Swahili: New Testament

Estonian

2 Corinthians

5

1Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono.
1Me ju teame, et kui meie maine telkhoone maha kistakse, on meil elamu Jumala käest, käteta tehtud igavene hoone taevas,
2Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
2sest selles maises me ägame, igatsedes rõivastuda taevasesse eluasemesse,
3Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
3et meid ka lahti rõivastatuna ei nähtaks olevat alasti.
4Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
4Meie, kes oleme selles telgis, ägame ju koorma all, sest me ei taha lahti rõivastuda, vaid olla taevaselt rõivastatud, et elu neelaks ära sureliku.
5Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
5See, kes meid selleks valmistab, on Jumal, kes on andnud meile käsirahaks Vaimu.
6Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
6Nii me oleme siis alati kindlad, teades, et kuni me oleme ihus, oleme eemal Issanda juurest;
7Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
7sest me käime usus, mitte nägemises,
8Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
8ent me oleme kindlad ning meile meeldib pigem ära olla ihust ja viibida Issanda juures.
9Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
9Seepärast me püüamegi olla temale meelepärased, kas oleme siis kodus või võõrsil,
10Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
10sest me kõik peame saama avalikuks Kristuse kohtujärje ees, et igaüks saaks kätte, mida ta ihus olles on teinud, olgu head või halba.
11Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
11Teades nüüd, mis on Issanda kartus, me püüame veenda inimesi uskuma. Jumalale me oleme täiesti avalikud ja ma loodan ka teie südametunnistuses olla täiesti avalik.
12Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
12Me ei hakka end taas teile soovitama, vaid anname teile alust kiidelda meist, et teil oleks midagi öelda nende vastu, kes võivad kiidelda sellega, mis on silma ees, ent mitte sellega, mis on südames.
13Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
13Sest kui me oleme olnud arust ära, siis on see Jumalale, kui oleme selge aruga, siis teile.
14Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
14Sest Kristuse armastus sunnib meid, kes me otsustame nõnda: kui üks on surnud kõikide eest, siis on kõik surnud;
15Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
15ja ta on surnud kõikide eest, et elavad ei elaks enam enestele, vaid temale, kes on nende eest surnud ja üles äratatud.
16Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
16Seepärast ei tunne me nüüdsest peale kedagi inimliku loomuse poolest; kui me ka oleksime tundnud Kristust inimliku loomuse poolest, siis nüüd me ei tunne teda enam nõnda.
17Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
17Niisiis, kui keegi on Kristuses, siis ta on uus loodu, vana on möödunud, vaata, uus on sündinud.
18Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
18See kõik on Jumalast, kes meid on enesega Kristuse läbi lepitanud ja andnud meile lepitusameti;
19Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
19kuna see oli Jumal, kes Kristuses lepitas maailma enesega ega arvestanud neile nende üleastumisi ning on pannud meisse lepitussõna.
20Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
20Meie oleme nüüd Kristuse käskjalad, otsekui Jumal ise julgustaks meie kaudu. Me palume Kristuse asemel: Andke endid lepitada Jumalaga!
21Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.
21Ta on teinud patuks meie asemel selle, kes patust midagi ei teadnud, et meie saaksime Jumala õiguseks tema sees.