Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

3

1Ndugu zangu watu wa Mungu ambao mmeitwa na Mungu, fikirini juu ya Yesu ambaye Mungu alimtuma awe Kuhani Mkuu wa imani tunayoiungama.
1Seepärast, pühad vennad, taevase kutsumise osalised, mõtelgem meie usutunnistuse apostli ja ülempreestri Jeesuse peale,
2Yeye alikuwa mwaminifu kwa Mungu aliyemteua kufanya kazi yake kama vile Mose alivyokuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu.
2kes - nagu ka Mooses tema kojas - on olnud ustav oma Ametisseseadjale.
3Mjenzi wa nyumba hupata heshima zaidi kuliko hiyo nyumba yenyewe. Hali kadhalika naye Yesu anastahili heshima kubwa zaidi kuliko Mose.
3Sest tema vääris suuremat kirkust kui Mooses, nii nagu valmistajal on suurem au kui kojal.
4Kila nyumba hujengwa na mjenzi fulani--na Mungu ndiye mjenzi wa vitu vyote.
4Igal kojal on ju oma valmistaja, aga kes kõik on valmistanud, see on Jumal.
5Mose alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Bwana kama mtumishi, na alinena juu ya mambo ambayo Mungu atayasema hapo baadaye.
5Mooses oli küll ustav kogu tema kojas otsekui sulane tunnistuseks kõigest, mida veel pidi räägitama,
6Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana mwenye mamlaka juu ya nyumba ya Mungu. Sisi ni nyumba yake kama tukizingatia uhodari wetu na uthabiti wetu katika kile tunachotumainia.
6Kristus on aga tema koja üle kui ustav Poeg. Ja tema koda oleme meie, kui me vaid peame kinni julgusest ja lootusest, mille üle me kiitleme.
7Kwa hiyo, basi, kama asemavyo Roho Mtakatifu: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo,
7Seepärast on nõnda, nagu Püha Vaim ütleb: 'Täna, kui teie tema häält kuulete,
8msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu; kama walivyokuwa siku ile kule jangwani,
8ärge tehke oma südant kõvaks nagu nurina ajal, kiusatusepäeval kõrbes,
9Huko wazee wenu walinijaribu na kunichunguza, asema Bwana, ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu kwa miaka arobaini.
9kus teie esiisad kiusasid mind proovile pannes, kuigi nad olid minu tegusid näinud nelikümmend aastat.
10Kwa sababu hiyo niliwakasirikia watu hao nikasema, Fikira za watu hawa zimepotoka, hawajapata kamwe kuzijua njia zangu.
10Seepärast tõusis mu viha selle sugupõlve vastu ja ma ütlesin: Nad aina eksivad oma südames, aga minu teid nad ei ole ära tundnud.
11Basi, nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
11Nii ma vandusin oma vihas: Nad ei saa minu hingamisse!'
12Basi ndugu, jihadharini asije akawako yeyote miongoni mwenu aliye na moyo mbaya hivyo na asiyeamini hata kujitenga na Mungu aliye hai.
12Vaadake, vennad, kas ehk kellelgi teie seast ei ole kuri süda, mis uskmatuses ära taganeb elavast Jumalast!
13Maadamu hiyo "Leo" inayosemwa katika Maandiko bado inatuhusu sisi, mnapaswa kusaidiana daima, ili mtu yeyote miongoni mwenu asidanganywe na dhambi na kuwa mkaidi.
13Pigem julgustagem üksteist iga päev, niikaua kui veel öeldakse 'täna', et keegi teist ei paaduks patu pettuse läbi!
14Maana sisi tunashirikiana na Kristo ikiwa tutazingatia kwa uthabiti tumaini tulilokuwa nalo mwanzoni.
14Me oleme ju saanud Kristuse osalisteks, kui me vaid lõpuni kinni peame sellest, mis meil alguses oli.
15Maandiko yasema hivi: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu kama wazee wenu walivyokuwa wakati walipomwasi Mungu."
15Selles ütlemises: 'Täna, kui teie tema häält kuulete, ärge tehke oma südant kõvaks nagu nurina ajal' -
16Ni akina nani basi, waliosikia sauti ya Mungu wakamwasi? Ni wale wote walioongozwa na Mose kutoka Misri.
16kes siis olid need kuuljad, kes nurisesid? Eks ju kõik need, kes olid Egiptusest välja läinud Moosese juhtimisel?
17Mungu aliwakasirikia akina nani kwa miaka arobaini? Aliwakasirikia wale waliotenda dhambi, maiti zao zikatapakaa kule jangwani.
17Aga kelle peale ta viha tõusis neljakümneks aastaks? Eks nende peale, kes patustasid, kelle kehad langesid kõrbes surnuna?
18Mungu alipoapa: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko," alikuwa anawasema akina nani? Alikuwa anasema juu ya hao walioasi.
18Aga kellele ta siis vandus, et nemad ei saa tema hingamisse, kui mitte neile, kes olid sõnakuulmatud?
19Basi, twaona kwamba hawakuingia huko kwa sababu hawakuamini.
19Nii me näeme, et nad ei võinud sisse pääseda oma uskmatuse pärast.