Swahili: New Testament

Estonian

Hebrews

4

1Mungu alituahidia kwamba tutaweza kupata pumziko hilo alilosema. Basi, na tuogope ili yeyote kati yenu asije akashindwa kupata pumziko hilo.
1Kartkem siis, kuni tõotus saada tema hingamisse on veel jõus, et kedagi teie seast ei leita maha jäänud olevat!
2Maana Habari Njema imehubiriwa kwetu kama vile ilivyohubiriwa kwa hao watu wa kale. Lakini ujumbe huo haukuwafaa chochote, maana waliusikia lakini hawakuupokea kwa imani.
2Meile on kuulutatud evangeeliumi nõnda nagu neilegi, kuid kuuldud sõnast ei olnud neil kasu, sest see ei talletunud usu läbi kuulajaisse.
3Basi, sisi tunaoamini tunapata pumziko hilo aliloahidi Mungu. Kama alivyosema: "Nilikasirika, nikaapa: Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko." Mungu alisema hayo ingawa kazi yake ilikuwa imekwisha malizika tangu alipoumba ulimwengu.
3Meie aga, kes oleme uskunud, saame hingamisse, millest ta on öelnud: 'Nii ma vandusin oma vihas: Nad ei saa minu hingamisse!' Kuigi Jumala teod on olnud valmis juba maailma rajamisest peale -
4Maana Maandiko yasema mahali fulani kuhusu siku ya saba: "Mungu alipumzika siku ya saba, akaacha kazi zake zote."
4kusagil on ju öeldud seitsmenda päeva kohta nõnda: 'Ja Jumal hingas seitsmendal päeval kõigist oma tegudest',
5Tena jambo hili lasemwa pia: "Hawataingia huko ambako ningewapa pumziko."
5siin aga: 'Nad ei saa minu hingamisse'.
6Wale waliotangulia kuhubiriwa Habari Njema hawakupata pumziko hilo kwa sababu hawakuamini. Wapo, basi, wengine ambao wangejaliwa kulipata.
6Nii jääb nüüd võimalus, et mõned saavad sinna sisse. Ja et need, kellele evangeeliumi esmalt kuulutati, ei ole sinna sisse saanud oma sõnakuulmatuse pärast -,
7Jambo hili ni wazi, kwani Mungu aliweka siku nyingine ambayo inaitwa "Leo". Miaka mingi baadaye Mungu alisema juu ya hiyo siku kwa maneno ya Daudi katika Maandiko yaliyokwisha tajwa: "Kama mkisikia sauti ya Mungu leo, msiifanye mioyo yenu kuwa migumu."
7siis ta määrab jälle ühe päeva tänaseks päevaks, kui ta nii pika aja pärast Taaveti kaudu ütles, nõnda nagu varem on öeldud: 'Täna, kui te kuulete tema häält, ärge tehke oma südant kõvaks!'
8Kama Yoshua angaliwapa watu hao hilo pumziko, Mungu hangalisema baadaye juu ya siku nyingine.
8Sest kui Joosua oleks nad viinud hingamisse, siis ta ei oleks rääkinud pärast seda ühest teisest päevast.
9Kwa hiyo, basi, bado lipo pumziko kwa watu wa Mungu kama kule kupumzika kwake Mungu siku ya saba.
9Nii on siis Jumala rahva hingamisaeg alles ees,
10Maana, kila anayepata pumziko aliloahidi Mungu atapumzika baada ya kazi yake kama vile pia Mungu alivyopumzika baada ya yake.
10sest kes läheb tema hingamisse, see hingab ka ise oma tegudest, nii nagu Jumal oma tegudest.
11Basi, tujitahidi kupata pumziko hilo, ili asiwepo yeyote miongoni mwenu atakayeshindwa, kama walivyofanya wao kwa sababu ya ukosefu wao wa imani.
11Olgem siis agarad sisse minema sellesse hingamisse, et keegi ei langeks sellesama sõnakuulmatuse eeskujul!
12Neno la Mungu ni hai na lina nguvu; ni kali zaidi kuliko upanga wenye makali kuwili. Hukata kabisa mpaka mahali ambapo moyo na roho hukutana, mpaka pale vikutanapo viungo vya mwili na mafuta. Neno hilo huchambua nia na fikira za mioyo ya watu.
12Sest Jumala sõna on elav ja tõhus ja vahedam kui ükski kaheterane mõõk ning tungib läbi, kuni ta eraldab hinge ja vaimu, liigesed ja üdi, ning on südame meelsuse ja kaalutluste hindaja.
13Hakuna kiumbe chochote kilichofichika mbele ya Mungu; kila kitu kimefunuliwa wazi mbele ya macho yake. Kwake, sisi sote tutapaswa kutoa hoja ya matendo yetu.
13Ja ükski loodu ei ole tema ees nähtamatu, vaid kõik on alasti ja paljastatud tema silma ees - tema ees, kellele meil tuleb aru anda.
14Basi, tunapaswa kuzingatia kwa uthabiti imani tunayoiungama. Maana tunaye Kuhani Mkuu aliyeingia mpaka kwa Mungu mwenyewe--Yesu, Mwana wa Mungu.
14Et meil nüüd on suur ülempreester Jeesus, Jumala Poeg, kes on läbinud taevad, siis hoidkem kinni usust, mida me tunnistame!
15Huyu Kuhani Mkuu wetu si mmoja ambaye hawezi kutuunga mkono katika unyonge wetu, ila ni Kuhani Mkuu ambaye alijaribiwa kama sisi kwa kila namna lakini hakutenda dhambi.
15Sest meil pole niisugune ülempreester, kes ei suuda kaasa tunda meie nõrkustele, vaid selline, kes on olnud kõigiti kiusatud nii nagu meie, ja siiski ilma patuta.
16Basi, na tukikaribie bila hofu kiti cha enzi cha Mungu, palipo na neema, ili tukajipatie huruma na neema ya kutusaidia wakati wa lazima.
16Läki siis julgusega armu aujärje ette, et me halastust saaksime ja armu abiks leiaksime parajal ajal!