Swahili: New Testament

Estonian

Romans

11

1Basi, nauliza: je, Mungu amewakataa watu wake? Hata kidogo! Mini binafsi ni Mwisraeli mzawa wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
1Ma küsin siis: Kas Jumal on oma rahva ära tõuganud? Mitte sugugi! Minagi olen ju Iisraeli mees, Aabrahami soost, Benjamini suguharust.
2Mungu hakuwakataa watu wake aliowateua tangu mwanzo. Mnakumbuka yasemavyo Maandiko Matakatifu juu ya Eliya wakati alipomnung'unikia Mungu kuhusu Israeli:
2Jumal pole ära tõuganud oma rahvast, keda ta on ette ära tundnud. Kas te siis ei tea, mida Pühakiri ütleb Eelija loos, kuidas ta kaebab Jumala ees Iisraeli peale:
3"Bwana, wamewaua manabii wako na kubomoa madhabahu yako. Ni mimi tu peke yangu niliyebaki, nao wanataka kuniua?"
3'Issand, nad on tapnud sinu prohvetid ja maha kiskunud sinu altarid. Mina üksi olen järele jäänud, ja nad püüavad ka minu hinge.'
4Je, Mungu alimjibu nini? Alimwambia: "Nimejiwekea elfu saba ambao hawakumwabudu Baali."
4Kuid mida ütleb talle Jumala vastus? 'Ma olen enesele alles jätnud seitse tuhat meest, kes ei ole nõtkutanud põlvi Baali ees.'
5Basi, ndivyo ilivyo pia wakati huu wa sasa: ipo idadi ya waliobaki ambao Mungu aliwateua kwa sababu ya neema yake.
5Nõnda siis on ka nüüdsel ajal jääk alles jäänud armuvaliku järgi.
6Uteuzi wake unatokana na neema yake, na si kwa sababu ya matendo yao. Maana, kama uteuzi wake ungetegemea matendo ya watu, neema yake haingekuwa neema tena.
6Kui aga armust, siis mitte tegudest, sest muidu ei oleks arm enam arm. [Kui aga tegudest, siis mitte armust, sest muidu ei oleks tegu enam tegu.]
7Sasa, je? Watu wa Israeli hawakukipata kile walichokuwa wanakitafuta; lakini wote walioteuliwa walikipata. Wengine walipumbazwa,
7Kuidas siis nüüd? Mida Iisrael taotleb, seda ta ei ole saavutanud, ent äravalitud on selle saavutanud, aga ülejäänud on paadunud.
8kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Mungu ameifanya mioyo yao kuwa mizito, na mpaka leo hii hawawezi kuona kwa macho yao wala kusikia kwa masikio yao."
8Nõnda nagu on kirjutatud: 'Jumal on andnud neile tuimuse vaimu, silmad, mis ei näe, ja kõrvad, mis ei kuule kuni tänapäevani.'
9Naye Daudi anasema: "Karamu zao na ziwe mtego wa kuwanasa, waanguke na kuadhibiwa.
9Ja Taavet ütleb: 'Nende söögilaud saagu neile silmuseks ja püüniseks ja võrgutuseks ja kättemaksuks!
10Macho yao yatiwe giza wasiweze kuona. Migongo yao ipindike kwa taabu daima!"
10Nende silmad mingu pimedaks, et nad ei näeks, ja kõverda nende selg jäädavalt!'
11Basi, nauliza: je, Wayahudi wamejikwaa hata wakaangamia kabisa? Hata kidogo! Kutokana na kosa lao ukombozi umewajia watu wa mataifa mengine, ili Wayahudi wapate kuwaonea wivu.
11Ma küsin siis: Kas nad on komistanud, et nad kukuksid? Mitte sugugi! Vaid nende väärsammu tõttu on paganatele osaks saanud pääste, et teha Iisraeli lapsi kiivaks.
12Kosa la Wayahudi limesababisha baraka nyingi kwa ulimwengu, na utovu wao kwa kiroho umeleta baraka nyingi kwa watu wa mataifa mengine. Basi, ni dhahiri zaidi kwamba utimilifu wao utasababisha baraka nyingi zaidi.
12Kui aga juba nende väärsamm on rikkus maailmale ning nende kaotus rikkus paganatele, kui palju enam siis nende täisarv!
13Basi, sasa nawaambieni ninyi watu wa mataifa mengine: Maadamu mimi nimekuwa mtume kwa watu wa mataifa mengine, ninajivunia huduma yangu,
13Aga ma räägin teile, paganatele: Kuna ma olen paganate apostel, austan ma oma ametit -
14nipate kuwafanya wananchi wenzangu wawaonee ninyi wivu, na hivyo nipate kuwaokoa baadhi yao.
14ehk ma saan kuidagi teha kiivaks neid, kelle veresugulane ma olen, ning mõned nende seast päästa.
15Maana ikiwa kukataliwa kwao kulisababisha ulimwengu upatanishwe na Mungu, itakuwaje wakati watakapokubaliwa na Mungu? Wafu watafufuka!
15Sest kui juba nende kõrvaleheitmine on maailma lepitus, mis on siis nende vastuvõtmine muud kui surnuist ellutõusmine?
16Ikiwa kipande cha kwanza cha mkate kimewekwa wakfu, mkate wote umewekwa wakfu; mizizi ya mti ikiwa mizuri, na matawi yake huwa mazuri pia.
16Aga kui uudsevili on püha, siis on ka taigen püha, ja kui juur on püha, siis on ka oksad pühad.
17Naam, baadhi ya matawi ya mzeituni bustanini yalikatwa, na mahali pake tawi la mzeituni mwitu likapandikizwa. Ninyi watu wa mataifa mengine ndio hilo tawi la mzeituni mwitu; na sasa mnashiriki nguvu na utomvu wa mzeituni bustanini.
17Kui nüüd okstest mõned on ära murtud, sina aga kui metsõlipuu oled nende asemele poogitud ja saad osa õige õlipuu mahlakast juurest,
18Basi, msiwadharau wale waliokatwa kama matawi! Na, hata kama kuna la kujivunia, kumbukeni kwamba si ninyi mnaoitegemeza mizizi, bali mizizi ndiyo inayowategemeza ninyi.
18siis ära hoople okste ees. Ja kui sa hoopled, siis pea meeles, et sina ei kanna juurt, vaid juur kannab sind.
19Lakini utasema: "Matawi yalikatwa kusudi mimi nipandikizwe mahali pake."
19Sina ehk ütled nüüd: 'Oksad on ära murtud, et mind asemele pookida.'
20Sawa! Yalikatwa kwa sababu ya kukosa imani, bali wewe unasimama kwa imani yako. Lakini usijivune; ila uwe na tahadhari.
20Õige küll! Nemad on ära murtud uskmatuse pärast, sina püsid aga usu läbi. Ära mõtle kõrgilt, vaid karda,
21Kwa maana, ikiwa Mungu hakuwahurumia Wayahudi ambao ni kama matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe?
21sest kui Jumal ei säästnud loomulikke oksi, ega ta siis sindki säästa!
22Kumbuka, basi, jinsi Mungu alivyo mwema na mkali. Yeye ni mkali kwa wale walioanguka, na ni mwema kwako wewe ikiwa utaendelea katika wema wake; la sivyo, nawe pia utakatwa.
22Vaata siis Jumala heldust ja karmust: karmust küll nende vastu, kes on langenud, heldust aga sinu vastu, kui sa jääd heldusesse, muidu raiutakse sindki maha.
23Nao Wayahudi, hali kadhalika; wakiacha utovu wao wa imani, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
23Aga ka nemad, kui nad ei jää uskmatusse, poogitakse puu külge, sest Jumal suudab nad jälle külge pookida.
24Ninyi watu wa mataifa mengine, kwa asili ni kama tawi la mzeituni mwitu, lakini mmeondolewa huko, mkapandikizwa katika mzeituni bustanini mahali ambapo kwa asili si penu. Lakini, Wayahudi kwa asili ni kama mzeituni bustanini, na itakuwa jambo rahisi zaidi kwao kupandikizwa tena katika mti huohuo wao.
24Sest kui sina, loomu poolest metsõlipuu oks, oled sealt ära raiutud ja loomuvastaselt poogitud väärisõlipuu külge - kui palju enam neid, loomu poolest sinna kuuluvaid, poogitakse omaenese õlipuu külge!
25Ndugu zangu, napenda mjue ukweli huu uliofichika msije mkajiona wenye akili sana. Ukaidi wa Wayahudi ulikuwa ni wa muda tu, mpaka watu wa mataifa mengine watakapokuwa wamemfikia Mungu.
25Vennad, ma ei taha ju, et teile jääks teadmata see saladus - et teie poleks enda meelest targad -, et Iisraelile on osaliselt tulnud paadumus, kuni paganate täiskogus on sisse astunud,
26Hapo ndipo taifa lote la Israeli litakapookolewa, kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Mkombozi atakuja kutoka Sioni, atauondoa uovu wa Yakobo.
26ja nõnda pääseb lõpuks kogu Iisrael, nagu on kirjutatud: 'Siionist tuleb vabastaja, tema kõrvaldab Jaakobist jumalakartmatuse.
27Hili ndilo agano nitakalofanya nao wakati nitakapoziondoa dhambi zao."
27Ja see on minu leping nendele, kui ma kustutan ära nende patud.'
28Kwa sababu wanaikataa Habari Njema, Wayahudi wamekuwa adui wa Mungu, lakini kwa faida yenu nyinyi watu wa mataifa. Lakini, kwa kuwa waliteuliwa, bado ni rafiki wa Mungu kwa sababu ya baba zao.
28Evangeeliumi poolelt vaadates on nad küll Jumala vaenlased teie heaks, aga valiku poolelt vaadates on nad armastatud esiisade pärast.
29Maana Mungu akisha wapa watu zawadi zake na kuwateua, hajuti kwamba amefanya hivyo.
29Jumal ei kahetse ju oma armuande ega kutsumist.
30Hapo awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmepata huruma yake kutokana na kuasi kwao.
30Sest otsekui teie tollal olite Jumalale sõnakuulmatud, nüüd on aga teie peale nende sõnakuulmatuse tõttu halastatud,
31Hali kadhalika, kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi, Wayahudi wanamwasi Mungu sasa ili nao pia wapokee sasa huruma ya Mungu.
31nõnda on nüüd ka nemad muutunud sõnakuulmatuks teile osaks saanud halastuse pärast, et ka nende peale halastataks.
32Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi wao ili wapate kuwahurumia wote.
32Sest Jumal on kõik inimesed kinni pannud sõnakuulmatuse alla, et kõikide peale halastada.
33Utajiri, hekima na elimu ya Mungu ni kuu mno! Huruma zake hazichunguziki, na njia zake hazieleweki! Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu:
33Oh seda Jumala rikkuse ja tarkuse ja tunnetuse sügavust! Ei suudeta uurida tema kohtumõistmisi ega jälgida tema teed!
34"Nani aliyepata kuyajua mawazo ya Bwana? Nani awezaye kuwa mshauri wake?
34Sest kes on ära tundnud Issanda meele? Või kes on olnud talle nõuandjaks?
35Au, nani aliyempa yeye kitu kwanza hata aweze kulipwa tena kitu hicho?"
35Või kes on talle midagi enne andnud, et talle tuleks tasuda?
36Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, vyote vipo kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Utukufu na uwe kwake hata milele! Amina.
36Jah, temast ja tema läbi ja temasse on kõik. Temale olgu kirkus igavesti! Aamen.