1Jesus chidia andek than le desh u do disiplon ai dia le zor ai putiera pe sa le beng, ai e zor te sastiaren le naswalen.
1Yesu aliwaita wale kumi na wawili, akawapa uwezo juu ya pepo wote, na uwezo wa kuponya wagonjwa.
2Tradia len te mothon e viasta le rhaioski le Devleski, ai te sastiaren le naswalen.
2Halafu akawatuma waende kuhubiri Ufalme wa Mungu na kuponya wagonjwa.
3Porme phendia lenge, "Na len kanchi tumensa kai zhan; chi rhai, chi gono, chi manrho, chi love, chi dui raxamia.
3Akawaambia, "Mnaposafiri msichukue chochote: msichukue fimbo, wala mkoba, wala chakula, wala fedha, wala hata koti la ziada.
4Andel khera kai zhana, beshen kotsar zhi kana zhanatar.
4Nyumba yoyote mtakayoingia na kukaribishwa, kaeni humo mpaka mtakapoondoka katika kijiji hicho.
5Ai te na primila tumen o narodo, anklen avri anda kodo gav, ai kosen e pulberia pa tumare punrhe te sikaven lenge so si won."
5Watu wakikataa kuwakaribisha, tokeni katika mji huo, nanyi mnapotoka kung'uteni mavumbi miguuni mwenu kama onyo kwao."
6Geletar, ai gele gav gavestar, ai phende e lashi viasta, sastiarenas le naswalen.
6Basi, wakaanza safari, wakapitia vijijini wakihubiri Habari Njema na kuponya wagonjwa kila mahali.
7Herod, o Tetrach, ashundia so godi kerdiolas, ai ferdi delas pe goji, ke uni mothonas ke o Iovano zhuvindisailo andal mule;
7Sasa, mtawala Herode, alipata habari za mambo yote yaliyokuwa yanatendeka, akawa na wasiwasi kwa vile walikuwa wakisema: "Yohane amefufuka kutoka wafu!"
8Uni mothonas ke o Elijah sikadilo; ai uni, ke iek phurano profeto zhuvindisailo.
8Wengine walisema kwamba Eliya ametokea, na wengine walisema kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amerudi duniani.
9Ai o Herod phendia, "Phendem te shinen o shero le Iovanosko; numa savo si, kado kai ashunav ai mothol kasavendar dieli?" Ai mangelas te dikhel les.
9Lakini Herode akasema, "Huyo Yohane nilimkata kichwa; sasa ni nani huyu ninayesikia habari zake?" Akawa na hamu ya kumwona.
10Le desh u dui disipluria kana avile palpale, phende ka Jesus so godi kerde. Lia le pesa, ai gelo karing o foro kai bushol Bethsaida.
10Wale mitume waliporudi, walimweleza yote waliyoyafanya. Yesu akawachukua, wakaenda peke yao mjini Bethsaida.
11Kana o narodo ashundia, liape pala leste, O Jesus primilas le, ai phendia lenge pa rhaio le Devlesko, ai sastiarelas kodolen kai trobulas te aven saste.
11Lakini wale watu walipojua alikokwenda, walimfuata. Yesu akawakaribisha akawazungumzia juu ya Ufalme wa Mungu, akawaponya wale waliohitaji kuponywa.
12Kana perelas e riat, le desh u dui disipluria avile leste, ai phende leske, "Trade le narodos te zhan andel gava ai kruglom te soven av te arakhen xaben ke katse kai sam pusta si."
12Jua lilipokuwa linaanza kutua, wale kumi na wawili walimwendea wakamwambia, "Waage watu waende kwenye vijiji na mashamba ya karibu, wakajipatie chakula na mahali pa kulala, kwa maana hapa tulipo ni nyikani."
13Numa O Jesus phendia lenge, "Den le tume te xan." Numa won phende, "Ferdi panzh manrhe ai dui mashe. Zhasa ame te chinas xaben kadale narodoske?"
13Lakini Yesu akawaambia, "Wapeni ninyi chakula." Wakamjibu, "Hatuna chochote ila mikate mitano na samaki wawili. Labda twende wenyewe tukawanunulie chakula watu wote hawa!"
14Sas pashte panzh mi zhene kotse. O Jesus phendia peske disiplonge, "Keren le te beshen tele ai te thon andek than po panvardesh zhene."
14(Walikuwepo pale wanaume wapatao elfu tano.) Basi, Yesu akawaambia wanafunzi wake, "Waambieni watu waketi katika makundi ya watu hamsinihamsini."
15Ai kerde kadia, kerde le te beshen tele.
15Wanafunzi wakafanya walivyoambiwa, wakawaketisha wote.
16O Jesus lia le panzh manrhe ai le dui mashe, ai vazdia le iakha karing o rhaio, ai naisisardias, porme phaglia ai dia le ka peske disiplonge te den ka narodo.
16Kisha Yesu akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akamshukuru Mungu, akavimega, akawapa wanafunzi wake wawagawie watu.
17Savorhe xale ai chailile; ai le disipluria chide le kotora kai ashshilia desh u dui shkonitsi pherde sas.
17Wakala wote, wakashiba; wakakusanya makombo ya chakula, wakajaza vikapu kumi na viwili.
18Andek jes O Jesus rhugilas pe korkorho, peske disipluria avile leste, ai phushlia le, "So mothon o narodo, ke sim?"
18Siku moja, Yesu alikuwa anasali peke yake, na wanafunzi wake walikuwa karibu. Basi, akawauliza, "Eti watu wanasema mimi ni nani?"
19Won phende, "O Iovano o baptisto; uni mothon, o Elijah; uni phenen, iek phurano profeto kai zhuvindisailo.
19Nao wakamjibu, "Wengine wanasema kuwa wewe ni Yohane mbatizaji, wengine wanasema wewe ni Eliya, hali wengine wanasema kuwa wewe ni mmoja wa manabii wa kale ambaye amefufuka."
20Phendia lenge, "Kon mothon ke sim?" O Petri dia atweto, "O Kristo le Devlesko."
20Hapo akawauliza, "Na ninyi je, mwasema mimi ni nani?" Petro akajibu, "Wewe ndiwe Kristo wa Mungu."
21Ai O Jesus dia le trad te na mothon kanikaske.
21Halafu Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote habari hiyo.
22Ai mai phendia, "Ke o Shav le manushesko chinuil but, wo avela shudino lendar, le phure, le bare le rashange, ai le Gramnoturia, Mudarena les ai o trito jes zhuvindila."
22Akaendelea kusema: "Ni lazima Mwana wa Mtu apate mateso mengi na kukataliwa na wazee na makuhani wakuu na walimu wa Sheria; atauawa, lakini siku ya tatu atafufuliwa."
23Porme phendia savorhenge, "Te mangela vari kon te lelpe pala mande, te bustrel pe pes, ai te lel swako jes pesko trushul ai te lelpe pala mande.
23Kisha akawaambia watu wote, "Mtu yeyote akitaka kuwa mfuasi wangu, ni lazima ajikane nafsi yake, auchukue msalaba wake kila siku, anifuate.
24Ke kodo kai mangela te skepil pesko traio xasarela les; numa kodo kai xasarela pesko traio pala mande, skepila les.
24Maana, mtu anayetaka kuyaokoa maisha yake mwenyewe, atayapoteza; lakini atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu, atayaokoa.
25Ai so nirila o manush te avel leske sa e lumia, ai te xasarela pe pes?
25Je, kuna faida gani mtu kuupata utajiri wote wa dunia kwa kujipoteza au kujiangamiza yeye mwenyewe?
26Ke kon godi lazhala mandar ai katar murhe vorbi, o Shav le Manushesko avela lestar lazhal, kana avela anda pesko barimos, ai ande barimos le Dadesko, ai le Swuntsi angeluria.
26Mtu akinionea aibu mimi na mafundisho yangu, Mwana wa Mtu atamwonea aibu mtu huyo wakati atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.
27Phenav tumenge chachimasa, uni kai si katse, chi merena mai anglal sar te dikhen o rhaio le Devlesko."
27Nawaambieni kweli, kuna wengine papa hapa ambao hawatakufa kabla ya kuuona Ufalme wa Mungu."
28Oxto jes pala kodia kana phendia kadala vorbi, O Jesus lia pesa O Petri ai o Iovano ai o Iakov, ai anklisto po plai te rhuginpe.
28Yapata siku nane baada ya kusema hayo, Yesu aliwachukua Petro, Yohane na Yakobo, akaenda nao mlimani kusali.
29Sar O Jesus rhugilaspe, lesko mui pharhudilo, ai leske tsalia parnile zurales.
29Alipokuwa akisali, sura yake ilibadilika, mavazi yake yakawa meupe na kung'aa sana.
30Eta, dui manush denas duma lesa, kai sas o Moses, ai o Elijah,
30Na watu wawili wakaonekana wakizungumza naye, nao ni Mose na Eliya,
31Kai dichonas ande barimos, ai denas duma pai leski martia ando Jerusalem kai trobul te kerdiol.
31ambao walitokea wakiwa wenye utukufu, wakazungumza naye juu ya kifo chake ambacho angekikamilisha huko Yerusalemu.
32O Petri, ai kodola kai sas lesa sovenas, numa sar beshenas vushtiarde, dikhle o barimos le Jesusoske, ai le dui manush kai sas lesa.
32Petro na wenzake walikuwa wamelemewa na usingizi mzito, hata hivyo waliamka, wakauona utukufu wake, wakawaona na wale watu wawili waliokuwa wamesimama pamoja naye.
33Sar le manush zhanastar katar O Jesus, o Petri phendia leske, "Gazda, mai mishto ke sam tusa. Keras trin tseri, tuke, iek le Mosesoske, iek o Elijahoske." Chi zhanelas so motholas.
33Basi, watu hao wawili walipokuwa wakiondoka, Petro alimwambia Yesu, "Bwana, ni vizuri kwamba tupo hapa: basi, tujenge vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya." --Kwa kweli hakujua anasema nini.
34Sar divinilas kadia, ek nuvero vulisto pe lende; ai le disipluria daraile kana dikhle sar o nuvero vulisto pe lende.
34Petro alipokuwa akisema hayo, mara wingu likatokea na kuwafunika; na wingu hilo lilipowajia, wale wanafunzi waliogopa sana.
35Ai anda nuvero avilo ek glaso, phenenas, "Kako si murho Shav kai si mange mai drago; ashunen leste."
35Sauti ikasikika kutoka katika hilo wingu: "Huyu ndiye Mwanangu niliyemchagua, msikilizeni."
36Kana ashundilo kodo glaso, O Jesus korkorho sas. Le disipluria chi mothonas kanch, ai ande kodia vriama chi phende kanikaske so dikhle.
36Baada ya hiyo sauti kusikika, Yesu alionekana akiwa peke yake. Wanafunzi walikaa kimya juu ya tukio hilo, na wakati ule hawakumwambia mtu yeyote mambo hayo waliyoyaona.
37Pe terharin kana vuliste pai plaiin, but narodo avelas karing O Jesus.
37Kesho yake walipokuwa wakishuka kutoka kule mlimani, kundi kubwa la watu lilikutana na Yesu.
38Ai mashkar o narodo ek manush tsipisardia, "Gazda, rhugiv ma tute, dikh pe murho shav, ke ferdi kado si ma!
38Hapo, mtu mmoja katika lile kundi akapaaza sauti, akasema, "Mwalimu! Ninakusihi umwangalie mwanangu--mwanangu wa pekee!
39O beng lia kodo raklorho ai kerelas les te tsipil; ai drechinilas les zurales, ai zhala leske spuma anda mui. Chinuilas les ai chi mekelas les vushoro.
39Pepo huwa anamshambulia, na mara humfanya apige kelele; humtia kifafa, na povu likamtoka kinywani. Huendelea kumtesa sana, asimwache upesi.
40Rhugisailem ka che disipluria te gonin le benges; ai nashtisarde."
40Niliwaomba wanafunzi wako wamfukuze, lakini hawakuweza."
41O Jesus phendia, "Tume kai chi pachan tume ai chorhe kai san! Sode virama trobul te beshav tumensa? Sode vriama rhevdiv tumen? An che shaves katse."
41Yesu akasema, "Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka! Nitakaa nanyi na kuwavumilia mpaka lini?" Kisha akamwambia huyo mtu, "Mlete mtoto wako hapa."
42Sar o shav pasholas karing O Jesus, o beng shudia les pe phuv, ai drechinisardia les zurales. Numa O Jesus gonisardia le benges, ai sastiardia le raklorhes, ai dia les palpale ka pesko dat.
42Wakati mtoto huyo alipokuwa anamjia Yesu, yule pepo alimwangusha chini na kumtia kifafa. Lakini Yesu akamkemea yule pepo mchafu akamponya mtoto na kumkabidhi kwa baba yake.
43Ai savorhe chudisaile anda barimos le Devlesko. Ai sar savorhe dikhenas o lashimos kai kerelas O Jesus, phendia leske disiplonge.
43Watu wote wakashangazwa na uwezo mkuu wa Mungu. Wale watu walipokuwa bado wanashangaa juu ya mambo yote aliyofanya, Yesu aliwaambia wanafunzi wake,
44"Tumenge ashunen mishto so mothav; O Shav le Manushesko trobul te avel dino andal vas le manushenge."
44"Tegeni masikio, myasikie mambo haya: Mwana wa Mtu anakwenda kutiwa mikononi mwa watu."
45Numa won chi haliarde kadia vorba, ke garado sas lendar, saxke te na haliaren; ai daraile te phushen lestar pa kadia vorba.
45Lakini wao hawakuelewa maana ya usemi huo. Jambo hilo lilikuwa limefichwa kwao ili wasitambue; nao wakaogopa kumwuliza juu ya msemo huo.
46Le disipluria marenas mui mashkar pende, te zhanen savo sas mai baro anda lende.
46Kukatokea majadiliano kati ya wale wanafunzi kuhusu nani kati yao aliyekuwa mkuu zaidi.
47O Jesus zhanglia so gindinaspe, lia ieke raklorhes, ai thodia les pasha peste,
47Yesu aliyajua mawazo yaliyokuwa mioyoni mwao; basi akamchukua mtoto mdogo akamweka karibu naye,
48Ai phendia lenge, "Kon godi primila ande murho anav kakala glata primil man, primil kodoles kai tradia ma. Ke kodo kai si o mai tsinorho mashkar tumende, kodo si o baro."
48akawaambia, "Mtu yeyote anayempokea mtoto huyu mdogo kwa jina langu, ananipokea mimi; na yeyote anayenipokea mimi, anampokea yule aliyenituma. Maana yule aliye mdogo kuliko wote kati yenu ndiye aliye mkubwa kuliko wote."
49O Iovano phendia, "Gazda, dikhliam ieke manushes kai gonil le bengen ande cho anav; ai ame aterdiardiam les, ke chi lelpe pala amende.
49Yohane alidakia na kusema, "Bwana, tumemwona mtu mmoja akitoa pepo kwa kulitumia jina lako nasi tukajaribu kumkataza kwa kuwa yeye si mmoja wetu."
50"Na aterdiaren les: O Jesus phendia leske ai le kolaver disipluria, "Ke kon chi rimol tumaro zakono tumensalo."
50Lakini Yesu akamwambia, "Msimkataze; kwani asiyepingana nanyi yuko upande wenu."
51E vriama pasholas kana O Jesus avela lino ando rhaio, wo manglia te zhal ande Jerusalem.
51Wakati ulipokaribia ambapo Yesu angechukuliwa juu mbinguni, yeye alikata shauri kwenda Yerusalemu.
52Tradia angla peste slugen kai gele; ai dine ande gav le Samaritanongo te lasharen lesko than,
52Basi, akawatuma wajumbe wamtangulie, nao wakaenda wakaingia kijiji kimoja cha Wasamaria ili wamtayarishie mahali.
53numa chi primisarde les, ke zhanas karing e Jerusalem.
53Lakini wenyeji wa hapo hawakutaka kumpokea kwa sababu alikuwa anaelekea Yerusalemu.
54Kana le disipluria o Iakov, ai o Iovano dikhle so kerdiolas, phende, "Devla, mangas te akharas iag anda cheri te phabarel les, sar kerdias o Elijah?"
54Basi, wanafunzi wake, kina Yohane na Yakobo, walipoona hayo, wakasema, "Bwana, wataka tuamuru moto ushuke kutoka mbinguni uwateketeze?"
55O Jesus boldiape karing lende, ai tsipisardia pe lende; ai phendia, "Chi zhanen savestar chorho duxo avilo pe tumende.
55Lakini yeye akawageukia, akawakemea akasema, "Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo;
56Ke O Shav le manushesko chi avilo te xasarel le manushen, numa te skepil le."
56kwa maana Mwana wa Mtu hakuja kuyaangamiza maisha ya watu, bali kuyaokoa." Wakatoka, wakaenda kijiji kingine.
57Ai gele ando aver foro. Sar zhanas po drom, iek manush phendia ka Jesus, "Devla, lav pala tute kai godi zhasa."
57Walipokuwa wakisafiri njiani, mtu mmoja akamwambia Yesu, "Nitakufuata kokote utakakokwenda."
58O Jesus phendia leske, "Le Renard si le gropi, ai le chiriklia si le kuiburia, numa O Shav le Manushes nai les chi iek than kai te thol pesko shero.
58Yesu akasema, "Mbweha wana mapango, na ndege wana viota; lakini Mwana wa Mtu hana mahali pa kupumzikia."
59Mai phendia avreske, "Aidi pala mande." Numa wo phendia, "Devla, mek mai anglal te gropov murhe dades."
59Kisha akamwambia mtu mwingine, "Nifuate." Lakini huyo akasema, "Bwana, niruhusu kwanza niende kumzika baba yangu."
60O Jesus phendia leske, "Mukh le mulen te gropon penge mulen, ai te zhan phen pa rhaio le Devlesko."
60Yesu akamwambia, "Waache wafu wazike wafu wao; bali wewe nenda ukatangaze Ufalme wa Mungu."
61Aver manush phendia, "Lava ma pala tute, Devla; numa mek ma te zhav mai anglal te dikhav murhe naimon."
61Na mtu mwingine akamwambia, "Nitakufuata, lakini niruhusu kwanza nikawaage wale walio nyumbani kwangu."
62O Jesus phendia leske, "Kon godi thol o vas ka wurdon, ai dikhel palpale, nai vuzho ka rhaio le Devlesko."
62Yesu akamwambia, "Yeyote anayeshika jembe tayari kulima na huku anaangalia nyuma, hafai kwa Ufalme wa Mungu."