1Kwa sababu hiyo tunapaswa kuzingatia kwa makini zaidi yote tuliyosikia, ili tusije tukapotoshwa.
1Seepärast tuleb meil palju hoolsamini panna tähele seda, mida me oleme kuulnud, et meid kõrvale ei uhutaks.
2Ujumbe ule waliopewa wazee wetu na malaika ulionyeshwa kuwa kweli, hata mtu yeyote ambaye hakuufuata au hakuutii aliadhibiwa kama alivyostahili.
2Sest kui juba inglite kaudu räägitud sõna jäi püsima ning iga üleastumine ja sõnakuulmatus sai oma õige palga,
3Basi, sisi tutaokokaje kama hatuujali wokovu mkuu kama huu? Kwanza Bwana mwenyewe aliutangaza wokovu huu, na wale waliomsikia walituthibitishia kwamba ni kweli.
3kuidas siis meie võiksime pageda, kui me ei hooli nii suurest päästest, mis sai alguse Issanda enda kuulutusest ja mida meile on kinnitanud need, kes kuulsid,
4Mungu pia aliongeza hapo ushahidi wake kwa kufanya kila namna ya miujiza na maajabu, na kwa kuwagawia watu vipaji vya Roho Mtakatifu kadiri ya mapenzi yake.
4kusjuures Jumal ise on kinnitanud nende tunnistust tunnustähtede ja imedega, mitmesuguste vägevate tegudega ning Püha Vaimu andidega, mida ta jagas oma tahtmise järgi.
5Mungu hakuwaweka malaika wautawale ulimwengu ujao, yaani ulimwengu ule tunaoongea habari zake.
5Ta ei alistanud ju inglitele tulevast maailma, millest me räägime.
6Tena yasemwa mahali fulani katika Maandiko: "Mtu ni nini ee Mungu, hata umfikirie; mwanaadamu ni nini hata umjali?
6Aga keegi kusagil ütleb tunnistades: 'Mis on inimene, et sa teda meeles peaksid, või Inimese Poeg, et sa temast hooliksid?
7Ulimfanya kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika; ukamvika taji ya utukufu na heshima,
7Sa tegid ta pisut alamaks inglitest, siis sa pärgasid ta kirkuse ja auga,
8ukaweka kila kitu chini ya miguu yake, avitawale." Yasemwa kwamba Mungu alimweka mtu kuwa mtawala wa vitu vyote yaani bila kuacha hata kimoja. Hata hivyo, hatuoni bado mtu akivitawala vitu vyote sasa.
8kõik sa alistasid tema jalge alla.' Selles kõige alistamises ei ole ta jätnud ju midagi talle alistamata. Aga praegu me ei näe veel, et kõik oleks talle alistatud.
9Lakini twamwona Yesu ambaye alifanywa kwa kitambo kidogo kuwa chini zaidi kuliko malaika, ili kwa neema ya Mungu afe kwa ajili ya watu wote. Sasa tunamwona ametawazwa kwa utukufu na heshima kwa sababu ya kifo alichoteseka.
9Ometi me näeme teda, Jeesust, kes oli tehtud pisut alamaks inglitest, nii et ta Jumala armu läbi kõigi eest maitseks surma, nüüd pärjatuna kirkuse ja auga surma kannatamise pärast.
10Ilikuwa haki tupu kwamba Mungu, ambaye huumba na kutegemeza vitu vyote, alimfanya Yesu kuwa mkamilifu kabisa kwa njia ya mateso, ili awalete watoto wengi waushiriki utukufu wake. Maana Yesu ndiye anayewaongoza kwenye wokovu.
10Sest Jumalale, kelle päralt on kõik ja kelle läbi on kõik, oli kohane, et ta teeks kannatuste kaudu täiuslikuks nende pääste Rajaja, selle, kes viib kirkusse palju lapsi.
11Yeye anawatakasa watu dhambi zao, naye pamoja na wale waliotakaswa, wote wanaye Baba mmoja. Ndiyo maana Yesu haoni aibu kuwaita hao ndugu zake;
11Jah, niihästi Pühitseja kui pühitsetavad on kõik ühe Isa lapsed. Sel põhjusel Jeesus ei häbenegi neid hüüda vendadeks.
12kama asemavyo: "Ee Mungu, nitawatangazia ndugu zangu matendo yako. Nitakusifu katika kusanyiko lao."
12Ta ütleb: 'Ma tahan kuulutada su nime oma vendadele, koguduse keskel tahan ma laulda sulle kiitust!'
13Tena asema: "Nitamwekea Mungu tumaini langu." Na tena: "Mimi niko hapa pamoja na watoto alionipa Mungu."
13Ja taas: 'Ma tahan loota tema peale.' Ja taas: 'Vaata, siin olen mina ja lapsed, keda Jumal on mulle andnud!'
14Basi, kwa vile watoto hao, kama awaitavyo, ni watu wenye mwili na damu, Yesu mwenyewe akawa kama wao na kushiriki ubinadamu wao. Alifanya hivyo ili kwa njia ya kifo chake amwangamize Ibilisi, ambaye ana mamlaka juu ya kifo,
14Et nüüd lapsed on liha ja vere osalised, siis on ka Jeesus ise otse samal viisil liha ja vere omaks võtnud, et ta surma kaudu kõrvaldaks selle, kellel on võimus surma üle - see tähendab kuradi -,
15na hivyo awaokoe wale waliokuwa watumwa maisha yao yote kwa sababu ya hofu yao ya kifo.
15ja vabastaks need, kes surma kartes olid kogu eluaja orjapõlves.
16Maana ni wazi kwamba yeye hakuja kwa ajili ya kuwasaidia malaika, bali kama yasemavyo Maandiko; "Anawasaidia wazawa wa Abrahamu."
16Sest ega ta ometi hoolitse inglite eest, vaid ta hoolitseb Aabrahami soo eest!
17Ndiyo maana ilimbidi awe kama ndugu zake kwa kila namna, ili awe Kuhani Mkuu wao aliye mwaminifu na mwenye huruma katika kumtumikia Mungu, ili dhambi za watu ziondolewe.
17Seepärast ta pidigi kõiges saama vendade sarnaseks, et temast saaks halastav ja ustav ülempreester Jumala ees rahva pattude lepitamiseks.
18Na, anaweza sasa kuwasaidia wale wanaojaribiwa na kuteswa.
18Sest seetõttu, et ta ise on kannatanud kiusatuna, võib ta aidata neid, keda kiusatakse.