Swahili: New Testament

Estonian

Romans

9

1Nasema ukweli mtupu; nimeungana na Kristo nami sisemi uongo. Dhamiri yangu ikiongozwa na Roho Mtakatifu inanithibitishia jambo hili pia.
1Ma räägin tõtt Kristuses, ma ei valeta, minu kaastunnistaja on mu südametunnistus Pühas Vaimus,
2Nataka kusema hivi: nina huzuni kubwa na maumivu yasiyopimika moyoni mwangu
2et mul on suur kurbus ja südamel lakkamatu valu,
3kwa ajili ya watu wangu, walio damu moja nami! Kama ingekuwa kwa faida yao, ningekuwa radhi kulaaniwa na kutengwa na Kristo.
3sest ma sooviksin pigem ise olla neetud ja Kristusest lahutatud oma vendade heaks, kes on mu veresugulased,
4Hao ndio watu wa Israeli ambao Mungu aliwateua wawe watoto wake, akawashirikisha utukufu wake; aliagana nao, akawapa Sheria yake, imani ya kweli na ahadi zake.
4kes on iisraellased, kelle päralt on lapseõigus ja kirkus ja lepingud ja seadustik ja jumalateenistus ja tõotused,
5Wao ni wajukuu wa mababu, naye Kristo, kadiri ya ubinadamu wake, ametoka katika ukoo wao. Mungu atawalaye juu ya yote, na atukuzwe milele! Amina.
5kelle päralt on esiisad ja kelle seast Kristus on ihu poolest. Jumal, kes on üle kõige, olgu kiidetud igavesti! Aamen.
6Sisemi kwamba ahadi ya Mungu imebatilika; maana si watu wote wa Israeli ni wateule wa Mungu.
6Aga see pole nõnda, et Jumala sõna oleks läinud tühja. Ei ole ju need kõik, kes pärinevad Iisraelist, veel Iisrael,
7Wala, si wazawa wote wa Abrahamu ni watoto wake wa kweli. Ila, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Wazao wake watatokana na Isaka."
7ega ole kõik Aabrahami lapsed sellepärast, et nad on tema järglased, vaid on öeldud: 'Sinu sugu loetakse Iisakist.'
8Nido kusema, wale waliozaliwa kimaumbile ndio watoto wa Mungu, bali wale waliozaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ndio watakaoitwa watoto wake.
8See tähendab: mitte lihased lapsed ei ole Jumala lapsed, vaid tema sooks arvatakse tõotuse lapsed.
9Maana ahadi yenyewe ni hii: "Nitakujia wakati maalum, naye Sara atapata mtoto."
9Sest see on tõotusesõna: 'Ma tulen tagasi sellesama aastaaja paiku, ja Saaral on siis poeg.'
10Tena si hayo tu ila pia Rebeka naye alipata mapacha kwa baba mmoja, yaani Isaka, babu yetu.
10Ent mitte ainult temaga, vaid ka Rebekaga oli sama lugu, kui ta jäi lapseootele meie esiisast Iisakist,
11Lakini, ili Mungu aonekane kwamba anao uhuru wa kuchagua, hata kabla wale ndugu hawajazaliwa na kabla hawajaweza kupambanua jema na baya,
11sest kui kaksikud veel ei olnud sündinud ega teinud midagi head ega halba, siis - et valikule põhinev Jumala kavatsus jääks püsima
12Rebeka aliambiwa kwamba yule mtoto wa kwanza atamtumikia yule wa nyuma. Hivyo uchaguzi wa Mungu unategemea jinsi anavyoita mwenyewe, na si matendo ya binadamu.
12mitte tegude, vaid kutsuja pärast - öeldi talle: 'Suurem orjab vähemat',
13Kama Maandiko Matakatifu yasemavyo: "Yakobo nilimpenda, lakini Esau nilimchukia."
13nagu on kirjutatud: 'Jaakobit ma armastasin, Eesavit aga vihkasin.'
14Basi, tuseme nini? Je, Mungu amekosa haki? Hata kidogo!
14Mis me siis ütleme? Kas Jumala juures on ebaõiglust? Mitte sugugi!
15Maana alimwambia Mose: "Nitamhurumia mtu yeyote ninayetaka kumhurumia; nitamwonea huruma mtu yeyote ninayetaka."
15Ta ju ütleb Moosesele: 'Ma halastan, kellele ma halastan, ja heidan armu, kellele ma heidan armu.'
16Kwa hiyo, yote hutegemea huruma ya Mungu, na si bidii au mapenzi ya mtu.
16Nõnda siis ei sõltu see inimese tahtest ega pingutusest, vaid Jumalast, kes halastab.
17Maana Maandiko Matakatifu yasema hivi kwa Farao: "Nilikufanya mfalme ili kwa njia yako, uwezo wangu ujulikane, na jina langu litangazwe popote duniani."
17Ütleb ju Pühakiri vaarao kohta: 'Just selleks olen ma sind üles äratanud, et sinu juures näidata oma väge, ja et minu nime kuulutataks kogu maal.'
18Ni wazi, basi, kwamba Mungu humhurumia yeyote anayetaka kumhurumia, na akipenda kumfanya mtu awe mkaidi, hufanya hivyo.
18Niisiis, ta halastab, kellele tahab, ning kalgistab, keda tahab.
19Labda utaniuliza: "Ikiwa mambo yako hivyo, Mungu anawezaje kumlaumu mtu? Nani awezaye kuyapinga mapenzi yake?"
19Nüüd sa ütled mulle: 'Mis ta siis enam ette heidab! Kes saab vastu panna tema tahtmisele?'
20Lakini, ewe binadamu, u nani hata uthubutu kumhoji Mungu? Je, chungu chaweza kumwuliza mfinyanzi wake: "Kwa nini umenitengeneza namna hii?"
20Oh inimene, kes sina õigupoolest oled, et sa tahad Jumalaga vaielda? Ega siis savinõu ütle oma voolijale: 'Miks sa mu nõnda oled teinud?'
21Mfinyanzi anaweza kuutumia udongo apendavyo na kufinyanga vyungu viwili kwa udongo uleule; kimoja kwa matumizi ya heshima, na kingine kwa matumizi ya kawaida.
21Või kas pole potissepal meelevalda savi üle - valmistada samast segust üks nõu auliseks, teine aga autuks tarbeks?
22Hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu. Alitaka kuonyesha ghadhabu yake na kujulisha uwezo wake, Basi, alikuwa na saburi sana, akiwavumilia wale ambao walikuwa lengo la ghadhabu yake, ambao walistahili kuangamizwa.
22Eks Jumal, tahtes näidata oma viha ja teha tuntavaks oma väge, ole suure pikameelsusega talunud vihanõusid, mis olid valmistatud hukatuseks,
23Alitaka pia kudhihirisha wingi wa utukufu wake ambao alitumiminia sisi tulio lengo la huruma yake; sisi ambao alikwisha kututayarisha kuupokea utukufu wake.
23ja teinud seda selleks, et ilmutada oma kirkuse rikkust armunõude vastu, mis ta oli juba enne valmistanud kirkuseks?
24Maana sisi ndio hao aliowaita, si tu kutoka miongoni mwa Wayahudi bali pia kutoka kwa watu wa mataifa mengine.
24Nende hulka on ta kutsunud meidki, mitte üksnes juutide, vaid ka paganate seast.
25Maana ndivyo asemavyo katika kitabu cha Hosea: "Wale waliokuwa Si watu wangu nitawaita: Watu wangu! Naye Sikupendi ataitwa: Mpenzi wangu!
25Nõnda nagu ta ütleb ka Hoosea raamatus: 'Ma hüüan oma rahvaks teda, kes ei olnud minu rahvas, ja armsaks teda, kes ei olnud mulle armas.
26Na pale walipoambiwa: Ninyi si wangu hapo wataitwa: Watoto wa Mungu hai."
26Ja siis sünnib selles paigas, kus neile öeldi: Teie pole minu rahvas!, et seal hüütakse neid elava Jumala poegadeks.'
27Naye nabii Isaya, kuhusu Israeli anapaaza sauti: "Hata kama watoto wa Israeli ni wengi kama mchanga wa pwani, ni wachache tu watakaookolewa;
27Aga Jesaja hüüab Iisraeli kohta: 'Kui Iisraeli laste arv oleks nagu mereliiv, siiski pääsevad neist vaid riismed,
28maana, Bwana ataitekeleza upesi hukumu yake kamili juu ya ulimwengu wote."
28sest lõplikult ja kiiresti teeb Issand tõeks oma sõna maa peal.'
29Ni kama Isaya alivyosema hapo awali: "Kama Bwana Mwenye Nguvu asingalituachia baadhi ya watoto wa Israeli, tungalikwisha kuwa kama Sodoma, tungalikwisha kuwa ma Gomora."
29Ja nõnda on Jesaja ette öelnud: 'Kui vägede Issand poleks meile jätnud seemet, siis oleksime olnud nagu Soodom ja saanud Gomorra sarnaseks.'
30Basi, tuseme nini? Ni hivi: watu wa mataifa ambao hawakutafuta kukubaliwa kuwa waadilifu, wamekubaliwa kuwa waadilifu kwa njia ya imani,
30Mis me siis ütleme? Seda, et paganad, kes õigust ei taotlenud, on õiguse kätte saanud, ent õiguse, mis tuleb usust.
31hali watu wa Israeli waliokuwa wakitafuta Sheria iletayo kukubaliwa kuwa waadilifu, hawakuipata.
31Aga Iisrael, kes taotles õigust Seaduse varal, ei ole Seaduseni ulatunud.
32Kwa nini? Kwa sababu walitegemea matendo yao badala ya kutegemea imani. Walijikwaa juu ya jiwe la kujikwaa
32Mispärast? Sellepärast, et nad ei lähtunud usust, vaid arvasid õigeks saavat tegudest. Nad komistasid vastu komistuskivi,
33kama yesemavyo Maandiko Matakatifu: "Tazama! Naweka huko Sioni jiwe likwazalo, mwamba utakaowafanya watu waanguke. Mtu atakayemwamini yeye aliye hilo jiwe, hataaibishwa!"
33nagu on kirjutatud: 'Ennäe, ma panen Siionisse komistuskivi ja pahanduskalju, ja see, kes usub temasse, ei jää häbisse.'