1Kwa hiyo, ndugu zangu, maadam Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: jitoleeni nafsi zenu kwa Mungu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu.
1Nüüd, vennad, kutsun ma teid üles Jumala suure halastuse pärast tooma oma ihud Jumalale elavaks, pühaks ja meelepäraseks ohvriks; see olgu teie mõistlik jumalateenistus.
2Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu, kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu.
2Ja ärge muganduge praeguse ajaga, vaid muutuge meele uuendamise teel, et te katsuksite läbi, mis on Jumala tahtmine, mis on hea ja meelepärane ja täiuslik.
3Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni ninyi nyote: msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kufuatana na kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.
3Sest selle armu tõttu, mis mulle on antud, ütlen ma igaühele teie seast, et ta ei mõtleks üleolevalt selle kohta, mida tuleb mõtelda, vaid mõtleks nõnda, et saaks arukaks sedamööda, kuidas Jumal igaühele usu mõõdu on jaganud.
4Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake.
4Sest otsekui meil on ühes ihus palju liikmeid, aga kõigil liikmeil ei ole sama tegevus,
5Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake.
5nõnda oleme meie paljud üks ihu Kristuses, üksikult aga üksteise liikmed.
6Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake.
6Aga meil on meile antud armu järgi erinevaid armuande: olgu prohvetliku kuulutamise and, mida kasutatagu usu mõõtu mööda;
7Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe.
7olgu teenimine, mis toimugu teenimisametis; olgu keegi õpetaja, siis toimigu ta õpetajaametis;
8Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.
8olgu keegi hingehoidja, siis toimigu ta hingehoidjaametis; kes teistele jagab, andku siira südamega; kes teist juhatab, olgu innukas; kes on hoolekandja, olgu oma ametis sõbralik.
9Mapendo yenu na yawe bila unafiki wowote. Chukieni jambo lolote ovu, zingatieni jema.
9Armastus olgu siiras. Kurjast hoidudes kiinduge heasse!
10Pendaneni kidugu; kila mmoja amfikirie mwenzake kwanza kwa heshima.
10Vennaarmastuses olge üksteise vastu hellad, vastastikuses austuses jõudke üksteisest ette!
11Msilegee katika bidii, muwe wachangamfu rohoni katika kumtumikia Bwana.
11Teenige Issandat tüdimatu innuga ja vaimult tulisena!
12Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida na kusali daima.
12Olge rõõmsad lootuses, vastupidavad viletsuses, püsivad palves!
13Wasaidieni watu wa Mungu katika mahitaji yao; wapokeeni wageni kwa ukarimu.
13Abistage pühasid nende puuduses, püüdke olla külalislahked!
14Watakieni baraka wote wanaowadhulumu ninyi; naam, watakieni baraka na wala msiwalaani.
14Õnnistage oma tagakiusajaid, õnnistage ja ärge needke!
15Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
15Rõõmustage rõõmsatega, nutke nutjatega!
16Muwe na wema uleule kwa kila mtu. Msijitakie makuu, bali jishugulisheni na watu wadogo. Msijione kuwa wenye hekima sana.
16Olge omavahel üksmeelsed! Ärge mõtelge kõrgilt, vaid laske end tõmmata madalate hulka! Ärge olge endi meelest targad!
17Msilipe ovu kwa ovu. Zingatieni mambo mema mbele ya wote.
17Ärge tasuge kellelegi kurja kurjaga, hoolitsege selle eest, mis on hea kõigi inimeste silmis!
18Kadiri inavyowezekana kwa upande wenu, muwe na amani na watu wote.
18Kui võimalik, niipalju kui oleneb teist, pidage rahu kõigi inimestega!
19Wapenzi wangu, msilipize kisasi, bali mwachieni Mungu jambo hilo; maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kulipiza kisasi ni shauri langu; mimi nitalipiza asema Bwana."
19Ärge makske ise kätte, armsad, vaid andke maad Jumala vihale, sest on kirjutatud: 'Minu päralt on kättemaks, mina tasun kätte' - nii ütleb Issand.
20Tena, Maandiko yasema: "Adui yako akiwa na njaa, mpe chakula; akiwa na kiu, mpe kinywaji. Maana kwa kufanya hivyo utamfanya apate aibu kali kama makaa ya moto juu ya kichwa chake."
20Veel enam: 'Kui sinu vaenlane nälgib, toida teda, kui tal on janu, anna talle juua, sest seda tehes sa kuhjad tuliseid süsi tema pea peale!'
21Usikubali kushindwa na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
21Ära lase kurjal võitu saada enese üle, vaid võida sina kuri heaga!