Swahili: New Testament

Estonian

1 Thessalonians

4

1Hatimaye, ndugu zangu, mmejifunza kutoka kwetu namna mnavyopaswa kuishi ili kumpendeza Mungu. Na kweli mmekuwa mnaishi hivyo. Sasa tunawaombeni na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu mfanye vema zaidi.
1Viimaks nüüd veel, vennad, me palume ja keelitame teid Issandas Jeesuses, et nagu te olete meilt saanud teada, kuidas teil tuleb elada ja Jumalale meeldida - nõnda te ju elategi -, et te selles veelgi enam edeneksite.
2Maana mnayajua yale maagizo tuliyowapeni kwa mamlaka ya Bwana Yesu.
2Te ju teate, millised korraldused me teile oleme Issandas Jeesuses andnud.
3Mungu anataka ninyi muwe watakatifu na mjiepushe kabisa na maisha ya zinaa.
3Jah, see on Jumala tahtmine: teie pühitsus, et te hoiduksite hooruse eest,
4Kila mwanamume anapaswa kujua namna ya kuishi na mkewe kwa utakatifu na heshima,
4et igaüks teie seast oskaks pidada oma astjat pühitsuses ja aus,
5na si kwa tamaa mbaya kama watu wa mataifa mengine wasiomjua Mungu.
5mitte himude kires, nõnda nagu paganad, kes ei tea midagi Jumalast,
6Basi, mtu yeyote asimkosee au kumpunja mwenzake kuhusu jambo hili. Tulikwisha waambieni hayo na kuwaonya kwamba Bwana atawaadhibu wanaofanya mambo hayo.
6et ükski ei oleks üleastuja ega petaks oma venda asjaajamises, sest Issand maksab kõige säärase eest kätte, nii nagu me oleme seda teile ka enne ütelnud ja tunnistanud.
7Mungu hakutuita tuishi maisha ya zinaa, bali tuishi katika utakatifu.
7Jumal ei ole meid ju kutsunud rüvedusele, vaid pühitsusele.
8Kwa hiyo basi, anayedharau mafundisho hayo hamdharau mtu, bali amdharau Mungu mwenyewe anayewapeni Roho wake Mtakatifu.
8Seepärast siis, kes on selle suhtes hoolimatu, see on hoolimatu mitte inimese, vaid Jumala vastu, kes oma Püha Vaimu teisse annab.
9Hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya kuwapenda ndugu zenu waumini. Ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu namna mnavyopaswa kupendana.
9Aga vennaarmastusest ei ole vaja teile kirjutada, sest Jumal on teid endid õpetanud armastama üksteist,
10Na mmekuwa mkiwatendea hivyo ndugu zenu wote kila mahali katika Makedonia. Basi, ndugu tunawaombeni mfanye hata zaidi.
10ja seda teie osutategi kõigile vendadele terves Makedoonias. Meie aga manitseme teid, vennad, et te veelgi edeneksite.
11Muwe na nia ya kuishi maisha ya utulivu, kila mmoja ashughulikie mambo yake mwenyewe na afanye kazi kwa mikono yake mwenyewe kama tulivyowaagiza pale awali.
11Ja arvake auks elada vaikselt, ajada oma asju ning teha tööd oma kätega, nagu meie teid oleme käskinud,
12Kwa namna hiyo mtajipatia sifa nzuri kutoka kwa wale wasio Wakristo, na hamtakuwa na lazima ya kuwategemea wengine kwa mahitaji yenu.
12nii et te elaksite kombekalt nende ees, kes on väljaspool, ega oleks teil kelleltki midagi vaja.
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini.
13Meie ei taha aga, vennad, et teil jääks teadmata nende järg, kes on läinud magama, et teie ei oleks kurvad nagu need teised, kellel ei ole lootust.
14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
14Sest kui me usume, et Jeesus on surnud ja üles tõusnud, siis usume ka, et Jumal äratab Jeesuse kaudu üles need, kes koos temaga on läinud magama.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana; sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki, wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia.
15Jah, seda me ütleme teile Issanda sõnana, et meie, kes me üle jääme elama Issanda tulekuni, ei jõua ette magamaläinutest,
16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza.
16sest Issand ise tuleb sõjahüüu, peaingli hääle ja Jumala pasuna saatel alla taevast ning esmalt tõusevad üles surnud, kes on läinud magama Kristuses,
17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana.
17pärast kistakse meid, kes me oleme üle jäänud elama, ühtviisi koos nendega pilvedes üles õhku Issandale vastu, ja nõnda me saame alati olla koos Issandaga.
18Basi, farijianeni kwa maneno haya.
18Julgustage siis üksteist nende sõnadega!