1Ndugu zangu, ninataka na kutazamia kwa moyo wangu wote hao wananchi wenzangu wakombolewe. Tena nawaombea kwa Mungu daima.
1Vennad, minu südamesoov ja eestpalve Jumala poole Iisraeli laste eest on, et nad pääseksid.
2Maana naweza kuthibitisha kwa niaba yao kwamba wanayo bidii ya kumtafuta Mungu; lakini bidii hiyo haikujengwa juu ya ujuzi wa kweli.
2Ma tunnistan neile, et neil on indu Jumala suhtes, kuid mitte tunnetuse kohaselt;
3Maana hawakufahamu jinsi Mungu anavyowafanya watu wawe waadilifu, na wamejaribu kuanzisha mtindo wao wenyewe, na hivyo hawakuikubali njia hiyo ya Mungu ya kuwafanya wawe waadilifu.
3sest nad ei mõista Jumala õigust ning, püüdes kehtestada oma õigust, ei ole alistunud Jumala õigusele.
4Maana kwa kuja kwake Kristo, Sheria imefikia kikomo chake, ili kila mtu anayeamini akubaliwe kuwa mwadilifu.
4Sest Seaduse lõpp on Kristus, õiguseks igaühele, kes usub.
5Kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa kuitii Sheria, Mose aliandika hivi: "Mtu yeyote anayetimiza matakwa ya Sheria ataishi."
5Sest Mooses kirjutab Seadusest tuleneva õiguse kohta: 'Inimene, kes seda teeb, jääb elama selle kaudu.'
6Lakini, kuhusu kukubaliwa kuwa mwadilifu kwa njia ya imani, yasemwa hivi: "Usiseme moyoni mwako: Nani atapanda mpaka mbinguni? (yaani, kumleta Kristo chini);
6Ent õigus, mis tuleb usust, ütleb: 'Ära ütle oma südames: Kes läheb üles taevasse? - see tähendab Kristust alla tooma,
7wala usiseme: Nani atashuka mpaka Kuzimu (yaani, kumleta Kristo kutoka kwa wafu)."
7või: Kes läheb alla sügavusse? - see tähendab Kristust üles tooma surnuist.'
8Maandiko Matakatifu yesema hivi, "Ujumbe huo wa Mungu uko karibu nawe, uko kinywani mwako na moyoni mwako" nao ndio ile imani tunayoihubiri.
8Kuid mida see siis ütleb? 'Sõna on su lähedal, sinu suus ja su südames.' See on ususõna, mida me kuulutame.
9Kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba Yesu ni Bwana na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka wafu, utaokoka.
9Kui sa oma suuga tunnistad, et Jeesus on Issand, ja oma südames usud, et Jumal on ta üles äratanud surnuist, siis sind päästetakse,
10Maana tunaamini kwa moyo na kukubaliwa kuwa waadilifu; na tunakiri kwa midomo yetu na kuokolewa.
10sest südamega usutakse õiguseks, suuga aga tunnistatakse päästeks.
11Maandiko Matakatifu yasema: "Kila amwaminiye hatakuwa na sababu ya kuaibika."
11Sest Pühakiri ütleb: 'Ükski, kes usub temasse, ei jää häbisse.'
12Jambo hili ni kwa wote, kwani hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi; Bwana wa wote ni mmoja, naye ni mkarimu sana kwao wote wamwombao.
12Ei ole ju erinevust juudi ja kreeklase vahel, sest seesama Issand on kõikide Issand, rikas kõikide heaks, kes teda appi hüüavad.
13Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
13Sest igaüks, kes hüüab appi Issanda nime, päästetakse.
14Basi, watamwombaje yeye ambaye hawamwamini? Tena, watamwaminije kama hawajapata kusikia habari zake? Na watasikiaje habari zake kama hakuna mhubiri?
14Kuidas nad siis saaksid appi hüüda teda, kellesse nad ei ole uskunud? Aga kuidas nad saaksid uskuda sellesse, kellest nad ei ole kuulnud? Kuidas nad saaksid kuulda ilma kuulutajata?
15Na watu watahubirije kama hawakutumwa? Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Ni jambo la kupendeza mno kuja kwa wale wanaohubiri Habari Njema!"
15Kuidas aga saadaks kuulutada, kui ei olda läkitatud? Just nagu on kirjutatud: 'Kui kaunid on nende jalad, kes kuulutavad head rõõmusõnumit.'
16Lakini wote hawakuipokea hiyo Habari Njema. Maana Isaya alisema: "Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?"
16Siiski mitte kõik ei ole saanud kuulekaks evangeeliumile. Sest Jesaja ütleb: 'Issand, kes on uskunud meie kuulutust?'
17Hivyo basi, imani inatokana na kuusikiliza ujumbe, na huo ujumbe unatokana na neno la Kristo.
17Järelikult, usk tuleb kuulutusest, kuulutus aga Kristuse sõna kaudu.
18Lakini nauliza: je, hawakuusikia huo ujumbe? Naam, waliusikia; kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Sauti yao imeenea duniani kote; maneno yao yamefika mpaka kingo za ulimwengu."
18Kuid ma küsin: Kas nad ei ole siis kuulnud? Muidugi on, sest: 'Kogu maale on kostnud nende hääl ja ilmamaa äärteni nende sõnad.'
19Tena nauliza: je, yawezekana kwamba watu wa Israeli hawakufahamu? Mose mwenyewe ni kwa kwanza kujibu: "Nitawafanyeni mwaonee wivu watu ambao si taifa; nitawafanyeni muwe na hasira juu ya taifa la watu wapumbavu."
19Kuid ma küsin: Kas Iisrael ei ole aru saanud? Mooses ise ütleb esimesena: 'Ma teen teid kiivaks nende peale, kes ei ole rahvas, ja teen teid vihaseks mõistmatu rahva peale.'
20Tena Isaya anathubutu hata kusema: "Wale ambao hawakunitafuta wamenipata; nimejionyesha kwao wasiouliza habari zangu."
20Jesaja aga ütleb julgemalt: 'Minu leidsid need, kes mind ei otsinud, ma sain avalikuks neile, kes minu järgi ei küsinud.'
21Lakini kuhusu Israeli anasema: "Mchana kutwa niliwanyoshea mikono yangu watu waasi na wasiotii."
21Aga Iisraeli kohta ta ütleb: 'Kogu päeva olen ma sirutanud oma käsi sõnakuulmatu ja vasturääkiva rahva poole.'