1Siku moja ya Sabato, Yesu alikuwa anapita katika mashamba ya ngano, na wanafunzi wake wakaanza kukwanyua masuke ya ngano, wakaondoa punje zake kwa mikono, wakala.
1Aga ühel hingamispäeval, kui Jeesus juhtus minema läbi viljapõldude, katkusid tema jüngrid viljapäid, hõõrusid neid käte vahel ja sõid.
2Baadhi ya Mafarisayo wakawauliza, "Mbona mnafanya jambo ambalo si halali siku ya Sabato?"
2Mõned variserid ütlesid: 'Miks te teete seda, mida ei tohi teha hingamispäeval?'
3Yesu akawajibu, "Je, hamjasoma jinsi alivyofanya Daudi pamoja na wenzake wakati walipokuwa na njaa?
3Ja Jeesus vastas neile: 'Kas te ei ole seda lugenud, mida tegi Taavet, kui tema ja ta mehed olid näljas?
4Yeye aliingia ndani ya nyumba ya Mungu, akachukua ile mikate iliyowekwa mbele ya Mungu, akala na kuwapa wenzake. Kisheria, ni makuhani tu peke yao ndio walioruhusiwa kula mikate hiyo."
4Kuidas ta läks Jumala kotta ja võttis ohvrileibu, sõi ja andis oma meestele, ehkki neid ei tohi süüa keegi peale preestrite?'
5Hivyo akawaambia, "Mwana wa Mtu ni Bwana wa Sabato."
5Ja ta ütles neile: 'Inimese Poeg on hingamispäeva isand.'
6Siku nyingine ya Sabato, Yesu aliingia katika sunagogi, akafundisha. Mle ndani mlikuwa na mtu ambaye mkono wake wa kuume ulikuwa umepooza.
6Aga see juhtus ühel teisel hingamispäeval, kui Jeesus läks sünagoogi ja õpetas. Seal oli inimene, kelle parem käsi oli kuivanud.
7Walimu wa Sheria na Mafarisayo walitaka kupata kisingizio cha kumshtaki Yesu na hivyo wakawa wanangojea waone kama angemponya mtu siku ya Sabato.
7Aga kirjatundjad ja variserid varitsesid teda, kas ta peaks tegema terveks hingamispäeval, et leida põhjust tema peale kaevata.
8Lakini Yesu alijua mawazo yao, akamwambia yule mwenye mkono uliopooza, "Inuka, simama katikati." Yule mtu akaenda akasimama katikati.
8Jeesus teadis nende mõtteid ja seepärast ütles mehele, kellel oli kuivanud käsi: 'Tõuse püsti ja astu keskele!' Too tõusis ja jäi seisma.
9Kisha Yesu akawaambia, "Nawaulizeni, je, ni halali siku ya Sabato kutenda jambo jema au kutenda jambo baya; kuokoa maisha au kuyaangamiza?"
9Jeesus ütles neile: 'Ma küsin teilt, kas hingamispäeval tohib teha head või halba, hinge päästa või hukata.'
10Baada ya kuwatazama wote waliokuwa pale, akamwambia yule mtu, "Nyosha mkono wako." Naye akafanya hivyo, na mkono wake ukawa mzima tena.
10Ja vaadanud neist igaühe peale, ütles Jeesus mehele: 'Siruta oma käsi!' Ja too tegi seda ning ta käsi sai jälle terveks.
11Lakini wao wakakasirika sana, wakajadiliana jinsi ya kumtendea Yesu maovu.
11Nemad läksid aga raevu ja arutasid omavahel, mida nad küll saaksid teha Jeesusele.
12Siku moja Yesu alikwenda mlimani kusali, akakesha huko usiku kucha akimwomba Mungu.
12Aga neil päevil sündis, et Jeesus läks mäele palvetama ja veetis kogu öö Jumalat paludes.
13Kesho yake aliwaita wanafunzi wake, na miongoni mwao akachagua kumi na wawili ambao aliwaita mitume:
13Ja kui valgeks läks, kutsus ta oma jüngrid enese juurde ja valis nende seast kaksteist, keda ta nimetas ka apostliteks:
14Simoni (ambaye Yesu alimpa jina Petro) na Andrea ndugu yake, Yakobo na Yohane, Filipo na Bartholomayo,
14Siimona, keda ta nimetas ka Peetruseks, ja tema venna Andrease, ja Jaakobuse ja Johannese ja Filippuse ja Bartolomeuse
15Mathayo na Thoma, Yakobo wa Alfayo na Simoni (aliyeitwa Zelote),
15ja Matteuse ja Tooma ja Jaakobuse, Alfeuse poja, ja Siimona, keda hüütakse Selooteseks,
16Yuda wa Yakobo na Yuda Iskarioti ambaye baadaye alikuwa msaliti.
16ja Juuda, Jaakobuse poja, ja Juudas Iskarioti, kes sai äraandjaks.
17Baada ya kushuka mlimani pamoja na mitume, Yesu alisimama mahali palipokuwa tambarare. Hapo palikuwa na kundi kubwa la wanafunzi wake na umati wa watu waliotoka pande zote za Yudea na Yerusalemu na pwani ya Tiro na Sidoni. Wote walifika kumsikiliza Yesu na kuponywa magonjwa yao.
17Ja kui Jeesus oli tulnud koos nendega mäelt alla, peatus ta lagedas paigas; seal oli suur hulk tema jüngreid ja väga palju rahvast kogu Juudamaalt ja Jeruusalemmast ning Tüürose ja Siidoni rannikualalt.
18Aliwaponya pia wote waliokuwa wanasumbuliwa na pepo wachafu.
18Nad kõik olid tulnud teda kuulama ja saama paranemist oma haigustest. Ja terveks said ka need, keda rüvedad vaimud piinasid.
19Watu wote walitaka kumgusa, kwa maana nguvu ilikuwa inatoka ndani yake na kuwaponya wote.
19Ja igaüks rahvast püüdis teda puudutada, sest temast läks vägi välja ja parandas kõik.
20Yesu akawageukia wanafunzi wake, akasema: "Heri ninyi mlio maskini, maana Ufalme wa Mungu ni wenu.
20Ja Jeesus tõstis silmad oma jüngrite poole ja ütles: 'Õndsad olete teie, vaesed, sest teie päralt on Jumala riik!
21Heri ninyi mnaosikia njaa sasa, maana baadaye mtashiba. Heri ninyi mnaolia sasa, maana baadaye mtacheka kwa furaha.
21Õndsad olete teie, kes te nüüd nälgite, sest teie saate küllaga! Õndsad olete teie, kes te nüüd nutate, sest teie saate naerda!
22"Heri yenu ninyi iwapo watu watawachukia, watawatenga, watawatukana na kuwaharibieni jina kwa ajili ya Mwana wa Mtu!
22Õndsad olete teie, kui inimesed teid vihkavad ja kui nad teid endi keskelt välja lükkavad ja teid häbistavad ja teie nime põlu alla panevad Inimese Poja pärast!
23Wakati hayo yatakapotokea, furahini na kucheza, maana hakika tuzo lenu ni kubwa mbinguni. Kwa maana wazee wao waliwatendea manabii vivyo hivyo.
23Olge rõõmsad sel päeval ja hüpake, sest vaata, teie palk on suur taevas! Just samal kombel tegid nende isad prohvetitele.
24Lakini ole wenu ninyi mlio matajiri, maana mmekwisha pata faraja yenu.
24Ent häda teile, rikkaile, sest teil on lohutus juba käes!
25Ole wenu ninyi mnaoshiba sasa, maana baadaye mtasikia njaa. Ole wenu ninyi mnaocheka kwa furaha sasa, maana baadaye mtaomboleza na kulia.
25Häda teile, kes te nüüd olete täissöönud, sest teie näete veel nälga! Häda teile, kes te nüüd naerate, sest teie saate leinata ja nutta!
26Ole wenu ninyi iwapo watu wote wanawasifu, maana wazee wao waliwafanyia manabii wa uongo vivyo hivyo.
26Häda teile, kui kõik inimesed räägivad teist hästi, sest nõndasamuti tegid ju nende vanemad valeprohvetitele.
27"Lakini nawaambieni ninyi mnaonisikiliza: wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale wanaowachukieni.
27Kuid ma ütlen teile, kes kuulete: Armastage oma vaenlasi, tehke head neile, kes teid vihkavad,
28Watakieni baraka wale wanaowalaani, na waombeeni wale wanaowatendea vibaya.
28õnnistage neid, kes teid neavad, palvetage nende eest, kes teid halvustavad!
29Mtu akikupiga shavu moja mgeuzie na la pili. Mtu akikunyang'anya koti lako mwachie pia shati lako.
29Kes sind lööb põse pihta, sellele paku ka teine, ja kes sinult võtab kuue, sellele ära keela ka särki!
30Yeyote anayekuomba mpe, na mtu akikunyang'anya mali yako usimtake akurudishie.
30Anna igaühele, kes sinult palub, ja sellelt, kes võtab sinu oma, ära küsi tagasi!
31Watendeeni wengine kama mnavyotaka wawatendee ninyi.
31Ja nii, nagu te tahate, et inimesed teile teeksid, nõnda tehke neile!
32"Na ikiwa mnawapenda tu wale wanaowapenda ninyi, je, mtapata tuzo gani? Hakuna! Kwa maana hata wenye dhambi huwapenda wale wanaowapenda wao.
32Ja kui te armastate neid, kes teid armastavad, mis lahkust te selle eest ootate? Isegi patused armastavad neid, kes neid armastavad.
33Tena, kama mkiwatendea mema wale tu wanaowatendeeni mema, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo!
33Ja kui te teete head neile, kes teile head teevad, mis tänu te selle eest ootate? Isegi patused teevad sedasama.
34Na kama mnawakopesha wale tu mnaotumaini watawalipeni, je, mtapata tuzo gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi wenzao ili warudishiwe kima kilekile!
34Ja kui te laenate neile, kellelt te loodate tagasi saada, mis tänu te selle eest ootate? Ka patused laenavad patustele, et nad samavõrra tagasi saaksid.
35Ila nyinyi wapendeni adui zenu, na kuwatendea mema; kopesheni bila kutazamia malipo, na tuzo lenu litakuwa kubwa, nanyi mtakuwa watoto wa Mungu aliye juu. Kwa maana yeye ni mwema kwa wale wasio na shukrani na walio wabaya.
35Aga armastage oma vaenlasi ning tehke head ning laenake ilma midagi tagasi lootmata, ja teie palk on suur ja te olete Kõigekõrgema lapsed, sest tema on helde tänamatute ja kurjade vastu!
36Muwe na huruma kama Baba yenu alivyo na huruma.
36Olge armulised, nagu teie Isa on armuline!
37"Msiwahukumu wengine, nanyi hamtahukumiwa; msiwalaumu wengine, nanyi hamtalaumiwa; wasameheni wengine, nanyi mtasamehewa.
37Ärge mõistke kohut, ja ka teie üle ei mõisteta kohut! Ärge mõistke hukka, ja ka teid ei mõisteta hukka! Andke andeks, ja teile antakse andeks!
38Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
38Andke, ja teile antakse - hea, tihedaks vajutatud, raputatud, kuhjaga mõõt antakse teie rüppe, sest selle mõõduga, millega teie mõõdate, mõõdetakse teile tagasi.'
39Akawaambia mfano huu: "Je, kipofu anaweza kumwongoza kipofu mwenzake? La! Wote wataanguka shimoni.
39Aga ta rääkis neile ka tähendamissõna: 'Ega pime suuda pimedat juhtida teel? Eks nad mõlemad kuku auku?
40Mwanafunzi hamshindi mwalimu wake, lakini kila mwanafunzi akisha hitimu huwa kama mwalimu wake.
40Ei ole jünger õpetajast üle, aga iga koolitatu on samasugune nagu ta õpetaja.
41Unawezaje kukiona kibanzi kilicho katika jicho la mwenzio, usione boriti iliyo katika jicho lako mwenyewe?
41Aga miks sa näed pindu oma venna silmas, palki iseenese silmas aga ei märka?
42Au, unawezaje kumwambia mwenzako, Ndugu, ngoja nikuondoe kibanzi katika jicho lako, na huku huioni boriti iliyoko katika jicho lako mwenyewe? Mnafiki wewe! Toa kwanza boriti iliyoko jichoni mwako, na hivyo utaona sawasawa kiasi cha kuweza kuondoa kibanzi kilicho katika jicho la ndugu yako.
42Kuidas sa võid oma vennale öelda: Vend, lase ma tõmban välja pinnu, mis on su silmas! ja ise ei näe palki oma silmas? Sa silmakirjatseja, tõmba esmalt palk oma silmast, siis sa näed tõmmata välja pindu, mis on su venna silmas!
43"Mti mwema hauzai matunda mabaya, wala mti mbaya hauzai matunda mazuri.
43Ei ole head puud, mis kannaks halba vilja, ega jälle halba puud, mis kannaks head vilja.
44Watu huutambua mti kutokana na matunda yake. Ni wazi kwamba watu hawachumi tini katika michongoma, wala hawachumi zabibu katika mbigili.
44Iga puu tuntakse ära ju tema viljast, sest ei korjata viigimarju kibuvitstelt ega koguta ohakailt viinamarjakobaraid.
45Mtu mwema hutoa yaliyo mema kutoka katika hazina bora iliyo moyoni mwake; na mtu mbaya hutoa yaliyo mabaya katika hazina mbaya iliyo moyoni mwake, kwa maana mtu huongea kutokana na yale yaliyojaa moyoni mwake.
45Hea inimene toob välja head oma südame heast tagavarast ja paha inimene toob pahast välja paha, sest ta suu räägib sellest, millest on tulvil ta süda.
46"Mbona mwaniita Bwana, Bwana, na huku hamtimizi yale ninayosema?
46Aga miks te mind hüüate: 'Issand, Issand!' ega tee, mida ma ütlen?
47Nitawapeni mfano unaofaa kuonyesha alivyo yeyote yule anayekuja kwangu, akasikia maneno yangu na kuyatimiza:
47Igaüks, kes tuleb minu juurde ja kuuleb mu sõnu ning teeb nende järgi - ma näitan teile, kelle sarnane ta on.
48Huyo anafanana na mtu ajengaye nyumba, ambaye amechimba chini na kuweka msingi wake juu ya mwamba; kukatokea mafuriko ya mto, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, lakini haukuweza kuitikisa, kwa sababu ilikuwa imejengwa imara.
48Ta on inimese sarnane, kes maja ehitades kaevas ja süvendas ja rajas selle aluse kaljule. Kui siis tuli suurvesi, paiskus vool vastu seda maja, aga ei suutnud seda kõigutada, sest see oli ehitatud hästi.
49Lakini yeyote anayesikia maneno yangu lakini asifanye chochote, huyo anafanana na mtu aliyejenga nyumba juu ya udongo, bila msingi. Mafuriko ya mto yakatokea, mkondo wa maji ukaipiga nyumba ile, ikaanguka na kuharibika kabisa!"
49Aga kes kuuleb ega tee, see on inimese sarnane, kes ehitas maja maa peale ilma aluseta; tulvaveed paiskusid selle vastu ja see varises kohe kokku, ja selle maja varisemine oli ränk.'