1Ndugu, hakuna haja ya kuwaandikieni juu ya nyakati na majira yatakapotukia mambo haya.
1Aegade ja tundide kohta, vennad, ei ole aga vaja teile kirjutada,
2Maana ninyi wenyewe mwajua kwamba Siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajavyo usiku.
2sest te teate täpselt, et Issanda päev tuleb just nii nagu varas öösel.
3Watu watakapokuwa wanasema: "Kila kitu ni shwari na salama" ndipo uharibifu utakapowaangukia ghafla! Mambo hayo yatatukia ghafla kama uchungu wa uzazi unavyomjia mama anayejifungua, wala watu hawataweza kuepukana nayo.
3Kui öeldakse: 'Nüüd on rahu ja kindel olek', siis langeb äkiline hukatus nende peale nagu sünnitusvalud lapseootel naise peale, ja nad ei pääse pakku.
4Lakini ninyi ndugu, hamko gizani, na siku hiyo haipaswi kuwajieni ghafla kama vile mwizi.
4Teie aga, vennad, ei ole pimeduses, nii et see päev saaks teid tabada nagu varas.
5Ninyi nyote ni watu mnaoishi katika mwanga, watu wa mchana. Sisi si watu wa usiku, wala wa giza.
5Teie kõik olete ju valguse lapsed ja päeva lapsed. Meie ei ole öö ega pimeduse lapsed.
6Basi, tusilale usingizi kama wengine; tunapaswa kukesha na kuwa na kiasi.
6Niisiis, ärgem magagem nagu teised, vaid olgem ärkvel ja kained,
7Wanaolala hulala usiku, na walevi hulewa usiku.
7sest magajad magavad öösel ja joomarid on joobnud öösel.
8Lakini sisi ni watu wa mchana na tunapaswa kuwa na kiasi. Tunapaswa kuvaa imani na upendo kama vazi la kujikinga kifuani, na tumaini letu la wokovu kama kofia ya chuma.
8Aga meie, kes me oleme päeva lapsed, olgem kained, rõivastatud usu ja armastuse kaitserüüga ning päästelootuse kiivriga,
9Maana Mungu hakututeua ili tuangamizwe na ghadhabu yake, bali tuupate wokovu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo,
9sest Jumal ei ole meid asetanud viha alla, vaid pääste saamiseks meie Issanda Jeesuse Kristuse läbi,
10ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, iwe tu hai au tumekufa.
10kes meie eest on surnud, et meie, kas me oleme ärkvel või magame, üheskoos temaga elaksime.
11Kwa hiyo farijianeni na kusaidiana ninyi kwa ninyi kama mnavyofanya sasa.
11Seepärast julgustage üksteist ja igaüks kosutagu teist, nagu te seda teetegi!
12Ndugu, tunawaombeni muwastahi wale wanaofanya kazi kati yenu, wale wanaowaongoza na kuwafundisheni kuhusu maisha ya Kikristo.
12Ent me palume teid, vennad, tunnustada neid, kes teie seas tööd teevad ja teid Issandas juhatavad ning noomivad,
13Wapeni heshima kubwa na kuwapenda kwa sababu ya kazi wanayofanya. Muwe na amani kati yenu.
13ja pidada neist armastuses üliväga lugu nende töö pärast. Hoidke omavahel rahu!
14Ndugu, tunawahimizeni muwaonye watu walio wavivu, muwatie moyo watu wanyonge, muwasaidie watu dhaifu, muwe na subira kwa wote.
14Meie aga manitseme teid, vennad: noomige korratuid, julgustage pelglikke, aidake nõrku, olge pika meelega kõikide vastu!
15Angalieni mtu yeyote asimlipe mwingine maovu kwa maovu, ila nia yenu iwe kutendeana mema daima na kuwatendea mema watu wote.
15Vaadake, et keegi teisele kurja ei tasuks kurjaga, vaid taotlege alati head üksteisele ja kõikidele!
16Furahini daima,
16Rõõmustage alati,
17salini kila wakati
17palvetage lakkamatult,
18na muwe na shukrani katika kila hali. Hayo ndiyo anayotaka Mungu kwenu katika kuungana kwenu na Kristo Yesu.
18tänage kõige eest - sest see on, mida Jumal teilt tahab Jeesuses Kristuses!
19Msimpinge Roho Mtakatifu;
19Ärge kustutage Vaimu,
20msidharau unabii.
20ärge põlastage prohvetiandi,
21Pimeni kila kitu: zingatieni kilicho chema,
21katsuge läbi kõik, pidage kinni heast,
22na epukeni kila aina ya uovu.
22hoiduge igasuguse kurja eest!
23Mungu anayetupatia amani awafanye ninyi watakatifu kwa kila namna na kuzilinda nafsi zenu--roho, mioyo na miili yenu--mbali na hatia yoyote wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
23Aga rahu Jumal ise pühitsegu teid läbinisti ning teie vaim ja hing ja ihu olgu tervikuna hoitud laitmatuna meie Issanda Jeesuse Kristuse tulemiseks!
24Yeye anayewaita ninyi atafanya hivyo kwani ni mwaminifu.
24Ustav on see, kes teid kutsub; küll tema teebki seda.
25Ndugu, tuombeeni na sisi pia.
25Vennad, palvetage meie eest!
26Wasalimuni ndugu wote kwa ishara ya upendo.
26Tervitage kõiki vendi püha suudlusega!
27Nawahimizeni kwa jina la Bwana muwasomee ndugu zetu wote barua hii.
27Ma vannutan teid Issanda nimel, et see kiri loetaks ette kõikidele vendadele!
28Tunawatakieni neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.
28Meie Issanda Jeesuse Kristuse arm olgu teiega!