1Kisha nikaona mbingu mpya na dunia mpya. Mbingu ile ya kwanza na dunia ile ya kwanza vilikuwa vimetoweka, nayo bahari pia haikuweko tena.
1Ma nägin uut taevast ja uut maad; sest esimene taevas ja esimene maa olid kadunud ning merd ei olnud enam.
2Nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni. Ulikuwa umetayarishwa vizuri kama bibi arusi aliyepambwa tayari kukutana na mumewe.
2Ja ma nägin püha linna, uut Jeruusalemma, taevast Jumala juurest alla tulevat, valmistatud otsekui oma mehele ehitud mõrsja.
3Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka katika kiti cha enzi ikisema, "Tazama! Mungu amefanya makao yake kati ya watu. Atakaa kati yao, nao watakuwa watu wake, naye atakuwa Mungu wao.
3Ja ma kuulsin valju häält troonilt hüüdvat: 'Vaata, Jumala telk on inimeste juures ning tema asub nende juurde elama ning nemad saavad tema rahvaiks ning Jumal ise on nende juures nende Jumalaks.
4Yeye atayafuta machozi yao yote; maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu; maana ile hali ya kale imepita!"
4Tema pühib ära iga pisara nende silmist ning surma ei ole enam ega leinamist ega kisendamist, ning valu ei ole enam, sest endine on möödunud.'
5Kisha yule aliyeketi juu ya kiti cha enzi akasema, "Tazama, nafanya yote mapya." Tena akaniambia, "Andika hili, maana maneno haya ni ya kuaminika na ya kweli!"
5Ja troonil istuja ütles: 'Vaata, ma teen kõik uueks!' Tema ütles: 'Kirjuta, sest need sõnad on ustavad ja tõelised!'
6Kisha akaniambia, "Yametimia! Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Aliye na kiu nitampa kinywaji cha bure kutoka katika chemchemi ya maji ya uzima.
6Ja ta ütles mulle: 'See on sündinud! Mina olen A ja O, algus ja ots. Mina annan janusele ilma tasuta eluvee allikast.
7Yeyote atakayeshinda atapokea hiki, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
7Võitja pärib selle kõik ning mina saan temale Jumalaks ja tema saab minule pojaks.
8Lakini watu waoga, wasioamini, wapotovu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, na waongo wote, mahali pao patakuwa ndani ya lile ziwa linalowaka moto na kiberiti; hicho ndicho kifo cha pili."
8Aga argade ja uskmatute ja jäledate ja mõrtsukate ja hoorajate ja nõidade ja ebajumalateenijate ja kõigi valetajate osa on tule ja väävliga põlevas järves, see on teine surm.'
9Kisha mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba yaliyokuwa yamejaa mabaa saba ya mwisho, akaja na kuniambia, "Njoo! Mimi nitakuonyesha bibi arusi, mkewe Mwanakondoo!"
9Minu juurde tuli üks seitsmest inglist, neist, kelle käes on seitse kaussi täis seitset viimset nuhtlust, ning ta rääkis minuga ja ütles: 'Tule, ma näitan sulle mõrsjat, Talle naist!'
10Basi, Roho akanikumba, naye malaika akanipeleka juu ya mlima mrefu sana. Akanionyesha mji mtakatifu, ukishuka kutoka kwa Mungu mbinguni,
10Ja ta kandis mu vaimus suurele ja kõrgele mäele ning näitas mulle linna, püha Jeruusalemma, mis on alla tulemas taevast Jumala juurest
11uking'aa kwa utukufu wa Mungu. Mwangaza wake ulikuwa kama wa jiwe la thamani kubwa kama yaspi, angavu kama kioo.
11ja millel on Jumala kirkus, ning ta valgus on kõige kallima kivi sarnane, otsekui jaspis, mis hiilgab nagu mägikristall.
12Ulikuwa na ukuta mrefu na mkubwa, wenye milango kumi na miwili, na malaika wanangojea kumi na wawili. Majina ya wangoja milango kumi na mawili ya Israeli yalikuwa yameandikwa juu ya milango hiyo.
12Sellel on suur ja kõrge müür ning kaksteist väravat ja väravate peal kaksteist inglit; ning väravate peale on kirjutatud nimed, mis on Iisraeli laste kaheteistkümne suguharu nimed.
13Kila upande ulikuwa na milango mitatu: upande wa mashariki, milango mitatu, kaskazini milango mitatu, kusini milango mitatu na magharibi milango mitatu.
13Päevatõusu pool on kolm väravat, põhja pool kolm väravat, lõuna pool kolm väravat, õhtu pool kolm väravat.
14Kuta za mji huo zilikuwa zimejengwa juu ya mawe ya msingi kumi na mawili, na juu ya mawe hayo yalikuwa yameandikwa majina na mitume kumi na wawili wa Mwanakondoo.
14Ja linna müüril on kaksteist aluskivi ning nende peal Talle kaheteistkümne apostli nimed.
15Basi, yule malaika aliyekuwa anasema nami alikuwa na kijiti cha dhahabu cha kupimia, kwa ajili ya kuupima huo mji, milango yake na kuta zake.
15Ja sellel, kes minuga rääkis, oli käes kuldpilliroog, et mõõta linna ja selle väravaid ja selle müüri.
16Mji wenyewe ulikuwa wa mraba, upana na urefu wake sawa. Basi, malaika akaupima mji huo kwa kijiti chake: ulikuwa na urefu, upana na urefu wa kwenda juu, kama kilomita elfu mbili na mia nne.
16Linn on nelinurkne ning ta pikkus on võrdne laiusega. Ta mõõtis linna pillirooga - kaksteist tuhat vagu. Ta pikkus ja laius ja kõrgus on võrdsed.
17Kisha akaupima ukuta wake pia; nao ulikuwa mita sitini kwa kipimo cha macho cha kibinadamu ambacho malaika alitumia.
17Ja ta mõõtis tema müüri - sada nelikümmend neli küünart inimese, see tähendab ingli mõõdu järgi.
18Ukuta huo ulikuwa umejengwa kwa mawe mekundu ya thamani, na mji wenyewe ulikuwa umejengwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
18Selle müür on jaspisest ning linn ise puhtast kullast, selge klaasi sarnane.
19Mawe ya msingi wa ukuta huo yalikuwa yamepambwa kwa kila aina ya mawe ya thamani. Jiwe la kwanza la msingi lilikuwa jiwe la thamani jekundu, la pili yakuti samawati, la tatu kalkedoni, la nne zamaradi,
19Ja linna müüri aluskivid on ehitud igasuguste kalliskividega. Esimene aluskivi on jaspis, teine safiir, kolmas kaltsedon, neljas smaragd,
20la tano sardoniki, la sita akiki, la saba krisolito, la nane zabarijadi, la tisa topazi, la kumi krisopraso, la kumi na moja yasinto, na la kumi na mbili amethisto.
20viies sardoonüks, kuues karneool, seitsmes krüsoliit, kaheksas berüll, üheksas topaas, kümnes krüsopraas, üheteistkümnes hüatsint, kaheteistkümnes ametüst.
21Na ile milango kumi na miwili ilikuwa lulu kumi na mbili; kila mlango ulikuwa umetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji ilikuwa imetengenezwa kwa dhahabu safi, angavu kama kioo.
21Kaksteist väravat on kaksteist pärlit, iga värav ühest pärlist, ning linna tänav on puhtast kullast otsekui läbipaistev klaas.
22Sikuona hekalu katika mji huo, maana Bwana Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwanakondoo ndio Hekalu lake.
22Templit ma ei näinud seal, sest Issand, Kõigeväeline Jumal, on selle tempel, ning Tall.
23Mji huo hauhitaji jua wala mwezi kuangazia, maana utukufu wa Mungu huuangazia, na taa yake ni yule Mwanakondoo.
23Ja linnale ei ole vaja päikest ega kuud, et need talle paistaksid, sest Jumala kirkus valgustab teda, ning tema lamp on Tall.
24Watu wa mataifa watatembea katika mwanga wake, na wafalme wa dunia watauletea utajiri wao.
24Rahvad hakkavad käima tema valguses ning ilmamaa kuningad toovad sinna oma hiilguse.
25Milango ya mji huo itakuwa wazi mchana wote; maana hakutakuwa na usiku humo.
25Tema väravaid ei lukustata päeval, ent ööd seal ei olegi.
26Fahari na utajiri wa watu wa mataifa utaletwa humo ndani.
26Ja rahvaste hiilgus ja au kantakse sinna sisse.
27Lakini hakuna chochote kilicho najisi kitakachoingia humo; wala mtu yeyote atendaye mambo ya kuchukiza au ya uongo hataingia humo. Ni wale tu walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo ndio watakaoingia ndani.
27Sinna ei saa midagi, mis on rüve, ega keegi, kes teeb jäledusi ja valet, vaid üksnes need, kes on kirjutatud Talle eluraamatusse.