Swahili: New Testament

Estonian

1 Corinthians

11

1Niigeni mimi kama ninavyomwiga Kristo.
1Võtke mind eeskujuks, nagu mina võtan Kristuse!
2Nawapeni hongera kwa sababu mnanikumbuka na kwa sababu mnayashikilia yale maagizo niliyowapeni.
2Ma kiidan teid, vennad, et te mind igati meeles peate ja hoiate pärimusi, nõnda nagu ma need teile andsin.
3Lakini napenda pia mjue kwamba Kristo ni kichwa cha kila mwanamume, na mwanamume ni kichwa cha mkewe, na Mungu ni kichwa cha Kristo.
3Aga ma tahan, et te teaksite: Kristus on iga mehe pea, aga mees on naise pea, ja Jumal on Kristuse pea.
4Basi, kila mwanamume anayesali au anayetangaza ujumbe wa Mungu huku amefunika kichwa chake, huyo anamdharau Kristo.
4Iga mees, kes kaetud peaga palvetab või prohvetlikult kõneleb, häbistab oma pead.
5Na mwanamke akisali au kutangaza ujumbe wa Mungu bila kufunika kichwa chake, anamdharau mumewe; anayefanya hivyo ni sawa tu na mwanamke aliyenyoa kichwa chake.
5Ja iga naine, kes paljapäi palvetab või prohvetlikult kõneleb, häbistab oma pead, sest see on otse nõnda, nagu oleks ta paljakspöetu.
6Mwanamke asiyefunika kichwa chake, afadhali anyoe nywele zake. Lakini ni aibu kwa mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa; basi, afadhali afunike kichwa chake.
6Kui naine ei kata oma pead, siis ta lasku ka oma juuksed maha lõigata; kui aga naisele on häbiks lasta juukseid lõigata või pead paljaks pügada, siis ta katku oma pea kinni!
7Haifai mwanamume kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano wa Mungu na kioo cha utukufu wake Mungu; lakini mwanamke ni kioo cha utukufu wa mwanamume.
7Mees ei ole kohustatud oma pead katma, kuna ta on Jumala kuju ja aupaiste, naine aga on mehe aupaiste.
8Mwanamume hakutoka kwa mwanamke, ila mwanamke alitoka kwa mwanamume.
8Sest mees ei ole ju naisest, vaid naine mehest,
9Mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, ila mwanamke aliumbwa kwa ajili ya mwanamume.
9ega ole ka mees loodud naise pärast, vaid naine mehe pärast.
10Ndiyo maana mwanamke hufunika kichwa chake, iwe ishara ya mamlaka yaliyo juu yake, na pia kwa sababu ya malaika.
10Seepärast on naine kohustatud kandma meelevalla tunnust pea peal inglite pärast.
11Hata hivyo, mbele ya Bwana mwanamke si kitu bila mwanamume, naye mwanamume si kitu bila mwanamke.
11Ometi ei ole Issanda ees mees ilma naiseta midagi ega naine ilma meheta midagi,
12Kama vile mwanamke alivyotokana na mwanamume, vivyo hivyo mwanamume huzaliwa na mwanamke; kila kitu hutoka kwa Mungu.
12sest nii nagu naine on mehest, nõnda on ka mees naise läbi, aga kõik on Jumalast.
13Amueni wenyewe: Je, inafaa mwanamke kumwomba Mungu bila kuvaa kitu kichwani?
13Otsustage ise: kas naisel on kohane paluda Jumalat paljapäi?
14Hata maumbile yenyewe huonyesha wazi kwamba kwa mwanamume kuwa na nywele ndefu ni aibu kwake mwenyewe;
14Eks loodus ise õpeta teile, et mehele ei ole auks kanda pikki juukseid,
15lakini kwa mwanamke kuwa na nywele ni heshima kwake; nywele zake ndefu amepewa ili zimfunike.
15aga kui naine kannab pikki juukseid, siis on see temale auks, sest pikad juuksed on talle antud katte eest.
16Kama mtu anataka kuleta ubishi juu ya jambo hili, basi, na ajue kwamba sisi hatuna desturi nyingine, wala makanisa ya Mungu hayana desturi nyingine.
16Kui aga keegi kavatseb kiusu ajada, siis ta teadku, et meil ega Jumala kogudustel ei ole seesugust kommet.
17Nikiwa bado nawapeni maagizo haya, siwezi hata kidogo kuwapa ninyi hongera kuhusu haya yafuatayo: mikutano yenu ninyi waumini yaleta hasara zaidi kuliko faida.
17Kuid seda käskides ma ei kiida teid, sest teie kokkutulekud ei ole teile kasuks, vaid kahjuks.
18Awali ya yote, nasikia kwamba mnapokutana pamoja hutokea mafarakano kati yenu. Nami naamini kiasi,
18Sest esmalt ma kuulen, et kui te tulete kokku kogudusena, esineb teie seas lõhesid, ja osalt ma usun seda.
19maana ni lazima fikira tofauti ziweko miongoni mwenu, ili wale walio thabiti wapate kutambulikana.
19Teie seas peabki ju olema lahkarvamusi, et tunnustatud teie seast saaksid avalikuks.
20Kweli mnakutana, lakini si kwa ajili ya kula chakula cha Bwana!
20Kui te nüüd kokku tulete, siis ei saa pidada Issanda õhtusöömaaega,
21Maana mnapokula kila mmoja hukikalia chakula chake mwenyewe, hata hutokea kwamba baadhi yenu wana njaa, na wengine wamelewa!
21sest igaüks võtab sööma asudes ette omaenda toidu, ja mõni jääb nälga, ja mõni on joobnud.
22Je, hamwezi kula na kunywa nyumbani kwenu! Au je, mnalidharau kanisa la Mungu na kuwaaibisha hao wasio na kitu? Niwaambie nini? Niwasifu? La hasha! Si kuhusu jambo hili.
22Kas teil siis tõesti ei ole kodasid, kus te võite süüa ja juua? Või te põlastate Jumala kogudust ja häbistate neid, kel midagi ei ole? Mis ma pean teile ütlema? Kas pean teid kiitma? Selle poolest ma teid küll ei kiida.
23Maana mimi nilipokea kwa Bwana yale maagizo niliyowaachieni: kwamba, usiku ule Bwana Yesu aliotolewa, alitwaa mkate,
23Sest mina olen Issandalt saanud, mida ma olen andnud teilegi: et Issand Jeesus sel ööl, mil tema ära anti, võttis leiva,
24akamshukuru Mungu, akaumega, akasema: "Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa kunikumbuka."
24tänas, murdis ja ütles: 'See on minu ihu, mis teie eest antakse. Tehke seda minu mälestuseks!'
25Vivyo hivyo, baada ya kula, akatwaa kikombe akasema: "Hiki ni kikombe cha agano jipya linalothibitishwa kwa damu yangu. Fanyeni hivi, kila mnapokunywa, kwa kunikumbuka."
25Selsamal kombel võttis ta ka karika pärast õhtusöömaaega ja ütles: 'See karikas on uus leping minu veres. Nii sagedasti kui te sellest joote, tehke seda minu mälestuseks!'
26Maana kila mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mwatangaza kifo cha Bwana, mpaka atakapokuja.
26Sest iga kord, kui te seda leiba sööte ja karikast joote, kuulutate teie Issanda surma, kuni tema tuleb.
27Kwa hiyo, kila aulaye mkate huo au kunywa kikombe cha Bwana bila kustahili, atakuwa na hatia dhidi ya mwili na damu ya Bwana.
27Niisiis, kes iial seda leiba sööb või Issanda karikast joob vääritul viisil, on süüdi Issanda ihu ja vere vastu.
28Basi, kila mtu ajichunguze mwenyewe kwanza, ndipo ale mkate huo na anywe kikombe hicho;
28Inimene katsugu ennast läbi ja alles siis söögu sellest leivast ja joogu sellest karikast!
29maana anayekula na kunywa bila kutambua maana ya mwili wa Bwana, anakula na kunywa hukumu yake yeye mwenyewe.
29Sest kes sööb ja joob, see sööb ja joob enesele nuhtlust, kui ta ei anna aru sellest ihust.
30Ndiyo maana wengi kati yenu ni dhaifu na wagonjwa, na wengine kadhaa wamekufa.
30Seepärast ongi teie seas palju nõrku ja põduraid ning paljud on surnud.
31Kama tungejichunguza wenyewe vizuri hatungeadhibiwa hivyo.
31Kui me aga iseenda üle õigesti otsustame, siis ei mõisteta meid hukka;
32Lakini tunapohukumiwa na Bwana, tunafunzwa tuwe na nidhamu, ili tusije tukahukumiwa pamoja na ulimwengu.
32kui meie eneste üle mõistame kohut, siis Issand kasvatab meid, et meid koos maailmaga hukka ei mõistetaks.
33Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokutana kula chakula cha Bwana, kila mmoja amngoje mwenzake.
33Niisiis, mu vennad, kui te tulete kokku sööma, siis oodake üksteist.
34Na kama kuna yeyote aliye na njaa, na ale nyumbani kwake, ili kukutana kwenu kusisababishe hukumu. Lakini, kuhusu yale mambo mengine, nitawapeni maelezo nitakapokuja.
34Kui kellelgi on nälg, siis ta söögu enne kodus, et te ei tuleks kokku nuhtluseks. Muud asjad ma korraldan siis, kui tulen.