntsi pasha drom, kai le manush phiravenas ai le sumuntsi sas telal punrhe, ai le chiriklia avile ai xale le.
5"Mpanzi alikwenda kupanda mbegu zake. Alipokuwa akipanda zile mbegu, nyingine zilianguka njiani, na wapita njia wakazikanyaga, na ndege wakazila.
6Ai uni pele po than kai sas bax; ai kana barile shuchile; ke nas vov si chingo.
6Nyingine zilianguka penye mawe, na baada ya kuota zikanyauka kwa kukosa maji.
7Ai uni pele mashkar le kanrhe; kodola kanrhe barile mashkar le patria ai tasade le.
7Nyingine zilianguka kati ya miti ya miiba. Ile miti ya miiba ilipoota ikazisonga.
8Uni sumuntsi pele ande lashi phuv; barile le sumuntsi ai dine fruta iek shel pek shel." Ai kana dia duma kadia, O Jesus phendia, "Ashun, kodo kai si les khan te ashunel, trobul e ashunel."
8Nyingine zilianguka katika udongo mzuri, zikaota na kuzaa asilimia mia." Baada ya kusema hayo, akapaaza sauti, akasema, "Mwenye masikio na asikie!"
9Leske disipluria phushle les, "So znachil kadia paramichi?"
9Wanafunzi wake wakamwuliza Yesu maana ya mfano huo.
10O Jesus dia le atweto, "Ke tumenge sas shinado te zhanen so si garado pa e amperetsia le Devleski, numa le kolavrenge si phendo ande paramichi, saxke te dikhen numa chi dikhen, ai te ashunen numa chi haliaren kanch."
10Naye akajibu, "Ninyi mmejaliwa kujua siri za Ufalme wa Mungu, lakini hao wengine sivyo; ila hao huambiwa kwa mifano, ili wakitazama wasiweze kuona, na wakisikia wasifahamu.
11"Eta, so znachil kadia paramichi: e sumuntsa si E Vorba le Devleski.
11"Basi, maana ya mfano huu ni hii: mbegu ni neno la Mungu.
12Le sumuntsi kai pele pasha drom si kodola kai ashunen; numa o beng avel ai lel anda lengo ilo e vorba, ke zhanel ke te pachanape si te skepinpe.
12Zile zilizoanguka njiani zinaonyesha watu wale wanaosikia lile neno, halafu Ibilisi akaja na kuliondoa mioyoni mwao wasije wakaamini na hivyo wakaokoka.
13Le sumuntsi kai pele po than kai sas bax si kodola kai ashunen e vorba ai lel la raduimasa, numa nai vov si vuni ande lende; pachalpe xantsi vriama, ai kana avel o beng te zumavel le, peren.
13Zile zilizoanguka penye mawe zinaonyesha watu wale ambao wanaposikia juu ya lile neno hulipokea kwa furaha. Hata hivyo, kama zile mbegu, watu hao hawana mizizi maana husadiki kwa kitambo tu, na wanapojaribiwa hukata tamaa.
14Le sumuntsi kai pele mashkar le kanrhe si kodola kai ashundesas; numa o nekazo, o barvalimos, ai le dieli le traioske tasaven le, ai lenge fruta shoxar chi bariol.
14Zile zilizoanguka kwenye miti ya miiba ni watu wale wanaosikia lile neno, lakini muda si muda, wanapokwenda zao, husongwa na wasiwasi, mali na anasa za maisha, na hawazai matunda yakakomaa.
15Le sumuntsi kai pelia ande lashi phuv si kodola kai ashunen e vorba, won garaven la ande lasho ilo, ai ankeren e vorba, ai anen fruta chachimasa."
15Na zile zilizoanguka kwenye udongo mzuri ndio watu wale wanaolisikia lile neno, wakalizingatia kwa moyo mwema na wa utii. Hao huvumilia mpaka wakazaa matunda.
16"Khonik chi del iag iek lampo, ai te garavel les telai e vadra vai telai e skafidi, numa thol les opral pe skafidi te del e vediara savorhenge kai den ando kher.
16"Watu hawawashi taa na kuifunika kwa chombo au kuiweka mvunguni. Lakini huiweka juu ya kinara ili watu wanapoingia ndani wapate kuona mwanga.
17Ke nai kanchi garado, kai trobul te avel sikado; kanchi garado, kai trobul te zhanen ai te dikhen savorhe.
17"Chochote kilichofichwa kitafichuliwa na siri yoyote itagunduliwa na kujulikana hadharani.
18No len sama sar ashunen; ke avela dino kodoles kai si les, numa ka kodo kai nai avela lestar lino vi savo gindin ke si les."
18"Kwa hiyo, jihadharini jinsi mnavyosikia; maana aliye na kitu ataongezewa, lakini yule asiye na kitu, hata kile anachodhani kuwa anacho, kitachukuliwa."
19E dei ai le phral le Jesusoske avile leste, numa nashti aresle leste pala but narodo.
19Hapo mama na ndugu zake Yesu wakamjia, lakini hawakuweza kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu.
20Ai mothol leske, "Chi dei ai che phral avri le, ai mangen te dikhen tu."
20Yesu akapewa habari kwamba mama na ndugu zake walikuwa nje, wanataka kumwona.
21O Jesus phendia lenge, "Murhi dei ai murhe phral si kodola kai ashunen E Vorba le Devleski, ai kai keren lesko zakono."
21Lakini Yesu akawaambia watu wote, "Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulishika."
22Andek dies O Jesus anklisto ando pharaxoditsi peska disiplonsa ai phende lenge, "Aven pe kolaver rik le paieske," ai gele.
22Siku moja, Yesu alipanda mashua pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, "Tuvuke ziwa twende mpaka ng'ambo." Basi, wakaanza safari.
23Sar zhanas po pai O Jesus sovelas, ek bari barval avili po pai, ai pherdiolas o paraxodo le paiesa, ai xaiinas.
23Walipokuwa wanasafiri kwa mashua, Yesu alishikwa na usingizi, akalala. Dhoruba kali ikaanza kuvuma, maji yakaanza kuingia ndani ya mashua, wakawa katika hatari.
24Le disipluria pashile pasha Jesus, ai vushtiarde les, phenenas, "Gazda, Gazda, xaiisavas." Porme O Jesus vushtilo, ai dia mui pe barval ai po pai; ai terdili ai sas trankilo.
24Wale wanafunzi wakamwendea Yesu, wakamwamsha wakisema, "Bwana, Bwana! Tunaangamia!" Yesu akaamka, akaikemea dhoruba na mawimbi, navyo vikatulia, kukawa shwari.
25Porme phendia le disiplonge, "Kai tumaro pachamos?" Daraile leske disipluria ai chudisaile, ai phende iek kavreske, "Che fielo manush kado? Ke dia mui pe barval ai pe maria, ai vi e barval ai e maria pachan lesko mui."
25Kisha akawaambia, "Iko wapi imani yenu?" Lakini wao walishangaa na kuogopa huku wakiambiana, "Huyu ni nani basi, hata anaamuru dhoruba na mawimbi, navyo vinamtii?"
26Aresle ando them le manushengo kai bushon Gadarenes, kai si inchal e Galilee.
26Wakaendelea na safari, wakafika pwani ya nchi ya Wagerase inayokabiliana na Galilaya, ng'ambo ya ziwa.
27Kana O Jesus vulisto pe phuv, avilo karing leste iek manush le forosko, kai sas ande leste but beng de dumut nas pe leste tsalia, ai vo chi beshelas khere numa andel mumuntsi.
27Alipokuwa anashuka pwani, mtu mmoja aliyekuwa amepagawa na pepo alimjia kutoka mjini. Kwa muda mrefu mtu huyo, hakuwa anavaa nguo, wala hakuwa anaishi nyumbani bali makaburini.
28Kana dikhlia le Jesusos, tsipisardia ai shudiape ka leske punrhe ai phendia zurales, "So si mashkar tute ai mashkar mande; Jesus, tu O Shav le Devlesko kai si opre! So mangesa mandar, na chinuisar ma."
28Alipomwona Yesu, alipiga kelele na kujitupa chini mbele yake, na kusema kwa sauti kubwa "We, Yesu Mwana wa Mungu Aliye Juu una shauri gani nami? Ninakusihi usinitese!"
29O Jesus dia ordina ka o beng te anklel avri anda kodo manush. Butivar o bi vuzho tsodiasaspe anda leste; le manush phandenas les lantsonsa ai sastrensa pel punrhe ai vi pel vas, numa wo shinelas le, ai o beng angerelas les ande pusta.
29Alisema hivyo kwa kuwa Yesu alikwishamwambia huyo pepo mchafu amtoke mtu huyo. Pepo huyo mchafu alikuwa anamvamia mtu huyo mara nyingi, na ingawa watu walimweka ndani na kumfunga kwa minyororo na pingu, lakini kila mara alivivunja vifungo hivyo, akakimbizwa na pepo huyo mchafu hadi jangwani.
30O Jesus phushlia les, "Sar bushos?" Wo dia atweto, "Le Legion" ke but beng sas ande leste.
30Basi, Yesu akamwuliza, "Jina lako nani?" Yeye akajibu, "Jina langu ni Jeshi" --kwa sababu pepo wengi walikuwa wamempagaa.
31Le beng rhuginaspe ka Jesus te na zhan ando pai.
31Hao pepo wakamsihi asiwaamuru wamtoke na kwenda kwenye shimo lisilo na mwisho.
32Sas kotse po plai but bale kai xanas. Le beng manglepe katar O Jesus te sai den andel bale, ai O Jesus phendia lenge te zhan andel bale.
32Kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha mlimani. Basi, hao pepo wakamsihi awaruhusu wawaingie. Naye Yesu akawapa ruhusa.
33Le beng ankliste avri anda kado manush ai dine andel bale; ai le bale shudepe pai xar ande maria, ai tasule.
33Kwa hiyo pepo hao wakamtoka yule mtu, wakawaingia wale nguruwe, nao wakaporomoka kwenye ule mteremko mkali, wakatumbukia ziwani, wakazama majini.
34Le manush kai ningerenas le balen dikhle so kerdilia, nashle, ai phende e viasta so dikhle andel gava ai avrial le gava.
34Wale wachungaji walipoona yote yaliyotokea walikimbia, wakaenda kuwapa watu habari, mjini na mashambani.
35Narodo zhalas te dikhel so kerdilia, avile ka Jesus, ai arakhle le manushes kai anklistesas le beng anda leste, ai beshelas tele kal punrhe le Jesusoske, vuriardo, ai leske goji vorta; ai daraile.
35Watu wakaja kuona yaliyotokea. Wakamwendea Yesu, wakamwona yule mtu aliyetokwa na pepo ameketi karibu na Yesu, amevaa nguo, ana akili zake, wakaogopa.
36Kodola kai dikhle so kerdiliasas phende sar kodo manush kai sas le beng ande leste sastilo.
36Wale watu walioshuhudia tukio hilo waliwaeleza hao jinsi yule mtu alivyoponywa.
37Antunchi sa o narodo kodole gavesko kai bushonas Gadarenes, rhugisaile ka Jesus te duriol lendar ke daranas. O Jesus anklisto ande pharaxoditsi, ai gelotar.
37Wakazi wa nchi ya Gerase walishikwa na hofu kubwa. Kwa hiyo wakamwomba Yesu aondoke, aende zake. Hivyo Yesu alipanda tena mashua, akaondoka.
38O manush kai; ankliste sas le beng anda leste mangliape katar O Jesus, "Mek ma te zhav tusa." Numa O Jesus tradia les ai phendia les,
38Yule mtu aliyetokwa na wale pepo akamsihi aende pamoja naye. Lakini Yesu hakumruhusu, bali akamwambia,
39"Zha ando cho kher, ai phen so godi kerdia tuke O Del." Gelotar ai phendia anda sa o foro so godi kerdia leske O Jesus.
39"Rudi nyumbani ukaeleze yote Mungu aliyokutendea." Basi, yule mtu akaenda akitangaza kila mahali katika mji ule mambo yote Yesu aliyomtendea.
40Kana avilo palpale O Jesus, o narodo primisarde les, ke savorhe azhukerenas les.
40Yesu aliporudi upande mwingine wa ziwa, kundi la watu lilimkaribisha, kwa maana wote walikuwa wanamngojea.
41Eta, avilo iek manush kai busholas Jairus, wo sas o baro pe synagogue; shudiape kal punrhe le Jesusoske, ai mangliape lestar te avel ande lesko kher.
41Hapo akaja mtu mmoja aitwaye Yairo, ofisa wa sunagogi. Alijitupa miguuni pa Yesu, akamwomba aende nyumbani kwake,
42Ke sas les ferdi iek shei, kai sas desh u do bershengi merimaski sas. Numa sar O Jesus zhalas late le manush avenas pasha leste katar swako rik.
42kwa kuwa binti yake wa pekee, mwana wa pekee mwenye umri wa miaka kumi na miwili, alikuwa mahututi. Yesu alipokuwa akienda, watu wakawa wanamsonga kila upande.
43Sas iek zhuvli, kai xasarelas pesko rat de desh u dui bersh, ai kai xaliasas sa peske love kal dokxturia, numa chi iek chi sastiardia la.
43Kulikuwa na mwanamke mmoja kati ya lile kundi la watu, ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, ingawa alikuwa amekwisha tumia mali yake yote kwa waganga, hakuna aliyefaulu kumponya.
44Avili palal pala leste ai azbadia e tivala la bundako kai sas po Jesus, ai strazo o rat kai xasarelas terdilo.
44Huyo mwanamke alimfuata Yesu nyuma, akagusa pindo la vazi lake. Papo hapo akaponywa ugonjwa wake wa kutokwa damu.
45O Jesus phushlia, "Kon azbadian ma?" Numa savorhe phende ke chi azbade les, ai o Petri phendias, "Gazda, but narodo si pasha tute ai tu mothos "Kon azbadia ma?"
45Yesu akasema, "Ni nani aliyenigusa?" Wote wakasema kwamba hapakuwa na mtu aliyemgusa. Naye Petro akasema, "Mwalimu, umati wa watu umekuzunguka na kukusonga!"
46Numa O Jesus phendia, "Vari kon azbadia ma; ke haliardem ke zor anklisto anda mande."
46Lakini Yesu akasema, "Kuna mtu aliyenigusa, maana nimehisi nguvu imenitoka."
47Ai kana e zhuvli dikhlia ke nas garadi, geli ai izdralas, ai shudiape kal punrhe le Jesusoske, ai phendia angla sa o narodo sostar azbadia le Jesusos, ai sar sastili strazo.
47Yule mwanamke alipoona kwamba hawezi kujificha, akajitokeza akitetemeka kwa hofu, akajitupa mbele ya Yesu. Hapo akaeleza mbele ya wote kisa cha kumgusa Yesu na jinsi alivyoponyeshwa mara moja.
48O Jesus phendia lake, "Murhi shei, cho pachamos sastiardia tu, zha pachasa."
48Yesu akamwambia, "Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani."
49Sar delas duma inker, avilia vari kon katar o baro le kheresko, ai phendia, "Chi shei muli, na mai dziliaren le Jesusos.
49Alipokuwa bado akiongea, Yairo akaletewa habari kutoka nyumbani: "Binti yako ameshakufa, ya nini kumsumbua Mwalimu zaidi?"
50Numa O Jesus ashundia ai phendia ka Jairus, "Na dara; ferdi pachas tu, ai woi avela sastiarel."
50Yesu aliposikia hayo akamwambia Yairo, "Usiogope; amini tu, naye atapona."
51Kana areslo ka kher O Jesus chi meklia te del khonik lesa ando kher, ferdi o Petri, o Iovano, ai o Iakov, ai o dat ai e dei la glatake.
51Alipofika nyumbani hakumruhusu mtu kuingia ndani pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohane, Yakobo na wazazi wa huyo msichana.
52Savorhensa roven ai pherde nekezhime. Antunchi O Jesus phendia, "Na roven; chi muli, numa sovel!"
52Watu wote walikuwa wakilia na kuomboleza kwa ajili yake. Lakini Yesu akawaambia, "Msilie, kwa maana mtoto hajafa, amelala tu!"
53Asanas lestar, ke won zhanenas ke muli.
53Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
54Numa O Jesus lia la le vastesa, ai phendia zurales, "Vushti opre, Glata!"
54Lakini Yesu akamshika mkono akasema, "Mtoto amka!"
55Ai lako duxo avilo ande late, ai strazo vushtilo opre; ai O Jesus phendia, "Den la te xal."
55Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
56Lako dat ai laki dei chudisaile, ai O Jesus phendia lenge te na mothon kanikaske.
56Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.