1Basi, Mungu, kwa huruma yake, ametukabidhi kazi hii na hivyo hatufi moyo.
1Sellepärast et meil on selline amet, nagu see on antud meile halastuse kaudu, me ei tüdi ära.
2Tumeyaacha kabisa mambo yote ya aibu na ya kisirisiri. Hatuishi tena kwa udanganyifu, wala kwa kulipotosha neno la Mungu; bali tunaudhihirisha ukweli kwa kuufanya ukweli, na hivyo kujiweka chini ya uamuzi wa dhamiri za watu mbele ya Mungu.
2Me oleme lahti öelnud häbiväärseist asjust, mida peidetakse, me ei kasuta riukaid ega moonuta Jumala sõna, vaid esitame end tõe avaldamisega kõikide inimeste südametunnistusele Jumala ees.
3Maana, kama Habari Njema tunayohubiri imefichika, imefichika tu kwa wale wanaopotea.
3Kui meie evangeelium on siiski kinni kaetud, siis on see kinni kaetud neile, kes hukkuvad,
4Hao hawaamini kwa sababu yule mungu wa ulimwengu huu amezitia giza akili zao wasipate kuuona wazi mwanga wa Habari Njema ya utukufu wa Kristo, ambaye ni mfano kamili wa Mungu.
4neile uskmatuile, kellel praeguse aja jumal on mõtted sõgestanud, nii et neile ei koida evangeeliumi valgus Kristuse kirkuses, kes on Jumala kuju.
5Maana hatujitangazi sisi wenyewe, ila tunamhubiri Yesu Kristo aliye Bwana, sisi wenyewe tukiwa watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
5Me ei kuuluta ju iseendid, vaid Jeesust Kristust Issandana, endid aga teie sulastena Jeesuse pärast.
6Mungu ambaye alisema, "Mwanga na uangaze kutoka gizani," ndiye mwenye kuiangaza mioyo yetu, na kutupatia mwanga wa ujuzi wa utukufu wa Mungu uangazao katika uso wa Kristo.
6Sest see, kes ütles: 'Pimedusest paistku valgus!', on Jumal, kes on hakanud särama meie südames, et tekiks tunnetuse valgus Jeesuse Kristuse isikus olevast Jumala kirkusest.
7Basi, sisi tulio na hazina hii tuko tu kama vyombo vya udongo, ili ionekane wazi kwamba nguvu hiyo kuu yatoka kwa Mungu wala si kwetu sisi wenyewe.
7See aare on meil aga saviastjates, et võrratult suur vägi oleks Jumala oma ja ei midagi meist.
8Daima twapata taabu, lakini hatugandamizwi; twapata mashaka, lakini hatukati tamaa;
8Meid ahistatakse igati, kuid me ei ole kitsikuses; me oleme nõutud, kuid mitte meeleheitel;
9twateseka, lakini hatuachwi bila msaada; na ingawa tumeangushwa chini, hatukuangamizwa.
9meid kiusatakse taga, kuid me pole hüljatud; meid rõhutakse maha, kuid me ei hukku;
10Kila wakati tumekuwa tukichukua mwilini mwetu kifo cha Kristo, ili uhai wake Yesu pia udhihirike katika miili yetu.
10me kanname alati oma ihus Jeesuse surma, et ka Jeesuse elu avalduks meie ihus.
11Naam, katika maisha yetu yote tunakabiliwa na kifo daima kwa ajili ya Yesu, ili uzima wake Yesu udhihirike katika miili yetu inayokufa.
11Sest meid, kes me elame, antakse alatasa surma Jeesuse pärast, et ka Jeesuse elu avalduks meie surelikus ihus.
12Hii ina maana kwamba ndani yetu kifo kinafanya kazi, lakini ndani yenu uhai unafanya kazi.
12Nii on surm tegev meis, elu aga teis.
13Maandiko Matakatifu yasema: "Niliamini, ndiyo maana nilinena." Nasi pia, tukiwa na moyo huohuo wa imani, tunaamini, na kwa sababu hiyo twanena.
13Aga et meil on sellesama usu vaim, millest on kirjutatud: 'Ma usun, seepärast ma räägin', siis meiegi usume ja ka räägime,
14Tunajua kwamba yule aliyemfufua Bwana Yesu atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuweka mbele yake pamoja nanyi.
14teades, et see, kes äratas üles Issanda Jeesuse, äratab meidki koos Jeesusega üles ja seab enda ette koos teiega.
15Yote haya ni kwa faida yenu; ili kama vile neema ya Mungu inavyoenea kwa watu wengi zaidi na zaidi vivyo hivyo watu wengi zaidi watoe shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
15Kõik sünnib ju teie heaks, et arm üha enamate inimeste tänu kaudu rohkenedes kasvaks Jumala austuseks.
16Kwa sababu hiyo hatufi moyo; na hata kama maumbile yetu ya nje yataoza, lakini kwa ndani tunafanywa wapya siku kwa siku.
16Seepärast me ei tüdi, vaid kuigi meie väline inimene kulub, uueneb seesmine inimene ometi päev-päevalt.
17Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.
17Sest see praeguse hetke kerge ahistus saavutab meile määratult suure igavese au,
18Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.
18meile, kes me ei pea silmas nähtavat, vaid nähtamatut, sest nähtav on mööduv, nähtamatu aga igavene.