Swahili: New Testament

Estonian

1 Thessalonians

2

1Ndugu, ninyi wenyewe mnafahamu kwamba ziara yetu kwenu haikuwa bure.
1Teie, vennad, teate ju meie tulekut teie juurde, et see ei ole läinud tühja.
2Mnajua jinsi tulivyodhulumiwa na kutukanwa kule Filipi kabla ya kufika kwenu Thesalonike. Ingawa kulikuwa na upinzani mwingi, Mungu wetu alitujalia uhodari wa kuwahubirieni Habari Njema yake.
2Kuigi me just enne, nagu te teate, olime kannatanud ja meid teotati Filippi linnas, andis Jumal meile siiski julguse kuulutada Jumala evangeeliumi suure võitlusega.
3Jambo tunalosisitiza kwenu si jambo linalotegemea uongo au nia mbaya; wala hatupendi kumdanganya mtu yeyote.
3Meie manitsused ei tulene eksitusest ega ebapuhtusest ega pettusest.
4Sisi twanena daima kama atakavyo Mungu kwani yeye alituona kwamba tunafaa, akatukabidhi hii Habari Njema. Si nia yetu kuwapendeza watu hata kidogo, bali twataka kumpendeza Mungu ambaye anajua mioyo yetu mpaka ndani.
4Vastupidi, me räägime nõnda, nagu Jumal meid on arvanud kõlblikuks, et usaldada meie kätte evangeelium: me ei räägi, et meeldida inimestele, vaid Jumalale, kes meie südamed läbi katsub.
5Ninyi mnajua kwamba sisi hatukuja kwenu na maneno matamu ya kubembeleza wala hatukutumia maneno ya kijanja ya kuficha ubinafsi fulani; Mungu ni shahidi!
5Sest nagu te teate, ei ole me kunagi tulnud lipitsevate kõnedega ega ajendatuna ahnusest, Jumal on tunnistajaks.
6Hatukutafuta sifa kutoka kwa watu, wala kutoka kwenu, wala kutoka kwa mtu yeyote,
6Me ei otsi kiitust inimestelt, ei teilt ega muilt,
7ingawa sisi tukiwa mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulikuwa Wapole kati yenu kama alivyo mama kwa watoto wake.
7kuigi me kui Kristuse apostlid oleksime võinud olla tähtsad; vaid me olime malbed teie keskel, nii nagu toitja ema hellitab oma lapsi;
8Tuliwapenda ninyi sana hata tukawa tayari kuwashirikisha si tu Habari Njema ya Mungu, bali pia na maisha yetu. Ndivyo mlivyokuwa wapenzi wetu!
8nõnda oleksime meiegi hellusest teie vastu andnud heameelega teile mitte üksnes Jumala evangeeliumi, vaid ka oma hinge, kuna te olite saanud meile armsaks.
9Ndugu, mnakumbuka jinsi tulivyofanya kazi na kutaabika. Tulipowaleteeni Habari Njema ya Mungu tulifanya kazi mchana na usiku kusudi tusiwe mzigo kwa mtu yeyote miongoni mwenu.
9Teie ju mäletate, vennad, meie vaeva ja pingutust! Töötades ööd ja päevad, et mitte saada koormaks kellelegi teist, kuulutasime teile Jumala evangeeliumi.
10Ninyi mnaweza kushuhudia, na Mungu pia ni shahidi, jinsi mwenendo wetu kati yenu ninyi mnaoamini ulivyokuwa mzuri, mwadilifu na usio na lawama.
10Teie ja Jumal olete tunnistajaks, kui vagalt ja õiglaselt ja laitmatult me oleme käitunud teiega, kes te usute;
11Mnajua kwamba sisi tulimtendea kila mmoja wenu kama vile baba anavyowatendea watoto wake mwenyewe.
11nagu te teate sedagi, kuidas me igaühte teie seast otsekui isa oma lapsi
12Tuliwapeni moyo, tuliwafarijini na kuwahimiza ili mpate kuishi maisha yampendezayo Mungu ambaye aliwaiteni mshiriki Utawala na utukufu wake.
12julgustasime ja lohutasime ja keelitasime, et te elaksite Jumala vääriliselt, kes teid kutsub oma kuningriiki ja kirkusse.
13Tena tunayo sababu nyingine ya kumshukuru Mungu: tulipowaleteeni ujumbe wa Mungu, ninyi mliusikia mkaupokea, si kama vile ujumbe wa binadamu, bali kama ujumbe wa Mungu, na kweli ndivyo ulivyo. Maana Mungu anafanya kazi ndani yenu ninyi mnaoamini.
13Ja seepärast me tänamegi alatasa Jumalat, et kui te meie käest saite kuulda Jumala sõna, siis te ei võtnud seda vastu mitte inimeste sõnana, vaid sellena, mida see tõepoolest on - Jumala sõnana, mis on tegev ka teis, kes te usute.
14Ndugu, ninyi mmepatwa na mambo yaleyale yaliyoyapata makanisa ya Mungu kule Yudea, mambo yaliyowapata watu walio wake Kristo Yesu. Ninyi mlidhulumiwa na wananchi wenzenu kama vile wao walivyodhulumiwa na wenzao Wayahudi,
14Sest teie, vennad, olete saanud nende Kristuses Jeesuses olevate Jumala koguduste järgijaiks, mis on Juudamaal, sest teiegi olete saanud kannatada oma suguvendade poolt, niisamuti nagu nemad juutide poolt,
15ambao walimuua Bwana Yesu na manabii, wakatutesa na sisi pia. Watu hao wanamchukiza Mungu, tena ni adui za kila mtu!
15kes tapsid ka Issanda Jeesuse ning prohvetid ja kiusasid meid taga; nemad ei ole Jumalale meelepärased ja on kõigi inimeste vastased,
16Hata walijaribu kutuzuia kuwahubiria watu wa mataifa mengine ujumbe utakaowaletea wokovu. Ndivyo walivyokamilisha orodha ya dhambi zote walizotenda siku zote. Lakini sasa hasira ya Mungu imewaangukia.
16takistades meid rääkimast paganaile nende päästmiseks; nii täidavad nad igati oma pattude mõõtu. Aga viha on jõudnud nende peale lõplikult.
17Ndugu, kuachana kwetu nanyi kulikuwa kwa muda tu, tena kuachana huko kulikuwa kwa mwili tu na si kwa roho. Kitambo kifupi baadaye, tulishikwa na hamu kubwa ya kuwaoneni tena!
17Meie aga, vennad, olles mõnda aega teist lahutatud küll palge, mitte südame poolest, oleme suure igatsusega soovinud näha teie palet.
18Kwa hiyo tuliamua kuwatembeleeni tena. Nami, Paulo, nilijaribu kuja kwenu zaidi ya mara moja, lakini Shetani alituzuia.
18Seepärast oleme tahtnud - mina, Paulus, küll rohkem kui korra - tulla tagasi teie juurde, kuid saatan on meid takistanud.
19Je, tutakaposimama mbele ya Bwana Yesu wakati atakapokuja, fahari ya ushindi wetu itakuwa nini? Itakuwa ni ninyi wenyewe; ninyi ndio tumaini letu na furaha yetu.
19Sest kes on meie lootus, meie rõõm, meie kiitlemise aupärg meie Issanda Jeesuse Kristuse palge ees tema tulemisel kui mitte teie?
20Naam, ninyi ni utukufu wetu na furaha yetu!
20Jah, teie olete meie kirkus ja rõõm!