Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

1

1Hapo zamani, Mungu alisema na babu zetu mara nyingi kwa namna nyingi kwa njia ya manabii,
1Jumal, kes muiste palju kordi ja mitmel viisil rääkis esivanematele prohvetite kaudu,
2lakini siku hizi za mwisho, amesema nasi kwa njia ya Mwanae. Yeye ndiye ambaye kwa njia yake Mungu aliumba ulimwengu na akamteua avimiliki vitu vyote.
2on nüüd päevade lõpul meile rääkinud Poja kaudu, kelle ta on seadnud kõigi asjade pärijaks, kelle läbi ta on ka maailmad teinud,
3Yeye ni mng'ao wa utukufu wa Mungu, na mfano kamili wa hali ya Mungu mwenyewe, akiutegemeza ulimwengu kwa neno lake lenye nguvu. Baada ya kuwapatia binadamu msamaha wa dhambi zao, aliketi huko juu mbinguni, upande wa kulia wa Mungu Mkuu.
3kes, olles tema kirkuse kiirgus ja tema olemuse kuju ning kandes kõiksust oma väe sõnaga, on pärast seda, kui ta oli täide viinud pattudest puhastamise, istunud Ausuuruse paremale käele kõrgeimas taevas
4Mwana ni mkuu zaidi kuliko malaika, kama vile jina alilopewa na Mungu ni kuu zaidi kuliko jina lao.
4ning saanud ülemaks inglitest, kuivõrd ta on pärinud neist ülevama nime.
5Maana Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: "Wewe ni Mwanangu; Mimi leo nimekuwa Baba yako." Wala hakusema juu ya malaika yeyote: "Mimi nitakuwa Baba yake, naye atakuwa Mwanangu."
5Sest missugusele inglile on Jumal kunagi öelnud: 'Sina oled mu Poeg, täna ma sünnitasin sinu.'? Ja veel: 'Mina olen temale Isaks ja tema saab minule Pojaks!'?
6Lakini Mungu alipokuwa anamtuma Mwanae mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, alisema: "Malaika wote wa Mungu wanapaswa kumwabudu."
6Aga kui ta toob oma esmasündinu maa peale, siis ta ütleb: 'Ka kõik Jumala inglid kummardagu teda!'
7Lakini kuhusu malaika, Mungu alisema: "Mungu awafanya malaika wake kuwa pepo, na watumishi wake kuwa ndimi za moto."
7Inglite kohta ta ütleb küll: 'Ta teeb oma inglid tuulteks ja oma teenijad tuleleegiks.'
8Lakini kumhusu Mwana, Mungu alisema: "Utawala wako ee Mungu, wadumu milele na milele! Wewe wawatawala watu wako kwa haki.
8Aga Pojale ta ütleb: 'Sinu troon, Jumal, seisab igavesest ajast igavesti ja õiglus on su kuningakepp.
9Wewe wapenda uadilifu na kuchukia uovu. Ndiyo maana Mungu, Mungu wako amekuweka wakfu na kukumiminia furaha kubwa zaidi kuliko wenzako."
9Sa oled armastanud õigust ja vihanud ülekohut, seepärast on Jumal, sinu Jumal sind võidnud rõõmuõliga enam kui su kaaslasi.'
10Pia alisema: "Bwana, wewe uliumba dunia hapo mwanzo, mbingu ni kazi ya mikono yako.
10Ja: 'Sina, Issand, oled alguses rajanud maa ja taevad on su kätetöö.
11Hizo zitatoweka, lakini wewe wabaki daima, zote zitachakaa kama vazi.
11Need hävivad, aga sina jääd seisma, kõik nad kuluvad nagu kuub
12Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilishwa kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule daima, na maisha yako hayatakoma."
12ja sa keerad nad kokku just nagu rõiva, nagu kuue, ja nad muudetakse. Aga sina oled ikka seesama ja sinu aastad ei lõpe.'
13Mungu hakumwambia kamwe hata mmoja wa malaika wake: "Keti upande wangu wa kulia, mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako."
13Või missugusele inglile on ta kunagi öelnud: 'Istu mu paremale käele, kuni ma panen su vaenlased su jalajäriks!'?
14Malaika ni roho tu wanaomtumikia Mungu, na Mungu huwatuma wawasaidie wale watakaopokea wokovu.
14Eks nad kõik ole vaid teenijad vaimud, läkitatud abistama neid, kes ükskord pärivad pääste?