Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

10

1Ndugu, nataka mjue kwamba babu zetu wote walikuwa chini ya ulinzi wa lile wingu, na kwamba wote walivuka salama ile bahari.
1Vennad, ma ei taha, et teil jääks teadmata, et kõik meie esiisad olid pilve all ja kõik läksid läbi mere
2Wote walibatizwa katika umoja na Mose kwa lile wingu na ile bahari.
2ja kõik ristiti Moosesesse pilves ja meres,
3Wote walikula chakula kilekile cha kiroho,
3ja kõik sõid sama vaimulikku rooga
4wakanywa pia kinywaji kilekile cha kiroho, maana walikunywa kutoka ule mwamba wa kiroho uliowafuata; mwamba huo ulikuwa Kristo mwenyewe.
4ja kõik jõid sama vaimulikku jooki, sest nad jõid vaimulikust kaljust, mis saatis neid; see kalju oli aga Kristus.
5Hata hivyo, wengi wao hawakumpendeza Mungu, na maiti zao zilisambazwa jangwani.
5Kuid enamik neist ei olnud Jumalale meelepärased ning nad löödi maha kõrbes.
6Sasa, mambo hayo yote ni mfano tu kwetu; yanatuonya sisi tusitamani ubaya kama wao walivyotamani.
6Need lood on saanud meile näiteiks, et meie ei himustaks kurja, nii nagu nemad himustasid.
7Msiwe waabudu sanamu kama baadhi yao walivyokuwa; kama yasemavyo Maandiko: "Watu waliketi kula na kunywa, wakasimama kucheza."
7Ärge ka saage ebajumalateenijateks, nõnda kui mõned neist, nagu on kirjutatud: 'Rahvas istus maha sööma ja jooma ning tõusis üles mängima.'
8Wala tusizini kama baadhi yao walivyozini, wakaangamia siku moja watu ishirini na tatu elfu.
8Ärgem ka langegem kõlvatusse, nõnda kui mõned neist langesid ning ühel päeval hukkus kakskümmend kolm tuhat.
9Tusimjaribu Bwana kama baadhi yao walivyomjaribu, wakauawa na nyoka.
9Ärgem ka kiusakem Issandat, nagu mõned neist kiusasid ning hukkusid madude läbi.
10Wala msinung'unike kama baadhi yao walivyonung'unika, wakaangamizwa na Mwangamizi!
10Ärge ka nurisege, nagu mõned neist nurisesid ning hukkusid laastaja käe läbi.
11Basi, mambo hayo yaliyowapata wao ni kielelezo kwa wengine, na yaliandikwa ili kutuonya sisi, ambao mwisho wa nyakati unatukabili.
11Aga kõik see sai neile osaks näite pärast ning on kirjutatud hoiatuseks meile, kelle ajal jõuab kätte ajastu lõpp.
12Anayedhani amesimama imara ajihadhari asianguke.
12Niisiis, kes enese arvab seisvat, vaadaku, et ta ei langeks!
13Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
13Senini pole teid tabanud muu kui inimlik kiusatus. Aga Jumal on ustav, kes ei luba teid kiusata rohkem, kui te suudate taluda, vaid koos kiusatusega valmistab ka väljapääsu, nii et te suudate taluda.
14Kwa hiyo, wapenzi wangu, epeni ibada za sanamu.
14Just seepärast, mu armsad, põgenege ebajumalateenistuse eest!
15Naongea nanyi, watu wenye busara; jiamulieni wenyewe hayo nisemayo.
15Ma räägin teile kui arusaajaile, otsustage ise, mida ma räägin:
16Tunapomshukuru Mungu kwa kikombe kile cha baraka, je, huwa hatushiriki damu ya Kristo? Na tunapoumega mkate, je, huwa hatushiriki mwili wa Kristo?
16Õnnistuse karikas, mida me õnnistame, - eks see ole Kristuse vere osadus? Leib, mida me murrame, - eks see ole Kristuse ihu osadus?
17Kwa kuwa mkate huo ni mmoja, sisi, ingawa ni wengi, tu mwili mmoja; maana sote twashiriki mkate huohuo.
17Et leib on üks, siis ka meie, paljud, oleme üks ihu, sest me kõik saame osa sellest ühest leivast.
18Chukueni, kwa mfano, Wayahudi wenyewe: kwao, wenye kula vilivyotambikiwa madhabahuni waliungana na hiyo madhabahu.
18Vaadake neid, kes ihu poolest on Iisrael! Eks need, kes ohvreid söövad, ole altari osaduses?
19Nataka kusema nini, basi? Kwamba chakula kilichotambikiwa sanamu ni kitu zaidi ya chakula? Na hizo sanamu, je, ni kitu kweli zaidi ya sanamu?
19Mida ma siis nüüd ütlen? Kas seda, et ebajumalaohver on midagi? Või et ebajumal on midagi?
20Hata kidogo! Ninachosema ni kwamba tambiko wanazotoa watu wasiomjua Mungu wanawatolea pepo, sio Mungu. Sipendi kamwe ninyi muwe na ushirika na pepo.
20Ei! Vaid ma ütlen, et seda, mida ohverdatakse, ei ohverdata Jumalale, vaid kurjadele vaimudele. Aga ma ei taha, et teie saaksite kurjade vaimude kaaslasteks.
21Hamwezi kunywa kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo; hamwezi kushiriki katika meza ya Bwana na katika meza ya pepo.
21Te ei või juua Issanda karikast ja kurjade vaimude karikast, te ei või osa saada Issanda lauast ja kurjade vaimude lauast.
22Au je, tunataka kumfanya Bwana awe na wivu? Mnadhani tuna nguvu zaidi kuliko yeye?
22Või tahame Issandat teha kiivaks? Kas oleme temast tugevamad?
23Vitu vyote ni halali, lakini si vyote vinafaa. Vitu vyote ni halali lakini si vyote vinajenga.
23Öeldakse: 'Kõik on lubatud!' - Siiski kõigest ei ole kasu. 'Kõik on lubatud!' - Siiski kõik ei ehita kogudust.
24Mtu asitafute faida yake mwenyewe, ila faida ya mwenzake.
24Ärgu ükski otsigu oma, vaid teise kasu!
25Kuleni chochote kile kiuzwacho sokoni bila ya kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu;
25Kõike, mida lihaturul müüakse, sööge, ja ärge hakake kõhklema sisetunde pärast,
26maana Maandiko yasema: "Dunia na vyote vilivyomo ni mali ya Bwana."
26sest maa ja tema täius on Issanda päralt!
27Kama mtu ambaye si muumini akiwaalikeni nanyi mkakubali kwenda, basi, kuleni vyote atakavyowaandalieni bila kuulizauliza kwa sababu ya dhamiri zenu.
27Kui keegi uskmatuist kutsub teid külla ja te tahate minna, siis sööge kõike, mida teile ette pannakse, kõhklemata sisetunde pärast.
28Lakini mtu akiwaambieni: "Chakula hiki kimetambikiwa sanamu," basi, kwa ajili ya huyo aliyewaambieni hivyo na kwa ajili ya dhamiri, msile.
28Kui aga keegi peaks teile ütlema: 'See on ohvriliha', siis ärge sööge selle inimese pärast, kes tegi märkuse, ning sisetunde pärast.
29Nasema, "kwa ajili ya dhamiri," si dhamiri yenu, bali dhamiri yake huyo aliyewaambieni. Mtaniuliza: "Kwa nini uhuru wangu utegemee dhamiri ya mtu mwingine?
29Aga ma ei räägi sinu, vaid teise sisetundest.Sa ehk ütled: 'Mispärast peab nüüd teise sisetunne minu vabaduse suhtes olema määrav?
30Ikiwa mimi nashiriki chakula hicho huku namshukuru Mungu, kwa nini nilaumiwe kwa chakula ambacho kwa ajili yake nimemshukuru Mungu?"
30Kui mina seda tänuga vastu võtan, miks mind siis teotatakse selle pärast, mille eest ma tänan?'
31Basi, chochote mfanyacho iwe ni kula au kunywa, fanyeni yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.
31Niisiis, kas te nüüd sööte või joote või teete midagi muud - tehke seda Jumala austamiseks!
32Msiwe kikwazo kwa Wayahudi au kwa Wagiriki au kwa kanisa la Mungu.
32Ärge olge komistuseks ei juutidele ega kreeklastele ega Jumala kogudusele,
33Muwe kama mimi; najaribu kuwapendeza wote kwa kila njia, bila kutafuta faida yangu mwenyewe ila faida ya wote, wapate kuokolewa.
33nii nagu minagi püüan igati kõigile meeldida ning ei otsi oma, vaid paljude kasu, et nad päästetaks.